Rugemarila, Tibaijuka, Mujulizi, Ruhangisa, Rwabukoba ni kashfa nyingine kwa mkoa wa Kagera!

Kaguta

JF-Expert Member
Jan 31, 2013
414
504
Katika awamu za sasa za uongozi viongozi toka mkoa wangu wameingia ktk kashfa kubwa na kuondoa heshima ya uaminifu na uasilifu wa wazee watangulizi wao kama Kinyondo, Rwabuti, Sir Kahama, Balozi Ruhinda, Mzee Kyaruzi, Rwegasira nk.

Karamagi aliingia kashfa ya Buzwagi kabla ya kuondoka na Richmond. Kagasheki alifurumishwa na operesheni Tokomeza. Wakati sisi wa mkoa wa Kagera tukianza kusahau ikaja baba wa Scandal "Escrow". Ukisikia majina utadhani ni akaunti labda ilifunguliwa Kagera Farmers Bank! Majina mengi ni ya kwetu.

Mbaya zaidi ni ukiwauliza mabilioni waliyafanyia nini kwetu, utaambiwa hakuna hata aliyeweka kibanda. Fedha wanawekeza maghorofa Dar na nyingine wanaficha nje ya nchi.

Wilaya pekee unapoona nyumba za kisasa ni Karagwe mkoa mzima. Bukoba ni nyumba zilizojengwa na wazee niliotaja mwanzoni na wenzao wa wakati huo, wa sasa wanaishia kuchafua jina la mkoa wakati mkoa unaishia kurudi nyuma kimaendeleo.
 
Bora hao Chenge jee?kila ufisadi yumo na bariadi hakuna maendeleo kama ya chato yenye mbunge wa muda mfupi maghufuli
 
Inakuwa ngumu sana kwa watu wa Kagera na Kaskazini watu kuwaelewa kuhusu ufisadi.
 
Inakuwa ngumu sana kwa watu wa Kagera na Kaskazini watu kuwaelewa kuhusu ufisadi.

Siyo kweli, Mkoa wa Kagera hauna historia ya ufisadi. Isipokuwa udhaifu wa serikali za awamu hizi umefanya kuchungulia hili shamba la bibi. Ingawa hii kashfa ya sasa ni sawa hata kuiita Kagera scandal.
 
  • Thanks
Reactions: yok
Confirmed: Jana ilikuwa niandika thread ya namna hii nikashindwa ila nafurahi kuona kuwa mmeliona hili. Nilikuwa nimekaa na mchagga............akaropoka mbele ya wateja baa kuwa kwa sasa WAHAYA wezi kuliko WACHAGGA...............eti wachaga wanaiba fedha ndogo ila wao wanapiga Billions................kazi kunadika plate number zenye majina kwenye magari yao. Huku wasilite hela za wizi kutuletea laana........walete walizopiga kihalali.
 
Kwahiyo tatizo ni kutokujenga Kagera????

Kwani lazima wao Wajenge???.. Kama wao wameshindwa jenga wewe..
 
Kwani wakiwekeza dar tatizo liko wapi ama dar si Tz? uko poor minded sana na haujuhi unachokisema kuhusu kuwekeza,jiulize waliosoma shule za St.Mathew,Tusiime,Anne Marie,Marys na wale wa chuo cha Kairuki na hospitali yake wanavyoshukuru taasisi hizo na mchango wao katika Taifa.Wewe ulitaka vyote viende Kagera kwani dar sio watanzania? kwani kwenye hizi taasisi wahaya hawapati huduma ama mpaka wazipate huko kwao? fanya kazi na wewe ukawekeze vya kwako siyo kila kitu mnakalia kuja na hoja za kipuuzi kama hizo Kagera kama kwingine watanzania wote wanaruhusiwa kuwekeza ilimradi mtu kapenda,ukianza eti kila kabila wakawekeze kwao kuna maeneo mengine hawana uwezo na hayo si maendeleo bali ni ukabila
 
Mbna hao hawajaiba jaman.wamegawiw tu.alieba c anajulika.wengine walipewa kama family support tu
 
Kwahiyo tatizo ni kutokujenga Kagera????

Kwani lazima wao Wajenge???.. Kama wao wameshindwa jenga wewe..

Una uhakika sijajenga? tofauti yagu ni kwamba sijajengea jasho la watanzania.
 
wahaya wanazidi kunipa sababu za kulihama kabila lao..hawa jamaa wanachefua..
 
Wahaya ni wezi sana. Tanzania nzima hamna anayaewapata kwa wizi wa mali za umma
wewe nawe una lako jambo. Kwenye scandal hii.... werema, muhongo na maswi nao wanatoka mkoa mmoja, je nao tunawaweka wapi? Maana bila wao hao wahaya wasingepata pesa hizi. Na walio wengi wamegawiwa tu.... kugeneralize kwa kusema wahaya wote ni wezi ni makosa......
 
