USSR
JF-Expert Member
- Jul 15, 2015
- 9,884
- 22,601
Wanajukwaa bunge la 11 linakwenda kumaliza muda wake ,kiongozi shupavu wa bunge hili ameonesha ubora wake wa hali ya juu hii inamaana Tanzania inamuhitaji kuliko yeye anavyoihitaji Tanzania hapa naweka madokezo kumi kwa nini anafaa kurejea tena kama kiongozi wa muhimili huu muhimu wa taifa letu :
1.Kusimamia Serikali katika miradi ya kimkakati .Job amekuwa makini na bunge lake kuhakikisha serkali ya awamu hii inafanikisha miradi kwa kutoa haki kwa wabunge wote kujadili pasina kungalia chama ,bunge limepitisha pesa za miradi na kamati za kibunge kufanya kazi ya kupitia kila uchao kuhakikisha ile dhana ya kuisimamia serkali,ukiona hii miradi jua speka wetu alikuwa kuwa nyuma yake.
2. Kutoruhusu Bunge kudhalilishwa
Kila aliyethubutu kulidhalilisha bunge letu tukufu amekipata cha mtemakuni kuanzia Makonda,Asadi na wabunge wa upinzania kulidhalilisha bunge amehakikisha chombo hiki cha wananchi hakidhalilishwi maana kukidharau ni kuwadharau wananchi walikiweka pale.
3.Kushirikiana na Serikali na Mahakama.
Hapa ameonesha kuwa ili bunge liisimamie serkali ni lazima lifanye kazi kwa ukaribu,urafiki na uwazi na sio uadui ,amewafunza watanzania kuwa kuisimamia serkali sio kuishambulia na kuidharau bali kuwa nayo karibu katika kutatua kero za wananchi huu ndio udugu wa watanzania
4. Kusimamia haki za wabunge bila kujali vyama vyao.
Mh spika ameonesha upekee ndio mara ya kwanza kuwatetea wabunge hadharani pale walipopitia mateso kutoka vyama vyao wabunge kama lijualikali,silinde,mwambe na lwakatale hawa ni mifano ya wazi kuwa spika alionesha kuwa na busara kwa kuwa wananchi wangekosa wawakilisha kwa kuonewa wabunge wako ,
Hakuna aliyetegemea kumuona spika akienda hospital kumtembelea KUB pamoja na matamshi ya dharau,dhihaka ya wabunge wa upinzania dhidi ya afya yake akiwemo mwenyewe K.U.B
5. Kilichangamsha bunge ukisikiliza jinsi anavyoendesha vikao vya bunge kwa uchangamfu analifanya hata kama umeboreka upende kulitazama matani ya hapa na pale na kuwafanya wabunge wajisikie huru kuzungumza
6. Kuwatumikia wananchi wa Kongwa .
Hapa job mtoto wa Yustino ameonesha kufanya kazi bora jimboni maana kwa miaka ya hivi karibuni kongwa inapaa sambamba na dodoma yake wananchi wa kongwa walilamba dume haswahaswa kwa huyu spika
7. Mabadiriko ya mfumo wa Bunge.
Bunge letu sasa linaenda sambamba na mabunge ya duania ya kwanza bunge limekuwa kidijitali sasa sio mambo ya makaratasi wabunge wanapata information hata wakiwa nje ya nchi na pia wanaweza kushiriki mijadala kama kawaida
8. Gawio la Serikali
Haijawahi kutokea kwa sasa pesa zinazobakia katika hurejeshwa serkalini ilizipangiwe matumizi mengine sio kuliwa kama zamani hii imeonesha kuwa bunge liko imara na spika anajielewa
9. Kuondoa matumizi mabaya ya pesa za wananchi.
Kama mbunge hayupo bungeni na amekula posho nairejesha na hakuna janjajanja ya kulipa pesa za matibabu kama mbunge hakufuata taratibu za kimatibabu za kibunge ,hii imemjengea heshima ndio maana Tanzania imekuwa mfano kwa mabunge ya commonwealth,SADC na EAC kwa kupewa heshima na hata bunge letu kila mwaka tangu2015-2020 linakula hati safi
10. Kuanzisha shule ya kimkakati ya wasichana (Bunge girls special school) yenye mchepuoa wa masomo ya sayansi ,hapa kweli aliona mbali sana na kuonesha kuwa vision yake inaweza kuleta matokeoa chanya siku zijazo,watoto wa maskini wanasoma katika shule ya kisasa kabisa
USSR
1.Kusimamia Serikali katika miradi ya kimkakati .Job amekuwa makini na bunge lake kuhakikisha serkali ya awamu hii inafanikisha miradi kwa kutoa haki kwa wabunge wote kujadili pasina kungalia chama ,bunge limepitisha pesa za miradi na kamati za kibunge kufanya kazi ya kupitia kila uchao kuhakikisha ile dhana ya kuisimamia serkali,ukiona hii miradi jua speka wetu alikuwa kuwa nyuma yake.
2. Kutoruhusu Bunge kudhalilishwa
Kila aliyethubutu kulidhalilisha bunge letu tukufu amekipata cha mtemakuni kuanzia Makonda,Asadi na wabunge wa upinzania kulidhalilisha bunge amehakikisha chombo hiki cha wananchi hakidhalilishwi maana kukidharau ni kuwadharau wananchi walikiweka pale.
3.Kushirikiana na Serikali na Mahakama.
Hapa ameonesha kuwa ili bunge liisimamie serkali ni lazima lifanye kazi kwa ukaribu,urafiki na uwazi na sio uadui ,amewafunza watanzania kuwa kuisimamia serkali sio kuishambulia na kuidharau bali kuwa nayo karibu katika kutatua kero za wananchi huu ndio udugu wa watanzania
4. Kusimamia haki za wabunge bila kujali vyama vyao.
Mh spika ameonesha upekee ndio mara ya kwanza kuwatetea wabunge hadharani pale walipopitia mateso kutoka vyama vyao wabunge kama lijualikali,silinde,mwambe na lwakatale hawa ni mifano ya wazi kuwa spika alionesha kuwa na busara kwa kuwa wananchi wangekosa wawakilisha kwa kuonewa wabunge wako ,
Hakuna aliyetegemea kumuona spika akienda hospital kumtembelea KUB pamoja na matamshi ya dharau,dhihaka ya wabunge wa upinzania dhidi ya afya yake akiwemo mwenyewe K.U.B
5. Kilichangamsha bunge ukisikiliza jinsi anavyoendesha vikao vya bunge kwa uchangamfu analifanya hata kama umeboreka upende kulitazama matani ya hapa na pale na kuwafanya wabunge wajisikie huru kuzungumza
6. Kuwatumikia wananchi wa Kongwa .
Hapa job mtoto wa Yustino ameonesha kufanya kazi bora jimboni maana kwa miaka ya hivi karibuni kongwa inapaa sambamba na dodoma yake wananchi wa kongwa walilamba dume haswahaswa kwa huyu spika
7. Mabadiriko ya mfumo wa Bunge.
Bunge letu sasa linaenda sambamba na mabunge ya duania ya kwanza bunge limekuwa kidijitali sasa sio mambo ya makaratasi wabunge wanapata information hata wakiwa nje ya nchi na pia wanaweza kushiriki mijadala kama kawaida
8. Gawio la Serikali
Haijawahi kutokea kwa sasa pesa zinazobakia katika hurejeshwa serkalini ilizipangiwe matumizi mengine sio kuliwa kama zamani hii imeonesha kuwa bunge liko imara na spika anajielewa
9. Kuondoa matumizi mabaya ya pesa za wananchi.
Kama mbunge hayupo bungeni na amekula posho nairejesha na hakuna janjajanja ya kulipa pesa za matibabu kama mbunge hakufuata taratibu za kimatibabu za kibunge ,hii imemjengea heshima ndio maana Tanzania imekuwa mfano kwa mabunge ya commonwealth,SADC na EAC kwa kupewa heshima na hata bunge letu kila mwaka tangu2015-2020 linakula hati safi
10. Kuanzisha shule ya kimkakati ya wasichana (Bunge girls special school) yenye mchepuoa wa masomo ya sayansi ,hapa kweli aliona mbali sana na kuonesha kuwa vision yake inaweza kuleta matokeoa chanya siku zijazo,watoto wa maskini wanasoma katika shule ya kisasa kabisa
USSR