MANILABHONA
JF-Expert Member
- Apr 1, 2015
- 434
- 500
Nimemsikliza Mstaafu Dr. Rwaitama, ki ukweli sikuwahi kumuelewa kwa miaka yote ambayo amekuwa akialikwa na kuongea kwenye televisheni na radio, jana kwa mara ya kwanza nimemuelewa alipokuwa akihojiwa EATV.
Kiukweli mheshimiwa amezungukwa na watu wanaokula kupitia uteuzi wake hivyo siku zote wanamsifia wakati mwingine hata katika kitu ambacho hakistahili sifa.
Hawa Dr.aliwaita wanafiki. na kweli hata mimi naafiki unafiki unaodhihiri miongoni mwa watendaji. Hebu angalia hotuba za kupokea ripoti ya Zungu na Biteko leo, walioongea badala ya kuongelea kwa kina yaliyokuwemo kwenye ripoti, robotatu ya muda wameongelea kumpa sifa raisi wakati anayoyafanya ni wajibu wake kuyafanya.
Inabidi mheshimiwa ajiongeze afuatilie utendaji wao sio ajae sifa tena sifa zenyewe nyingi za kinafiki. Namshauri aende kwa watu wa chini watu wa kawaida na asipende kusifiwa awe akiuliza zaidi ni wapi angefanya nini wananchi wangeona matokeo mazuri zaidi au maendeleo. akifanya hivyo atapata ukweli na sio unafiki
Kiukweli mheshimiwa amezungukwa na watu wanaokula kupitia uteuzi wake hivyo siku zote wanamsifia wakati mwingine hata katika kitu ambacho hakistahili sifa.
Hawa Dr.aliwaita wanafiki. na kweli hata mimi naafiki unafiki unaodhihiri miongoni mwa watendaji. Hebu angalia hotuba za kupokea ripoti ya Zungu na Biteko leo, walioongea badala ya kuongelea kwa kina yaliyokuwemo kwenye ripoti, robotatu ya muda wameongelea kumpa sifa raisi wakati anayoyafanya ni wajibu wake kuyafanya.
Inabidi mheshimiwa ajiongeze afuatilie utendaji wao sio ajae sifa tena sifa zenyewe nyingi za kinafiki. Namshauri aende kwa watu wa chini watu wa kawaida na asipende kusifiwa awe akiuliza zaidi ni wapi angefanya nini wananchi wangeona matokeo mazuri zaidi au maendeleo. akifanya hivyo atapata ukweli na sio unafiki