Mchaka Mchaka
JF-Expert Member
- Jul 20, 2010
- 4,516
- 1,404
Ndoa kama hii iliyofanyika nchini Marekani itakuwa ruhsa kufanyika kanisani nchini Uingereza Monday, February 14, 2011 3:05 AM
Serikali ya nchini Uingereza inapitisha sheria wiki hii ambayo itabadili maana halisi ya ndoa na kufanunua kuwa ndoa si lazima iwe ni mwanamke na mwanaume bali watu wa jinsia moja nao wanaweza kuoana na pia ndoa zao kufungwa kanisani. Watu wa jinsia moja wataweza kufunga ndoa kanisani kwa mujibu wa sheria mpya zinazotarajiwa kutangazwa wiki hii nchini Uingereza.
Mashoga na wasagaji wataweza kufunga ndoa kanisani na sherehe zao zitaongozwa na wachungaji na viongozi wengine wa dini.
Mbali ya ruhusa hiyo, serikali ya Uingereza ina mpango wa kuibadili maana ya ndoa katika katiba ambapo ndoa ilikuwa ikijulikana kuwa ni kati ya watu wa jinsia mbili tofauti, mwanamke na mwanaume.
Sheria hiyo mpya itawawezesha wanaume kuwaita wanaume wenzao "Mume wangu" au "Mke wangu" hali kadhalika kwa wanawake nao wataweza kuitana mume na mke.
Kanisa la Anglikana limesema kuwa litakubalina na sheria hiyo na liko tayari kuruhusu majengo ya makanisa yake kutumika kuwafungisha ndoa mashoga na wasagaji.
Hata hivyo kanisa la Church of England limetangaza kuwa halitaruhusu ndoa kama hizo kufanyika kwenye makanisa yao.
Chama cha siasa cha Liberal Democrats ndicho kilichoipigia kampeni sheria hiyo ili kutimiza ahadi za usawa walizozitoa wakati wa kampeni ambazo ziliwafanya wapate kura nyingi kiasi cha kuweza kuunda serikali ya mseto na chama cha Conservative Party.
Jumuiya za kiislamu na jumuiya za kanisa katoliki zimeendelea kusisitiza kuwa mafundisho yao yanasema kuwa ndoa ni kati ya mwanaume na mwanamke.