Rwanda inaendelea kwa kufuta taratibu sisi tunaendelea kwa vululu vululu

Kamgomoli

JF-Expert Member
May 3, 2018
1,865
3,801
1. Unaishi kwenye nyumba nzuri lakini pembeni yako kuna choo kinatililisha kinyesi,harufu mbaya kila kona

2. Nyumba nzuri zinajengwa hovyo hovyo kwenye skwata msimu wa mvua zinageuka madampo ya maji taka.

3. Nyumba zinajengwa juu milimani , siasa chafu na za kishamba ole wake atakaewafukuza wapiga kura wangu.

4. Barabara nzuri zinajengwa zikimalizika tu machinga wanazigeuza masoko. Ole wake atakaewagusa wapiga kura wangu.

5. Wafugaji na wakulima wanavamia vyanzo vya na hifadhi tengefu. Ole wake atakaewasumbua wapiga kura wangu.Km unaona kilimo rahisi kalime na ww!

5. Unajenga barabara za mwendo kasi wakati mabasi yapo hoi bin taabani,watu wanajazana kama magunia ya korosho. WatanzaniaTuko vizuri tembeeni kifua mbele!

Rwanda wanajenga nchi yao huku wakizingatia taratibu na sheria za kisekta na nchi kwa ujumla. Usafi unazingatiwa, ujenzi holela haupo, bodaboda hawaingii katikati ya mji.

Ndio maana hata wakijenga chochote kile kinaonekana kinang'aa. Sisi hata mji ujengwe vipi hauwezi kupendeza kamwe kwa sababu tumeamua taifa lote kuwa gulio.

Hata Dodoma ni suala muda tu, na wenyewe utakuwa kama Kariakoo tu. Watalii (Wazungu) ni watu wa utaratibu. Mtu hawezi kuvutiwa kutembelea taifa ambalo kila kitu kinaendeshwa hovyo hovyo.

Uchafu kila kona. Ndio maana Rwanda wanaingiza zaidi ya dola Mil.4 kwa mwaka wakati sisi hata hesabu haieleweki. Sijui alivyoenda Rwanda alienda kujifunza nini?

Nadhani kama Taifa tunahitaji Rais mjanja anaejua nini maana ya maendeleo. Mwenye plan zinazoeleweka na za muda mrefu sio mkurupukaji.

La sivyo tutaendelea kutia aibu tu.
 
Kuna Rwanda na kuna Kigali, hivi ni vitu viwili tofauti. Kigali pazuri lakini huku Rwanda pa ovyo.
 
  • Thanks
Reactions: rr3
Tatizo la Tanzania ni wanasiasa. Ilitakiwa iwe marufuku Machinga kuwepo barabarani
Pikipiki isifike Magomeni
 
Mleta mada unaongelea Rwanda au Kigali? Maelezo yako yanaihusu Kigali.
 
YEHODAYA,

Atakuwa anaongelea kigali ila si kweli kuwa bodaboda hawaruhusiwi mjini, wanaruhusiwa, ila tofauti na hapa kwetu, wanasimamia sheria, bodaboda hawezi kuondoka mpaka uvae kofia na kubeba mshikaki ni mwiko.

Pia, TANROAD/TARURA wanachakujifunza kutoka NPD ya Rwanda kwenye ujenzi wa barabara ambapo, kingo za barabara zinatengezwa kwa pavement blocks na kuwekewa mitaro, wanahakikisha udongo pembeni mwa barabara ya lami umethibitiwa kwa landscaping na kuwekewa vitofali na kupandwa maua, ili kuzuia mchanga na udongo kuingia kwenye lami.

Huku kwetu barabara zinajengwa kwa lami, pembeni kuna udongo/mchanga, mvua ikinyesha, udongo wote unatiririka barabarani, lami inakuwa nusu udongo nusu lami.

Landscaping na uthibiti wa udongo pembezoni mwa barabara ungepunguza hata gharama za usafi wa barabara.

Kuna kipande cha barabara Goba Mbezi Mwisho, mvua ikinyesha udongo unaingia barabarani, mitaro iliyojengwa imezibwa na udongo ulioporomoka kutoka pembezoni mwa barabara.
 
1. Unaishi kwenye nyumba nzuri lakini pembeni yako kuna choo kinatililisha kinyesi,harufu mbaya kila kona

2. Nyumba nzuri zinajengwa hovyo hovyo kwenye skwata msimu wa mvua zinageuka madampo ya maji taka.

3. Nyumba zinajengwa juu milimani , siasa chafu na za kishamba ole wake atakaewafukuza wapiga kura wangu.

4. Barabara nzuri zinajengwa zikimalizika tu machinga wanazigeuza masoko. Ole wake atakaewagusa wapiga kura wangu.

5. Wafugaji na wakulima wanavamia vyanzo vya na hifadhi tengefu. Ole wake atakaewasumbua wapiga kura wangu.Km unaona kilimo rahisi kalime na ww!

5. Unajenga barabara za mwendo kasi wakati mabasi yapo hoi bin taabani,watu wanajazana kama magunia ya korosho. WatanzaniaTuko vizuri tembeeni kifua mbele!

Rwanda wanajenga nchi yao huku wakizingatia taratibu na sheria za kisekta na nchi kwa ujumla. Usafi unazingatiwa, ujenzi holela haupo, bodaboda hawaingii katikati ya mji.

Ndio maana hata wakijenga chochote kile kinaonekana kinang'aa. Sisi hata mji ujengwe vipi hauwezi kupendeza kamwe kwa sababu tumeamua taifa lote kuwa gulio.

Hata Dodoma ni suala muda tu, na wenyewe utakuwa kama Kariakoo tu. Watalii (Wazungu) ni watu wa utaratibu. Mtu hawezi kuvutiwa kutembelea taifa ambalo kila kitu kinaendeshwa hovyo hovyo.

Uchafu kila kona. Ndio maana Rwanda wanaingiza zaidi ya dola Mil.4 kwa mwaka wakati sisi hata hesabu haieleweki. Sijui alivyoenda Rwanda alienda kujifunza nini?

Nadhani kama Taifa tunahitaji Rais mjanja anaejua nini maana ya maendeleo. Mwenye plan zinazoeleweka na za muda mrefu sio mkurupukaji.

La sivyo tutaendelea kutia aibu tu.
Well said, nchi imejaa political stunt ,hakunajipya
 
Ukiacha Usafi wa Kigali, Rwanda huwa inajimwambafai kwenye vyombo vya habari vya kimataifa zaidi ya uhalisia. Ukienda kwenye ground utakuta vitu vichache vimefanyika Kigali. Hata hizo VW sijui wataziuza wapi.
 
Ukiacha Usafi wa Kigali, Rwanda huwa inajimwambafai kwenye vyombo vya habari vya kimataifa zaidi ya uhalisia. Ukienda kwenye ground utakuta vitu vichache vimefanyika Kigali. Hata hizo VW sijui wataziuza wapi.
VW wametoa Clarification kuwa Rwanda hakuna kiwanda bali kuna Car Renting Company ya magari yao hivyo tusichanganye maneno.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom