MAPOKEZI YA SHAKA USIPIME RUANGWA...KILA KONA WANACCM RAHA JUU YA RAHA.
Na Mwandishi Wetu, Ruangwa
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shaka Hamdu Shaka amepokelewa na mamia ya maelfu ya Wanachama wa CCM na Wananchi wa Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.
Shaka amewasili kwenye Wilaya hiyo akitokea katika Wilaya za Lindi Mjini na Lindi Vijijini ambapo amekuwa akiendelea na ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa Miradi ya maendeleo pamoja na kuangalia Uhai wa Chama hicho.
Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM alipokelewa katika eneo la Mandawa ambapo baada ya kuwasili shangwe kutoka kwa Wananchi waliokuwepo kwenye eneo hilo liliibuka huku baadhi ya akina mama walishindwa kuficha furaha zao kiasi cha kuamua kugalagala chini.
Katika eneo hilo la mapokezi Wananchi walipata nafasi ya kutoa shukrani zao kwa Shaka ambaye amefika kwenye Wilaya yao kwa ajili ya kushuhudia kazi kubwa na nzuri inayoendelea kufanywa na Serikali ya CCM Awamu ya Sita chini ya Uongozi mahiri wa Rais Samia Suluhu Hassan.
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi Hassan Ngoma ametumia nafasi hiyo kumueleza Shaka kwamba Wananchi wa Wilaya hiyo wameridhika na kazi inayofanywa na Rais Samia ya kuleta maendeleo kwenye nyanja mbalimbali."Katika Wilaya yetu tunashukuru Rais Samia, ameendelea kutuletea maendeleo, kwetu tunasema hatuna deni naye, Mama ameendelea kuupiga mwingi sana."
Ngoma aliendelea kusema "Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 tunasema Rais Samia asiwe na wasiwasi, Wananchi wa huku tumeshaamua kura zote ni za kwake. Rais Samia Samia ameongeza fedha za maendeleo kwenye Wilaya yetu,hivyo miradi ya maendeleo inaendelea kwa kasi kila Kona."
Wakati huo huo Shaka akiwa kwenye mapokezi hayo ameendelea kuwakikishia Wananchi kuwa Serikali ya CCM itaendelea kuwa kimbilio na suluhisho la changamoto kwa kuzitafutia ufumbuzi hatua kwa hatua. "Tunafahamu kuna kazi kubwa na nzuri inayoendelea kufanywa na serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan. Wananchi wenyewe tangu nimeingia Mkoa wa Lindi na leo niko hapa Ruangwa wanakiri Rais amekuwa chachu ya maendeleo.
Hamasa niliyoiona kwa CCM na Rais Samia Suluhu Hassan toka kwa wananchi tangu nimeingia mkoa wa Lindi na leo hapa Ruangwa ni kubwa sana. Hii ni ishara tosha kwamba serikali inafanya kazi nzuri ya kuwaletea wananchi maendeleo. Aidha, ni kielelezo tosha kwamba madiwani na Mbunge wenu Mheshimiwa Kassim Majaliwa wanafanya kazi nzuri sana, wapeni ushirikiano."
Baada ya mapokezi hayo Shaka na msafara wake amepata nafasi ya kutembelea miradi na kukagua ujenzi unaoendelea kwenye miradi hiyo ikiwemo ya ujenzi wa vituo vya Afya, miradi ya maji safi na salama, miradi ya ujenzi katika sekta ya elimu pamoja na kuzungumza na wanachama wa CCM katika ngazi ya mashina
Na Mwandishi Wetu, Ruangwa
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shaka Hamdu Shaka amepokelewa na mamia ya maelfu ya Wanachama wa CCM na Wananchi wa Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.
Shaka amewasili kwenye Wilaya hiyo akitokea katika Wilaya za Lindi Mjini na Lindi Vijijini ambapo amekuwa akiendelea na ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa Miradi ya maendeleo pamoja na kuangalia Uhai wa Chama hicho.
Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM alipokelewa katika eneo la Mandawa ambapo baada ya kuwasili shangwe kutoka kwa Wananchi waliokuwepo kwenye eneo hilo liliibuka huku baadhi ya akina mama walishindwa kuficha furaha zao kiasi cha kuamua kugalagala chini.
Katika eneo hilo la mapokezi Wananchi walipata nafasi ya kutoa shukrani zao kwa Shaka ambaye amefika kwenye Wilaya yao kwa ajili ya kushuhudia kazi kubwa na nzuri inayoendelea kufanywa na Serikali ya CCM Awamu ya Sita chini ya Uongozi mahiri wa Rais Samia Suluhu Hassan.
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi Hassan Ngoma ametumia nafasi hiyo kumueleza Shaka kwamba Wananchi wa Wilaya hiyo wameridhika na kazi inayofanywa na Rais Samia ya kuleta maendeleo kwenye nyanja mbalimbali."Katika Wilaya yetu tunashukuru Rais Samia, ameendelea kutuletea maendeleo, kwetu tunasema hatuna deni naye, Mama ameendelea kuupiga mwingi sana."
Ngoma aliendelea kusema "Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 tunasema Rais Samia asiwe na wasiwasi, Wananchi wa huku tumeshaamua kura zote ni za kwake. Rais Samia Samia ameongeza fedha za maendeleo kwenye Wilaya yetu,hivyo miradi ya maendeleo inaendelea kwa kasi kila Kona."
Wakati huo huo Shaka akiwa kwenye mapokezi hayo ameendelea kuwakikishia Wananchi kuwa Serikali ya CCM itaendelea kuwa kimbilio na suluhisho la changamoto kwa kuzitafutia ufumbuzi hatua kwa hatua. "Tunafahamu kuna kazi kubwa na nzuri inayoendelea kufanywa na serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan. Wananchi wenyewe tangu nimeingia Mkoa wa Lindi na leo niko hapa Ruangwa wanakiri Rais amekuwa chachu ya maendeleo.
Hamasa niliyoiona kwa CCM na Rais Samia Suluhu Hassan toka kwa wananchi tangu nimeingia mkoa wa Lindi na leo hapa Ruangwa ni kubwa sana. Hii ni ishara tosha kwamba serikali inafanya kazi nzuri ya kuwaletea wananchi maendeleo. Aidha, ni kielelezo tosha kwamba madiwani na Mbunge wenu Mheshimiwa Kassim Majaliwa wanafanya kazi nzuri sana, wapeni ushirikiano."
Baada ya mapokezi hayo Shaka na msafara wake amepata nafasi ya kutembelea miradi na kukagua ujenzi unaoendelea kwenye miradi hiyo ikiwemo ya ujenzi wa vituo vya Afya, miradi ya maji safi na salama, miradi ya ujenzi katika sekta ya elimu pamoja na kuzungumza na wanachama wa CCM katika ngazi ya mashina