Katika awamu za sasa za uongozi viongozi toka mkoa wangu wameingia ktk kashfa kubwa na kuondoa heshima ya uaminifu na uasilifu wa wazee watangulizi wao kama Kinyondo, Rwabuti, Sir Kahama, Balozi Ruhinda, Mzee Kyaruzi, Rwegasira nk.
Karamagi aliingia kashfa ya Buzwagi kabla ya kuondoka na Richmond. Kagasheki alifurumishwa na operesheni Tokomeza. Wakati sisi wa mkoa wa Kagera tukianza kusahau ikaja baba wa Scandal "Escrow". Ukisikia majina utadhani ni akaunti labda ilifunguliwa Kagera Farmers Bank! Majina mengi ni ya kwetu.
Mbaya zaidi ni ukiwauliza mabilioni waliyafanyia nini kwetu, utaambiwa hakuna hata aliyeweka kibanda. Fedha wanawekeza maghorofa Dar na nyingine wanaficha nje ya nchi.
Wilaya pekee unapoona nyumba za kisasa ni Karagwe mkoa mzima. Bukoba ni nyumba zilizojengwa na wazee niliotaja mwanzoni na wenzao wa wakati huo, wa sasa wanaishia kuchafua jina la mkoa wakati mkoa unaishia kurudi nyuma kimaendeleo.
Karamagi aliingia kashfa ya Buzwagi kabla ya kuondoka na Richmond. Kagasheki alifurumishwa na operesheni Tokomeza. Wakati sisi wa mkoa wa Kagera tukianza kusahau ikaja baba wa Scandal "Escrow". Ukisikia majina utadhani ni akaunti labda ilifunguliwa Kagera Farmers Bank! Majina mengi ni ya kwetu.
Mbaya zaidi ni ukiwauliza mabilioni waliyafanyia nini kwetu, utaambiwa hakuna hata aliyeweka kibanda. Fedha wanawekeza maghorofa Dar na nyingine wanaficha nje ya nchi.
Wilaya pekee unapoona nyumba za kisasa ni Karagwe mkoa mzima. Bukoba ni nyumba zilizojengwa na wazee niliotaja mwanzoni na wenzao wa wakati huo, wa sasa wanaishia kuchafua jina la mkoa wakati mkoa unaishia kurudi nyuma kimaendeleo.