Rupia ya Mjerumani: Ni kweli sarafu hii ina thamani kubwa au ni story tu?

Hahahaha umenifanya nicheke nimemkumbuka jamaa yangu mmoja mkoani huko pita pita zangu nikamuona kakaa sehemu kama wana kikao vile chini ya mti yupo na wazee kibao kama kikao cha mwenyekiti wa mtaa vile...

Namuuliza hapo vipi kuna kitu gani eti ana niambia kuna rupia wamezipata eti wana jadili jinsi ya kuziuza..nilichoka kwa majibu yake halafu ni mtu wa heshima tu nilicho fanya ni kumuambia biashara njema huyo nikapotea maana hata ninge muelimisha kuhusu hayo mambo ningekuwa napoteza muda tu Maana asinge nielewa.

Sijui wale wajomba huwa wanatumia NGUVU za giza kuwatapeli watu au ni ujinga tu wa watu maana hata umuelimishe vipi mtu akuelewi mpaka akisha pigwa kwanza ndiyo akili ina mkaa sawa.
Mkuu yan sio bure lazma kuna ndele inahusika kupumbaza watu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa muda mrefu watu wamekuwa wakihangaika kuipata Rupia wakiamini watatajilika Leo nataka kuwafumbua macho

Katika biashara ya Rupia Kuna vitu viwili pengine ulikiwa hujui

Ukisikia mtu anatafuta rupia na anasema atainunua kwa pesa nyingi ujue hapo Kuna Mambo mawili

>UTAPELI

Au

>USHIRIKINA

Ipo hivi Kuna watu wanatafuta Rupia wanaamini wakiwa na rupia inatunza pesa hii hasa kwa wenye pesa za kishirikina huwa wanaaminishwa na waganga kuwa wakiipata Rupia itawasaidia kutunza pesa na kuvuta zingine ndiyo maana anaitafuta

Tofauti na hapo ni utapeli baadhi ya matapeli huwa wanatumia Rupia kutapeli watu huweza kujifanya anaitafuta kumbe anataka kukutapeli pesa zako na ukizubaa unapigwa kweli

Hivyo Basi hakuna maajabu yoyote kwenye Rupia zaidi ya ushirikina na utapeli kuwa makini

Soon ntawaletea Uzi jinsi unavyoweza kutapeliwa kupitia Rupia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu kwenye kikao ulishindwa kuuliza kwa nini ajauzwa toka mwaka 2014?
ukuomba uonyeshwe mzigo?

Maswali masuri sana, inaonekana hata yeye alikuwa akiskilizia hizo hela sema anavunga tu kwamba wenzake ndo walikuwa mandezi.mchongo kama huo ushaushtukia niwa kipuuzi since day one why uhudhurie vikao vyao kwa miezi sita?
 
Umetumia fasihi vzur kufikisha ujumbe , wachache watakuelewa, ila mm naongezea kuwa wataendelea kungojea neema ya rupia hadi 2025
 
Dah we acha tu mkuu yan sio kama nilishindwa kuuliza ila advertise niliyosikia kuhusu wapi mzigo ulipo nilichoka mwenyewe. Huyo mwamba alikuwa anatuambia mzigo upo Church flan hv lililopo karbu na hilo eneo, alafu kituko zaid kilichonishangaza eti anasema mzigo umepatikana kwa msaada wa maombi ya zaburi ya 106 kwahiyo ili tufanikishe kuuza inabidi kila siku tukikutana tuwe tunasali asbh na jion. Alafu pia members tukaambiwa tuwe wasafi tusiwe wachafu, yaani utakiwi kufuga nywele maeneo yote nyeti, usivae nguo nyeusi wala nyekundu pia usiwe mtu wa totozi sababu ya hayo yote eti mali haitaki uchafu. Yaan kulikuwa na mambo ya ajabu ajabu kwa kweli hata kwa logic ya kawaida unaona tu huu usanii na ushirikina tu, ajabu wenyewe walikuwa hawana wasiwasi wachekelea tu kwa story pori hizo

Sent using Jamii Forums mobile app
Jibu hili mkuu
Maswali masuri sana, inaonekana hata yeye alikuwa akiskilizia hizo hela sema anavunga tu kwamba wenzake ndo walikuwa mandezi.mchongo kama huo ushaushtukia niwa kipuuzi since day one why uhudhurie vikao vyao kwa miezi sita?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama una mzuka na haya makitu, bora uzame Dr Congo

Nasikia huko mali ni nje nje, japo kuna risk zake, lakini rupia ni hadithi za kusadikika
Habari za j2 members. Niende madani direct, kwanza niwape intro kdogo jinsi nilivyoanza kusikia hadithi za rupia. Mara ya kwanza nasikia hizi mambo ilikuwa 2008 wakati huo nipo college mkoa flan, siku hiyo tumechil room na washkaj ndipo nikasikia wanaongelea haya mambo ya rupia. Kwa jinsi walivyokuwa wanasimuliana nikaona kama wananitisha vile maana nikasikia hadi uzipate hizi mambo lazima uwe umeoga dawa za kutosha! Maana ni makitu flan hv kama yana miujiza miujiza vile. Finally story zao nikaamua kuzipuuza nikaona kama haziniusu vile


KUTAPELIWA SASA.

