nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Mwandishi Wetu Toleo la 297 5 Jun 2013
KAMA rasimu ya Katiba iliyotangazwa wiki hii itaridhiwa, basi wapiga kura wanaweza kumng'oa mbunge wao kabla hata ya kukamilisha kipindi chake cha miaka mitano, wakirejea sababu mojawapo kati ya takriban 10 zinazotajwa kikatiba.
Ibara ya 124 (1) ya rasimu hiyo inaeleza; "......wananchi watakuwa na haki ya kumuondoa mbunge wao madarakani, endapo mbunge atafanya mojawapo ya mambo yafuatayo;
Mosi, kuunga mkono sera ambazo zinakwenda kinyume cha maslahi ya wapiga kura au kinyume cha maslahi ya Taifa. Pili, kushindwa kuwasilisha au kutetea kwa dhati hoja zinazotokana na kero za wapiga kura wake. Tatu, kuacha kuishi au kuhamisha makazi yake kutoka eneo la Jimbo la Uchaguzi kwa zaidi ya miezi sita bila sababu za msingi.
Nne, kutohudhuria vikao vya Bunge vitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika. Tano, kuajiriwa au kufanya kazi nyingine na kuacha kuzingatia kazi yake ya kuonana na wapiga kura wake. Sita; kufanya biashara, kumiliki kampuni au kuwa na hisa katika kampuni ambazo zina mikataba au uhusiano wa kibiashara na taasisi za umma kwa namna ambayo inaleta mgongano wa kimaslahi.
Saba; kutiwa hatiani kwa kosa linalohusiana na rushwa au kosa jingine la jinai. Nane, kutenda kitendo ambacho ni kinyume cha maadili au kukosa uaminifu. Tisa, kushindwa kuwasilisha au kutetea hoja zinazotokana na kero za wapiga kura wake au kumi: mambo mengine yatakayoainishwa kwenye sheria ya Bunge.
- Ni pamoja na kutoishi jimboni, kutohudhuria vikao vya Bunge
KAMA rasimu ya Katiba iliyotangazwa wiki hii itaridhiwa, basi wapiga kura wanaweza kumng'oa mbunge wao kabla hata ya kukamilisha kipindi chake cha miaka mitano, wakirejea sababu mojawapo kati ya takriban 10 zinazotajwa kikatiba.
Ibara ya 124 (1) ya rasimu hiyo inaeleza; "......wananchi watakuwa na haki ya kumuondoa mbunge wao madarakani, endapo mbunge atafanya mojawapo ya mambo yafuatayo;
Mosi, kuunga mkono sera ambazo zinakwenda kinyume cha maslahi ya wapiga kura au kinyume cha maslahi ya Taifa. Pili, kushindwa kuwasilisha au kutetea kwa dhati hoja zinazotokana na kero za wapiga kura wake. Tatu, kuacha kuishi au kuhamisha makazi yake kutoka eneo la Jimbo la Uchaguzi kwa zaidi ya miezi sita bila sababu za msingi.
Nne, kutohudhuria vikao vya Bunge vitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika. Tano, kuajiriwa au kufanya kazi nyingine na kuacha kuzingatia kazi yake ya kuonana na wapiga kura wake. Sita; kufanya biashara, kumiliki kampuni au kuwa na hisa katika kampuni ambazo zina mikataba au uhusiano wa kibiashara na taasisi za umma kwa namna ambayo inaleta mgongano wa kimaslahi.
Saba; kutiwa hatiani kwa kosa linalohusiana na rushwa au kosa jingine la jinai. Nane, kutenda kitendo ambacho ni kinyume cha maadili au kukosa uaminifu. Tisa, kushindwa kuwasilisha au kutetea hoja zinazotokana na kero za wapiga kura wake au kumi: mambo mengine yatakayoainishwa kwenye sheria ya Bunge.