RwandaAir yasitisha kwa muda safari zake Uganda

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,005
9,872
00520408 441f6eba7875f63f2333432e333b881b arc614x376 w1200.png

RwandaAirCopyright: RwandaAir

Shirika la ndege la Rwanda, RwandAir imetangaza kuwa imesitisha kwa muda safari zake za ndege za kwenda na kutoka kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa Uganda wa Entebbe mara moja.

“Kutokana na kuongezeka kwa visa vya Covid-19 nchini Uganda, RwandAir inatangaza kusitishwa kwa safari zake za ndege za kuelekea na kutoka Entebbe kuanzia tarehe 10 Juni 2021, hadi tangazo lingine litakapotolewa,” Taarifa ya shirika hilo la ndege ya Rwanda lilisema.

Liliongeza kuwa : “RwandAir inaomba radhi kwa usumbufu uliosababishwa na hatua hiyo.”

Shirika hilo lilisema kuwa wateja waliothiriwa ‘’wanaweza kupanga upya safari na kusafiri baadaye, pale safari hizo zitakaporejeshwa tena–au waombe kurejeshewa pesa zao za nauli.”

Uganda imeshuhudia ongezeko la idadi ya watu walioambukizwa virusi vya corona, jambo lililowalazimisha maafisa kuweka sheria inayowataka watu kupunguza shughuli na matembezi yasiyo ya lazima kwa muda wawiki sita.

Chanzo: BBC Swahili

1623398465651.gif
 
... hivi Kigali - Entebe si "mwendo punda" jirani kabisa!
 
Magufuli nae sijui anasubiri nini kufanya kama Rwanda yani bado anaamini maombi tu badala ya sayansi.

Yani anaongoza nchi kishamba sana.
 
Utakuwa na Mtindio wa Ubongo wewe,wala sio bure.
Mwambie Magufuli atumie sayansi sasa corona ipo sasa kwanini bado anafikiri Tz ni kama kisiwa? hadi sasa bado Tz hatueleweki msimamo wetu kwenye corona bado tumegoma kupima watu corona.
 
Mwambie Magufuli atumie sayansi sasa corona ipo sasa kwanini bado anafikiri Tz ni kama kisiwa? hadi sasa bado Tz hatueleweki msimamo wetu kwenye corona bado tumegoma kupima watu corona.
Lala na barakoa
 
Back
Top Bottom