Ruksa makampuni binafsi Tanzania kununua mabehewa ya reli

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,031
23,821
December 13, 2019
Kemondo Bay, Tanzania

Serikali Kuanza Kuruhusu Makampuni kununua Mabehewa na Vichwa vya treni



Hatimaye serikali kupitia Waziri wa Uchukuzi Mh. Isaack Kamwelwe imetoa kauli kuwa itaruhusu kampuni binafsi kununua mabehewa / rolling stock na vichwa vya treni / Locomotives ili kuchochea ukuajia wa sekta ya reli nchini.

Serikali itajikita ktk kutengeneza na kuimarisha miundo mbinu ya reli, madaraja, signals, makalavati huku sekta binafsi wakitozwa ushuru mabehewa yao kutumia njia na mifumo ya reli.



Source: Millard Ayo
 
Wazo zuri sana, pikiendelea hivi naona fursa zaidi katika kukuza uchumi na upatikanaji wa ajira huku ikichagiza urahisi katika usafirishaji.
 
December 3, 2019

Hii inafuatia mjadala mkali JamiiForums juu ya nafasi ya sekta binafsi zihusishwe ktk sekta ya uchukuzi ya majini, angani na reli ktk jukwa hili hapo December 3, 2019





Sera ya kilimo ni kila Mtu kujilimia shamba lake, hakuna shamba la ujamaa au la kijiji.
Sasa wewe unataka serikali ikulimie??
Kwenye kujenga reli na miundo mbinu hilo ni jukumu la serikali ukitilia maanani hakuna mtu binafsi ktk Tz ambaye anauwezo wa kufanya huo uwekezaji mkubwa uwe wa ndege, meli, na uzalishaji umeme au tuseme nishati.
Mambo mengine yanaangaliwa kiusalama zaidi ya commercials

Azam marine, Fastjet n.k watu binafsi wana uwezo hata kuwekeza ktk reli lakini mnadanganywa na awamu ya tano.

Pia makampuni kama MOTL na Bahkresa Group wanaweza kuchangia rolling stock yaani kununua mabehewa kwa ajili ya usafirishaji mizigo reli ya mkoloni huku kampuni hizo ikilipa tozo kutumia miundo mbinu ya reli ya mkoloni iliyokarabatiwa.


Hii ni kuipunguzia mzigo serikali kununua mabehewa hata vichwa. Serikali kazi yake itakuwa kutunza reli ya mkoloni iliyokarabatiwa kwa gharama nafuu kuliko ujenzi wa SGR reli mpya.

Nchi nyingi dunia zinaendesha sekta ya reli kwa mtindo wa makampuni kushirikiana na serikali.
 
Lakini serkali iweze kucontrol hiyo Biashara

La sivyo itahujumiwa na wafanyabiashara
 
Si waanze na mradi wa mwendo kasi? Inamaana hawaoni mabasi machache na abiria ni wengi? Hii inapelekea huduma kuwa kero na karaha.

Waruhusu makampuni na watu binafsi waweke mabasi yao walipe tozo serikalini kwa kutumia miundo mbinu. Hiyo itatoa fursa kwa watu kupata usafiri wa uhakika na magari bora kabisa.

Vinginevyo wanataka mabasi yaendelee kubaki machache waendelee kunufaika kupita na magari yao huko kukwepa foleni.
 
Zambia Railways
Photo : TAZARA Tanzania Zambia Railways rolling stock

South African freight firm Calabash Freight will start using the Tanzania-Zambia Railway Authority (TAZARA) line under an agreement aimed at maximising the line’s usage, the rail company has said.

The line is an important route for copper exports from Zambia and the Democratic Republic of Congo (DRC), Africa’s top producer, but the firms transporting the metal struggle with rail capacity challenges.

TAZARA spokesman Conrad Simuchile said Zambia- and Tanzania-based Calabash Freight Ltd, which focuses on rail logistics, had already started conducting trial runs between the two countries.
Source: Zambia : South African firm Calabash Freight to use Tanzania-Zambia Railway
 
Yaani wawe kama kina Richard Branson eti
Hapo naona Bakhressa atatuma maombi


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Hapo awali serikali na shirika la Reli Tanzania (TRC) walikuwa na mkakati huu ambao ulikuwa siyo shirikishi na wadau wa sekta binafsi. Ni vizuri kuona serikali imengamua kuwa watu wakishirikishwa kwa mawazo basi maendeleo ya watu pia yanaweza kupatikana na pia kuipunguzia serikali mzigo wa kufanya biashar zote.

Serikali kununua vichwa 22, mabehewa 1,490 kwa ajili ya SGR
Daniel Samson 0825Hrs   Julai 08, 2019 Habari
  • Mabehewa hayo yanajumuisha 1,430 ya mizigo na 60 ya abiria.
  • Safari ya kwanza ya majaribio ya treni ya wahandisi yazinduliwa.
  • Wakazi wa Arusha, Moshi kuanza kutumia usafiri wa treni Desemba hii.
Dar es Salaam. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema Serikali imeanza mchakato wa ununuzi wa vichwa 22 vya treni na mabehewa 1,490 yatakayotumika katika uendeshaji wa reli ya kisasa (SGR) ambayo ujenzi wake unaendelea.
Mabehewa hayo yanajumuisha 1,430 ya mizigo na 60 ya abiria yatakayotumika katika reli hiyo, inayojengwa na kampuni ya Yapi Merkez ya Uturuki, kutoka Bandari ya Dar es Salaam hadi jijini Dodoma na baadaye hadi nchi za jirani za Rwanda, Burundi na Congo DRC.
Kamwelwe ameweka wazi mipango hiyo wakati akizindua safari ya kwanza ya majaribio ya treni ya wahandisi kwenye eneo la Soga lililopo Kibaha mkoani Pwani.
Amesema mpango wa sasa ni kuwa na Seti tano za treni za SGR zitakazokuwa na mabehewa nane ya abiria, mpango ambao unalenga kuimarisha sekta ya usafirishaji wa reli.
“Ndugu zangu Watanzania leo hii tumezindua majaribio ya njia ya reli yetu, hii ina maana kwamba tupo katika mipango ya kuhakikisha reli inakamilika kwa wakati, tumetembea kilomita 20 za majaribio, reli ni salama kabisa, haina kikwazo.
“Sasa tumeanza mchakato wa kununua vichwa vya treni 22 na mabehewa yake 60 ya abiria na 1,430 ya mizigo,” amesema Waziri huyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa amesema zoezi la majaribio ya awali ya treni ya wahandisi ni hatua muhimu ya kuhakikisha reli hiyo inapitika bila kikwazo kwani inakagua na kuimarisha miundombinu ya reli hiyo.


Amesema zoezi hilo la awali limekuja kufuatia kukamilika kwa baadhi ya maeneo ya kupita treni kuanzia Soga Wilayani Kibaha Mkoani Pwani, kuelekea Morogoro na kuongeza kuwa treni rasmi kwa ajili ya kupita reli hiyo itawasili hivi karibuni.


Mpango wa sasa ni kuwa na Seti tano za treni za SGR zitakazokuwa na mabehewa nane ya abiria, mpango ambao unalenga kuimarisha sekta ya usafirishaji wa reli. Picha|Mtandao

Katika hatua nyingine, Kadogosa amesema TRC imeanza kukarabati njia ya Reli ya kati ya kutoka Dar Es Salaam mpaka Isaka wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga ili kuimarisha reli hiyo zoezi ambalo lilianza Juni mwaka huu na kutarajia kukamilika mwaka 2020.

Katika Ukarabati huo shirika hilo linatarajia kufunga njia za reli hiyo kwa saa 72 kwa wiki ikiwa kwa muda wa miezi mitano kuanzia Julai hadi Novemba 2019.

Kutokana na ukarabati huo ambao umefadhiliwa na Benki ya Dunia (WB), Serikali inatarajiwa kupata hasara ya Sh1.8 bilioni kutokana na kupungua kwa muda wa kufanya kazi.

Amesema kwa treni za kawaida za mjini (Cummuter Train) za kutoka Kamata kwenda Ubungo na Pugu zitafanya kazi siku za Jumatatu hadi Ijumaa huku treni za kawaida (Ordinary Train) za kutoka Dar Es Salaam kwenda Kigoma, Mwanza na Mpanda zitafanya kazi siku za Jumatatu na Jumatano na treni za Deluxe kutoka Dar kwenda Kigoma zitakuwepo siku ya Jumanne pekee.

Amesema ukarabati mwingine wa njia ya reli kutoka Tanga kwenda Arusha ulianza mapema mwaka huu ambapo njia hiyo itaanza kutumika mwezi Desemba mwaka huu.

“Ndugu zangu wa mikoa ya Kaskazini mtaanza kunufaika na usafiri wa treni ya Abiria kuanzia Desemba mwaka huu, yaani Sikukuu za Krismas na mwaka mpya mtaenda nyumbani na treni ya abiria ya TRC,” amesema Kadogosa.

Source: Nukta | Serikali kununua vichwa 22, mabehewa 1,490 kwa ajili ya SGR
 
March 12, 2019

Taasisi zinazomvuruga kichwa Waziri wa Uchukuzi Mh. Isack Kamwelwe katika sekta ya uchukuzi wa reli

Tanzania Revenue Authority, Tanzania Ports Authorty na Tanzania Raiways Corporations hawapeani ushirikiano kuhakikisha sekta ya reli inafanya kazi kwa ufanisi bila kucheewesha mizigo. Pia TRC na mabehewa zaidi ya 300 yanayohitaji ukarabati mkubwa ili yaweze kuruditena relini kubeba mizigo.

 
December 6, 2019
Tazara Delivers First Consignment 1,160tons of Maize To Zimbabwe

A contract with the Grain Marketing Board (GMB) of Zimbabwe to transport 17,000 Metric Tons of maize from Makambako and Vwawa in Tanzania to Bulawayo in Zimbabwe. Under the agreed terms, TAZARA would load the commodity from Makambako and Vwawa and relay it to ZRL at New Kapiri Mposhi who would in turn pass it to NRZ at Livingstone, for final delivery to various destinations in Zimbabwe. Courtesy : Tazara



Source: Zimbabwe Railways
 
Kwa nini wasiruhusu makampuni binafsi kuwa na treni zao zishindane na za serikali katika kutoa huduma? Na huko ndiko kuboresha maisha ya watu

Kununua mabehewa bila kichwa cha treni ni sawa na kununua kondomu wakati huna mwanamke wa kuzitumia ......!! Wala hujui utampata lini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ruksa imetolewa kwa wawekezaji binafsi kununua vichwa na mabehewa ya mizigo pekee yake au hadi na yale ya abiria?
 
Hatimaye serikali kupitia Waziri wa Uchukuzi Mh. Isaack Kamwelwe imetoa kauli kuwa itaruhusu kampuni binafsi kununua mabehewa / rolling stock na vichwa vya treni / Locomotives ili kuchochea ukuajia wa sekta ya reli nchini.


Kabla hawajafika kuchukua uamuzi huo wamefanya tafiti zozote? Na je wamejifunza nini kutoka DMT, KAMATA, UDA, SHIRIKA LA MELI, ATC nk
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom