Rushwa TRA: Suluhisho ni kukirudisha chuo cha kodi katika misingi yake vinginevyo makamishna watatumbuliwa kila siku

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,853
141,785
Tatizo la rushwa katika idara za kodi siyo jipya na lina historia ndefu na msingi wake ni wafanyabiashara kutotaka kulipa kodi halali.
Lakini pia kuna watoza ushuru ambao sio waaminifu na waliojawa na tamaa ambao hulazimisha kupewa rushwa.

Wakati awamu ya pili inaingia madarakani Sweden ilitoa msaada wa kujenga chuo cha kodi pale mikocheni kikiitwa Institute of Tax Administration ( ITA).

Chuo hiki kilikuwa ni maalumu kwa ajili ya wafanyakazi kufundishwa maadili ya kazi pamoja na mbinu mpya za ukusanyaji pale inapolazimu, lakini zaidi ni kuwafanya watoza ushuru wawe wabobezi katika utendaji wao.

Wakati ule taaluma ya kodi ilikuwa ikifundishwa pale IFM lakini ubobezi ulipatikana ITA.

Kwa sasa ITA imebadilishwa na kuwa chuo cha kibiashara na kwahiyo watumishi wa TRA wanakosa sehemu sahihi ya kuimarisha mbongo zao na kufanya rejea ya uadilifu na utendaji wao mara kwa mara.

Kutoza ushuru ni zaidi ya kukusanya kodi, kuna falsafa yake hata kwenye maisha ya kawaida ya mfanyakazi. Ndio maana maana makamishna karibia wote walioteuliwa nje ya mfumo au malezi ya kikodi walifeli. Kwa mfano Sanare aliyetoka ATC wakati ule, Kitilya aliyetoka TBL, Bashe aliyetoka Barclays bank na hata hawa akina Maswi, Mpango na Kadata wa awamu ya 5.

Kutoza ushuru ni tofauti na kuwa bank teller au afisa mikopo, tax collection inahitaji kubalance matumizi ya nguvu na akili ili vitumike kwa pamoja. Wakati TRA inaanzishwa July 1996 mtoza ushuru mmoja alikataa kuvaa koti na tai akidai kiutamaduni mtoza ushuru anapaswa kuvaa kaunda suti, hao ndio watoza ushuru!
Watoza ushuru wana lugha yao kama ambavyo wafanyabiashara wana lugha na hicho ndio kilichofundishwa pale ITA enzi zile.

Binafsi nimeshangaa kusikia takribani makampuni 17,446 yamepeleka financial statements wakideclare profit ndogo kule TRA at the same period profit kubwa kwenye banks zao wanakopewa mikopo.
Nimejiuliza hivi hiki chuo cha kodi cha sasa huwa kinafanya tafiti kweli au wanasubiri hadi ofisi ya Rais iingilie kati?
Itaendelea............

Naunga mkono pendekezo la waziri wa fedha la kuunda tume.

Maendeleo hayana vyama!
 
Tatizo ni siasa katika utendaji, mkuu huyuhuyu aliemtumbua Kichere ndio aliekuwa anampongeza kwa makusanyo makubwa bila kujali anakusanya haki au dhulma, watu wamefunga biashara ndio anaamka....heri lakini kajua kuna tatizo.
 
Tatizo ni siasa katika utendaji, mkuu huyuhuyu aliemtumbua Kichere ndio aliekuwa anampongeza kwa makusanyo makubwa bila kujali anakusanya haki au dhulma, watu wamefunga biashara ndio anaamka....heri lakini kajua kuna tatizo.
Tatizo la nchi hii haieleweki malengo ya TRA yanapangwa kwa vigezo gani kama ni GDP au nini?!

Na hii hoja hata Rais Magufuli aliwahi kuiibua!
 
Issue siyo elimu issue ni application ya hizo elimu. Hao watendaji wa TRA hawajawahi kuwa na biashara ata ya boda boda, wako theoretical sana. Wachenjuliwe makinikia yao mpaka watakapopata akili.
Kimsingi mtoza ushuru hapaswi kuwa na biashara!
 
kwani makamishna wote wa TRA ni wahitimu wa vyuo vya kodi? kama sivyo hilo si suluhisho pekee, suluhisho ni mbadala wa azimio la Arusha ambalo liliweka misingi ya uwajibikaji.
Hakuna kamishna aliyekuwa muhitimu wa ITA bali pale wanaenda kupikwa kimaadili na kiutendaji.
Ndio maana nimesema taaluma ya kodi ilikuwa ikifundishwa pale IFM!
 
Tatizo sio Chuo kwani Ukiritimba wa Watumishi wa Ardhi nao tatizo ni Chuo?
Vyuo vya wafanyakazi kwa kila sekta vilikuwa na maana kubwa sana, hata hivyo vuo vya ardhi vimegeuzwa kuwa vya kibiashara ndio unaona matatizo ya uadilifu kila uchwao katika sekta.

Palikuwepo Bandari collage, chuo cha Tanesco, chuo cha mipango, chuo cha posta nk vyote hivi vilijikita kwenye maadili!
 
Sidhani tatizo ni maadili au ubobezi au falsafa ya kodi na suluhisho ni mafunzo, dunia ya leo kila mahali wanajaribu kwa kiwango wanachoweza kutatua changamoto sugu na zinazojitokeza kwa kutumia TEKNOLOJIA cha ajabu, jana kwenye kikao hicho cha wafanya biashara na Serikali, kwa muda wote huo waliokaa zaidi ya masaa 8, si serikali wala wafanyabiashara waliokumbuka hata kutaja tu neno Teknolojia.

Kwa ufupi kabisa teknolojia inasaidia kupunguza human errors be it za kukusudia kama rushwa au kutokusudia, kwa hali ilivyo sasa kwa nchi yetu kuwa na walipa kodi wachache na viwango vya juu vya kodi huku kukiwa na sekta isiyo rasmi kubwa kiasi cha kufikia kuwa na mapato yanayokadiriwa kuwa asilimia 53.6 ya pato la taifa, lakini uwepo wa changamoto kama ya TRA kupendelea kukusanya kodi kwa mfumo wa lumpsum, na kusumbua walipa kodi..kinachoweza kupunguza malalamiko na kuongeza tija ni TEKNOLOJIA tu!

Nilitarajia wasaidizi wa Mteuzi kama wanafahamu kipaumbele chake ni ukusanyaji zaidi mapato, Boss wa TRA alipaswa kuwa mtu mwenye background ya IT au basi azungukwe na makamishna wenye ujuzi wa mambo ya IT, si hivyo tu nilitarajia sambamba na kualika wafanyabiashara wangealikwa pia watu wote wenye ujuzi na mambo ya IT ili wasikie changamoto na pengine wasaidie kutafuta majibu kitaalamu..kutokujua nature ya tatizo ni vigumu sana kupata jibu sahihi!

Naamini wako watanzania wana mifumo inayoweza kutatua changamoto za TRA kwa sasa..habari za kuteua sijui mchumi, lawyer nk hazitaleta badiliko kusaidia nchi yetu.
 
Vyuo vya wafanyakazi kwa kila sekta vilikuwa na maana kubwa sana, hata hivyo vuo vya ardhi vimegeuzwa kuwa vya kibiashara ndio unaona matatizo ya uadilifu kila uchwao katika sekta.

Palikuwepo Bandari collage, chuo cha Tanesco, chuo cha mipango, chuo cha posta nk vyote hivi vilijikita kwenye maadili!
Maadili na uadilifu hayafunzwi chuoni, nyumbani kwenye familia zetu ndio mahali sahihi, kama hata makanisa na misikiti yameshindwa vyuo ndio vitaweza..! lakini sheria inaweza mlazimisha mtu awe muadilifu hata kama hataki! so sio ishu ya mafunzo.
 
Maadili na uadilifu hayafunzwi chuoni, nyumbani kwenye familia zetu ndio mahali sahihi, kama hata makanisa na misikiti yameshindwa vyuo ndio vitaweza..! lakini sheria inaweza mlazimisha mtu awe muadilifu hata kama hataki! so sio ishu ya mafunzo.
Unafahamu kitu inaitwa organisation behavior and culture?
 
Binafsi nimeshangaa kusikia takribani makampuni 17,446 yamepeleka financial statements wakideclare profit ndogo kule TRA at the same period profit kubwa kwenye banks zao wanakopewa mikopo.
Kuwa wide katika thiking, do not be limited by your bos JPM. Inawezekana kabisa wanafanya hivyobank kupata mkopo mikubwa. Turn out ya mapato ina determine ukubwa wa mkopo. Hivyo wanatumia nji hiyo kupata mikopo mkubwa!
 
Kuwa wide katika thiking, do not be limited by your bos JPM. Inawezekana kabisa wanafanya hivyobank kupata mkopo mikubwa. Turn out ya mapato ina determine ukubwa wa mkopo. Hivyo wanatumia nji hiyo kupata mikopo mkubwa!
Na TRA wanatumia njia hiyo hiyo kukusanya kodi ili kufikia malengo.

Kuidanganya bank ni kuidanganya serikali kwa kuwa banks zote zina dhamana ya BoT!
 
Back
Top Bottom