Baada kama ya miaka 9 kupita toka nisikie hizo mambo sasa ndo nikawa nimekutana nayo rasmi yametokea kwangu na kufanya kuandika huu uzi. Nakumbuka ilikuwa 2017 siku sikumbuki ila ilikuwa usiku nimechil zangu home natafakari life, nikapokea cm toka kwa aunt yangu tukasalimiana then ndo akanieleza kuhusu huu upuuzi. Akaniambia kuna mtu flan (sitomtaja jina kwa sababu) ila place yupo Dar na nafikiri mpaka leo wanaendelea na ndoto yao ya "alinacha".

Akaanza kuniambia ooh huyo mtu amepata rupia box zima amezitoa huko milima ya Kisarawe kwahiyo anatafuta members wajiunge nae wawe wengi ili akiziuza wapate kugawana pesa maana peke ake anasema hawezi kuzimaliza pesa ni nyingi atakazopata, hivyo anasema kila atakaejiunga itabidi atoe 20k kama ada ya kiingilio then atapata trillion 200 mgao zikishauzwa rupia. Me nilivyosikia habari za hela tu alarm ikalia kichwani nikajua hapa kuna kupigwa watu, ikabidi nimuulize "hv aunt hayo mambo unayaamini kweli?" akasema ndio ni kweli kuna padre amenihakikishia ni kweli na wote tumeshatoa kiingilio tayari sasa nilikuwa nakuomba wewe uwe unafatilia hili swala kama kuhudhuria vikao vyao na taratibu zao zingine maana si muda mrefu hela zitatoka tutakuwa matajiri.

Dah! Niliposikia hivyo nilihuzunika nikasema watu wameshapigwa hapa hivyo ili nisiwakatishe tamaa acha nikubali tu pia nifatilie kwa kina juu ya haya mambo nijue ni kweli au la

KUHUDHURIA VIKAO VYAO

Kiukweli wadau niwe muwazi tu ktk hili, yani inabidi ushukuru sana ukijaliwa maarifa ya kung'amua baadhi ya mambo hapa duniani maana kuna some people ni kama wamepigwa ndele vile. Siku hiyo nimefika kwenye kikao chao wenyewe walikuwa wanajadili jinsi ya kutumia pesa zao zikishatoka baada ya kuuza rupia, yani hapo kwenye eneo lao wanalokutania ni kama kwa mganga vile maana ni pemben ya mji wa Dar alafu nilisikitika baada ya kusikia kuna watu wametoka hadi mikoani wamekuja kuweka camp kabisa kuzisubiri pesa afu nikaambiwa wana miaka miwili wapo hapo hapo hawataki kurudi kwao wanaona kama watazikosa hela.

Yani ndugu zangu hii story ni ndefu sana nkisema niendelee kuchambua mambo niliyoyaona huko maana sikwenda siku moja kwenye hivyo vikao vyao, almost kama miezi kadhaa hv na kunifanya nijue kweli hii dunia ina vituko jamani mfano wa kituko kimoja kati ya vingi nilivyoshuhudia ni pale huyo mwamba wanaedai kapata hizo rupia... Alichukua chupa ya wine akaiweka juu ya mti wa mwembe then anawaambia watu kwenye hicho kikao eti hapa nimewekaa hii chupa ili kupata mawasiliano na nchi ya islael ili tukawauzie rupia zetu then people wakawa wanashangilia tu. Acha niishie hapa wazee ila mengine nitakuwa nawapa kulingana na comment zetu. Ila kifupi tu ni mpaka naandika huu uzi leo hii hao watu bado wanasubiri kuuza hizo rupia zao na wanaamini zipo watauza na wanamuamini huyo mtu wao wenyewe wanamwita mwalimu, ikimbukwe hapo hizo rupia wanazodai wamepata walizipata 2014 na mchakato wa kuuza pia ulianzia mwaka huo huo.

Kifupi me nilikacha kufatilia ujinga na nikamchana aunt kuwa hamna kitu kama hiko mmepigwa hela zenu tu na zaidi nikamwambia yule jamaa nahisi ana extra power anayotumia kupumbaza watu kwasabu haiwezekani 2014 hadi leo bado watu wanasubiri tu kama sio ndele ni nn sasa? Baada ya kumpanga sana ndo akaamini wamepigwa.


NB: nimesema tumepigwa sababu alichotoa aunt ndio sawa kama nimetoa mm



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani sio miaka 3 tena mkuu plus mpaka mwaka huu 2020 itakuwa 6 sasa maana juz kati nilishawafatilia kuuliza kama wameshauza rupia zao nikaambiwa bado hawajauza na bado wapo wanasubiri tu. Dah! Nawasikitikia sana wale watu maana wengi wao ni watu wazima na familia zao alafu wana waste time hawataki kurudi makwao wanasubiri kitu ambacho hakipo!.

Mkuu kuna siku nikipata muda wa kutype nitakuja na uzi mwingine kuhusu hao hao watu waliwai pia kuingizwa mkenge kwa habari ya "mercury" kama unaifaham au ushawai kusikia sikia, hii habari ya mercury niliipata kwa baadhi yao walinipa maana kwa muda niliokuwa naenda nilibahatika kujenga urafiki nao lengo ilikuwa kuwadadisi tu.

Pia nitawaletea uzi tena mwingine kuhusu vitu flan hv vinapatikana chini ya bahari vinaitwa "ambali na zinduna" kuwahusu hao hao people wenye imani kali ya kusubiri, ni vitu ambavyo wanasema ukivipata ni dili tena mara nyingi waganga ndo huwa wanavitumia ktk kutoa ndago za utajiri hivyo kupatikana kwake pia ni mziki lazma uwe vizuri na ww maana ni kama vitu vya maajabu ajabu tu. Yan wakuu kwa mda niliokaa nao hao watu nimepata kufahamu vitu vingi sana hasa hizi mali zilizofichika.
Sasa nani anayewahudumia msosi kwa kipindi chote hicho? Mana umedai wengine wametoka mikoani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za siku nyingi wana jf, mimi nina experience kidogo kuhusu rupia. kwanza story nyingi walizo post hapa ni uongo hakuna uchawi wa aina yoyote ile ambao unahusiana na hizo rupia. Rupia za kijerumani zipo na zinapatikana mimi binafsi ninazo 81pcs na zote ni silver, hazina uchawi wowote ni juhudi zako tu kuzitafuta kwa watu especial wazee mikoani wanazo...zangu zilikusanywa tabora.

Hazina bei sana ndio maana nimeamua kuziweka kwanza. unauza kwa coin collector Europe na America, zipo ambazo ni very rare kuzipata kama hiyo kwenye avatar yangu inaitwa Tabora pound bei yake kama 2000euro mpaka 5000euro depend na jamaa anayenunua na ni ya gold.

Sehemu nyingine unaweza kupata old coins ni kwenye magofu ya zamani, mimi ni hobby yangu kucollect old coins natafuta kwa kutumia metal detector...my last holiday nilikua kilwa for the same purpose. Hakuna shetani,jini,eagle wala nyoka ni story tu....ila its good story for me kwa sababu it makes easy to get coz wengine wanaogopa mizimu haa haaa.
At least una ka Idea kuhusu hii kitu ambayo ni sawa na Mega Busness.
 
Wadau,

Kuna watu huwa wanatafuta hivi vitu vya zamani, yaani pesa aina ya Rupia, noti/hela za zamani na Pasi za Mjerumani za zamani wakiamini kua watapata utajiri.

Mwenye uelewa naomba aje atusaidie hapa;

Utajiri unaopatikana na hivyo vitu hauna mashariti yoyote kama vile kutoa kafara?

Je ni utajiri wa nguvu za giza?

Msaada tafadhali juu ya hili maana huku napoishi mimi watu wanavitafuta sana na inasemekana kuna watu wamepata utajiri mkubwa sana kupitia Rupia, Pasi za Mjerumani na hizi noti za zamani sana za hapa nchini kwetu Tanzania.
Inawezakuwa na Masharti ya Maisha na inaweza isiwe na hayo Mashart ya matumizi na kwenye Masharti hutokea sana kwa awale wanao Batua hizo Rupia na siyo kila unayioona kuwa ni rupia Basi Kuwa ni deal.sarafu za kudeal nazo zenye uhakika ni Fanfumark,Rupia Nyekundu ya simba wawili,Rupia ya Kitumbua na Dinar tu.
 
MMOJA, Utapeli wa wazi huu. Mwenye akili hujiuliza iweje rupia ambayo hata mtoto mdogo aliweza kuishika kwenda nayo dukani itengenezwe kwa madini yenye thamani kubwa kuliko rupia yenyewe ilichoweza kukinunua dukani! Wajinga ndio.........?
Tatizo una elimu ndogo kwenye hii field ndiyo maana unapinga kila kitu.
 
hata mimi nilivutiwa sana na simulizi za rupia, sina zaidi ndio maana nikaleta hapa lakini naona kama vile sio watu wengi wanafahamu hii habari ya rupia
Ni kweli Kabisa siyo wengi wenye uelewampana juu ya hii Field ya rupia.
 
Tatizo una elimu ndogo kwenye hii field ndiyo maana unapinga kila kitu.
anashindwa kujiuliza coin ya sh 500 hii ya mwanzo kwanini watu walikuwa wananunua ila sasa hivi hamna anayetaka
 
Back
Top Bottom