My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,932
- 13,283
Kuna vijana watano wapo mahabusu ya Kituo cha Polisi cha Bugarama wilaya ya Msalala wanateswa kikatili, walikamatwa siku zaidi ya kumi zilizopita wakituhumiwa kuiba TV ya hawara yake na Polisi.
Wanatishiwa kupewa kesi ya ujambazi wa kutumia silaha endapo hawatakiri kuiba hiyo TV.
Taarifa za uhakika kutoka kwa Police asiye na cheo aliyepo kituoni hapo ambaye ana hofu ya Mungu na ameumia kushuhudia ukatili huo zinadai kuwa, Police katili wanaowatesa vijana hao wamewaambia kuwa watawapeleka msituni na kuwapiga risasi kisha waseme kuwa walikuwa wakipambana na majambazi na kuwaua baada ya kuwazidi nguvu.
Nakutaarifu ili usije kupewa Report ya uongo na OCD kuwa wameua majambazi kumbe ni vijana hao.
Nyie Police wa Tanzania,mtavunja sheria hadi lini? Yaani mnawatesa Watanzania mtakavyo, ni kawaida yenu,yaani mnakamata watu bila kuwafikisha Mahakamani na mnawatesa,ndo maana sijawahi kuona Police mwenye mwisho mzuri Tanzania,wengi wenu hata mkistaafu mnataabika sana, kwa sababu mikono yenu ina Damu za watu wasio na hatia na mmeua watu wengi mno wasio na hatia.
Yaani mnashikilia watu na kuwatesa siku kumi bila kuwafikisha Mahakamani?
Ukatili gani huu?
Watanzania ndo mjue bila CCM kuondolewa madarakani mtaendelea kuteswa tu, hawa Police wanavunja sheria wakidekezwa na Serikali ya CCM.
Ila uonevu huu una mwisho, The day is coming in which you'll pay the price.
Wanatishiwa kupewa kesi ya ujambazi wa kutumia silaha endapo hawatakiri kuiba hiyo TV.
Taarifa za uhakika kutoka kwa Police asiye na cheo aliyepo kituoni hapo ambaye ana hofu ya Mungu na ameumia kushuhudia ukatili huo zinadai kuwa, Police katili wanaowatesa vijana hao wamewaambia kuwa watawapeleka msituni na kuwapiga risasi kisha waseme kuwa walikuwa wakipambana na majambazi na kuwaua baada ya kuwazidi nguvu.
Nakutaarifu ili usije kupewa Report ya uongo na OCD kuwa wameua majambazi kumbe ni vijana hao.
Nyie Police wa Tanzania,mtavunja sheria hadi lini? Yaani mnawatesa Watanzania mtakavyo, ni kawaida yenu,yaani mnakamata watu bila kuwafikisha Mahakamani na mnawatesa,ndo maana sijawahi kuona Police mwenye mwisho mzuri Tanzania,wengi wenu hata mkistaafu mnataabika sana, kwa sababu mikono yenu ina Damu za watu wasio na hatia na mmeua watu wengi mno wasio na hatia.
Yaani mnashikilia watu na kuwatesa siku kumi bila kuwafikisha Mahakamani?
Ukatili gani huu?
Watanzania ndo mjue bila CCM kuondolewa madarakani mtaendelea kuteswa tu, hawa Police wanavunja sheria wakidekezwa na Serikali ya CCM.
Ila uonevu huu una mwisho, The day is coming in which you'll pay the price.