SABABU 10 za kwanini Dk. John Pombe Magufuli atashinda uchaguzi wa mwaka huu

Maramla

JF-Expert Member
Jan 8, 2014
581
642
1. Tanzania bara na visiwani yako majimbo ya uchaguzi 266, CCM imesimamisha wagombea Ubunge katika majimbo yote 266 huku Chadema na washirika wake wa Ukawa wakiwa wamesimamisha wagombea katika majimbo 211 (138 toka Chadema). Kati ya majimbo hayo 266, CCM tayari imepita bila kupingwa majimbo 7. Ukichukua majimbo 259 yaliyobaki na kutoa 211 ambayo Chadema na washirika wake wamesimamisha wagombea unabaki na majimbo 48 ambayo CCM haina upinzani wa Chadema wala washirika wake wa Ukawa. Majimbo haya 48 CCM ina uhakika wa kushinda walau kwa asilimia 90, ushindi huu si kwa Wabunge tu bali pia kwa mgombea Urais wa CCM.

2. Watanzania waliojiandikisha kupiga kura mwaka 2015 ni milioni 24.2. Takwimu zinaonyesha CCM ina wanachama hai wapatao milioni 8 wenye kadi na wanaolipia ada zao za uanachama kila mwaka. Kuondoka kwa Edward Lowassa katika Chama Cha Mapinduzi kunamaanisha Magufuli hatapata kura zote milioni 8 za wana CCM na pia kihesabu si rahisi wana CCM wote milioni 8 kujitokeza siku ya kupiga kura. Utafiti unaonyesha kwamba wana CCM watakaopiga kura hawatazidi asilimia 90 ya wanachama wake (milioni 7.2) huku milioni 7 kati yao wakimpigia kura John Magufuli. Historia ya CCM inaonyesha ni wanachama wachache sana humpigia kura kada mwenzao anapohama kugombea nafasi kwa chama kingine, hasa nafasi ya Urais (Rejea: Uchaguzi wa Urais 1995, mgawanyo wa kura za Augustine Lyatonga Mrema)

3. Mizunguko ya kampeni huzaa kura za ziada mbali na zile za wanachama. Tayari inaonyesha kwamba Magufuli anapita karibu kila kata ya Tanzania akitumia barabara huku upande wa Lowassa na shirikisho la Ukawa hali ikiwa tofauti, ambako amekuwa akifika sehemu chache akitumia usafiri wa ndege na helkopta na ni wazi hana stamina ya kuzunguka kwa gari nchi nzima kutokana na tatizo la kiafya. CCM ina mizizi kwenye mashina kuanzia ngazi ya nyumba kumi. Mtandao huu wa Chama pamoja na safari za mgombea wao kila kata ni kiashiria kwamba atafikia wapiga kura wengi zaidi hasa sehemu za vijijini na ambazo si rahisi kufikika. Tafiti zinaonyesha huko ndiko kwenye wapiga kura wengi na kuwafikia ni hatua moja kuelekea kuzipata kura zao na kushinda.

4. Chaguzi za Serikali za Mitaa mwaka 2014 zinaonyesha kwamba CCM ilishinda kwa zaidi ya asilimia 80 kwenye nafasi za uongozi za serikali za vijiji na mitaa. Ikumbukwe kwamba CCM ilipata ushindi huu licha ya ushindani mkubwa uliokolezwa na sakata la Escrow wakati huo. Hii inaonyesha kwamba CCM iliweza kushinda hata wakati huo wa changamoto. Ni mwaka mmoja tu umepita tangu chaguzi hizo zifanyike. Kitafiti, hiki ni kiashiria kikubwa kwamba katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, CCM kama chama kinaenda kwenye sanduku la wapiga kura kikiwa na rekodi nzuri kuweza kushinda.

5. Rekodi ya Utendaji ya Magufuli inavutia Watanzania wengi. Utafiti unaonyesha kwamba wapinzani wake majukwaani mpaka sasa wanapata wakati mgumu kutaja jina lake moja kwa moja kumuhusisha na utendaji wa hovyo. Mitandaoni zipo video na nukuu nyingi zikiwemo za Mgombea wa Ukawa Edward Lowassa, Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na wengineo wakisifia utendaji wa Magufuli. Katika siasa na kampeni, hatua moja kuonyesha mgombea anashinda ni kushindwa kwa wapinzani wake kumnyooshea kidole moja kwa moja au kukosa mabaya ya kusema dhidi yake. Asiye na la kukusema vibaya anawapa wananchi nafasi ya kuona mazuri yako na kushinda.

6. Suala la afya ya wagombea limekuwa gumzo kubwa katika uchaguzi wa mwaka huu. Huku ikiwa wazi kwamba Mgombea wa Ukawa Edward Lowassa anaugua ugonjwa wa Parkinson's kwa muda mrefu sasa, Magufuli hajawa na changamoto ya afya. Ugonjwa wa Parkinson's alio nao Edward Lowassa unaathiri ubongo wa kati, moyo, mishipa ya fahamu na uwezo wa kufikiri (Afya ya mwili maeneo hayo ni muhimu kiongozi kuwa nayo). Kwa muda mrefu Lowassa amekuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa huu katika hospitali maarufu ya Franziskus-Krankenhus mtaa wa Budapester jijini Berlin, Ujerumani. Kiumri Magufuli ana miaka 55 huku Lowassa akiwa na miaka 63. Wapiga kura huchagua kiongozi kwa kutazama muonekano na ni wazi kabisa kwamba kwa muonekano na hali ya kiafya ya Lowassa ni dhoofu na inazidi kudorora siku hadi siku na kuwakatisha tamaa hata wanaomuunga mkono. Tangu kampeni zianze hakuna mahala ambapo amewahi kuzungumza kwa zaidi ya dakika 15. Hivyo basi, kwa kadiri siku zinavyoenda Watanzania watazidi kubaini kwamba Lowassa hana afya ya kuhimili vishindo vya kampeni wala uwezo wa kumudu majukumu ya Urais.

7. Nguvu ya vyama, oganaizesheni na ilani. Magufuli anatokea CCM ambayo kama nilivyoeleza juu ina nguvu ya kuwepo kila kijiji na kila nyumba kumi Tanzania; imetoa marais waliotangulia, na hata wapinzani wametoka katika CCM hiyo hiyo baada ya kukosa nafasi za kugombea kupitia chama hicho. Kwa miaka mitatu iliyopita Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amezunguka kila kona ya nchi akikinadi chama chake, hii ni aina ya kampeni ambayo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa. Kwa upande wa upinzani hali iko tofauti. Mgombea wao, Lowassa alikuwa mwanachama wa CCM miezi miwili iliyopita, kuingia kwake Chadema kumeleta mpasuko huku Katibu Mkuu wake akitokomea kusikojulikana, na Mwenyekiti wa CUF, Lipumba naye akijiuzulu uongozi kupinga Lowassa kukaribishwa Ukawa. Hii inaonyesha hali si shwari katika upinzani. Kwa sasa Ukawa wanaficha mpasuko huo kwa propaganda lakini madhara yatajitokeza kabla ya siku ya uchaguzi. Moja ya viashiria vya mpasuko katika Ukawa ni kuvunjika kwa makubaliano ya kuweka mgombea mmoja wa Ubunge katika kila jimbo. Zaidi ya asilimia 70 ya majimbo yana wagombea Ubunge toka vyama vyote vinavyounda Ukawa. Kwa mfano Lowassa, kama mgombea Urais wa Ukawa, akienda Ubungo ambapo kuna wagombea toka Chadema, CUF na NCCR atamnadi mgombea yupi?

8. Kuondoka kwa Dr Slaa Chadema, tuhuma za Mbowe kuiuza Chadema kwa Lowassa kwa TZS bilioni 10 (ambazo Dr Slaa amezithibitisha) na ukawa kuhama kutoka kumuita Edward Lowassa fisadi mkuu wa nchi miaka michache iliyopita hadi sasa kumfanya kuwa mgombea wao. Hii imewakanganya Watanzania wengi na wote wanaochukua muda kulitafakari wanazidi kupata maswali zaidi. Uamuzi wa mpigakura katika hali kama hii ni kuendelea kulipigia kura zimwi alijualo (CCM) kuliko zimwi jipya asiloelewa (Ukawa).

