RUKWA: Mtu mmoja auawa kwa kukatwa mapanga baada ya kufumaniwa na mke wa mtu

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Pius Luteko mkazi wa kijiji cha Nankanga mkoani Rukwa, ameuawa kwa kukatwa mapanga baada ya kufumaniwa akifanya mapenzi na mke wa mtu.

nyumbaaaa.jpg

Akithibitisha kutokea tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa George Kyando amesema tukio hilo lilitokea june 5 mwaka huu majira ya saa 11: 40 baada ya watuhumiwa watatu kumvizia mtu huyo na kufanikiwa kumkuta akifanya tendo la ndoa na mwanamke huyo kwenye pagala na kuchukua hatua ya kumkata mapanga kisogoni na kumsababishia kifo papo hapo.

Kamanda Kyando amesema baada ya kufanya mauaji hayo mmoja kati ya watu walioshiriki kufanya unyama huo alifanikiwa kukimbia na serikali ya kijiji iliwakamata watuhumiwa wawili akiwamo mume wa mwanamke huyo na kuwafikisha polisi.


Chanzo: IPP
 
Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Pius Luteko mkazi wa kijiji cha Nankanga mkoani Rukwa, ameuawa kwa kukatwa mapanga baada ya kufumaniwa akifanya mapenzi na mke wa mtu.

Chanzo: EATV
 
Wale wanawake wanaosemaga "kuchepuka raha" wachangie hapa,halikadhalika wale wanaume ambao badala yajuelekeza mapenzi yao kwa wake zao,wanatembea na wake za watu,ni hatari sana,hii huwa hatari ukikamatwa,ila usipokamatwa ndio maneno kama raha hutamalaki.
 
PAPUCHI KIBAO LAKINI BADO WATU WANAUANA KWA AJILI YA PAPUCHI.AU NDO ILE KAULI MKE WA MWENZIO MTAMU
 
Asingemuua angemuachia alama ili ajifunze hapo ukute ana mke wake, huo msiba mke wake anauchukulia vipi akipata mwanaume mwingine hata ndani yawiki aolewe tu hakuna namna huyo kajitakia kifo, R.I.P mgoni sijui muda wa kutubu aliupata au alishitukizwa na panga jamani!
 
Back
Top Bottom