Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Sakata la Mwanaume,Moses Palangyo mkazi wa kijiji cha Kilinga Wilayani Arumeru kumuuwa kinyama kwa shoka mwanamke anayedaiwa kuwa mke wake, Mary Richard Mushi(24) limechukua sura mpya Mara baada ya jeshi la polisi mkoani hapa kuapa kumsaka mtuhumiwa huyo uvungu kwa uvungu nyumba kwa nyumba na kumtaka ajisalimishe akiwa hai popote alipo.
Akiongea na Vyombo Vya Habari ofisini kwake,mkuu wa jeshi hilo Mkoa wa Arusha,Jonathan Shana amesema kuwa kitendo kilichofanya na mtuhumiwa huyo ni cha kinyama na halikubaliki na kumtaka mtuhumiwa huyo popote alipo ajisalimishe kabla jeshi hilo halijatumia nguvu kubwa kumsaka.
"Nawahakikishia polisi tumeingia kazini tutamkamata mtuhumiwa muda sio mrefu ,tutatumia style ya dog kunusanusa na kama yupo juu ya mti tutatumia nyani style kufuata alipo na kama yupo pangoni tutapiga mpaka atatoka" amesema Shana
Kwa mujibu wa kamanda Shana ,tukio hilo limetokea Jana Majira ya SAA NNE asubuhi huku chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika huku taarifa za awali zikiwa bado zinatatanisha .
Kamanda ameeleza kuwa baadhi ya wakazi wa eneo hilo waliohojiwa na polisi wamedai kuwa wapenzi hao walikuwa na mgogoro wa kifamilia na kupelekea Mke kukimbilia kwa Wazazi wake huku taarifa zingine zikidai huenda ni wivu wa mapenzi.
Amewataka wananchi kusaidia kumfichua mhalifu huyo na kwamba iwapo kama kuna MTU atakuwa amemficha atachukuliwa hatua Kali za kisheria.
Katika hatua nyingine kamanda Shana ameeleza hali ya utulivu imetawaka katika Mkoa wa Arusha katika kipindi cha sikukuu ya X mass na kwamba wananchi wamesherehekea bila kuwepo kwa matukio ya uvunjifu wa Amani.
Akiongea na Vyombo Vya Habari ofisini kwake,mkuu wa jeshi hilo Mkoa wa Arusha,Jonathan Shana amesema kuwa kitendo kilichofanya na mtuhumiwa huyo ni cha kinyama na halikubaliki na kumtaka mtuhumiwa huyo popote alipo ajisalimishe kabla jeshi hilo halijatumia nguvu kubwa kumsaka.
"Nawahakikishia polisi tumeingia kazini tutamkamata mtuhumiwa muda sio mrefu ,tutatumia style ya dog kunusanusa na kama yupo juu ya mti tutatumia nyani style kufuata alipo na kama yupo pangoni tutapiga mpaka atatoka" amesema Shana
Kwa mujibu wa kamanda Shana ,tukio hilo limetokea Jana Majira ya SAA NNE asubuhi huku chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika huku taarifa za awali zikiwa bado zinatatanisha .
Kamanda ameeleza kuwa baadhi ya wakazi wa eneo hilo waliohojiwa na polisi wamedai kuwa wapenzi hao walikuwa na mgogoro wa kifamilia na kupelekea Mke kukimbilia kwa Wazazi wake huku taarifa zingine zikidai huenda ni wivu wa mapenzi.
Amewataka wananchi kusaidia kumfichua mhalifu huyo na kwamba iwapo kama kuna MTU atakuwa amemficha atachukuliwa hatua Kali za kisheria.
Katika hatua nyingine kamanda Shana ameeleza hali ya utulivu imetawaka katika Mkoa wa Arusha katika kipindi cha sikukuu ya X mass na kwamba wananchi wamesherehekea bila kuwepo kwa matukio ya uvunjifu wa Amani.