Rushwa, ufisadi na wizi wa mali za umma Tanzania hautakoma mpaka pale Serikali itakapoamua rasmi nchi hii iendeshwe Kijamaa

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,646
35,981
Habari waungwana!
Kwa mujibu wa katiba yetu Tanzania ni nchi ya kijamaa. Ukisoma sura ya kwanza utaliona hili.
Ila misingi ya ujamaa ni kuwa mbali na rushwa, ufisadi na wizi wa mali za umma jambo ambalo tuko kinyume nalo.
Wizi upo
Ufisadi upo
Rushwa ipo na
Unyonyaji upo.

Unyonyaji ndio baba wa ufisadi, rushwa na wizi wa mali za umma.

Hebu fikiria mtumishi wa umma mmoja ndani ya taasisi moja analipwa milioni 5 huku mwingine analipwa laki 3. Je,huo sio unyonyaji?

Je, anayelipwa milioni 5 hataona kuwa ana haki zote za kuendelea kumnyonya huyu anayelipwa laki 3 kwa kujilimbikizia mali zaidi kwa njia zisizo halali?

Je, huyu anayelipwa laki tatu hatachukua rushwa kwa mwananchi ili file lake likae mbele ahudumiwe haraka?. Ni nini kitampa hofu huyu mtumishi asichukue rushwa?

Kwa nchi ya kijamaa ni halali kiongozi kutembea na msururu wa magari 50 yenye thamani ya juu huku ndani ya nchi hiyohiyo watoto wanakaa chini ya sakafu iliyotoboka baadhi ya shule?

Dar es Salaam nimepita shule kadhaa nimebaini kuwa kuna madarasa ya primary, darasa moja linachukua wanafunzi zaidi ya Mia kwa wakati mmoja. The same time mbunge wa hilo jimbo analipwa zaidi ya milioni kumi. Huo sio ukabaila na unyonyaji?

Kama watunga sheria wabunge pamoja na mawaziri wao wanakubali unyonyaji je, ufisadi, rushwa na wizi utaisha?

Dawa ya kukomesha rushwa, ufisadi na wizi Serikalini na taasisi binafsi ni kuuondoa rasmi mfumo wa kikabaila na kibwenyenye na sio kuunda taasisi za kupambana na hayo matatizo.
 
Ujamaa ni mfumo unaokinzana na kanuni za kimaumbile, na ndio maana ulifeli na unaendelea kufeli ktk mataifa yote yaliyowaui kujinasibisha na mfumo huu.


Ama kuhusu Unyonyaji hata wajamaa pia ni wanyonyaji ktk namna yao, moja ya kanuni zao ni kwamba
Yqtakapotokea mapinduzi ya kijamaa basi nchi iongozwe na Wakulima na Wafanyakazi, kutokana na kanuni hii tu ni moja kwa moja wanayabagua makundi mengine ambayo kimsingi yana mchango mkubwa ktk maendeleo ya nchi kama Wafanyabiashara.
Vilevile katika kanuni yao ya 'communal ownership' wanawafanya wale wenye bidii ktk uzalishaji kuwa sawa na hata wale wavivu... Yaani aliyepata kingi ni lazima agawane na aliyepata kidogo, nonesense!

Ujamaa unapokonya watu uhuru wao, Hata kama una fedha za kununua vitu vya gharama mfumo wa Ujamaa hudhibiti matumizi ya pesa zako ulizotafuta mwenyewe, watu hawapo huru kuukosoa mfumo, na hawapo huru kufanya vitu vyako wanavyovipenda kwa hofu ya kwenda kinyume na Matakwa ya kimfumo.

Ujamaa ni Mfumo mbaya kabisa na umefeli kutokana na kukiuka kanuni za kimaumbile, ikiwemo ile ya watu wamezaliwa na vipawa tofauti, uwezo tofauti, utofauti huu ndio huwafanya watu kujipa utambulisho ktk jamii... Utofauti huu huwafanya baadhi kupata mali nyingi na wengine kukosa, suala la kuwalazimisha wote kuwa sawa ni kuwanyonya wale wenye bidii kwa kuwapokonya vingi walivyonavyo na kuwapa waso na bidii au bahati kwa kuwaongezea wasivyostahili.
 
