Ruaha: Mwenyekiti wa kijiji atangaziwa polisi

Lua

JF-Expert Member
May 19, 2011
704
305
Baada ya wananchi wiki iliyopita kuandamana kwa kumkataa mwenyekiti wa kijiji aliyeteuliwa na CCM kukabidhiwa ofisi, hatimaye leo mkurugenzi wa wilaya pamoja na mkuu wa wilaya ya Kilosa wamemteua na kumtangaza mwenyekiti wa kijiji katika kituo cha polisi cha Ruembe K2, badala ya kwenda kumtangaza kwa wananchi.

Nimeongea na wananchi wa Ruaha wanasema huyo ni mwenyekiti wa kijiji wa polisi na si wa wananchi.

Nawasilisha.

Muda si mrefu uliopita, Viongozi wa CCM chini ya Mkuu wa wilaya ya Kilosa wamemtawaza Ndugu Kisaluni kuwa mwenyekiti wa kijiji, kinyume na Kanuni za uchaguzI wa serikali za mitaa. ZoezI hilo limefanyika mbele ya zaidi ya polisi 50 katka kituo cha polisi Ruhembe.

Tangu uchaguzi ufanyike kwa kumuengua mgombea wa CHADEMA bila sababu, wananchi wameapa kumkataa mwenyekiti huyo wa CCM kupitia mkutano mkuu.

Hata hivyo kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa mitaa, tayari siku 7 zimepita tangu tarehe ya uchaguzi 28/04. hivyo mwenyekiti huyo hana uhalali.

DURU ZA NDANI zinasema kawaida kiwanda cha sukari hutoa mamilion kwa maendeleo na hivyo CCM wamefanya juu chini kumweka mtu wao ili wapige pesa. Nitawa-update.

SOURCE: Me
 
Kuna mtu kanisimulia, nimecheka sana. Masikini CCM, wewe mtu na akili yako unawaacha akina NAPE, MWIGULU na LUSINDE eti ndio nguzo za chama. Na wazee nao wameshajichokea wengine wanaleta vurugu makanisani akina Job Lusinde za huku wameachana nazo.....
 
Hicho kijiji kina madini au? Mbona dola imkikomalia sana?
 
CCM mimi nawashangaa kwani hamna watu wa kuwashauri polisi ni watu wachache sana tukiamua hata leo kituo hicho na hao mawatch men kitabaki historia. waacheni wananchi wafanye democrasia jamini
 
Hivi masisiem yna nini vichwani mwao???kwa nini wanaleta uchochezi hapa nchini?kama wananchi wamewakataa mnalazimisha ili iweje....kwa taarifa yenu hata msafishwe kwa jiki mnanuka uvundo na raia hawataki madhalimu...
 
Hicho kijiji kina madini au? Mbona dola imkikomalia sana?

Unaambiwa ni Kijiji chenye Kiwanda cha sukari ambacho hakikuuzwa kimebaki kuwa mradi wa wakubwa waliokoo CCM makao makuu ni ulaji unafanya wakiuke na kuvunja haki za binadamu kiasi hicho
 
:biggrin1: eti wamemtangazia polisi!! na bora ofisi zake zikae humo humo polisi lasivyo awe tayari kuchezea kichapo
safi sana wananchi,huu ndio uzalendo wa kutetea HAKI.....awe mwenyekiti wa polisisiem na report ampelekee shemeji yake gamba chair!!!
 
Kwa hiyo atakuwa anaongoza wananchi au atakuwa anawaongoza polisi? kweli akili ndogo
kuongoza akili kubwa ni tatizo'
 
endeleeni kudanganyana hapo.. CCM inaongoza nchi halafu ing'ang'anie kijiji kimoja kwa shida gani???
 
Back
Top Bottom