NYAMKANG'ILI
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 223
- 112
Uchaguzi ndani ya CCM utafanyika ngazi ya Wilaya nchini kote 29/09/2012. CCM imeandika barua kwa polisi ikiwaambia kwamba siku hiyo ya uchaguzi watatumia MALORI, PIKI2, MATREKTA, MAKWAMA, MABASI nk kusafirisha wajumbe kwenda maeneo ya kupigia kura na kwamba WASIBUGHUDHIWE. Kama inavyofahamika ni kuwa vyombo kama MALORI, MATREKTA na MAKWAMA haviruhusiwi kwa mujibu wa sheria (ROAD TRAFFIC ACT, 1975) kusafirisha mabiria bali mizigo. MASWALI ni je, polisi wataruhusu uvunjifu huu wa sheria utendwe na CCM? Je, kama ingekuwa ni vyama vingine vya siasa hali ingekuwaje? Je, kuna haki hapo? JE, kunaweza kukawapo amani bila usawa ktk jamii? Je, polisi haipaswi kutii sheria bila shuruti? nk