Kwani wakiwekeza dar tatizo liko wapi ama dar si Tz? uko poor minded sana na haujuhi unachokisema kuhusu kuwekeza,jiulize waliosoma shule za St.Mathew,Tusiime,Anne Marie,Marys na wale wa chuo cha Kairuki na hospitali yake wanavyoshukuru taasisi hizo na mchango wao katika Taifa.Wewe ulitaka vyote viende Kagera kwani dar sio watanzania? kwani kwenye hizi taasisi wahaya hawapati huduma ama mpaka wazipate huko kwao? fanya kazi na wewe ukawekeze vya kwako siyo kila kitu mnakalia kuja na hoja za kipuuzi kama hizo Kagera kama kwingine watanzania wote wanaruhusiwa kuwekeza ilimradi mtu kapenda,ukianza eti kila kabila wakawekeze kwao kuna maeneo mengine hawana uwezo na hayo si maendeleo bali ni ukabila

Unachonishambulia sikioni. Mkoa wa Kagera ulikuwa kwenye top three ya taifa hili kwa maendeleo, leo tuko namba 19! Hawa mafisadi hawakumbuki kuwekeza nyumbani. Huko nyuma siyo kwamba mkoa ulipendelewa bali wale wazee walipenda kwao, waliwekeza, walijenga nyumbani.
 
Confirmed: Jana ilikuwa niandika thread ya namna hii nikashindwa ila nafurahi kuona kuwa mmeliona hili. Nilikuwa nimekaa na mchagga............akaropoka mbele ya wateja baa kuwa kwa sasa WAHAYA wezi kuliko WACHAGGA...............eti wachaga wanaiba fedha ndogo ila wao wanapiga Billions................kazi kunadika plate number zenye majina kwenye magari yao. Huku wasilite hela za wizi kutuletea laana........walete walizopiga kihalali.
Wahaya mlianza zamani, kibaya sasa ni kwamba mmewaingiza mkengeni watani zenu toka Kanda Maalumu.
 
Confirmed: Jana ilikuwa niandika thread ya namna hii nikashindwa ila nafurahi kuona kuwa mmeliona hili. Nilikuwa nimekaa na mchagga............akaropoka mbele ya wateja baa kuwa kwa sasa WAHAYA wezi kuliko WACHAGGA...............eti wachaga wanaiba fedha ndogo ila wao wanapiga Billions................kazi kunadika plate number zenye majina kwenye magari yao. Huku wasilite hela za wizi kutuletea laana........walete walizopiga kihalali.

Ta Muganyizi, With due respect your observation has made me low. Did not expect a man your caliber to meet trouble half way. There's a been a silent move phobia and stereotype against some tribes of Bahaya and Wachagga have been highly victimized. Do not succumb to such phobia. Katika hili la ESCROW tusubiri both CAG and PCCB resports ziwekwe wazi na hapo ndipo tutaambiwa VIP maana sitaki personalize hii issue as the former is living personality legally kwa kuuza 30% of his and paying to TRA legal taxes bado anastahili kuitwa mwizi. Tutapenda wabunge watuambie through both reports and in their wisdom due process was in place and followed to the letter. Na hapo ndio tutajua aliyeuza 30% kweupe na aliyenunua 70% za Mechmar kwa Tsh.6m, ni nani amesababisha hasara kwa Taifa. Tuwe na subira kabla ya kuwapa watu majina mabaya. Ukisikia mtu kama rafiki yako Mchaga anasema hivyo ujue anafikiri two wrongs make right. Wachaga kama ni wezi maana na hilo siwezi kulitolea conclusion basi hawawezi kutakasika kwa wizi wa Wahaya uwe wa kweli au wa kupikwa kama ilivyo kwa wizi wa wengine hauwezi kuwa confession stage ya wengine
 
thread ina shibe japo wasio gt huenda wakaiona ni upuuzi!

Don't blind whoever has posted the thread. He might have something tangible but the presentation depicts nothing except poor analysis coupled with prejudice, biasness, phobia and stereotype. To this effect the thread makes people discuss bahaya and not the scandal. Hii kitu ni sawa na mchezo pin pong ndani ya chumba. Lazima kuwepo na parties. With ESCROW kuna BOT, TANESCO na IPTL . Kwa mtu ambaye hana hila ndani mwake lazima aeleze kwa ufasaha ushiri wao na nani alikubali na kwanini. Kwanini badaaela ya kuangalia VIP kama corpote entity kuna ushabiki wa kumwngelea Rugemalira. Tunatakiwa kutoka kwenye upofu wa aina hii na tuvae miwani inayoona mbali. Jukwaa hili ndipo tutakuwa tumelitendea haki kwa sasa na siku zijazo. Tuache habari za kusikia vijiweni na tutafute official reports na sasa ziko bungeni.
 
Ta Muganyizi, With due respect your observation has made me low. Did not expect a man your caliber to meet trouble half way. There's a been a silent move phobia and stereotype against some tribes of Bahaya and Wachagga have been highly victimized. Do not succumb to such phobia. Katika hili la ESCROW tusubiri both CAG and PCCB resports ziwekwe wazi na hapo ndipo tutaambiwa VIP maana sitaki personalize hii issue as the former is living personality legally kwa kuuza 30% of his and paying to TRA legal taxes bado anastahili kuitwa mwizi. Tutapenda wabunge watuambie through both reports and in their wisdom due process was in place and followed to the letter. Na hapo ndio tutajua aliyeuza 30% kweupe na aliyenunua 70% za Mechmar kwa Tsh.6m, ni nani amesababisha hasara kwa Taifa. Tuwe na subira kabla ya kuwapa watu majina mabaya. Ukisikia mtu kama rafiki yako Mchaga anasema hivyo ujue anafikiri two wrongs make right. Wachaga kama ni wezi maana na hilo siwezi kulitolea conclusion basi hawawezi kutakasika kwa wizi wa Wahaya uwe wa kweli au wa kupikwa kama ilivyo kwa wizi wa wengine hauwezi kuwa confession stage ya wengine

Well said kiongozi.umeongea point sana.atakae kuelewa akuelew na asiekuelewa atakua na yake
 
18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom