voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,551
- 11,881
Nilikuwa mmoja wa wale tulioangalia Royal Tour Documentary huko YouTube.
Na leo nimeangalia hii Royal Tour inayozinduliwa Dar es salaam mbele ya Marais wetu wawili.
Rais Samia wa JMT na Rais Mwinyi wa Zanzibar.
Wakiwa na wageni mbalimbali wa kitaifa na kimataifa wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania.
Pamoja na viongozi mbalimbali waandamizi wa kiserikali na kisiasa.
Kuna tofauti kubwa kati ya ile iliyoko YouTube na hii ya Dsm.
Kile kipande ambacho muongoza filamu anamsema Magufuli alikuwa mkono wa chuma na maarufu kama Bulldozer.
Kwamba alikuwa akiidharau Covid19 na Rais Samia anajibu.....
"usisahau alikuwa mkemia pia!"
Baadae Peter Greenberg anamsema.....
"Samia aliingia Madarakani baada ya kifo cha Magufuli ambacho serikali ilitangaza kilisababishwa na ugonjwa wa Moyo wakati Magufuli alifariki kwa kutokana na Covid19"
Je serikali imeogopa nini hadi kukikata kipande hicho wakati kule Marekani na Ulaya,wao wanaangalia original yenye hayo maneno!
Tutaendelea kudanganywa na serikali mpaka lini?
Kama mnatudanganya kwenye mambo ya wazi kama haya ambayo tayari yako hewani.
Itakuwaje yale yaliyoko ndani ya makabrasha ya maofisi yenu?
Itakuwaje kwenye mambo ya mikataba mikubwa yenye maslahi makubwa kwa watanzania?
Je tuendelee kuwaamini serikali kwa lipi?
Na leo nimeangalia hii Royal Tour inayozinduliwa Dar es salaam mbele ya Marais wetu wawili.
Rais Samia wa JMT na Rais Mwinyi wa Zanzibar.
Wakiwa na wageni mbalimbali wa kitaifa na kimataifa wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania.
Pamoja na viongozi mbalimbali waandamizi wa kiserikali na kisiasa.
Kuna tofauti kubwa kati ya ile iliyoko YouTube na hii ya Dsm.
Kile kipande ambacho muongoza filamu anamsema Magufuli alikuwa mkono wa chuma na maarufu kama Bulldozer.
Kwamba alikuwa akiidharau Covid19 na Rais Samia anajibu.....
"usisahau alikuwa mkemia pia!"
Baadae Peter Greenberg anamsema.....
"Samia aliingia Madarakani baada ya kifo cha Magufuli ambacho serikali ilitangaza kilisababishwa na ugonjwa wa Moyo wakati Magufuli alifariki kwa kutokana na Covid19"
Je serikali imeogopa nini hadi kukikata kipande hicho wakati kule Marekani na Ulaya,wao wanaangalia original yenye hayo maneno!
Tutaendelea kudanganywa na serikali mpaka lini?
Kama mnatudanganya kwenye mambo ya wazi kama haya ambayo tayari yako hewani.
Itakuwaje yale yaliyoko ndani ya makabrasha ya maofisi yenu?
Itakuwaje kwenye mambo ya mikataba mikubwa yenye maslahi makubwa kwa watanzania?
Je tuendelee kuwaamini serikali kwa lipi?