radika
JF-Expert Member
- Jul 15, 2014
- 20,427
- 32,196
Mwenyekiti Chama Cha Mapinduzi ‘CCM’ Wilaya ya Rorya katika Mkoa wa Mara, Samwel Kiboye ameahidi kuwafuta uanachama wagombe wa nafasi za Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi ‘UVCCM’ baada ya kunasa sauti za kupeana rushwa kwenye uchaguzi huo.
Akizungumza na Ayo TV na millardayo.com, Kiboye amesema, wamewahoji wanaodaiwa kufanya hivyo na baadhi yao wamekiri kuhusika, hivyo watachukuliwa hatua zinazostahili.