Steve Dii
JF-Expert Member
- Jun 25, 2007
- 6,402
- 1,254
WanaJF, naomba maoni yenu na kueleweshwa vizuri kuhusiana na hili swala.
--- Mgawanyo wa ruzuku kwa vyama vya siasa hapa nchini Tanzania ukoje?
--- Vyanzo vya ruzuku hizi ni nini?
--- Makadirio ya mapato kutoka vyanzo hivyo ni yapi?
--- Je, kuna limitations zozote katika kupokea michango kwa ajili ya ruzuku za vyama (kutoka watu binafsi, miradi, mashirika, etc..)?
--- Ni taasisi gani inashughulika na ufatiliaji wa michango katika vyama vyetu?
--- Je, taratibu zipi na adhabu zipi zipo iwapo miongozo iliyopo inakiukwa katika upatikanaji wa ruzuku na matumizi yake?
Ninasoma mengi kuhusiana na wizi wa mabillioni nchini. Shutuma nyingi zinaelekezwa kwa chama tawala, CCM. Ya kwamba, kuna pesa nyingi kutoka vyombo mbalimbali vimepoteza mabillioni ya pesa kwa ajili ya jaribio la kufanikisha uchaguzi wa 2005. Wahusika wengi wametajwa. Kila ninavyozidi kusoma, utetezi wa shutuma hizi ni kama vile unakosekana, hivyo kupelekea shutuma hizi kuwa kweli pamoja na kwamba kuna kesi mbalimbali bado zinashughulikiwa mbele ya sheria.
--- Ninachojiuliza mimi hivi sasa ni kwamba iwapo shutuma hizi zote ni kweli, funding ya uchaguzi itafanikiwa vipi kwa uchaguzi ujao kwa upande wa CCM?
Kutapakaa kwa pesa kama ilivyokuwa kwa miaka 2 - 4 iliyopita kumepungua na kunazidi kupungua kwa kasi kubwa sana pahali pengi duniani kutokana na financial crisis iliyopo. Nchi wahisani (donor nations) zimekumbwa na recession, hapa kwetu yaonekana bado tunajirusha kama kawa...
--- Swali: Vyama vyetu vimejihimu vipi na crisis hii kwenye upande wa ruzuku zake kiutendaji na kwenye uchaguzi ujao?
Hivi karibuni kumeibuka ufunguaji wa matawi ya vyama nchi za ughaibuni, haswa yale ya chama tawala, CCM.
--- Maswali: Funding ya uendeshaji wa matawi hayo vyanzo vyake ni vipi?
--- Kama kuna michango mbalimbali ya pesa kwenye matawi hayo kutoka kwa wanachama au chanzo chochote kile, pesa hizo zinaratibiwa vipi kwa hapa nyumbani?
--- Je, kuna limitation yoyote katika funding za matawi hayo na nani mratibu wa hili kwa serikali?
--- Je, matawi ya vyama vya upinzani yanaruhusiwa?
--- Je, nguvu ya wanachama hao (tawala na upinzani) ni ipi katika chaguzi zetu hapa nchini? (je wanaweza kupiga kura kuwakilisha uchaguzi fulani hivi hapa nchini wakiwa huko huko, au?)
--- Iwapo linatokea tatizo kwenye matawi hayo ya ng'ambo, serikali yetu inashughulikiaje tatizo hilo? (Scenario ni kwamba - kunatokea mgongano kati ya wanachama wa vyama tofauti nje ya nchi)
Ahsanteni, ni haya tu kwa sasa.
SteveD.
--- Mgawanyo wa ruzuku kwa vyama vya siasa hapa nchini Tanzania ukoje?
--- Vyanzo vya ruzuku hizi ni nini?
--- Makadirio ya mapato kutoka vyanzo hivyo ni yapi?
--- Je, kuna limitations zozote katika kupokea michango kwa ajili ya ruzuku za vyama (kutoka watu binafsi, miradi, mashirika, etc..)?
--- Ni taasisi gani inashughulika na ufatiliaji wa michango katika vyama vyetu?
--- Je, taratibu zipi na adhabu zipi zipo iwapo miongozo iliyopo inakiukwa katika upatikanaji wa ruzuku na matumizi yake?
Ninasoma mengi kuhusiana na wizi wa mabillioni nchini. Shutuma nyingi zinaelekezwa kwa chama tawala, CCM. Ya kwamba, kuna pesa nyingi kutoka vyombo mbalimbali vimepoteza mabillioni ya pesa kwa ajili ya jaribio la kufanikisha uchaguzi wa 2005. Wahusika wengi wametajwa. Kila ninavyozidi kusoma, utetezi wa shutuma hizi ni kama vile unakosekana, hivyo kupelekea shutuma hizi kuwa kweli pamoja na kwamba kuna kesi mbalimbali bado zinashughulikiwa mbele ya sheria.
--- Ninachojiuliza mimi hivi sasa ni kwamba iwapo shutuma hizi zote ni kweli, funding ya uchaguzi itafanikiwa vipi kwa uchaguzi ujao kwa upande wa CCM?
Kutapakaa kwa pesa kama ilivyokuwa kwa miaka 2 - 4 iliyopita kumepungua na kunazidi kupungua kwa kasi kubwa sana pahali pengi duniani kutokana na financial crisis iliyopo. Nchi wahisani (donor nations) zimekumbwa na recession, hapa kwetu yaonekana bado tunajirusha kama kawa...
--- Swali: Vyama vyetu vimejihimu vipi na crisis hii kwenye upande wa ruzuku zake kiutendaji na kwenye uchaguzi ujao?
Hivi karibuni kumeibuka ufunguaji wa matawi ya vyama nchi za ughaibuni, haswa yale ya chama tawala, CCM.
--- Maswali: Funding ya uendeshaji wa matawi hayo vyanzo vyake ni vipi?
--- Kama kuna michango mbalimbali ya pesa kwenye matawi hayo kutoka kwa wanachama au chanzo chochote kile, pesa hizo zinaratibiwa vipi kwa hapa nyumbani?
--- Je, kuna limitation yoyote katika funding za matawi hayo na nani mratibu wa hili kwa serikali?
--- Je, matawi ya vyama vya upinzani yanaruhusiwa?
--- Je, nguvu ya wanachama hao (tawala na upinzani) ni ipi katika chaguzi zetu hapa nchini? (je wanaweza kupiga kura kuwakilisha uchaguzi fulani hivi hapa nchini wakiwa huko huko, au?)
--- Iwapo linatokea tatizo kwenye matawi hayo ya ng'ambo, serikali yetu inashughulikiaje tatizo hilo? (Scenario ni kwamba - kunatokea mgongano kati ya wanachama wa vyama tofauti nje ya nchi)
Ahsanteni, ni haya tu kwa sasa.
SteveD.