9. Matumizi makubwa ya fedha katika kutafuta madaraka. Mpaka mwisho wa mwezi Agosti 2015 Lowassa alikuwa tayari ametumia zaidi ya TZS bilioni 106 kwa kipindi cha miaka miwili na nusu kwanza kutafuta nafasi kugombea ndani ya CCM na kisha kuhamia Ukawa. Wananchi wengi wanahoji zinapotoka fedha hizi, wengi wakikumbuka kauli ya Mwalimu Nyerere kwamba "Mtanzania wa leo hawezi kukununua kabla ya yeye kwanza kununuliwa". Wananchi wanahoji namna gani Lowassa anapanga kurejesha fedha hizi iwe zake (pia wanahoji kazipataje) au za marafiki zake (lengo lao kumpa fedha ni nini). Magufuli hana kashfa ya namna hii na hata kampeni zake za kuomba kuteuliwa ndani ya CCM hazikuwa za matumizi ya fedha kabisa. Kama wananchi watapiga kura kwa kuangalia uadilifu katika kupata na kutumia fedha, na pia kama watapiga kura wakiamini kwamba Ikulu si mahali pa kufanya biashara ili mtu arejeshe fedha alizotumia wakati wa kampeni na kuhonga kupata nafasi basi Magufuli ana nafasi kubwa ya kushinda.

10. Mzimu wa Mwalimu Nyerere: Mwaka 1995 Mwalimu Nyerere alisema wazi kwamba Lowassa hafai kuwa Rais wa Tanzania, alikatwa jina lake kwa haki (video ya Mwalimu akisema haya iko mitandaoni na ni moja ya video zinazotazamwa kwa wingi wakati huu wa uchaguzi mkuu) na hakuna maana kuendelea kumjadili na kwamba chama kisonge mbele. Watu wanaomjua vizuri Lowassa na shughuli anazozifanya wanasema kwa miaka 20 Lowassa hajabadili zile sifa zilizomfanya Mwalimu kutamka maneno yale mwaka 1995. Hata alipoomba familia ya Mwalimu Nyerere kumuunga mkono alipoondoka CCM alijibiwa wazi kwamba yeye hajawahi kuwa chaguo la Mwalimu. Watanzania bado wanamuheshimu na kumuamini Mwalimu Nyerere na ni wazi watachagua kiongozi wakifuata wosia wake. Uadilifu wa Magufuli utamuwezesha kuaminiwa na Watanzania na kushinda nafasi hii.
 
Hakuna hata hoja moja hapo juu ambayo imethibitika kiutafiti, wala yenye elements of reality. Those are just your assumptions kama zile za uvccm na ushindi wa 85%. Mfano, Mwaka 2010 Nape alisema ccm ina wanachama 6,000,000, Ukweli ni kuwa kila mwaka ccm imeendelea kudhoofika badala ya kuimarika. Idadi ya wanachama wa ccm ni chini kabisa ya 6,000,000. Pili ni hoja yako ya kwanza kuwa majimbo 48 Magufuli atapata kura nyingi kwa kuwa UKAWA hawakusimamisha mgombe (poor assumption). Kutokusimamisha mgombea haimaanishi kuwa chama hakitaruhusiwa kufanya kampeni ktk jimbo husika na pia haimaanishi eti kwa kuwa tu hawajamsimamisha mgombea. Na pia sio kigezo kuwa mgombea wa upinzani kwa tiketi ya urais hakubaliki eti tu kwa sababu chama chake hakikusimamisha mgombea. Hoja zote 10 ni dhaifu sana.
 
hapakazitu watanzania wanataka kiongozi mwenye kufanya kazi na kuwajibisha viongozi wengine pale wanaposhindwa kufanya aunkutimiza majukumu yao naimani na magufuli!
 
Nyie ndio watu ambao sheria za Mitandao inabidi iwapitie tena iwafunge jela kabisa....... Nijibu haya maswali yangu kwanza

1) wewe ni Dactari wa Lowasa mpaka ujue ugonjwa wake ?

2) wewe ni mhasibu wa Lowasa Mpaka ujue kiasi alichotumia?
 
