Waswahili walisema kusikia kwa kenge ni tofauti sana na viumbe wengine wote:
Hata sisi hatuna namma nyingine kama ni nia yetu ya dhati kusikika.
Kwamba ni ripoti za CAG? Kwamba ni wahalifu sugu kuachiwa lakini si wanaoshikiliwa kisiasa?
Bado tungependa tunayosema kucha kutwa yaweze hatimaye kusikika? Kwa namma hii ya kupiga makelele tu? Kwa hakika kama ni magonjwa, tutakuwa na Magonjwa Mtambuka!
--------------
Jumapili, Aprili Pili, 2023, jua la Magharibi, Rais wa Kenya, William Rutto, alitoa hotuba ya kumwomba Kiongozi wa Upinzani, Raila Odinga na timu yake ya Azimio la Umoja One Kenya, kusitisha maandamano.
Wakati Ruto akitoa ombi hilo kwa Raila na Azimio, tayari hali ilishakuwa mbaya. Watu watatu walishapoteza maisha kutokana na maandamano yaliyoitishwa na Raila. Mali za watu ziliharibiwa na kuporwa na waandamanaji bandia. Biashara zilisimama na kuharibiwa.
Nyumba za ibada zilichomwa moto, kuna watu waliteka gari la polisi na kutokomea nalo Oyugis, Homa Bay. Watu zaidi ya 400, waliripotiwa kujeruhiwa, wengine majeraha yakiwa mabaya mno. Tamko lilikuwa maandamano ya amani, ila vitendo havikuakisi amani. Polisi walipotaka kutumia nguvu kudhibiti, machafuko yakawa makubwa. Polisi walikufa na kujeruhiwa.
Ombi la Ruto kwa Raila lilikuwa, maandamano yasitishwe ili kuruhusu mazungumzo ya vyama bungeni katika madai ambayo aliyatoa na kuyatumia kushawishi maandamano nchi nzima, vilevile na yeye (Ruto), milango yake ipo wazi kukutana na kiongozi huyo wa upinzani.
Saa moja baadaye, Raila alijibu hotuba ya Ruto kwa kutoa tamko la kusitisha maandamano ili kuruhusu mazungumzo ya vyama kuchukua nafasi. Vilevile kuheshimu mfungo wa mwezi wa Ramadhan, Kwaresma na ujio wa Pasaka.
Raila alisema, kama mazungumzo hayataleta matunda, watarudi tena kwenye maandamano baada ya wiki moja. Hivyo, aliomba wananchi wasiendelee na maandamano kupisha nafasi ya mazungumzo.
Kiini cha maandamano; Raila alikuwa na hoja mbili. Mosi, ikiwa ni manung’uniko ya kutotendewa haki kwenye Uchaguzi Mkuu Kenya uliofanyika Agosti 9, 2022 na mazingira yake. Pili, ni kupaa kwa gharama za maisha.
Awali, Raila alitoa muda wa siku 14, Ruto kushughulikia malalamiko hayo. Kipindi hicho alichokitoa kilipopita pasipo maombi aliyoyatoa kushughulikiwa, ndipo aliitisha maandamano na yakaitikiwa.
Nyakati za mwanzo za maandamano, ungemwona Ruto akihutubia makundi ya watu, akicheka na kufanya mzaha kuwa Raila amwache arekebishe nchi kwa sababu mapatano yake na Rais mstaafu, Uhuru Kenyatta, ndiyo yaliyoharibu nchi.
Naibu Rais, Rigathi Kachagua, alikuwa mkali. Alisema, Raila aliitisha maandamano kumtisha Ruto ili waketi na kugawana mamlaka ya kuongoza, kama ilivyokuwa wakati wa Rais wa pili, Daniel Moi, Rais wa tatu, Mwai Kibaki na Uhuru.
Rigathi alisema, Ruto na yeye sio watu wa kutishwa. Aliongeza kuwa Uhuru, mtoto wa Rais wa Kwanza wa Kenya, Jomo Kenyatta, amekuzwa kwa virutubisho vya kiwandani (cerelac), ndio maana alipotishwa na Raila, aliketi wakazungumza.
Si hivyo tu, Rigathi aliahidi kuwa hata siku ambayo Ruto angekubali kukutana na Raila, yeye (Rigathi), angekwenda Ikulu ya Kenya na kuzuia mageti yote, kuhakikisha kiongozi huyo wa upinzani, hapati nafasi ya kupeana mkono na bosi wake.
Kinachotokea sasa, ni tofauti mno na mtazamo wa Ruto na tambo za Rigathi. Dirisha la mazungumzo limefunguliwa. Muhimu zaidi, aliyeomba ni Ruto. Kisha Raila akapokea. Rigathi akampongeza bosi wake kwa uamuzi wake wa busara.
Source: Mwananchi
"Ruto anapojifunza maridhiano kwa maandamano"
Hata sisi hatuna namma nyingine kama ni nia yetu ya dhati kusikika.
Kwamba ni ripoti za CAG? Kwamba ni wahalifu sugu kuachiwa lakini si wanaoshikiliwa kisiasa?
Bado tungependa tunayosema kucha kutwa yaweze hatimaye kusikika? Kwa namma hii ya kupiga makelele tu? Kwa hakika kama ni magonjwa, tutakuwa na Magonjwa Mtambuka!
--------------
Ruto anapojifunza maridhiano kwa maandamano
Jumapili, Aprili Pili, 2023, jua la Magharibi, Rais wa Kenya, William Rutto, alitoa hotuba ya kumwomba Kiongozi wa Upinzani, Raila Odinga na timu yake ya Azimio la Umoja One Kenya, kusitisha maandamano.
Wakati Ruto akitoa ombi hilo kwa Raila na Azimio, tayari hali ilishakuwa mbaya. Watu watatu walishapoteza maisha kutokana na maandamano yaliyoitishwa na Raila. Mali za watu ziliharibiwa na kuporwa na waandamanaji bandia. Biashara zilisimama na kuharibiwa.
Nyumba za ibada zilichomwa moto, kuna watu waliteka gari la polisi na kutokomea nalo Oyugis, Homa Bay. Watu zaidi ya 400, waliripotiwa kujeruhiwa, wengine majeraha yakiwa mabaya mno. Tamko lilikuwa maandamano ya amani, ila vitendo havikuakisi amani. Polisi walipotaka kutumia nguvu kudhibiti, machafuko yakawa makubwa. Polisi walikufa na kujeruhiwa.
Ombi la Ruto kwa Raila lilikuwa, maandamano yasitishwe ili kuruhusu mazungumzo ya vyama bungeni katika madai ambayo aliyatoa na kuyatumia kushawishi maandamano nchi nzima, vilevile na yeye (Ruto), milango yake ipo wazi kukutana na kiongozi huyo wa upinzani.
Saa moja baadaye, Raila alijibu hotuba ya Ruto kwa kutoa tamko la kusitisha maandamano ili kuruhusu mazungumzo ya vyama kuchukua nafasi. Vilevile kuheshimu mfungo wa mwezi wa Ramadhan, Kwaresma na ujio wa Pasaka.
Raila alisema, kama mazungumzo hayataleta matunda, watarudi tena kwenye maandamano baada ya wiki moja. Hivyo, aliomba wananchi wasiendelee na maandamano kupisha nafasi ya mazungumzo.
Kiini cha maandamano; Raila alikuwa na hoja mbili. Mosi, ikiwa ni manung’uniko ya kutotendewa haki kwenye Uchaguzi Mkuu Kenya uliofanyika Agosti 9, 2022 na mazingira yake. Pili, ni kupaa kwa gharama za maisha.
Awali, Raila alitoa muda wa siku 14, Ruto kushughulikia malalamiko hayo. Kipindi hicho alichokitoa kilipopita pasipo maombi aliyoyatoa kushughulikiwa, ndipo aliitisha maandamano na yakaitikiwa.
Nyakati za mwanzo za maandamano, ungemwona Ruto akihutubia makundi ya watu, akicheka na kufanya mzaha kuwa Raila amwache arekebishe nchi kwa sababu mapatano yake na Rais mstaafu, Uhuru Kenyatta, ndiyo yaliyoharibu nchi.
Naibu Rais, Rigathi Kachagua, alikuwa mkali. Alisema, Raila aliitisha maandamano kumtisha Ruto ili waketi na kugawana mamlaka ya kuongoza, kama ilivyokuwa wakati wa Rais wa pili, Daniel Moi, Rais wa tatu, Mwai Kibaki na Uhuru.
Rigathi alisema, Ruto na yeye sio watu wa kutishwa. Aliongeza kuwa Uhuru, mtoto wa Rais wa Kwanza wa Kenya, Jomo Kenyatta, amekuzwa kwa virutubisho vya kiwandani (cerelac), ndio maana alipotishwa na Raila, aliketi wakazungumza.
Si hivyo tu, Rigathi aliahidi kuwa hata siku ambayo Ruto angekubali kukutana na Raila, yeye (Rigathi), angekwenda Ikulu ya Kenya na kuzuia mageti yote, kuhakikisha kiongozi huyo wa upinzani, hapati nafasi ya kupeana mkono na bosi wake.
Kinachotokea sasa, ni tofauti mno na mtazamo wa Ruto na tambo za Rigathi. Dirisha la mazungumzo limefunguliwa. Muhimu zaidi, aliyeomba ni Ruto. Kisha Raila akapokea. Rigathi akampongeza bosi wake kwa uamuzi wake wa busara.
Source: Mwananchi
"Ruto anapojifunza maridhiano kwa maandamano"