"Rudi huko huko" au "Kalale huko unakotoka"... wanatarajia nini?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Hivi mpenzi wako au mwenza wako anapokasiria umekuwa ukichelewa chelewa nyumbani na hivyo anakujia juu na kukuambia rudi huko huko kweli anafikiria nini? Hivi ukiamua kugeuza mlangoni na kwenda "huko huko" hadi kesho yake au mtondogoo anaweza kukulaumu? Lakini pia kwaninii tufike mahali mtu atamani usilale nyumbani kwako mwenyewe? Nini kitamfanya mtu awe anachelewa nyumbani namna hiyo hadi kumfanya mwenzie atamani arudi "huko huko".

Hivi kweli wanaume wakirudi huko "wanakotoka" familia zitasalimika? Hivi wapo wanaume wanaowaambia wake zao au wenza wao "wakalale huko huko"?

Vipi wale wanaowaambia watoto wao hivyo?
 
hizo huwa zina sababishwa na hasira ambapo akikaa muda kidogo anakuwa mpole..na kwa upande wa mtoto akiambiwa hivyo basi baada ya muda utamuona mzazi anaanza tena kumtafuta hiyo yote ni sababu ya hasira tu
 
Hivi mpenzi wako au mwenza wako anapokasiria umekuwa ukichelewa chelewa nyumbani na hivyo anakujia juu na kukuambia rudi huko huko kweli anafikiria nini? Hivi ukiamua kugeuza mlangoni na kwenda "huko huko" hadi kesho yake au mtondogoo anaweza kukulaumu? Lakini pia kwaninii tufike mahali mtu atamani usilale nyumbani kwako mwenyewe? Nini kitamfanya mtu awe anachelewa nyumbani namna hiyo hadi kumfanya mwenzie atamani arudi "huko huko".

Hivi kweli wanaume wakirudi huko "wanakotoka" familia zitasalimika? Hivi wapo wanaume wanaowaambia wake zao au wenza wao "wakalale huko huko"?

Vipi wale wanaowaambia watoto wao hivyo?


IMO nafikiri ni hasira mara nyingi... na mwanaume akikuta kua Mkewe anamuambia hivo ajue kabisa hamtendei haki for yaonesha wazi huyo mwanamke bado anampenda... For angekua hampendi angefungua mlango kimya kimya bila hata lawama... na lawama yaweza kua more of kumsumbua kumtoa kitandani kuliko sababu ya kuchelewa... hapa mume asishangae mkewe akichongesha funguo na kumkabidhi ili walau asisumbuliwe usiku....

Kuhusu why wanaume wanachelewa siku zoote kurudi... hapa sababu ni lukuki kwa kweli tokana na kwamba matatizo ya ndoa hu-vary from one to another... sababu ya kuchelewa yaweza kua sababu ya Mke ama Mme ama Wooote.
 
Mwanakijiji,ngoja nikupe kisa cha ukweli.Jamaa yangu kuna siku alirudi usiku sana,mkewe akaleta hizo 'kalale huko huko'akagoma kufungua mlango.Jamaa alikuwa na landrover,all he did alichukua mnyororo akafunga kwenye mlango wa mbele akatia gia,vruuuuuuuu akaung'oa,mama akashtuka kishindo kutoka chumbani mlango wa mbele aliukuta barazani.Kilichofuata ni kibondo.Kesho yake namuuliza jamaa kulikoni,akasema 'nyumba yangu unifungie nje?'
 
Hivi mpenzi wako au mwenza wako anapokasiria umekuwa ukichelewa chelewa nyumbani na hivyo anakujia juu na kukuambia rudi huko huko kweli anafikiria nini?
Ni hasira hizo. Tabia imemkera kiasi kwamba anaona uende "hukohuko"!


Hivi ukiamua kugeuza mlangoni na kwenda "huko huko" hadi kesho yake au mtondogoo anaweza kukulaumu?
Yes. Atakulaumu kwa kuendeleza "irresponsibility"!


Lakini pia kwaninii tufike mahali mtu atamani usilale nyumbani kwako mwenyewe?
Very good question. Amependa tu kulala nje bila kujali consequences zake.

Nini kitamfanya mtu awe anachelewa nyumbani namna hiyo hadi kumfanya mwenzie atamani arudi "huko huko".
Affair....pombe....marafiki....labda ni watchman au muuguzi. Ana kazi za usiku...