Hakuna wa Kumzuia Mh. Lowassa Kuingia Magogoni... Ndia ni Nyeupe.
Toeni vigezo kama mwenzenu alivyotoa. Hivi you cannt analyse the situation kabisa. Unaishia kusema eti njia nyeupe. Hii sio akili ya ushindani. Kama majibu yenyewe ndio haya , basi tutapigwa asubuhi mapeeeema na Magufuli.
Wafuasi wa Dr Slaa tumeshasema POPOTE ALIPO TUPO.! ameshatuambia Lowasa hafai basi na sisi tunasema HAFAI KUWA RAIS WA TANZANIA. LABDA URAIS WA MONDULI NA FAMILIA YAKE. AENDE AKAENDELEE NA BIASHARA ZAKE HATUMUHITAJI.
HATUHITAJI MTU MCHAFU KAMA YEYE KAMA VIONGOZI WETU WALIVYOTUAMINISHA.
Biashara anazo nyingi za kufa mtu, viwanja kibao Tanzania hii, majumba kadhaa nchi nzima kama viongozi makamanda wetu walivyotuaminisha. Sasa anataka nini.
LABDA ANATAKA KUUZA NCHI TUTAJUAJE.
LABDA ANATAKA KUHAMISHA GESI ILIYOPO KUPELEKA NJE
LABDA ANATAKA AWALIPE FADHILA WALE WALIOKUWA NAO WAKITOA MABILIONI YAO KUM SUPPORT.
LABDA ANATAKA KULIPA KISASI KWA WALE WALIOKUWA WAKIMUANDAMA.
LABDA ANATAKA KUKABIDHI NCHI HII SASA KWA TEAM YAKE ILI NAO WAPATE NAFASI YA KUCHOTA MAHELA
Haaaahahahah WANANCHI TUMESHAZINDUKA.! WALA ASIHANGAIKE AKAFILISIKA BUREE
 
"CCM mkitaka #KURA yangu semeni ukweli nani anahusika na hizi tuhuma? na wahusika wamechukuliwa hatua gani?
-Katiba pendekezwa nani aliyaondoa maoni ya wananchi ambayo yalikuwepo kwenye rasimu ya Warioba?
-Mabehewa feki
-Kiwira
-Richmond
-Epa
-Escrow
-Epa
-Dowans
-IPTL
-NET GROUP SOLUTIONS
-Usafirishaji wa wanyama nje ya nchi mfano twiga alipandaje ndege?
-Biashara ya pembe za ndovu
-Biashara ya madawa ya kulevya
-Meremeta
-Mikataba ya gesi na mafuta
-Uuzwaji wa nyumba za serikali
Nahitaji majibu ya hayo maswali siyo poro
 
Mimi nina attack tu hoja yako ya kwanza zingine hata sikuwa na haja nazo kuzisoma. CCM imesimamisha majimbo 266 wakati UKAWA wamesimamisha 211 sawa kabisa. Ungesupport hoja yako kuonyesha kwamba uwezekano wa kushinda hayo yote 266 upo au hata nusu yake tu. UKAWA ikishinda majimbo 200 CCM itabakiwa na Mangapi? 66?...Halafu eti unajiita Mchambuzi. Tizama upepo unvovuma ndugu, ni dhahili miti yote inateleza. CCM msijisifie kuwa mmesimamisha majimbo mengi wakati uwezekano wakushinda hata nusu haupo.
 
Ngonjera, ngonjera na ngonjera. Hizo kura 2 za Dk. Mihogo na mamsap wake ndio mnafika milioni 8?

Nyie tulieni jua lipambazuke. Mlizoea kura wa wanawake wasio jitambua, sasa mjue mwaka huu 50/50 au hujashtuka kwamba muitikio wa kupokea Khanga umekuwa mdogo?

Wale wazee baada ya kuutukana umma wamelala mbele, wamemuacha halimselema halija peke yake jukwaani akitoa ahadi zile zile za tangu 1995.

Watanzania wa leo sio wa kuwaahidi 'tukiingia Ikulu tutawalipa fidia watu wa Kipunguni A' hii ni dalili ya udhalimu. Yaani haki yao hawaipati mpk wakuhongeni kura? Mnajichosha bure na ngonjera, muda huu mjiimarishe kwenye mapambio ya msiba na rambirambi
 
Back
Top Bottom