Rushwa imepeleka Kombe la Dunia Qatar, majuto yamebaki kwa mashabiki

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,357
8,069
Wakati Mashindano ya Kombe la Dunia 2022 yakiwa karibu kabisa kuanza, kupitia video fupi Mhariri wa uchambuzi kutoka shirika la habari la BBC Ros Atkin ameiongelea miaka ya tuhuma za rushwa ndani ya FIFA inayosadikiwa kupelekea Qatar kutunukiwa uwenyeji wa Kombe la Dunia 2022.

”Jumatatu iliyopita Rais wa zamani wa FIFA Sepp Blatter alitamka kuwa ”kufanya mashindano haya nchini Qatar ni kosa”

Jumanne, Balozi wa Kombe la Dunia nchini Qatar Khalid Salman alisema kuwa ”mahusiano ya jinsia moja ni uharibifu katika akili”

Swali kubwa ni je ”iliwezekanaje kwa nchi yenye watu milioni 3 , joto kali sana, na ambapo mahusiano ya jinsia moja ni kinyume na sheria kuchaguliwa kuwa wenyeji wa Kombe la Dunia?”

Kabla ya kupigwa kura, wanakamati wawili wa kamati kuu ya FIFA walitolewa baada ya uchunguzi uliofanywa na Sunday Times kubaini kuwa watu hao walikuwa wametoa ofa ya kuuza kura zao. Wanakamati wengine wote waliichagua Qatar na kuiacha Marekani ambayo ilionekana kupendwa zaidi.

Mwaka 2011 gazeti la Sunday Times liliripoti kuwa wanakamati wengine wawili walikuwa wamelipwa dola milioni moja na nusu kila mmoja ili kuipigia kura Qatar.

Siku chache baadae, barua pepe ilivuja iliyoonyesha Katibu wa FIFA wa kipindi kile Jerome Valcke akiwaongelea maafisa wa Qatar kwa kusema ”alidhani inawezekana kununua FIFA kama walivyonunua Kombe la Dunia.”

Kufikia mwaka 2012 uchunguzi mzito kuhusiana na mienendo ndani ya FIFA ulishaanza. Baadae ilijulikana kuwa FBI imekuwa ikiichunguza FIFA kwa miaka mingi na iligundua rushwa, utakatishaji fedha, malipo haramu yakiwa kama sehemu ya kufanya biashara ndani ya FIFA.

Hata hivyo mambo hayo hayakuhusiana moja kwa moja na jinsi Qatar iliyopata uwenyeji wa Kombe la Dunia.

Tunachofahamu ni kuwa hadi sasa wanakamati 11 kati ya 22 wa Kamati Kuu ya FiFA waliofikia uamuzi ule wamesimamishwa, kulipishwa faini, kufungiwa na wengine kushtakiwa kwa sababu mbalimbali.

Wiki hii Blatter amesema, "Ni hakika hii ilihusu pia pesa, kwa hili namaanisha nchi na siyo watu."

Miaka 12 baadae Qatar bado inakanusha kuhusika na lolote ambalo ni kinyume na sheria au maadili. Swali linabakia, kwanini mashindano haya yanafanyikia Qatar?
 
Kwahiyo kwakuwa Qatar inapinga mahusiano ya jinsia moja wazungu wanaona haikutakiwa kuwa mwenyeji wa World Cup?

Laana kabisa.
Marekani ina Mashoga wengi
Ushoga ni km utamaduni wao
Ila
Qatar hakuna mashoga
Ushoga sio utamaduni wao

Walioanza kulialia ni mashoga baada ya kuona wamezuiwa kwenda Qatar kwenda kufanya ushoga kwenye Kombe la Dunia
 
Hivi rushwa Huwa inaonekana pale tu marekani anaposhindwa, wamesahau kuhusu ujerumani alivyoshinda uwenyeji wa kombe la dunia dhidi ya Africa kusini

Marekani keshaona jinsi mpira wa miguu unavyopendwa Kwa hiyo anataka kuucontrol na kuingiza upuuzi wake wa mambo ya ushoga
 
Screenshot_20221113-172010.png
ukipata mda itafute hii documentary itazame. akikisha unaitazam kabla ya kuanza kwa kombe la dunia.
 
Mh! Hili laana mbona inaanza kututafuna!!? Hivi ipo ligalized kabisaa! Inabidi kuwe na kampeni kila nyumba kua ukihisi una mmoja mwenye laana hii nyumbani kwako fanya vile akili inakutuma bila jusita muwahishe hamna namna
 
Hivi rushwa Huwa inaonekana pale tu marekani anaposhindwa, wamesahau kuhusu ujerumani alivyoshinda uwenyeji wa kombe la dunia dhidi ya Africa kusini

Marekani keshaona jinsi mpira wa miguu unavyopendwa Kwa hiyo anataka kuucontrol na kuingiza upuuzi wake wa mambo ya ushoga
Juzi
USA walicheza na Germany wanawake mechi ya kirafiki ya Kimataifa, USA kafa Goli 2 kwa 1
 
Ivi awa majuba walishindwa ata kupeleka kombe la dunia China huko


Mimi sisapoti ushoga ila kombe la dunia quatar wamezingua sjui waliona nini huko hakuna ata mvuto aise.
 
Marekani kuna amsha amsha ila Ushoga mwingi,
Fata yako tu, na huenda hata huko limepelekwa kimkakati tu ili kueneza huo ushoga. Sema ndo ivo jamaa wamekaza hawataki hizo mambo.

Watawaandama na kuleta kashkash tu ili kwa namna moja au nyingine waeneze huo ushoga huko Qatar.

Pombe walikaza sasa wameirhusu kampuni moja kuiuza hadharani, hivyo ndivyo marekani wanataka.

Hata Qatar wakiruhusu hata kwa kiwango kidogo kwao ni furaha kubwa sana.
 
Back
Top Bottom