Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
Mwenyekiti wa Tume ya marekebisho ya katiba; Joseph Sinde Warioba, hivi karibuni amekuwa akitoa matamshi yanayoonyesha dhahiri kutunyanyapaa wananchi ambao tumekuwa mstari wa mbele kutoa maoni yetu kwenye tume tajwa!
Pamoja na kauli zake tata, Warioba amedai maoni yetu yamefanana kupindukia na ni kwa sababu tunayatoa maoni hayo kwa mashinikizo ya NGOs, vyama vya kisiasa na taasisi za kidini! (La ajabu, hakuzitaja!)
Kauli hizi zinatia mashaka makubwa katika maeneo yafuatayo kwa tume tajwa kututendea haki:-
1) Tuhuma za Warioba dhidi yetu hajazipa ushahidi wowote hata basi kuwataja kwa majina taasisi husika ikiashiria kuwa haheshimu utawala bora ambao unamsukuma ahakikishe ya kuwa tuhuma zinaandamana na ushahidi ili ziweze kupatiwa majibu fasaha........na watuhumiwa.
2) Ni dhahiri kwa vile tunaishi nchi moja na kukabiliana na changa moto zinazofanana ni wazi maoni ya majibu ya kero zetu pia yatashabihiana.......................sasa sijui kwanini Warioba atushangae kwa hilo?
3) Tusisahau wajumbe wote wanaounda tume ni matunda ya mfumo mbovu tulionao wa kiutawala hivyo tunapowaona wameanza kupembua uhalali wa maoni yetu hata kabla ya wao kuikamilisha kazi ya kuyakusanya maoni tajwa wasiwasi wetu ni kuwa huenda kwenye mikoba yao wana katiba wanayoitaka kuishinikiza tuipigie kura ya maoni na ushirikishwaji wetu ni "danganya toto" tu!
4) Kitendo cha tume kuhoji uhalali wa maoni yetu lakini bado wanaendelea kuyakusanya ili kuhalalisha malipo makubwa ya posho wanazojilipa inatuthibitishia ya kuwa lengo siyo kuutafuta ukweli bali kuupotosha ukweli kwa malipo lukuki kwenye vibindo vyao!
5) Wajumbe wote hawana wasifu wa kuupigania na kuutetea mfumo wa utawala bora na hata kuhatarisha mkate wao. Wengi wao wamebandikwa huko kwa sababu ya kuutetea udhalimu na hivyo si rahisi siye kuwaamini kama watatutendea haki na kuwakilisha kile ambacho tumewaambia na baadhi ya mifano ya taswira zao ni kama ifuatavyo:-
i) Bw. Warioba kupanda kwake kwenye chati ya uongozi hapa nchini kwa kiasi kikubwa alinufaika na kivuno cha "ukabila" wakati wa utawala wa Nyerere. Sidhani kama Raisi kama asingelikuwa anatoka Musoma angeliweza kuteua Mwanasheria Mkuu kwa kiwango cha duni cha uzoefu alichokuwa nacho Warioba wakati alipoteuliwa. Mwaka 1990, Mwinyi aliunda tume ya kumchunguza Warioba njia alizozitumia kuukwaa ubunge wa Bunda na tume ilithibitisha ya kuwa alitumia vibaya madaraka yake ya dhamana ya Uwaziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Uraisi na kushauri aenguliwe.
Aidha tume feki ya kuthibiti mianya ya ufisadi ambayo aliisimamia wakati wa Mkapa ilitutupia changa la machoni pale msisitizo wake ulipokuwa kuwakomoa baadhi ya watendaji serikalini badala ya kuona mfumo mzima wa kiutawala ulikuwa ni tatizo kubwa la uchocheaji wa ufisadi serikalini. Mapendekezo yake yalijaa visasi na akina Bw. Nalaila Kiula na wenzie baadaye walikuja kusafishwa na mahakama na hadi leo Warioba au serikali haijawahi kuwaomba msamaha waathirika hawa au hata kuwafidia!
Pengine baya kuliko yote Warioba amehusishwa moja kwa moja na ufisadi wa EPA na hadi leo hajarudisha hata sumuni au hata kufikishwa kwenye vyombo vya dola kuchunguzwa kama kweli njia alizozitumia kujichotea mabilioni BOT zilizingatia sheria zilizopo.
Katika wasifu wa Warioba kama ulivyo wasifu wa wajumbe karibuni wote wa tume ni kuwa nafasi zote walizowahi kuzishika za kiutendaji serikalini hawajawahi kuziomba au hata kushindana na mtu yoyote na hivyo kuwatarajia wapendekeze nafasi zote serikalini kupatikana kwenye mazingira ya uwazi na ushindani kuwa ni njozi za ajuza.
ii) Makamu wao wa tume, Jaji Mkuu mstaafu - Augustine Ramadhani- alijivika joho la kuishinikiza mahakama ya Rufaa ambayo alikuwa akiisimamia kuzuia mgombea binafsi akidai siyo kazi ya mahakama kuliingilia bunge wakati katiba kama ilivyo sheria nyingine mahakama ndicho chombo pekee iliyopewa mamlaka ya kuzitafsiri sheria zote zikiwemo za kikatiba kuona kama zinalinda utawala bora. Jaji Ramadhani kwa kasi ya mithili ya mwewe, aliteua tume ya majaji wenzie saba badala kuanzia majaji watatu ili kuzika haki yetu hiyo ya kimsingi kabisa. Hivi leo jaji Ramadhani kweli atakuwa kabadilika na huku yeye mwenyewe alikiri kuwa ule uamuzi aliutoa kwa mashinikizo ya kisiasa? Ni vigumu kwetu kumkubali kuwa anaweza kututendea haki pale ambapo Ikulu ileile ya JK iliyomteua kuwa jaji Mkuu kwenye mazingira yasiyoeleweka na aliiogopa kwenye suala la mgombea binafsi leo ageuka kuwa ngangari! Labda atueleze ile khofu aliyokuwa nayo kama jaji Mkuu sasa imezimwa na na nini...........................???????
iii) Dr. Senkondo Mvungi ni kinara wa kuzuia utawala bora ndani ya NCCR Mageuzi na mfano ni pale aliposhangilia kufukuzwa uanachama kwa mbunge wao wa Kigoma kwa kosa la kuwania kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama chao. Hivi kama kugombea nafasi ambayo ni haki ya kikatiba ni nongwa je inapokuja masuala ambayo watawala hawayataki kwa sababu yanahatarisha mkate wao huyu ni mwakilishi wa kutumainiwa au ni sehemu ya uwakilishi haramu?
iv) Uwakilishi wa cdm pia una sura kama hiyo ambapo madiwani wanatimuliwa na hivyo kudhoofisha maana halisi ya "people's power" ambayo wamekuwa wakituzuga nayo.................................kama walaji wawili, watatu kule Dar-CDM ambao hawakushiriki kwenye chaguzi za kuchagua madiwani wana nguvu ya kufutilia mbali "people's power" ya wapigakura kweli unawategema watusaidie katiba ambayo italinda misingi ya utu ndani ya katiba tarajiwa kama siyo ubabaishaji mtupu?
v) Wajumbe wote wa tume hawana wasifu wa kutetea utawala bora zaidi ya kutetea mkate wao unapokuwa hatarani kuangukiwa na vumbi tu............
6) Kwa vile wajumbe wa tume hawajajitokeza hadharani na kumpinga Warioba na kauli zake za kubeza demokrasia na ambazo zimo nje ya hadidu za rejea alizopewa ni sahihi kwetu kuchukulia tume nzima iliukubali msimamo tajwa na hivyo haina uhalali tena wa kuendelea na ukusanyaji wa maoni tajwa bali kufungasha virago na kurudia kazi zao zenye kipato cha mwendo wa kinyonga..............
7) Tume wakati ikijitungia hadidu ya rejea ya kutupasha madhaifu yetu kazi ambayo siyo yao, wamesahahu kujipanga na kuja na mkakati wa jinsi gani sheria mpya ziundwe kabla ya uchaguzi wa 2015 ambazo bila ya sheria hizo katiba mpya hata iwe imeboreshwa vipi kamwe hatutaweza kuitekeleza. Wao wamejipanga kumaliza zoezi hili mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu wakati sheria nyingi za kuuongoza uchaguzi huo zinadai miaka angalau 3 kama uzoefu wa majirani zetu wa kenya unatoa busara zozote hapa..................
8) Kutojenga njia pana na kuwagharimia taasisi huria katika kuhakiki jinsi tume inavyofanya kazi ni dhahiri tume utendaji wake haiwajibiki kwa yeyote yule jambo ambalo linatia dosari zoezi zima. Tulipaswa tuwe na vyombo vingi huria ambavyo navyo vitahakiki utendaji wa kazi wa tume badala ya sisi kusubiria ghiliba za tambo za Warioba kama sehemu ya hakiki tajwa........................
9) Sheria inayoanzisha tume tajwa haijaipa tume mamlaka ya kuyawakilisha maoni ya wananchi kwa bunge badala yake wanayapeleka kwa Raisi ambaye ana kila shauku ya kuchakachua maoni tajwa. Kumbuka JK ni sehemu ya serikali ya Mkapa ambayo ilikuja na "white paper" ambayo ni misimamo ya serikali ya katiba ya watawala na waliipitisha kwa mabavu nyakati hizo. Hivi leo unapoona JK anapokataa kulimilikisha bunge zoezi hilo na kulichakachua kwa kulichanganya na la wakilishi visiwani wakati kuna Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na marekebisho haya yanafanyika nje ya katiba yetu...........................sasa tutarajie nini?..........mimi naendelea kushangaa tunaruhusu watu wale pesa zetu kwa utapeli wa kutuandikia katiba mpya kwa mfumo wa utaratibu ambao hautambuliki ndani ya katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania ila sheria inatumika kutengua mantiki zote zilizomo ndani ya katiba!!!!!!!!!!........Uandikaji wa katiba mpya lazima unahitaji marekebisho ya kikatiba ili zoezi hilo liweze kuwa na meno ya kisheriana wala siyo vinginevyo.
10) Uteuzi wa tume haukuwa wazi, shirikishi na wenye ushindani lakini bado tunaitegemea tume ije na mapendekezo ambayo ni shirikishi, wazi na yenye ushindani katika kutupatia watendaji serikalini. Hii ni sawasawa kabisa na kumwomba chui mwenye njaa kali akulindie sungura...........
Pamoja na kauli zake tata, Warioba amedai maoni yetu yamefanana kupindukia na ni kwa sababu tunayatoa maoni hayo kwa mashinikizo ya NGOs, vyama vya kisiasa na taasisi za kidini! (La ajabu, hakuzitaja!)
Kauli hizi zinatia mashaka makubwa katika maeneo yafuatayo kwa tume tajwa kututendea haki:-
1) Tuhuma za Warioba dhidi yetu hajazipa ushahidi wowote hata basi kuwataja kwa majina taasisi husika ikiashiria kuwa haheshimu utawala bora ambao unamsukuma ahakikishe ya kuwa tuhuma zinaandamana na ushahidi ili ziweze kupatiwa majibu fasaha........na watuhumiwa.
2) Ni dhahiri kwa vile tunaishi nchi moja na kukabiliana na changa moto zinazofanana ni wazi maoni ya majibu ya kero zetu pia yatashabihiana.......................sasa sijui kwanini Warioba atushangae kwa hilo?
3) Tusisahau wajumbe wote wanaounda tume ni matunda ya mfumo mbovu tulionao wa kiutawala hivyo tunapowaona wameanza kupembua uhalali wa maoni yetu hata kabla ya wao kuikamilisha kazi ya kuyakusanya maoni tajwa wasiwasi wetu ni kuwa huenda kwenye mikoba yao wana katiba wanayoitaka kuishinikiza tuipigie kura ya maoni na ushirikishwaji wetu ni "danganya toto" tu!
4) Kitendo cha tume kuhoji uhalali wa maoni yetu lakini bado wanaendelea kuyakusanya ili kuhalalisha malipo makubwa ya posho wanazojilipa inatuthibitishia ya kuwa lengo siyo kuutafuta ukweli bali kuupotosha ukweli kwa malipo lukuki kwenye vibindo vyao!
5) Wajumbe wote hawana wasifu wa kuupigania na kuutetea mfumo wa utawala bora na hata kuhatarisha mkate wao. Wengi wao wamebandikwa huko kwa sababu ya kuutetea udhalimu na hivyo si rahisi siye kuwaamini kama watatutendea haki na kuwakilisha kile ambacho tumewaambia na baadhi ya mifano ya taswira zao ni kama ifuatavyo:-
i) Bw. Warioba kupanda kwake kwenye chati ya uongozi hapa nchini kwa kiasi kikubwa alinufaika na kivuno cha "ukabila" wakati wa utawala wa Nyerere. Sidhani kama Raisi kama asingelikuwa anatoka Musoma angeliweza kuteua Mwanasheria Mkuu kwa kiwango cha duni cha uzoefu alichokuwa nacho Warioba wakati alipoteuliwa. Mwaka 1990, Mwinyi aliunda tume ya kumchunguza Warioba njia alizozitumia kuukwaa ubunge wa Bunda na tume ilithibitisha ya kuwa alitumia vibaya madaraka yake ya dhamana ya Uwaziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Uraisi na kushauri aenguliwe.
Aidha tume feki ya kuthibiti mianya ya ufisadi ambayo aliisimamia wakati wa Mkapa ilitutupia changa la machoni pale msisitizo wake ulipokuwa kuwakomoa baadhi ya watendaji serikalini badala ya kuona mfumo mzima wa kiutawala ulikuwa ni tatizo kubwa la uchocheaji wa ufisadi serikalini. Mapendekezo yake yalijaa visasi na akina Bw. Nalaila Kiula na wenzie baadaye walikuja kusafishwa na mahakama na hadi leo Warioba au serikali haijawahi kuwaomba msamaha waathirika hawa au hata kuwafidia!
Pengine baya kuliko yote Warioba amehusishwa moja kwa moja na ufisadi wa EPA na hadi leo hajarudisha hata sumuni au hata kufikishwa kwenye vyombo vya dola kuchunguzwa kama kweli njia alizozitumia kujichotea mabilioni BOT zilizingatia sheria zilizopo.
Katika wasifu wa Warioba kama ulivyo wasifu wa wajumbe karibuni wote wa tume ni kuwa nafasi zote walizowahi kuzishika za kiutendaji serikalini hawajawahi kuziomba au hata kushindana na mtu yoyote na hivyo kuwatarajia wapendekeze nafasi zote serikalini kupatikana kwenye mazingira ya uwazi na ushindani kuwa ni njozi za ajuza.
ii) Makamu wao wa tume, Jaji Mkuu mstaafu - Augustine Ramadhani- alijivika joho la kuishinikiza mahakama ya Rufaa ambayo alikuwa akiisimamia kuzuia mgombea binafsi akidai siyo kazi ya mahakama kuliingilia bunge wakati katiba kama ilivyo sheria nyingine mahakama ndicho chombo pekee iliyopewa mamlaka ya kuzitafsiri sheria zote zikiwemo za kikatiba kuona kama zinalinda utawala bora. Jaji Ramadhani kwa kasi ya mithili ya mwewe, aliteua tume ya majaji wenzie saba badala kuanzia majaji watatu ili kuzika haki yetu hiyo ya kimsingi kabisa. Hivi leo jaji Ramadhani kweli atakuwa kabadilika na huku yeye mwenyewe alikiri kuwa ule uamuzi aliutoa kwa mashinikizo ya kisiasa? Ni vigumu kwetu kumkubali kuwa anaweza kututendea haki pale ambapo Ikulu ileile ya JK iliyomteua kuwa jaji Mkuu kwenye mazingira yasiyoeleweka na aliiogopa kwenye suala la mgombea binafsi leo ageuka kuwa ngangari! Labda atueleze ile khofu aliyokuwa nayo kama jaji Mkuu sasa imezimwa na na nini...........................???????
iii) Dr. Senkondo Mvungi ni kinara wa kuzuia utawala bora ndani ya NCCR Mageuzi na mfano ni pale aliposhangilia kufukuzwa uanachama kwa mbunge wao wa Kigoma kwa kosa la kuwania kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama chao. Hivi kama kugombea nafasi ambayo ni haki ya kikatiba ni nongwa je inapokuja masuala ambayo watawala hawayataki kwa sababu yanahatarisha mkate wao huyu ni mwakilishi wa kutumainiwa au ni sehemu ya uwakilishi haramu?
iv) Uwakilishi wa cdm pia una sura kama hiyo ambapo madiwani wanatimuliwa na hivyo kudhoofisha maana halisi ya "people's power" ambayo wamekuwa wakituzuga nayo.................................kama walaji wawili, watatu kule Dar-CDM ambao hawakushiriki kwenye chaguzi za kuchagua madiwani wana nguvu ya kufutilia mbali "people's power" ya wapigakura kweli unawategema watusaidie katiba ambayo italinda misingi ya utu ndani ya katiba tarajiwa kama siyo ubabaishaji mtupu?
v) Wajumbe wote wa tume hawana wasifu wa kutetea utawala bora zaidi ya kutetea mkate wao unapokuwa hatarani kuangukiwa na vumbi tu............
6) Kwa vile wajumbe wa tume hawajajitokeza hadharani na kumpinga Warioba na kauli zake za kubeza demokrasia na ambazo zimo nje ya hadidu za rejea alizopewa ni sahihi kwetu kuchukulia tume nzima iliukubali msimamo tajwa na hivyo haina uhalali tena wa kuendelea na ukusanyaji wa maoni tajwa bali kufungasha virago na kurudia kazi zao zenye kipato cha mwendo wa kinyonga..............
7) Tume wakati ikijitungia hadidu ya rejea ya kutupasha madhaifu yetu kazi ambayo siyo yao, wamesahahu kujipanga na kuja na mkakati wa jinsi gani sheria mpya ziundwe kabla ya uchaguzi wa 2015 ambazo bila ya sheria hizo katiba mpya hata iwe imeboreshwa vipi kamwe hatutaweza kuitekeleza. Wao wamejipanga kumaliza zoezi hili mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu wakati sheria nyingi za kuuongoza uchaguzi huo zinadai miaka angalau 3 kama uzoefu wa majirani zetu wa kenya unatoa busara zozote hapa..................
8) Kutojenga njia pana na kuwagharimia taasisi huria katika kuhakiki jinsi tume inavyofanya kazi ni dhahiri tume utendaji wake haiwajibiki kwa yeyote yule jambo ambalo linatia dosari zoezi zima. Tulipaswa tuwe na vyombo vingi huria ambavyo navyo vitahakiki utendaji wa kazi wa tume badala ya sisi kusubiria ghiliba za tambo za Warioba kama sehemu ya hakiki tajwa........................
9) Sheria inayoanzisha tume tajwa haijaipa tume mamlaka ya kuyawakilisha maoni ya wananchi kwa bunge badala yake wanayapeleka kwa Raisi ambaye ana kila shauku ya kuchakachua maoni tajwa. Kumbuka JK ni sehemu ya serikali ya Mkapa ambayo ilikuja na "white paper" ambayo ni misimamo ya serikali ya katiba ya watawala na waliipitisha kwa mabavu nyakati hizo. Hivi leo unapoona JK anapokataa kulimilikisha bunge zoezi hilo na kulichakachua kwa kulichanganya na la wakilishi visiwani wakati kuna Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na marekebisho haya yanafanyika nje ya katiba yetu...........................sasa tutarajie nini?..........mimi naendelea kushangaa tunaruhusu watu wale pesa zetu kwa utapeli wa kutuandikia katiba mpya kwa mfumo wa utaratibu ambao hautambuliki ndani ya katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania ila sheria inatumika kutengua mantiki zote zilizomo ndani ya katiba!!!!!!!!!!........Uandikaji wa katiba mpya lazima unahitaji marekebisho ya kikatiba ili zoezi hilo liweze kuwa na meno ya kisheriana wala siyo vinginevyo.
10) Uteuzi wa tume haukuwa wazi, shirikishi na wenye ushindani lakini bado tunaitegemea tume ije na mapendekezo ambayo ni shirikishi, wazi na yenye ushindani katika kutupatia watendaji serikalini. Hii ni sawasawa kabisa na kumwomba chui mwenye njaa kali akulindie sungura...........