Ruksa makampuni binafsi Tanzania kununua mabehewa ya reli

Kabla hawajafika kuchukua uamuzi huo wamefanya tafiti zozote? Na je wamejifunza nini kutoka DMT, KAMATA, UDA, SHIRIKA LA MELI, ATC nk

Njia za reli zitatumika kama barabara za TANROADS wanavyoweka mizani ili wenye magari mazito walipe ushuru.

Makampuni kama SIMBA CEMENT, BAKHRESA GROUP na METL Mohamed enterprise Tanzania Ltd wanauwezo wa kukarabati mabehewa chakavu 300 ya TRC au kukodisha mabehewa toka nje.

Kisha mabehewa ya kampuni binafsi kutumia njia za reli ya TRC ya mkoloni ambayo serikali ilikarabati kwa kuilipa malipo ya kutumia miundo mbinu ya reli ya TRC. Hiyo ndiyo dhana mpya shirikishi ya sekta binafsi na serikali ktk sekta ya reli.
 
Njia za reli zitatumika kama barabara za TANROADS wanavyoweka mizani ili wenye magari mazito walipe ushuru.

Makampuni kama SIMBA CEMENT, BAKHRESA GROUP na METL Mohamed enterprise Tanzania Ltd wanauwezo wa kukarabati mabehewa chakavu 300 ya TRC au kukodisha mabehewa toka nje.

Kisha mabehewa ya kampuni binafsi kutumia njia za reli ya TRC ya mkoloni ambayo serikali ilikarabati kwa kuilipa malipo ya kutumia miundo mbinu ya reli ya TRC. Hiyo ndiyo dhana mpya shirikishi ya sekta binafsi na serikali ktk sekta ya reli.
Ni kweli nia ya serikali inaweza kuwa njema, lakini ikumbukwe kuwa sekta binafsi ndiyo imekuwa ikihujumu miradi ya serikali, chukua mfano mdogo wa Tanesco inavyosulubiwa
 
Tatizo hii serikali inaweza kukugeuka wakati wowote na mibehewa ushainunua na huna pa kuipeleka.

Walichofanya kwenye korosho ni fundisho tosha.

Upo sahihi Mkuu, nakumbuka jinsi serikali ilivyoapa kupitia waziri wa uchukuzi Mh. Isack Kamwelwe kuwa watahakikisha shirika la ndege la Fastjet lisiinuke tena ili ndege za ATCL zisiwe na mpinzani ktk soko la usafirishaji wa anga.

Ni muhimu serikali kuwa na visheni sahihi jinsi ya kuhakikishia makampuni ya sekta binafsi ya watanzania na ya nje, imani kuwa haitatokea kiongozi wa kiserikali kukurupuka kutoa matamko kuhujumu wawekezaji wawe wa ndani au toka nje.
 
Back
Top Bottom