kisugujira
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 774
- 196
WanaJF,
Sasa hivi askari polisi wa usalama barabarani wametawanyika kila kona hapa jijini Dar es Salaam wakikamata magari hovyo kwa lengo la kujikusanyia pesa za Krismass kwa ajili ya matumizi ya familia zao na wakubwa zao! Tena cha kushangaza makundi ya askari hao wa usalama barabarani huongozana na wakaguzi wa magari (Vehicle Inspectors) ili zoezi zima la kukamata magari lionekane kuwa na uzito fulani!
Mfano mzuri wa hiki ninachokieleza katika uzi huu kipo barabara inayoingia Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na Mbagala ambapo kila siku wala rushwa hawa utawaona wakikamata magari na kupokea rushwa hadharani! Kama ni gari ya mauzo imekamatwa, iwe ya maji, sabuni, pipi, nk ikikamatwa na dereva akasema hana pesa, hulazimisha wapewe kitu fulani kati ya vitu vinavyouzwa!
Pia kutoka chanzo cha kuaminika pale Ubungo Bus Terminal, inasemekana wanausalama hawa wa barabarani wanahongwa pesa na wenye mabasi yanayokwenda mikoani ili wayaruhusu magari hayo kwa muda mrefu hasa saa za asubuhi na kusababisha msongamano mkubwa wa magari toka sehemu zingine na kuchangia wanaowahi kwenda maofisini kuchelewa!
Sasa hivi askari polisi wa usalama barabarani wametawanyika kila kona hapa jijini Dar es Salaam wakikamata magari hovyo kwa lengo la kujikusanyia pesa za Krismass kwa ajili ya matumizi ya familia zao na wakubwa zao! Tena cha kushangaza makundi ya askari hao wa usalama barabarani huongozana na wakaguzi wa magari (Vehicle Inspectors) ili zoezi zima la kukamata magari lionekane kuwa na uzito fulani!
Mfano mzuri wa hiki ninachokieleza katika uzi huu kipo barabara inayoingia Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na Mbagala ambapo kila siku wala rushwa hawa utawaona wakikamata magari na kupokea rushwa hadharani! Kama ni gari ya mauzo imekamatwa, iwe ya maji, sabuni, pipi, nk ikikamatwa na dereva akasema hana pesa, hulazimisha wapewe kitu fulani kati ya vitu vinavyouzwa!
Pia kutoka chanzo cha kuaminika pale Ubungo Bus Terminal, inasemekana wanausalama hawa wa barabarani wanahongwa pesa na wenye mabasi yanayokwenda mikoani ili wayaruhusu magari hayo kwa muda mrefu hasa saa za asubuhi na kusababisha msongamano mkubwa wa magari toka sehemu zingine na kuchangia wanaowahi kwenda maofisini kuchelewa!