Sababu 10 tu kwanini Magufuli ana nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi 2015

Apr 27, 2006
26,588
10,364

Sababu 10 kwa nini John Magufuli atashinda uchaguzi Mkuu wa Urais 2015


1. Tanzania bara na visiwani yako majimbo ya uchaguzi 266, CCM imesimamisha wagombea Ubunge katika majimbo yote 266 huku Chadema na washirika wake wa Ukawa wakiwa wamesimamisha wagombea katika majimbo 211 (138 toka Chadema). Kati ya majimbo hayo 266, CCM tayari imepita bila kupingwa jimbo 1. Ukichukua majimbo 260 yaliyobaki na kutoa 211 ambayo Chadema na washirika wake wamesimamisha wagombea unabaki na majimbo 48 ambayo CCM haina upinzani wa Chadema wala washirika wake wa Ukawa. Majimbo haya 48 CCM ina uhakika wa kushinda walau kwa asilimia 90, ushindi huu si kwa Wabunge tu bali pia kwa mgombea Urais wa CCM.

2. Watanzania waliojiandikisha kupiga kura mwaka 2015 ni milioni 24.2. Takwimu zinaonyesha CCM ina wanachama hai wapatao milioni 8 wenye kadi na wanaolipia ada zao za uanachama kila mwaka. Kuondoka kwa Edward Lowassa katika Chama Cha Mapinduzi kunamaanisha Magufuli hatapata kura zote milioni 8 za wana CCM na pia kihesabu si rahisi wana CCM wote milioni 8 kujitokeza siku ya kupiga kura.Utafiti unaonyesha kwamba wana CCM watakaopiga kura hawatazidi asilimia 90 ya wanachama wake (milioni 7.2) huku milioni 7 kati yao wakimpigia kura John Magufuli. Historia ya CCM inaonyesha ni wanachama wachache sana humpigia kura kada mwenzao anapohama kugombea nafasi kwa chama kingine, hasa nafasi ya Urais (Rejea: Uchaguzi wa Urais 1995, mgawanyo wa kura za Augustine Lyatonga Mrema)

3. Mizunguko ya kampeni huzaa kura za ziada mbali na zile za wanachama. Tayari inaonyesha kwamba Magufuli anapita karibu kila kata ya Tanzania akitumia barabara huku upande wa Lowassa na shirikisho la Ukawa hali ikiwa tofauti, ambako amekuwa akifika sehemu chache akitumia usafiri wa ndege na helkopta na ni wazi hana stamina ya kuzunguka kwa gari nchi nzima kutokana na tatizo la kiafya. CCM ina mizizi kwenye mashina kuanzia ngazi ya nyumba kumi. Mtandao huu wa Chama pamoja na safari za mgombea wao kila kata ni kiashiria kwamba atafikia wapiga kura wengi zaidi hasa sehemu za vijijini na ambazo si rahisi kufikika. Tafiti zinaonyesha huko ndiko kwenye wapiga kura wengi na kuwafikia ni hatua moja kuelekea kuzipata kura zao na kushinda.

4. Chaguzi za Serikali za Mitaa mwaka 2014 zinaonyesha kwamba CCM ilishinda kwa zaidi ya asilimia 80 kwenye nafasi za uongozi za serikali za vijiji na mitaa. Ikumbukwe kwamba CCM ilipata ushindi huu licha ya ushindani mkubwa uliokolezwa na sakata la Escrow wakati huo. Hii inaonyesha kwamba CCM iliweza kushinda hata wakati huo wa changamoto. Ni mwaka mmoja tu umepita tangu chaguzi hizo zifanyike. Kitafiti, hiki ni kiashiria kikubwa kwamba katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, CCM kama chama kinaenda kwenye sanduku la wapiga kura kikiwa na rekodi nzuri kuweza kushinda.

5. Rekodi ya Utendaji ya Magufuli inavutia Watanzania wengi. Utafiti unaonyesha kwamba wapinzani wake majukwaani mpaka sasa wanapata wakati mgumu kutaja jina lake moja kwa moja kumuhusisha na utendaji wa hovyo. Mitandaoni zipo video na nukuu nyingi zikiwemo za Mgombea wa Ukawa Edward Lowassa, Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na wengineo wakisifia utendaji wa Magufuli. Katika siasa na kampeni, hatua moja kuonyesha mgombea anashinda ni kushindwa kwa wapinzani wake kumnyooshea kidole moja kwa moja au kukosa mabaya ya kusema dhidi yake. Asiye na la kukusema vibaya anawapa wananchi nafasi ya kuona mazuri yako na kushinda.