Ujamaa ni mfumo unaokinzana na kanuni za kimaumbile, na ndio maana ulifeli na unaendelea kufeli ktk mataifa yote yaliyowaui kujinasibisha na mfumo huu.
ulifeli au ulifelishwa?? na waliofelisha unajua kwanin waliufelisha? , hile ndio system ya maisha ya mwanadamu kuongozwa kitem, hizo mambo za demokrasia sio mfumo halali wa uongoz ndy maana unaona hauna faida zaid ya malumbano,machafuko na ushenz wakila aina,
 
ulifeli au ulifelishwa?? na waliofelisha unajua kwanin waliufelisha? , hile ndio system ya maisha ya mwanadamu kuongozwa kitem, hizo mambo za demokrasia sio mfumo halali wa uongoz ndy maana unaona hauna faida zaid ya malumbano,machafuko na ushenz wakila aina,
Suala la Mfumo wa maisha ku-survive iwe ujamaa au ubepari ni lazima upitie vikwazo vingi vikiwepo uzandiki, fitna na figisu za watu za makusudi kutaka mfumo uanguke...kila mfumo hupitia haya hivyo aidha ulifeli au ulifelishwa huo ni mchakato wa kiasili.... Maana kama ulifelishwa maana yake watu ndio walioufelisha na maana yake ni kwamba watu hawakuupenda ndio maana ukafelishwa.

Wanadamu hawana mfumo mmoja wa kuishi, mifumo hubadilika kutokana na nyakati na mahitaji ya zama husika.
 
Habari waungwana!
Kwa mujibu wa katiba yetu Tanzania ni nchi ya kijamaa. Ukisoma sura ya kwanza utaliona hili.
Ila misingi ya ujamaa ni kuwa mbali na rushwa, ufisadi na wizi wa mali za umma jambo ambalo tuko kinyume nalo.
Wizi upo
Ufisadi upo
Rushwa ipo na
Unyonyaji upo.

Unyonyaji ndio baba wa ufisadi, rushwa na wizi wa mali za umma.

Hebu fikiria mtumishi wa umma mmoja ndani ya taasisi moja analipwa milioni 5 huku mwingine analipwa laki 3. Je,huo sio unyonyaji?

Je, anayelipwa milioni 5 hataona kuwa ana haki zote za kuendelea kumnyonya huyu anayelipwa laki 3 kwa kujilimbikizia mali zaidi kwa njia zisizo halali?

Je, huyu anayelipwa laki tatu hatachukua rushwa kwa mwananchi ili file lake likae mbele ahudumiwe haraka?. Ni nini kitampa hofu huyu mtumishi asichukue rushwa?

Kwa nchi ya kijamaa ni halali kiongozi kutembea na msururu wa magari 50 yenye thamani ya juu huku ndani ya nchi hiyohiyo watoto wanakaa chini ya sakafu iliyotoboka baadhi ya shule?

Dar es Salaam nimepita shule kadhaa nimebaini kuwa kuna madarasa ya primary, darasa moja linachukua wanafunzi zaidi ya Mia kwa wakati mmoja. The same time mbunge wa hilo jimbo analipwa zaidi ya milioni kumi. Huo sio ukabaila na unyonyaji?

Kama watunga sheria wabunge pamoja na mawaziri wao wanakubali unyonyaji je, ufisadi, rushwa na wizi utaisha?

Dawa ya kukomesha rushwa, ufisadi na wizi Serikalini na taasisi binafsi ni kuuondoa rasmi mfumo wa kikabaila na kibwenyenye na sio kuunda taasisi za kupambana na hayo matatizo.
Nyie watoto wa juzi hamjui hata ujamaa unafanana vipi.
Ukiwa radhi nikupeleke Mwanadilatu, moja ya viji vya ujamaa vya Mwalimu.
 
Ujamaa ni mfumo unaokinzana na kanuni za kimaumbile, na ndio maana ulifeli na unaendelea kufeli ktk mataifa yote yaliyowaui kujinasibisha na mfumo huu.


Ama kuhusu Unyonyaji hata wajamaa pia ni wanyonyaji ktk namna yao, moja ya kanuni zao ni kwamba
Yqtakapotokea mapinduzi ya kijamaa basi nchi iongozwe na Wakulima na Wafanyakazi, kutokana na kanuni hii tu ni moja kwa moja wanayabagua makundi mengine ambayo kimsingi yana mchango mkubwa ktk maendeleo ya nchi kama Wafanyabiashara.
Vilevile katika kanuni yao ya 'communal ownership' wanawafanya wale wenye bidii ktk uzalishaji kuwa sawa na hata wale wavivu... Yaani aliyepata kingi ni lazima agawane na aliyepata kidogo, nonesense!

Ujamaa unapokonya watu uhuru wao, Hata kama una fedha za kununua vitu vya gharama mfumo wa Ujamaa hudhibiti matumizi ya pesa zako ulizotafuta mwenyewe, watu hawapo huru kuukosoa mfumo, na hawapo huru kufanya vitu vyako wanavyovipenda kwa hofu ya kwenda kinyume na Matakwa ya kimfumo.

Ujamaa ni Mfumo mbaya kabisa na umefeli kutokana na kukiuka kanuni za kimaumbile, ikiwemo ile ya watu wamezaliwa na vipawa tofauti, uwezo tofauti, utofauti huu ndio huwafanya watu kujipa utambulisho ktk jamii... Utofauti huu huwafanya baadhi kupata mali nyingi na wengine kukosa, suala la kuwalazimisha wote kuwa sawa ni kuwanyonya wale wenye bidii kwa kuwapokonya vingi walivyonavyo na kuwapa waso na bidii au bahati kwa kuwaongezea wasivyostahili.
Wala hujui unatoa propaganda za magharabi za ile miaka ya 50 na 60 wakati wa vita baridi kati ya nchi za kibepari na kijamaa. Ujamaa unaruhusu kila mtu kupata kwa jasho lake iwe akili au kutumia nguvu zake. La msingi ujamaa unapinga unyonyaji wa nguvukazi ya mtu mwingine na kulenga maendeleo kwa raia wote bila kuruhusu kukua kwa tabaka la ubwanyenye. Hapa ndio tofauti kubwa na mfumo wa ubepari ambao hauzingatii kulinda maslahi ya wavuja jasho. Nchi yetu bado ni ya kijamaa kwa maoni yangu.
 
Wanaopenda Ujamaa ni wale walokosa mianya ya kupiga pesa. Baba wacha watu wajipigie pesa. Na hichi kipindi cha awamu ya 6 wacha watu wawe mabilionea
 
Wala hujui unatoa propaganda za magharabi za ile miaka ya 50 na 60 wakati wa vita baridi kati ya nchi za kibepari na kijamaa. Ujamaa unaruhusu kila mtu kupata kwa jasho lake iwe skili au nguvu. La msingi ujamaa unapinga unyonyaji wa nguvukazi ya mtu mwingine. Hapa ndio tofauti kubwa na mfumo wa ubepari ambao hauzingatii kulinda maslahi ya wavuja jasho. Nchi yetu bado ni ya kijamaa kwa maoni yangu.
Duh, mkuu ni msingi gani wa ujamaa unaruhusu kila mmoja kumiliki mali kulingana na kiwango alichojiingizia? Kma una mfano wowote hai tafadhali ulete vinginevyo itakua unautetea ujamaa kutokana na mahabba yako binafsi na si kwa uhalisia on the ground.
 
Wala hujui unatoa propaganda za magharabi za ile miaka ya 50 na 60 wakati wa vita baridi kati ya nchi za kibepari na kijamaa. Ujamaa unaruhusu kila mtu kupata kwa jasho lake iwe akili au kutumia nguvu zake. La msingi ujamaa unapinga unyonyaji wa nguvukazi ya mtu mwingine na kulenga maendeleo kwa raia wote bila kuruhusu kukua kwa tabaka la ubwanyenye. Hapa ndio tofauti kubwa na mfumo wa ubepari ambao hauzingatii kulinda maslahi ya wavuja jasho. Nchi yetu bado ni ya kijamaa kwa maoni yangu.
Tuwspeleke vijijini mlime mpaka muufarahie ujamaa na matunda la jasho lenu.
 
Duh, mkuu ni msingi gani wa ujamaa unaruhusu kila mmoja kumiliki mali kulingana na kiwango alichojiingizia? Kma una mfano wowote hai tafadhali ulete vinginevyo itakua unautetea ujamaa kutokana na mahabba yako binafsi na si kwa uhalisia on the ground.
Nadhani mfano wa china ndio mfano mkubwa. China uchumi unaendeshwa na makampuni na watu binafsi kwa kiasi kikubwa na ni nchi ya kijamaa. Tofauti upo na nchi za kibepari kwa namna kuna udhibiti wa uchumi ili raia wote wafaidike na kupata maendeleo. China leo inadai imefuta umaskini wa kupindukia kwa raia wake.
 
ulifeli au ulifelishwa?? na waliofelisha unajua kwanin waliufelisha? , hile ndio system ya maisha ya mwanadamu kuongozwa kitem, hizo mambo za demokrasia sio mfumo halali wa uongoz ndy maana unaona hauna faida zaid ya malumbano,machafuko na ushenz wakila aina,
Takwimu zinaonyesha mataifa ya kibepari ndiyo yenye uchumi mkubwa zaidi kuliko ya kijamaa
 
Dah hivi unaichukulia Uchina kama nchi ya kijamaa?

Sera za kiuchumi za Uchina zinakinzana moja kwa moja na zile za Kijamaa, Uchina inatumia sera za kibepari ktk Uchumi ndio maana unaona wapo pale walipo.

Walitenga maeneo tangu mwishoni mwa miaka ya 70 ambayo waliruhusu Uwekezaji toka nje na Biashara huria, hivi vyote havikubaliki Kijamaa. Hili na mengine mengi yanaitoa Uchina ktk nchi za Kijamaa japokuwa ni kweli bado wana chembe chembe za kijamaa lakini si ktk ukamilifu wake kiasi cha kuitwa Wajamaa.

Nimalize kwa kunukuu jibu la Charles Liu (financier and adviser to Chinese government,2019) alipoulizwa na Mehdi Hassan kuwa Uchina ni nchi ya kijamaa au kibepari ktk moja ya interview, yeye alijibu '...ni ya kijamaa kwa maneno na kibebari kwa vitendo...' (paraphrased).

Nadhani mfano wa china ndio mfano mkubwa. China uchumi unaendeshwa na makampuni na watu binafsi kwa kiasi kikubwa na ni nchi ya kijamaa. Tofauti upo na nchi za kibepari kwa namna kuna udhibiti wa uchumi ili raia wote wafaidike na kupata maendeleo. China leo inadai imefuta umaskini wa kupindukia kwa raia wake.
 
26be1b40ca85e3e7.jpeg
 
Ujamaa ni atheism ideology

Watu wa Mungu tunaamini katika ubepari, Adam na Hawa walikuwa wabepari

Mungu alivyotuondoa peponi na kutuleta duniani alituwekea spirit ya ubepari na ujasiriamali ili tuweze kutafuta riziki zetu.

Mjamaa ni adui wa Mungu
 
Ujamaa hauruhusu mtawaliwa kuwa na nguvu kuliko mtawala.
Ujamaa ubakie kwenye mgawanyo wa huduma za Jamii na sio kwenye uchumi
 
Back
Top Bottom