Rwanda imeweza kutangaza Utalii kupitia klabu ya Arsenal, Tanzania ilijaribu lakini fedha zikapigwa huko London

Yaani watu wataangalia neno "visit Rwanda" na suddenly wawe interested kwenda Rwanda kwa Kagame!!? Kuna "kivutio" kipi kwenye maneno hayo? Hawa Rwanda walifanya kweli investigation ya kutosha? Kwa nini wasingeingia deals na famous sports channels na kuonyesga vivutio vyao, au deal la Arsenal ndo cheap zaidi compared na alternatives nyingine?
 
Siyo waste of money kwasababu Rwanda wana ndege yao ambayo sasa inaenda London Gatwick, hivyo pamoja na kampeni hii, pia itawasaidia watalii kukata tiketi za moja kwa moja kwenda Kigali badala ya kuunganisha ama Dar au Nairobi.

Pili, kumbuka wamesema fedha zinazotumika ni sehemy ya fedha ya mapato yatokanayo na utalii huohuo, hivyo kuonyesha kwa kiasi kikubwa kwamba wanaweza kutumia fedha za aina hii kwa nidhamu badala ya kuzitapanya huku na kule.
Kama ilikuwa ni kwa ajili ya ndege basi wangetangaza ndege.

Kwa kawaida watalii wengi huwa wanakuja kupitia agents ambao huwa wanawafanyia bookings na all tour arrangements. Ndiyo maana wengi wao wanakuja kwenye groups. Tour operators wako aware na hizo routes ............. Vile vile such info wangeweza kuzitangaza through tourism Expo!!

Anyway, wanachojaribu kutangaza hapo ni nchi ........... na sisi tunachoangalia hapa kama hiyo marketing strategy ni nzuri. Probably, wangeweza kuja na other strategies zaidi ya hii na ambayo ingeattract more tourists kwa kuwaonyesha exactly what Rwanda has.......!!
 
Dah! haya mkuu, unazungumzia demokrasia.

Lakini Rwanda inapiga hatua mbele, Tanzania je tuliweza kuweka mabango huko London kutangaza vivutio vyetu vya utalii kwa angalau miezi sita?


Demokrasia ni muhimu sana, na hizi kesi unazozisikia mara leo kauliwa mtu,mara wameokotwa kwenye viroba, watu wamepotea hawajaonekana kwa nchi za kimaskini ni doa. Mabalozi waliopo wanazitendea haki nchi zao na wanawajali raia wao. Tatizo ni kubwa kwa Tanzania nadhani kodi hazitumiki zinavostahiki manake watalii wanaokuja na kodi wanazotoa hata uwanja wa ndege unaoitwa wa kimataifa unakosa ice. Kodi za utalii zinajenga barabara tena sio zile zinazoelekea kwenye vivutio. Kodi zinanunua ndege

UTALII UNAJITANGAZA HAUTANGAZWI, iyo kazi wataifanya wenyewe watalii wewe kazi yako ni kuzitendea haki kodi zao.
 
Mr. Zero,

Nakuelewa.

Ila Rwanda kupitia Rwanda Development Board imeona kwamba kuna haja ya kuitangaza Zaidi Rwanda kwa kuingia kwenye moja ya inner circle za jamii mojawapo ikiwa ni wapenzi wa mpira.

Hivyo mtu ataiona Visit Rwanda na kisha ataulizia kuhusu vivutio vya utalii , atakwenda ubalozini pale London, na kisha akiwa pale ubalozini pia ataona kwamba kumbe kuna ndege ya Dreamliner ambayo inakwenda moja kw amoja Kigali.

Mtalii mtarajiwa anaweza kuwa na options nyingi ila kuna uwezekani mkubwa akakata tiketi ya ndege kwa Rwandair na akamaliza na hoteli kabisa na vyote anaweza afanya direct kwa wahusika au kupitia hao travel agents.

Tuwapongeze Rwanda kwa hii hatua walochukua, kwa kweli wametupiga bao.
 
Yaani watu wataangalia neno "visit Rwanda" na suddenly wawe interested kwenda Rwanda kwa Kagame!!? Kuna "kivutio" kipi kwenye maneno hayo? Hawa Rwanda walifanya kweli investigation ya kutosha? Kwa nini wasingeingia deals na famous sports channels na kuonyesga vivutio vyao, au deal la Arsenal ndo cheap zaidi compared na alternatives nyingine?

Mkuu umefika Kigali, Rwanda?

Baada ya kahawa kama zao kuu la biashara, Utalii unashika namba mbili.

Vuvutio vyao vikubwa ni Mbuga ya Wanyama ya Akagera, mbuga ya Wanyama ingine ya Volcanoes ambayo kuna Sokwe mtu wa kutosha.

Kuna ziwa Kivu moja ya Great Lakes ambalo lina maji safi na limo kwenye bonde la ufa.

Pia kuna msitu wa Nyungwe ambao umehifadhiwa kama ulivyo kuupa ile asili yake kamili na moja ya vyanzo vya mto Nile.

Na vivutio vingine kadhalika na kadhalika.

Ni vichache lakini vinaingiza mapato na vinaboreshwa.

Sasa nikuulize suali, je bodi ya utalii ta Tanzania ni lini imewahi kufikiria kuweka matangazo ya zaidi hata ya miezi sita nje ya nchi kutangaza Utalii wetu?

Je, Tanzania ina vivutio vingapi vya utalii?

Kwanini tusiwe na mikakati ya namna ya kutangaza utalii wetu badala ya kuweka maonyesho mara Beijing mara wapi?

Ni nchi ngapi mbalimbali tuungeweza kuweka matangazo ya "Visit Tanzania" katika maeneo maalum lakini yenye mvuto na tukawa na uwezo wa kulipia kutokana na uwezo wa mapato yetu ukilinganisha na Rwanda?

Tukubali kisha tujifunze na kisha tupange tuanzie wapi kutangaza Utalii wetu hasa wakati huu ambao watalii wengi wanaonyesha kukubali kuanza kuja kuitembelea nchi yetu.
 
Habari,

Hivi karibuni nchi ya Rwanda ambayo kitalii ikijinasibu kama nchi ya vilima maelfu (the land of a thousand hills) imejipambanua zaidi kwa kuwekeza kwenye sekta ya utalii kwa manufaa na tija kuu. Nchi hii ya Afrika Mashariki pasipo kujali udogo wake na hata basi tuseme uhafifu wa vivutio vyake ukilinganisha na nchi kama Tanzania, imeonyesha 'tamaa na uchu' wa kutaka kupiga hatua kubwa ya kimapinduzi kwenye kuujuza ulimwengu juu ya uwepo wake lakini pia urithi wake wa asili.

Bwana Kagame, raisi wa Rwanda, ambaye ni mfuasi mkubwa wa timu ya mpira ya Arsenal yenye maskani yake jiji la London, Uingereza, aliona asiishie tu kuipenda timu hiyo bali pia aitumie kwenye 'kuipendezesha' zaidi nchi yake kwa kupitia fursa ya kibiashara ya kimatangazo, na kwakuwa basi Arsenal ni moja ya timu inayocheza kwenye ligi inayotazamwa zaidi Duniani, pia ina wapenzi maelfu na maelfu ulimwenguni kote, basi ni bayana faida ingalikuwapo kwa uhakika.

Kuthibitisha hilo tunaambiwa kwa kupitia mtandao NEW TIMES AFRICA kwamba tangu bandiko la 'VISIT RWANDA' liwekwe kwenye sare za Arsenal kumekuwa na ongezeko kubwa sana la watu 'kusearch' neno Rwanda mtandaoni ili kupata kujua yaliyomo huko, kwa takwimu idadi hiyo ni kubwa kuliko idadi ya mwaka mzima wa 2017 (January to December) wakati bandiko hilo halijadumu msimu mzima! Lakini pia Rwanda imepata 'media coverage' kubwa ulimwenguni kutokana na kufaidika na vyombo vyote vitakavyorusha matangazo ya timu ya Arsenal.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Hall & partners, asilimia 71% ya mashabiki wa Arsenal hawakuwa wanaiwazia Rwanda kama sehemu ya kufikia kiutalii kabla ya kuanza kuiona kwenye 'jerseys' zao. Zaidi katika asilimia hiyo, 51% walikiri kuwa ushirikiano baina yao na Rwanda umewafanya wafikirie kwenda huko kitalii kitu ambacho kimeanza kubadili taratibu mawazo ya watu juu ya nchi hii ya Rwanda (People's perception on Rwanda).

Zaidi, chaneli za mitandaoni za Rwanda zimefaidika kwa kiasi kikubwa na 'partnership' hii (Instagram +577%, Twitter +72% and Facebook +44%) ambapo huko pia wanatumia nafasi hiyo kuonyesha kila kitu ambacho kinaweza kuwashawishi watu ulimwenguni kutembelea nchi hiyo kitalii. Leo hii warwanda 142,000 (idadi inaweza ikawa imeongezeka) wameajiriwa moja kwa moja kwenye sekta ya utalii kutokana na mpanuko wa sekta hiyo ingali mwaka 2017 waajiriwa wa moja kwa moja walikuwa 90,000 tu!

Kama haitoshi, Rwanda sasa wanaangazia ligi yingine ya Ufaransa wakiwa wameadhimia kuteka 'French Market' na hata Ulaya nzima pia kwa kupitia mgongo wa klabu ya PSG kwa mtindo wa udhamini. Karibuni sasa utaona 'jerseys' za PSG zenye chapa 'VISIT RWANDA' na pia baadhi ya watu wake mashuhuri kufunga safari kuja kuitembelea Rwanda kwa ajili ya motisha ya kitalii.

Vipi kuhusu sisi? Ardhi ya mlima mrefu kuliko yote barani Afrika kupigwa kikumbo na Ardhi ya vilima (Land of a thousand hills)? Tunatumiaje fursa kuinua zaidi utalii wetu kwenye ulimwengu huu wa ushindani?

Hapa Tanzania walikuja wasanii na hata wanamichezo wengi mashuhuri duniani, mfano muigizaji Will Smith, je tulifyonza nafasi hiyo tukapata kila bora lake? (The best out of it)?

Ama hatuna 'njaa' kihivyo?
Screenshot_20191204-181949.jpg
Screenshot_20191204-182109.jpg
 
Unajua kitu ambacho nimeona Tanzania ni ubunifu. Hakuna watu wabunifu. Ikitokea kuna watu wabunifu basi watapata kitu kibaya sana.

Hebu tuangalie hata kwenye michezo na entertainments sio watu wenye hulka ya ubunifu hata kidogo.

Nathani sababu kuwa ni mfumo wa Elimu na uongozi.

Upande wa Rwanda, wengi wao wamekaa nje ya nchi. Wana-exposure and experiences ukija Nchi yetu Tanzania diaspora wanapingwa vikali sana. Tena, wanaitwa wasaliti lakini kitu hawajui ni kuwa hawa ndio assets kuu katika maendeleo ya nchi.

Tunahitaji kubadili mfumo na jinsi tunavyofanya mambo yetu.
 
Habari,

Hivi karibuni nchi ya Rwanda ambayo kitalii ikijinasibu kama nchi ya vilima maelfu (the land of a thousand hills) imejipambanua zaidi kwa kuwekeza kwenye sekta ya utalii kwa manufaa na tija kuu. Nchi hii ya Afrika Mashariki pasipo kujali udogo wake na hata basi tuseme uhafifu wa vivutio vyake ukilinganisha na nchi kama Tanzania, imeonyesha 'tamaa na uchu' wa kutaka kupiga hatua kubwa ya kimapinduzi kwenye kuujuza ulimwengu juu ya uwepo wake lakini pia urithi wake wa asili.

Bwana Kagame, raisi wa Rwanda, ambaye ni mfuasi mkubwa wa timu ya mpira ya Arsenal yenye maskani yake jiji la London, Uingereza, aliona asiishie tu kuipenda timu hiyo bali pia aitumie kwenye 'kuipendezesha' zaidi nchi yake kwa kupitia fursa ya kibiashara ya kimatangazo, na kwakuwa basi Arsenal ni moja ya timu inayocheza kwenye ligi inayotazamwa zaidi Duniani, pia ina wapenzi maelfu na maelfu ulimwenguni kote, basi ni bayana faida ingalikuwapo kwa uhakika.

Kuthibitisha hilo tunaambiwa kwa kupitia mtandao NEW TIMES AFRICA kwamba tangu bandiko la 'VISIT RWANDA' liwekwe kwenye sare za Arsenal kumekuwa na ongezeko kubwa sana la watu 'kusearch' neno Rwanda mtandaoni ili kupata kujua yaliyomo huko, kwa takwimu idadi hiyo ni kubwa kuliko idadi ya mwaka mzima wa 2017 (January to December) wakati bandiko hilo halijadumu msimu mzima! Lakini pia Rwanda imepata 'media coverage' kubwa ulimwenguni kutokana na kufaidika na vyombo vyote vitakavyorusha matangazo ya timu ya Arsenal.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Hall & partners, asilimia 71% ya mashabiki wa Arsenal hawakuwa wanaiwazia Rwanda kama sehemu ya kufikia kiutalii kabla ya kuanza kuiona kwenye 'jerseys' zao. Zaidi katika asilimia hiyo, 51% walikiri kuwa ushirikiano baina yao na Rwanda umewafanya wafikirie kwenda huko kitalii kitu ambacho kimeanza kubadili taratibu mawazo ya watu juu ya nchi hii ya Rwanda (People's perception on Rwanda).

Zaidi, chaneli za mitandaoni za Rwanda zimefaidika kwa kiasi kikubwa na 'partnership' hii (Instagram +577%, Twitter +72% and Facebook +44%) ambapo huko pia wanatumia nafasi hiyo kuonyesha kila kitu ambacho kinaweza kuwashawishi watu ulimwenguni kutembelea nchi hiyo kitalii. Leo hii warwanda 142,000 (idadi inaweza ikawa imeongezeka) wameajiriwa moja kwa moja kwenye sekta ya utalii kutokana na mpanuko wa sekta hiyo ingali mwaka 2017 waajiriwa wa moja kwa moja walikuwa 90,000 tu!

Kama haitoshi, Rwanda sasa wanaangazia ligi yingine ya Ufaransa wakiwa wameadhimia kuteka 'French Market' na hata Ulaya nzima pia kwa kupitia mgongo wa klabu ya PSG kwa mtindo wa udhamini. Karibuni sasa utaona 'jerseys' za PSG zenye chapa 'VISIT RWANDA' na pia baadhi ya watu wake mashuhuri kufunga safari kuja kuitembelea Rwanda kwa ajili ya motisha ya kitalii.

Vipi kuhusu sisi? Ardhi ya mlima mrefu kuliko yote barani Afrika kupigwa kikumbo na Ardhi ya vilima (Land of a thousand hills)? Tunatumiaje fursa kuinua zaidi utalii wetu kwenye ulimwengu huu wa ushindani?

Hapa Tanzania walikuja wasanii na hata wanamichezo wengi mashuhuri duniani, mfano muigizaji Will Smith, je tulifyonza nafasi hiyo tukapata kila bora lake? (The best out of it)?

Ama hatuna 'njaa' kihivyo?
View attachment 1281797View attachment 1281810
Nimekaa chini nikaandika uzi kwa juhudi zangu mwenyewe na nyie mkaona kwa mamlaka yenu muugeuze uwe post kwenye uzi mwingine. Haya ndo mambo yanayochosha kuweka uzi humu. Jirekebisheni! Maxence Melo Paw Moderator Invisible JamiiForums
 
Back
Top Bottom