6. Suala la afya ya wagombea limekuwa gumzo kubwa katika uchaguzi wa mwaka huu. Huku ikiwa wazi kwamba Mgombea wa Ukawa Edward Lowassa anaugua ugonjwa wa Parkinson's kwa muda mrefu sasa, Magufuli hajawa na changamoto ya afya. Ugonjwa wa Parkinson's alio nao Edward Lowassa unaathiri ubongo wa kati, moyo, mishipa ya fahamu na uwezo wa kufikiri (Afya ya mwili maeneo hayo ni muhimu kiongozi kuwa nayo). Kwa muda mrefu Lowassa amekuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa huu katika hospitali maarufu ya Franziskus-Krankenhus mtaa wa Budapester jijini Berlin, Ujerumani. Kiumri Magufuli ana miaka 55 huku Lowassa akiwa na miaka 63. Wapiga kura huchagua kiongozi kwa kutazama muonekano na ni wazi kabisa kwamba kwa muonekano na hali ya kiafya ya Lowassa ni dhoofu na inazidi kudorora siku hadi siku na kuwakatisha tamaa hata wanaomuunga mkono. Tangu kampeni zianze hakuna mahala ambapo amewahi kuzungumza kwa zaidi ya dakika 15. Hivyo basi, kwa kadiri siku zinavyoenda Watanzania watazidi kubaini kwamba Lowassa hana afya ya kuhimili vishindo vya kampeni wala uwezo wa kumudu majukumu ya Urais.

7. Nguvu ya vyama, oganaizesheni na ilani. Magufuli anatokea CCM ambayo kama nilivyoeleza juu ina nguvu ya kuwepo kila kijiji na kila nyumba kumi Tanzania; imetoa marais waliotangulia, na hata wapinzani wametoka katika CCM hiyo hiyo baada ya kukosa nafasi za kugombea kupitia chama hicho. Kwa miaka mitatu iliyopita Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amezunguka kila kona ya nchi akikinadi chama chake, hii ni aina ya kampeni ambayo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa. Kwa upande wa upinzani hali iko tofauti. Mgombea wao, Lowassa alikuwa mwanachama wa CCM miezi miwili iliyopita, kuingia kwake Chadema kumeleta mpasuko huku Katibu Mkuu wake akitokomea kusikojulikana, na Mwenyekiti wa CUF, Lipumba naye akijiuzulu uongozi kupinga Lowassa kukaribishwa Ukawa. Hii inaonyesha hali si shwari katika upinzani. Kwa sasa Ukawa wanaficha mpasuko huo kwa propaganda lakini madhara yatajitokeza kabla ya siku ya uchaguzi. Moja ya viashiria vya mpasuko katika Ukawa ni kuvunjika kwa makubaliano ya kuweka mgombea mmoja wa Ubunge katika kila jimbo. Zaidi ya asilimia 70 ya majimbo yana wagombea Ubunge toka vyama vyote vinavyounda Ukawa. Kwa mfano Lowassa, kama mgombea Urais wa Ukawa, akienda Ubungo ambapo kuna wagombea toka Chadema, CUF na NCCR atamnadi mgombea yupi?

8.Kuondoka kwa Dr Slaa Chadema, tuhuma za Mbowe kuiuza Chadema kwa Lowassa kwa TZS bilioni 10 (ambazo Dr Slaa amezithibitisha) na ukawa kuhama kutoka kumuita Edward Lowassa fisadi mkuu wa nchi miaka michache iliyopita hadi sasa kumfanya kuwa mgombea wao. Hii imewakanganya Watanzania wengi na wote wanaochukua muda kulitafakari wanazidi kupata maswali zaidi. Uamuzi wa mpigakura katika hali kama hii ni kuendelea kulipigia kura zimwi alijualo (CCM) kuliko zimwi jipya asiloelewa (Ukawa).

9. Matumizi makubwa ya fedha katika kutafuta madaraka. Mpaka mwisho wa mwezi Agosti 2015 Lowassa alikuwa tayari ametumia zaidi ya TZS bilioni 106 kwa kipindi cha miaka miwili na nusu kwanza kutafuta nafasi kugombea ndani ya CCM na kisha kuhamia Ukawa. Wananchi wengi wanahoji zinapotoka fedha hizi, wengi wakikumbuka kauli ya Mwalimu Nyerere kwamba "Mtanzania wa leo hawezi kukununua kabla ya yeye kwanza kununuliwa". Wananchi wanahoji namna gani Lowassa anapanga kurejesha fedha hizi iwe zake (pia wanahoji kazipataje) au za marafiki zake (lengo lao kumpa fedha ni nini). Magufuli hana kashfa ya namna hii na hata kampeni zake za kuomba kuteuliwa ndani ya CCM hazikuwa za matumizi ya fedha kabisa. Kama wananchi watapiga kura kwa kuangalia uadilifu katika kupata na kutumia fedha, na pia kama watapiga kura wakiamini kwamba Ikulu si mahali pa kufanya biashara ili mtu arejeshe fedha alizotumia wakati wa kampeni na kuhonga kupata nafasi basi Magufuli ana nafasi kubwa ya kushinda.

