Route za treni za Mwakyembe ndani ya jiji la Dar: TRL vs TAZARA

TRL

Treni hizi zitasimama kwenye vituo sita (6) vifuatavyo:

Stesheni ya Dar es Salaam, Kamata, Buguruni kwa Mnyamani, Tabata Matumbi, Mabibo na Ubungo Maziwa. Kila treni itakuwa na mabehewa sita yenye uwezo wa kubeba abiria waliokaa na wale waliosimama takriban 1,000 kila safari.

TAZARA:

vituo vya Dar es Salaam, Kwa fundi umeme, Yombo, Kwa Limboa, Lumo Kigilagila, Barabara ya Kitunda, Kipunguni B, Moshi Bar, Majohe, Shule ya Sekondari Magnus, Mwakanga, Chimwaga, Maputo, Mtoni relini, Kwa Azizi Ali relini hadi Kurasini. Kuanza kwa usafiri huu kutachangia kupunguza msongamano wa magari jijini Dar es Salaam na kuwezesha watu kufika katikati ya jiji haraka zaidi.
Kwa utaratibu huu inakisiwa kwamba treni hizi mbili zitaweza kusafirisha watu takriban 16,000 kwa siku kwa safari 8 asbi na 8 jioni
Izi project kuanza rasmi october 2012

Source:hotuba ya bajeti ya wizara 2012/13

Ministry of Transport, Tanzania - Publications | Waziri wa Uchukuzi awasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa mwaka 2012-13

Hivi ule mradi wa mabasi ya CRDB kubeba wanafunzi unaendeleaje?
 
339114993.jpg

Daladala Treni yaanza kufanya majaribio Dar es Salaam (picha zote Mwananchi Communications Ltd - facebook)
118349053.JPG

Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Charles Tizeba (Mb) dirisha la pili kutoka kulia, akiangalia nje wakati wa majaribio ya mabehewa sita kati ya kumi na mbili yatakayofanya safari zake kutoka Station mpaka Ubungo kuanzia mwezi wa Kumi mwaka huu,Treni hizo zitasaidia wananchi katika usafiri jijini Dar es Salaam

230651455.JPG

Kichwa cha treni pamoja na mabehewa sita ya awamu ya kwanza, yakisubiri kufanyiwa majaribio kwa Safari zitazoanzia Station Dar es Salaam mpaka Ubungo mnamo mwezi wa kumi, majaribia hayo yameongozwa asubuhi ya leo na Naibu Waziri wa Uchukuzi,Mhe. Dk Charles Tizeba (Mb) ambaye alipanda treni hiyo kuanzia Station Dar es Salaam Mpaka Ubungo.Serikali imetumia kiasi cha Sh. Bil 4.75 kwa ajili ya ukarabati wa njia, injini na mabehewa.
 
Idea nzuri lakini watu 16,000 ni wachache sana kwa treni ya siku nzima kuna kitu hakiko sawa hata gharama za kuilipia treni haita cover.
Chukulia kila kipanya kinabeba abiria 20 mpaka kumaliza route moja, utagundua makadirio ya route 800 za vipanya zimeondolewa kwa siku. Kama kila kipanya kinafanya wastani wa trip 10, utagundua huu mpango utaondoa vipanya kama 80 hivi kwa siku ya kawaida.
Swali la msingi ni kwenye collateral damage ambalo linaweza kufanya watu waanze kufitiniana.
Kama kila abiria akilipa Tsh 500, mapato kwa siku ni kama 8 milioni hivi. Je kati ya hizi ni ngapi zitarudi kwenye mtaji na ngapi zitawezesha uendeshaji wa kila siku. Labda tutaambiwa bajeti ijayo na hapo shaka lako la msingi litajibiwa.
 
Nampongeza sana Mwakyembe, na pia namtahadharisha awe makini sana hasa na uhai wake. Rizwani juzi kaingiza trailer 50 na 100 zipo njiani.

Sasa hizo trailer zitabeba abiria wangapi toka kati mpaka ubungo? Au tueleze hizo tela zina manufaa gani hapa
 
kwa sababu wanaolengwa siyo wenye magari! As a matter of fact nadhani itachangia zaidi ongezeko la magari jijini Dar. Think about it.

Mtazamo wangu

Nikienda mjini kwa gari inanichukua muda mrefu, nikipanda gari moshi kwa vile halina vizuzi njiani kama traffic lights na crossing stops nitachagua kutumia usafiri huu wa kunifikisha haraka kuliko kuunguza mafuta njiani kwa kusimama tu na kuhangaikia parking.

Labda tuseme biashara ya bodaboda na bajaji itashamiri zaidi.

Niambieni, Gongolamboto na Mbagala hakutakuwa na usafiri huu? Naona kando ya pugu road reli imepita kando tu, Mwakiembe afikirie hilo maana kudandia daladala madirishani hasa pale karibu na Kampala University balaa tupu.
 
Kwa hiyo hizo treni zimetengenezwa kwa ajili ya wakazi wa huko tabata, wale wa mbezi kawe mikocheni msasani obay imekula kwao sio
 
Kwa hiyo hizo treni zimetengenezwa kwa ajili ya wakazi wa huko tabata, wale wa mbezi kawe mikocheni msasani obay imekula kwao sio
Yule ambae yuko mbezi au kimara, anasogea na usafiri wa kawaida mpaka Ubungo, anapanda tren sio kila mtu imfikie kwake wamejaribu kurahisisha. Kwa wale wa Kawe kuna boti itapita baharini.

 
Yule ambae yuko mbezi au kimara, anasogea na usafiri wa kawaida mpaka Ubungo, anapanda tren sio kila mtu imfikie kwake wamejaribu kurahisisha. Kwa wale wa Kawe kuna boti itapita baharini.


hizo boti zimekaguliwa? mi sipandi boti bongo mpaka nijue umahiri wake...msije kutuzamisha bure ni bora tupange foleni ya barabarani
 
Sasa hizo trailer zitabeba abiria wangapi toka kati mpaka ubungo? Au tueleze hizo tela zina manufaa gani hapa

Ishu ni kwamba, anapambana na wasafirishaji wengine wakubwa...haitakuwa rahisi kukubali wapokonywe kitumbua mdomoni...hii ndio maana ya kumwambia awe makini.
 
Chukulia kila kipanya kinabeba abiria 20 mpaka kumaliza route moja, utagundua makadirio ya route 800 za vipanya zimeondolewa kwa siku. Kama kila kipanya kinafanya wastani wa trip 10, utagundua huu mpango utaondoa vipanya kama 80 hivi kwa siku ya kawaida.
Swali la msingi ni kwenye collateral damage ambalo linaweza kufanya watu waanze kufitiniana.
Kama kila abiria akilipa Tsh 500, mapato kwa siku ni kama 8 milioni hivi. Je kati ya hizi ni ngapi zitarudi kwenye mtaji na ngapi zitawezesha uendeshaji wa kila siku. Labda tutaambiwa bajeti ijayo na hapo shaka lako la msingi litajibiwa.

Embu toa umbumbumbu wako hapa. Nina uhakika hujawahi kwenda nje ya tanzania akili zako ni akili mgando.
 
Nakubaliana na Mwanakijiji,wataopanda hayo matreni ni walalahoi,mtu mwenye gari hawezi acha gari home aende akabanane na watu kwenye mabehewa wkt kashazoe full mziki na kiyoyozi kwenye gari...Halitapunguza foleni bali litapunguza mjazano wa abiria kwenye madaradara.
 
Faida ya biashara ya treni inategemea formula. Ni Load x Distance. Umbali wa treni dala dala ni mdogo sana na mzigo ni mdogo pia. Ni imani yangu wataalam wa uchumi wa masuala ya treni watakuwa wamezingatia hayo, kwani ili treni ilete faida ni lazima iende mbali na ibebe mzigo mkubwa. La sivyo itakuwa hasara na kuhitaji ruzuku. Kinyume na hapo ni lazima kutumia vichwa na mabehewa maalum ya abiria wa mjini ambayo yote yawe mepesi sana ili kutumia nishati kidogo. kwa kawaida vichwa vya treni ni vizito sana. Baadae ni vizuri kuanza kufikiria treni za umeme, dar moro au chalinze ili treni mwisho wa mwaka ihesabu vichwa kwa mamilioni ya abiria kwa mwaka. Mabasi yanayotoka mikoani yanaweza changia kwa kumwaga abiria chalinze na treni iwalete mjini abiria hao ili mabasi yafike umbali mdogo kidogo na treni iweze kubeba abiria wengi sana ili kuleta faida. Kwa kuwa tanzania itakuwa na umeme wa ziada 2016, ni vizuri kuanza kufikiria treni na mabasi ya umeme. Hayo yakichangwanywa na treni na mabasi ya kutumia Natural gasi, matatizo ya usafiri kwa wanafunzi itakuwa ni historia. Kiasi kikubwa sana cha fedha za kigeni kitatumika kwa matumizi mengine.
 

Niambieni, Gongolamboto na Mbagala hakutakuwa na usafiri huu?.

Kwa Gongo la mboto kutakuwa na usafiri wa Tazara, kuanzia Pugu, Moshi Bar na Majohe. Ila baadae kidogo, baada ya kuangalia ruti ya Ubungo inaendaje, kuna mpango wa TRL kupeleka treni hadi Pugu, kwa reli hii hii iliyopo, inayopitia kwa Mnyamani. Kwa habari nilizonazo
 
MKUKI, CCM Inatatizo ambalo linarekebishika kwa miezi sita. Wenzetu wasomi wa cdm wame-take advantage. Kuna maamuzi madogo sana yanatakiwa yafanywe na ccm ili kurudisha mvuto kwani ni lazima tukiri, kumekuwa na tatizo ndani ya ccm. Hata hivyo, nina rafiki zangu cdm wananiambia kama wangelikuwa wao wapo ndani ya ccm wangelikuwa na mengi sana ya kueleza mazuri ya ccm
 
Back
Top Bottom