Hivi kweli wanaume wakirudi huko "wanakotoka" familia zitasalimika?
Nope!

Hivi wapo wanaume wanaowaambia wake zao au wenza wao "wakalale huko huko"?
Yes! Tofauti ni ....pengine wengine wanarudi "huko huko" kama bado pako wazi. Wengine wanarudi kwa ndugu lawama ipungue nguvu.

Vipi wale wanaowaambia watoto wao hivyo?
Hasira pia! Tabia inakua imekithiri!
 
Nafikiri haya hii ni dhana hasi ambayo kama haimaanishi kuwa ulikotoka si pahala adilifu basi dhana hii haipo mbali na nadharia hii...na hii cancer ya mtu kukinai nyumbani kwake mwenyewe inachangiwa na mambo mengi..mojawapo ikiwa ni mhusika mojawapo(aliyebaki/anayetoka)...ila yatosha kabisa kusema hasira haina staha,hivyo lolote laweza kumtoka mtu pindi hasira ikimpata!
 
IMO nafikiri ni hasira mara nyingi... na mwanaume akikuta kua Mkewe anamuambia hivo ajue kabisa hamtendei haki for yaonesha wazi huyo mwanamke bado anampenda... For angekua hampendi angefungua mlango kimya kimya bila hata lawama... na lawama yaweza kua more of kumsumbua kumtoa kitandani kuliko sababu ya kuchelewa... hapa mume asishangae mkewe akichongesha funguo na kumkabidhi ili walau asisumbuliwe usiku....

Kuhusu why wanaume wanachelewa siku zoote kurudi... hapa sababu ni lukuki kwa kweli tokana na kwamba matatizo ya ndoa hu-vary from one to another... sababu ya kuchelewa yaweza kua sababu ya Mke ama Mme ama Wooote.

Bi Asha acha kutetea ukorofi,utamfungiaje nje mmeo eti ni mapenzi? What if anafukuzwa na majambazi,wakimuulia mlangoni utasemaje? unakumbuka kisa cha jamaa mmoja maarufu kwenye michezo aliyevunjika mguu akafa kisa anaruka ukuta aingie ndani baada ya mkewe kumfungia nje?ilitokea kimara mwaka juzi,do you remember that? Jamaa alikuwa mnyamwezi,last respects tulifanyia national stadium.
 
huwa wanakurupuka au wanajaribu kutumia udhaifu wake kwa kumfukuza au kumrudisha mtui alikotoka japo ni hatari zaidi kwani yatanengeneza mianya mingine isiyo na ulazima
 
Ukishaambiwa hivyo, dhubutu kuondoka ndo utakapojua kama anamaanisha au la!
 
Bi Asha acha kutetea ukorofi,utamfungiaje nje mmeo eti ni mapenzi? What if anafukuzwa na majambazi,wakimuulia mlangoni utasemaje? unakumbuka kisa cha jamaa mmoja maarufu kwenye michezo aliyevunjika mguu akafa kisa anaruka ukuta aingie ndani baada ya mkewe kumfungia nje?ilitokea kimara mwaka juzi,do you remember that? Jamaa alikuwa mnyamwezi,last respects tulifanyia national stadium.


Wanaume bana!!!!!!! Hamkosi sababu... Usiku wa manane unarudi nyumbani kwako... cha ajabu nini kukimbizwa na majambazi?? lol
 
Bi Asha acha kutetea ukorofi,utamfungiaje nje mmeo eti ni mapenzi? What if anafukuzwa na majambazi,wakimuulia mlangoni utasemaje? unakumbuka kisa cha jamaa mmoja maarufu kwenye michezo aliyevunjika mguu akafa kisa anaruka ukuta aingie ndani baada ya mkewe kumfungia nje?ilitokea kimara mwaka juzi,do you remember that? Jamaa alikuwa mnyamwezi,last respects tulifanyia national stadium.
Nadhani unamaanisha Charles Masanja..ryte??...Sikuwa najua kama alifungiwa nje na mkewe!!!
 
Hivi mpenzi wako au mwenza wako anapokasiria umekuwa ukichelewa chelewa nyumbani na hivyo anakujia juu na kukuambia rudi huko huko kweli anafikiria nini?
Ni hasira hizo. Tabia imemkera kiasi kwamba anaona uende "hukohuko"!


Hivi ukiamua kugeuza mlangoni na kwenda "huko huko" hadi kesho yake au mtondogoo anaweza kukulaumu?
Yes. Atakulaumu kwa kuendeleza "irresponsibility"!


Lakini pia kwaninii tufike mahali mtu atamani usilale nyumbani kwako mwenyewe?
Very good question. Amependa tu kulala nje bila kujali consequences zake.

Nini kitamfanya mtu awe anachelewa nyumbani namna hiyo hadi kumfanya mwenzie atamani arudi "huko huko".
Affair....pombe....marafiki....labda ni watchman au muuguzi. Ana kazi za usiku...

Hivi kweli wanaume wakirudi huko "wanakotoka" familia zitasalimika?
Nope!

Hivi wapo wanaume wanaowaambia wake zao au wenza wao "wakalale huko huko"?
Yes! Tofauti ni ....pengine wengine wanarudi "huko huko" kama bado pako wazi. Wengine wanarudi kwa ndugu lawama ipungue nguvu.

Vipi wale wanaowaambia watoto wao hivyo?
Hasira pia! Tabia inakua imekithiri!
haya ndugu naona uliipania hii mada
 
Bi Asha acha kutetea ukorofi,utamfungiaje nje mmeo eti ni mapenzi? What if anafukuzwa na majambazi,wakimuulia mlangoni utasemaje? unakumbuka kisa cha jamaa mmoja maarufu kwenye michezo aliyevunjika mguu akafa kisa anaruka ukuta aingie ndani baada ya mkewe kumfungia nje?ilitokea kimara mwaka juzi,do you remember that? Jamaa alikuwa mnyamwezi,last respects tulifanyia national stadium.

hahahahaaa Bishanga bana! Kwa hiyo akivamiwa akiwa njiani ndo itapendeza? Halafu huyo aliyeruka ukuta alijitakia mwenyewe for alijitia kuyaweza manyanga (sad), angepungukiwa nini endapo angejifanya mpole ili afunguliwe mlango? Au kwa nini asingeenda kulala hata kwa ndugu??
 
Wanaume bana!!!!!!! Hamkosi sababu... Usiku wa manane unarudi nyumbani kwako... cha ajabu nini kukimbizwa na majambazi?? lol

mmmmmmhhh cha ajabu nini kufukuzwa na majambazi........hii kali ya 2011!.....yaani mke wangu aniache nichinjiwe getini? Kisa mapenzi? Lol aanze yeye kuondoka kabla sijavunja mlango.
 
Hivi mpenzi wako au mwenza wako anapokasiria umekuwa ukichelewa chelewa nyumbani na hivyo anakujia juu na kukuambia rudi huko huko kweli anafikiria nini? Hivi ukiamua kugeuza mlangoni na kwenda "huko huko" hadi kesho yake au mtondogoo anaweza kukulaumu? Lakini pia kwaninii tufike mahali mtu atamani usilale nyumbani kwako mwenyewe? Nini kitamfanya mtu awe anachelewa nyumbani namna hiyo hadi kumfanya mwenzie atamani arudi "huko huko".

Hivi kweli wanaume wakirudi huko "wanakotoka" familia zitasalimika? Hivi wapo wanaume wanaowaambia wake zao au wenza wao "wakalale huko huko"?

Vipi wale wanaowaambia watoto wao hivyo?

Dah! Hii kitu imenikumbusha habari ya mkuu mmoja hivi (RIP).
Alichelewa kurudi home (sina hakika kama ilikuwa ndo kawaida yake). Mama akagoma kufungua mlango. Jamaa akaamua kupanga matofali ili adandie ukuta. Kwa bahati mbaya akaporomoka, akapelekwa hospitali, akapoteza maisha siku ya pili yake.
Sijui mkewe alifanyaje maskini!
 
hahahahaaa Bishanga bana! Kwa hiyo akivamiwa akiwa njiani ndo itapendeza? Halafu huyo aliyeruka ukuta alijitakia mwenyewe for alijitia kuyaweza manyanga (sad), angepungukiwa nini endapo angejifanya mpole ili afunguliwe mlango? Au kwa nini asingeenda kulala hata kwa ndugu??

tafazali Kipipi,nyumba nijenge mimi kulala nilale kwa jirani? Arrrrrrrrooooo tena usirudie kusema maneno hayo!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom