Rufaa ya Lema: Nini kinaendelea!?

Mjuni Lwambo

JF-Expert Member
Apr 25, 2012
9,387
8,835
Kwa yeyote mwenye habari kuhusu nini kinaendelea juu ya chadema kukata rufaa katika kesi iliyomuengua ubunge Godbless Jonathan Lema naomba anihabarishe, Kwa mujibu wa gazeti la mwananchi la tarehe 6 april,2012, kulikuwa na mkanganyiko katika hukumu na chadema walitangaza kukata rufaa. Likimnukuu mwanasheria wa upande wa mlalamikiwa bwana method kimomogolo, linasema kuwa Mheshimiwa Lema alipatikana na hatia ya kutenda makosa yanayojulikana kisheria kama illegal campaining( kifungu namba 108) ambayo humruhusu alieenguliwa kugombea tena, lakini katika hali ya kutatanisha katika ku sum up hukumu jaji alimhukumu Lema kwa kutumia makosa yajulikanayo kama illegal practice (kifungu namba 114) ambayo hayamruhusu aliyeenguliwa kugombea tena, hivyo basi kuwa na ulazima wa pekee kwa chadema kukata rufaa. je wameshakata au ni nini kinaendelea?.
 
Tuliza munkari majaji ywa mahakama ya rufaa wanapitia hukumu ya mahakama kuu na vifungu vilivotumika kutoa hukumu na kupitia ushahidi wa pande zote then watatoa hukumu yao!!
 
Hivi wakuu judgement ya appeal ina kikomo cha muda wa kutolewa tangu appeal inapofailiwa? I mean lazima ndani ya muda fulani lazima uamuzi utoke kama ilivyo kwa kesi za kawaida za uchaguzi?
 
Hivi wakuu judgement ya appeal ina kikomo cha muda wa kutolewa tangu appeal inapofailiwa? I mean lazima ndani ya muda fulani lazima uamuzi utoke kama ilivyo kwa kesi za kawaida za uchaguzi?

yeah mwaka mmoja ktk kesi kama ya lema ihusuyo kesi za election.
 
Kingmairo naungana nawe,what i see here jamaa walikuwa na njama tu ya kumvua ubunge kisha kumtoa kabisa kwenye medani ya siasa,ukiangalia mkanganyiko uliojitokeza kwenye mashtaka aliyofunguliwa nayo na aina ya hukumu+vifungu vilivyorejewa so wasije jichelewesha maksudi
 
Kesi za chaguzi zina muda maalum, kwa rufaa nimesahau kidogo, kesi ni within a year, rufaa nadhani ni within 6 months
 
Kwa yeyote mwenye habari kuhusu nini kinaendelea juu ya chadema kukata rufaa katika kesi iliyomuengua ubunge Godbless Jonathan Lema naomba anihabarishe, Kwa mujibu wa gazeti la mwananchi la tarehe 6 april,2012, kulikuwa na mkanganyiko katika hukumu na chadema walitangaza kukata rufaa. Likimnukuu mwanasheria wa upande wa mlalamikiwa bwana method kimomogolo, linasema kuwa Mheshimiwa Lema alipatikana na hatia ya kutenda makosa yanayojulikana kisheria kama illegal campaining( kifungu namba 108) ambayo humruhusu alieenguliwa kugombea tena, lakini katika hali ya kutatanisha katika ku sum up hukumu jaji alimhukumu Lema kwa kutumia makosa yajulikanayo kama illegal practice (kifungu namba 114) ambayo hayamruhusu aliyeenguliwa kugombea tena, hivyo basi kuwa na ulazima wa pekee kwa chadema kukata rufaa. je wameshakata au ni nini kinaendelea?.

Tunamshukuru Mungu kwa yote,ni kweli mda wa rufaa za uchagu ni ndani ya miezi sita.

Juu ya Mhe wetu kama itampendeza Mungu na mwanasheria kukamilisha kazi yake,tutarajie rufaa hiyo ianze kusikilizwa ndani ya wiki mbili zijazo.

Note:mimi si msemaji wa chama,japo napenda kutoa majibu kwa baadhi ya mambo kwa kidogo nachojua.
 
Tunamshukuru Mungu kwa yote,ni kweli mda wa rufaa za uchagu ni ndani ya miezi sita.

Juu ya Mhe wetu kama itampendeza Mungu na mwanasheria kukamilisha kazi yake,tutarajie rufaa hiyo ianze kusikilizwa ndani ya wiki mbili zijazo.

Note:mimi si msemaji wa chama,japo napenda kutoa majibu kwa baadhi ya mambo kwa kidogo nachojua.

Thanks mama tumekupata.
 
Back
Top Bottom