Rudisheni lugha ya Kiingereza shuleni kama lugha ya kufundishia

Tumedharau kiingereza na tunapoteza mno, wapo na wengine kama akina jpm waliochukia lugha hii na kuanzisha kampeni dhidi ya kiingereza ila ukweli unabaki palepale, lugha ya kiingereza ni muhimu kwa ajira za ndani au nje ya nchi ambapo kiingereza fasaha kinahitajika.
Lugha ya Kiingereza ndiyo iliyotujengea Tanzania. Waliosoma kwa kiingereza ndio wamejenga barabara, hospital , shule, viwanda.vyuo, mahoteli, magorofa, Wanatibu Wagonjwa kwa Elimu ya Kiingereza waliyopata hadi wanafanya upasuaji wa moyo na vichwa, Walianzisha Mabank, Posta, Simu, Miundo mbinu ya Maji, Mpangilio wa Ofisi za Umma na Mashirika. Hawajakosea.
Banda ya kuona tumeshindwa kuandaa Waalimu wa English ndio tunaona English Shuleni haifai.
Nilisoma kijijini enzi hiyo ya Mwalimu Primary nikabahatika kwenda Secondary Masomo yote kwa English. Nilijitahidi kusoma kwa bidii Novel na kujifunza English hakuna Somo nilikuwa sielewi na kujibu maswali yake sawasawa.
 
limekuwa gumzo kwa nini mawaziri na watu wanaojiweza wanapeleka watoto wao shule za kiingereza kwa gharama kuu wakati watoto wa masikini hawajaliwi katika shule za kata. sababu ni moja tuu ni kutafuta njia ya watoto wao waongee kiingereza vizuri kama ilivyokuwa enzi za darasa la nane .sasa badala ya kupigania kiingereza kirudishwe mashuleni msingini tunalalamika. watanzania wengi wanataka kiingereza kukiongea basi tukifanyie baby comeback mashuleni.

hivi mtanzania anaweza kujiajili mwenyewe katika nchi za watu wengine bila ya kujua lugha ya kiingereza? wasanii wetu hasa wachekeshaji mbona hawaendi kokote nje ya tanzania wakati wale wa kenya, ghana na Nigeria huenda popote pale kutafuta soko na kujiingizia dinari.

Wabunge wanalalamika kila kukicha eti wahitimu wa vyuo vikuu wengi husaga rami kutafuta ajira wakati huo huo hawaoni jinsi wakenya, waghana na Nigeria walivyo sambaa sehemu nyingi duniani wakijiari na kupata kazi kwa sababu moja tuu ya kujua lugha ya jumuia ya common wealth.

tungekuwa kiingereza ni lugha ya mtanzania ya pili Bongo flava muziki wake ungependwa africa yoooote na kuvuma kama vile enzi za CAVASHA ya zaire' jamani hata CNN, FOx na bbc mtoto ashindwe kujua nini kimetokea duniani.

Hongera sana mawaziri wote na wananchi wanaopeleka watoto wao english medium maana siku moja hawatashindwa kufanya kazi za ukatibu mkuu UN, AU,kuongoza mahakama za kimataifa,kupatanisha wagombanao, na kuchezesha mechi za world cup
Kiingereza mashuleni watafundishwa na nani? Maana, walimu nao hawakijui!
Kama kweli nchi inataka kuwa serious, waajiri walimu kutoka Uingereza au wapeleke walimu Uingereza wakasomee kufundisha kingereza fasaha mashuleni.
Chonde Chonde wasituletee waganda na wa Kenya! Wametuaribia kingereza!
Mfano utasikia Bathidai baada ya Beethidei (matamshi ovyo).
 
Mimi nimesema nitavaa hata magunia, lakini mtoto lazima aendelee kusoma shule ya mitalaa ya kiingereza. Hao viongozi wanajifanya wazalendo, lakini watoto wao wakiongea kiingereza wanatabasamu hadi jino la mwisho linaonekana. Nenda huko manyumbani mwao, wao na watoto wao wanaangalia DSTV na sio hizi local za michezo ya kina Mkojani. Halafu wakimaliza shule anayeajiriwa ni anayejua kiingereza fasaha.
😂😂hamna namna
 
Tafiti zimefanyika miaka na miaka. Lakini kwa sababu ya mentality ya kikoloni tumegoma kutumia kiswahili. Kuna professor mmoja anaitwa Martha Qorro, kafanya sana tafiti kuhusu jambo hili. Tafiti zake zimeonyesha kunafaids kubwa kutumia kiswahili kama lugha ya kufundishia.
... mbona huo utafiti hauendani na uhalisia?

Fanya utafiti mdogo; randomly choose a sample of Class 4 pupils from normal English medium schools. Similarly, choose a sample of Class 4 (of similar size) from the BEST Kiswahili medium schools. Perform some tests like mathematics, writing, and reading abilities as well as confidence, persuasion, general understanding of global issues, manner, etc. on those two samples. You will probably be surprised.

Nadhani alichofanya Profesa Qorro ni kufanyia utafiti wake ngazi za juu sekondari na elimu ya juu ambapo wanafunzi tayari walishapigika na kuchanganya lugha Kiswahili (msingi) then suddenly English (sekondari). Hapo matokeo lazima yawe na walakini. Hoja ni Kiingereza kianzie level za chini hadi za juu.
 
Mkuu tango, Kiingereza kina faida gani!Waliofanikia kimaisha wengi wao hawajasoma, wengine hata kuandika hawajui.


Wewe na kiingereza chako kimekufikisha wapi?
Hao waliofanikiwa bila elimu, ni wachache kati ya maelfu na maelfu ya ambao hawakusoma, ila waliosoma angalau wana kaunafuu kidogo wa maisha
 
... mbona huo utafiti hauendani na uhalisia?

Fanya utafiti mdogo; randomly choose a sample of Class 4 pupils from normal English medium schools. Similarly, choose a sample of Class 4 (of similar size) from the BEST Kiswahili medium schools. Perform some tests like mathematics, writing, and reading abilities as well as confidence, persuasion, general understanding of global issues, manner, etc. on those two samples. You will probably be surprised.

Nadhani alichofanya Profesa Qorro ni kufanyia utafiti wake ngazi za juu sekondari na elimu ya juu ambapo wanafunzi tayari walishapigika na kuchanganya lugha Kiswahili (msingi) then suddenly English (sekondari). Hapo matokeo lazima yawe na walakini. Hoja ni Kiingereza kianzie level za chini hadi za juu.

Nakuunga mkono hoja! Tunakosea kutupa kiingereza huku tukijua ukweli kuwa tunakihitaji katika elimu na maarifa kuliko kiswahili!!
 
Back
Top Bottom