10. Mzimu wa Mwalimu Nyerere: Mwaka 1995 Mwalimu Nyerere alisema wazi kwamba Lowassa hafai kuwa Rais wa Tanzania, alikatwa jina lake kwa haki (video ya Mwalimu akisema haya iko mitandaoni na ni moja ya video zinazotazamwa kwa wingi wakati huu wa uchaguzi mkuu) na hakuna maana kuendelea kumjadili na kwamba chama kisonge mbele. Watu wanaomjua vizuri Lowassa na shughuli anazozifanya wanasema kwa miaka 20 Lowassa hajabadili zile sifa zilizomfanya Mwalimu kutamka maneno yale mwaka 1995. Hata alipoomba familia ya Mwalimu Nyerere kumuunga mkono alipoondoka CCM alijibiwa wazi kwamba yeye hajawahi kuwa chaguo la Mwalimu. Watanzania bado wanamuheshimu na kumuamini Mwalimu Nyerere na ni wazi watachagua kiongozi wakifuata wosia wake. Uadilifu wa Magufuli utamuwezesha kuaminiwa na Watanzania na kushinda nafasi hii.





 
Maccm mnaangaika sana, lowasa na ukawa wanatakiwa kulinda kura kwa nguvu tu. Nchi inaondoka asubuhi mapema tarehe 25. Hizi nyingine ni propaganda za kujipa moyo tu.
 
Hapa Rorya kisima ambacho nikiwa mdogo miaka 42 iliopita mama yangu alikuwa anachota maji ndipo anapochota maji mpaka leo!nimekuwa mzee sasa!...haya ni maajabu.NITAPIGIA KURA MABADILIKO.
 
Magufuli kama sifa anazo kibaooo niongezeaaaa mwadilifuuu....,, mchapakaziii,,, kipenzi cha wengiii...,,, hana kashfa yeyote mbaya ya ufisadiiii...,,, afu jaman twende mbele turudi nyuma ni mfuatiliaji wa mambo mengi sana yanayohusu serikal kwenye suala la utendaji wa kazi kwa wafanyakazi haswa kwenye sekta ya ujenzi,,.. pia ni mtekelezaji akisema amesemaaa
 
Hivi huyu Lemutaz bado anatafuta U-DC hadi leo?nilidhani alishateuliwa kitambo
pole mzee wa selfie,kama wale wa juzi haukuwepo basi tena hiyo itabakia historia
 
Haiwezekani angelina jolie apewe contract ya kutangaza the celebrity apprentice wakati tayari Schwarzenegger ashapewa.hii si haki kabisa.
 
Magufuli kama sifa anazo kibaooo niongezeaaaa mwadilifuuu....,, mchapakaziii,,, kipenzi cha wengiii...,,, hana kashfa yeyote mbaya ya ufisadiiii...,,, afu jaman twende mbele turudi nyuma ni mfuatiliaji wa mambo mengi sana yanayohusu serikal kwenye suala la utendaji wa kazi kwa wafanyakazi haswa kwenye sekta ya ujenzi,,.. pia ni mtekelezaji akisema amesemaaa

Kabisa,tatizo ni mfumo,hata mkwere alikuja na mziki huo huo,kasi zaidi,nguvu zaidi na sijui nini ndo hapo tumeishia badala ya uchumi kukua unarudi nyuma hamna jipya tunamtaka LOWASA full stop
 
Kabisa,tatizo ni mfumo,hata mkwere alikuja na mziki huo huo,kasi zaidi,nguvu zaidi na sijui nini ndo hapo tumeishia badala ya uchumi kukua unarudi nyuma hamna jipya tunamtaka LOWASA full stop

- Tunamtaka wewe na nani mkuu? hahahahah

le Mutuz
 
haiwezekani genge la ukawa likapewa kuongoza nchi kwa kuwa hawajajipanga,hawa ni watu waliokusanyana tu kwa mslahi yao binafsi,hawatufai hata kidogo,wachumia tumbo hawa,lengo lao ni kujinufaisha wao na familia zao,ndio maana huu ukawa umekuja tu kama uyoga, tulio wengi hatuwezi kukubali kudanganywa kama watoto kwa kupewa peremende na maneno matamu ya udanganyifu yanayotoka kwa ukawa.hapa kazi tu,Magufuli ataosha
 
Hivi huyu Lemutaz bado anatafuta U-DC hadi leo?nilidhani alishateuliwa kitambo
pole mzee wa selfie,kama wale wa juzi haukuwepo basi tena hiyo itabakia historia

- hahahahahaha I am business man so relax karibu ofisini kwangu hapa Tancot House 2nd fl anytime kama una deal U know hahahahaha ninajiajiri siajiriwi okeee!!

le Mutuz
 
haiwezekani genge la ukawa likapewa kuongoza nchi kwa kuwa hawajajipanga,hawa ni watu waliokusanyana tu kwa mslahi yao binafsi,hawatufai hata kidogo,wachumia tumbo hawa,lengo lao ni kujinufaisha wao na familia zao,ndio maana huu ukawa umekuja tu kama uyoga, tulio wengi hatuwezi kukubali kudanganywa kama watoto kwa kupewa peremende na maneno matamu ya udanganyifu yanayotoka kwa ukawa.hapa kazi tu,Magufuli ataosha

Ww ndio hautampa kura Lowassa na UKAWA, ula wenzako wote watampa kura. Subir bado siku 17 ndio utaelewa zaidi. Endelea kujipa matumaini kama mgonjwa anaesubili kufa
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom