Route za treni za Mwakyembe ndani ya jiji la Dar: TRL vs TAZARA

Mipango mbali kutekeleza mbali ccm tafuteni hela zenu ndio muweke hyo miradi sio mnaplan nyingiiii kwa kutegemea hela sa wavuja jasho(wanachama wa nssf/ppf)
 
tulipiga kelele sana kuwa mradi wa mabasi hauwezekani UMEWEZEKANA.......sasa tunapiga kelele kuwa hilo la treni haliwezekani MWAKYEMBE na timu yake WANAANZA KUONYESHA WANAWEZA
Sisi TUNAONGEA wao WANAFANYA........mwisho wa siku tutasema wameiba kura kwa sababu mikutano yao haijazi watu....KUMBE WENZETU HAWAONGEI KWA MIDOMO BALI VITENDO

Mwakyembe pamoja na serikali mmeonyesha njia na sasa wale wakosoaji na wapiga porojo ambao dua zao za kila siku ni kuomba kila kitu kishindikane ili wakigeuze mtaji wa kisiasa sasa wanakwama. Nina hakika huu utakuwa ni muafaka mujarabu ambao utaua kero hii iliyopitiliza. After all, gharama za uendeshaji magari ambazo ziko juu sasa zitakwepwa ikiwa safari hizi zitakuwa na mafanikio. Kudos Mwakyembe na timu yako!
 
Mipango mbali kutekeleza mbali ccm tafuteni hela zenu ndio muweke hyo miradi sio mnaplan nyingiiii kwa kutegemea hela sa wavuja jasho(wanachama wa nssf/ppf)


Ni lini utakuwa bipartisan? Unategemea CCM au serilkali yoyote iliyoko madarakani itatekelezaje miradi au mipango yake bila kutumia fedha za walipa kodi? Kwanza huu si mradi wa chama. Ni juhudi za serikali kutatua kero za wananchi wake. Fungua macho mkubwa!
 
hakuna mtu anayekataa kuwa mabasi yaendayo kasi (kama ni kweli) na treni zitasaidia kwa muda kupunguza msongamano. Ila sio suluhisho la muda mrefu. Nigeria ni moja ya nchi zenye mfumo wa mabasi hayo lakini hali ya usafiri Lagos bado sio nzuri. Wale wenye umri uliosogea kukaribia mafao watakumbuka enzi zile UDA ilikuwepo yenyewe. Baadaye ilipozidiwa marehemu Sokoinne aliruhusu dala dala (wakati huo nauli ilikuwa shs 5) tatizo la usafiri likapungua sana. kwa vile hatukuwa na mipango endelevu tatizo likarudi pale pale kwa kiasi kikubwa. Hili litatatua kwa mwaka mmoja halafu tutarudi pale pale. Kutatua tatizo hili lazima ulitatue kwa jicho la uchumi mkubwa (macro economy). 1. treni kwa vile zinapita chini zitasababisha msongamano zaidi wa magari kwa vile njia zitafungwa mara kwa mara. (kumbuka network yake haikufikishi unapotaka kwenda. Mfano nakaa Tegeta nataka kuwahi mechi uwanja wa taifa nafikaje?
2. foleni zingine zinasababishwa na magari mabovu yanayofia njiani, kutokuwepo vituo/nadhamu kwa dala dala matokeo yake wanasimama barabarani na ujenzi usiozingatia maegesho unaoendelea.

Kila jambo lazima liwe na mwanzo wake na huu ni mwanzo mzuri. Katika maendeleo ya nchi yoyote kuna mipango ya maendeleo ya vipindi tofauti. Muda mrefu, wa kati na muda mfupi. Mpango wa train ni wa muda mfupi na ni stopgap arrangement wakati ule wa mabasi yaendayo kasi ni wa muda wa kasi lakini kutakuwa na complementary effect. Wakati huo huo ipo mipango ya kutengenzea flyovers and bypasses lakini pia kuimarisha barabara za pembezoni ili ku- decongest hizi barabara kubwa. Ieleweke pia kwamba Lagos, jiji la watu karibu milioni 20 lina changamoto tofauti na Dar es Salaam na kila moja ina mikakati tofauti ya utekelezaji kutegemeana na ukubwa na chanzo cha matatizo.

Hata hivyo nakubaliana na wewe kwamba suala la vituo vya mabasi holela na magari ambayo ni vimeo ni mambo yanayohitaji kufanyiwa kazi. Lakini kukiwa na usafiri wa umma wenye heshima, staha na wa kuaminika kama nchi za wenzetu, ule ulevi wa kila mtu kuwa kwenye gari yake binafsi utapungua na hivyo kuondoa msongamano.
 
....Mimi najiuliza jinsi watakavyoweza kudhibiti wadandiaji wa njiani watakaokuwa wanataka kusafiri bure kwenda/kutoka mjini kwa kutumia treni hizi ambazo zitakuwa haziendi kasi sana..
 
Pongezi kwa Mwakymbe umethubutu ni hatua nzuri ya kupambana na msongamano wa magari.
 
Hivi mwakyembe anajua kweli anafanya nini ..treni dar? Heee
 
Pongezi kwa Mwakymbe umethubutu ni hatua nzuri ya kupambana na msongamano wa magari.

Ndugu Ritz1, huu mpango wa treni hauonekani kupambana na msongamano wa magari, bali ni kuwapunguzia adha watumiaji wa daladala, yaani wenzagu pangupakavu, kajampanani - uamuzi ambao hatuna budi kuupongeza. Msongamano wa magari unasababishwa na kakundi kadogo sana ka wabongo wanaomiliki magari kwa kutimia miundombinu iliyojengwa enzi za ujamaa - kumbuka itikadi ya ujamaa haikuwa imelenga kupanua miji wala kujenga tabaka la wenye magari vs wasiokuwa na magari, bali ilikuwa ni MAENDELEO VIJIJINI. Kwa kifupi, tatizo la msongamano wa magari jijini Dar ni kukumbatia 'usoko huria' lakini kuendelea kutumia miundombinu ya 'ujamaa'.
 
Mwakyembe adai Sh317.7 bilioni zinatosha bajeti yake Send to a friend
Saturday, 04 August 2012 10:44


dk-mwakyembe-top2.jpg
Waziri wa Uchukuzi,Dk Harrison Mwakyembe

Boniface Meena,Dodoma
WAZIRI wa Uchukuzi,Dk Harrison Mwakyembe amesema Sh 317.7 bilioni alizoliomba Bunge kwa ajili ya bajeti yake kwa mwaka wa fedha 2012/13 zinamtosha hata kama kuna watu wanasema kiasi hicho ni kidogo.

Alisema ili wizara yake iweze kutekeleza majukumu na malengo yake katika mwaka huu wa fedha kiasi hicho kinatosha kuitoa sekta ya uchukuzi ICU.

Dk Mwakyembe alisema hayo juzi wakati akijibu hoja za wabunge waliochangia hotuba yake ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2012/13.

"Bajeti hii mimi inanitosha kwani sekta ya uchukuzi ilikuwa ICU,"alisema Dk Mwakyembe.

Alisema kati ya fedha hizo Sh 64.9 bilioni zitakuwa ni za matumizi ya kawaida na Sh252.7bilioni ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

"Fedha za matumizi ya kawaida zinajumuisha Sh37.0 bilioni za mishahara ya watumishi na Sh27.8 , fedha za matumizi mengineyo,"alisema Dk Mwakyembe.

Alisema fedha za miradi ya maendeleo zinajumuisha Sh189.7 bilioni ambazo ni fedha za ndani na Sh52.9 bilioni fedha za nje.

Wakati Dk Mwakyembe akiomba kiasi hicho cha fedha, Kamati ya Bunge ya Miundombinu imesema, wizara hiyo imetengewa fedha kidogo ikilinganishwa na mahitaji halisi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Peter Serukamba aliliambia bunge kuwa wizara ya uchukuzi ni miongoni mwa wizara chache zinazoweza kuchochea ukuaji wa uchumi kwa haraka kwa kuwa fedha inayowekezwa katika wizara hiyo inakwenda kuzalisha fedha zitakazotumika kuboresha sekta nyingine.

"Pamoja na ukweli huu, wizara hii imetengewa fedha kidogo ikilinganishwa na mahitaji halisi kwani mwaka wa fedha 2011/12 ilitengewa jumla ya Sh167.9 bilioni baada ya Bunge kushinikiza fedha za maendeleo ziongezwe katika sekta ya reli na bandari,"alisema Serukamba.

Alisema Serikali iliahidi kuongeza Sh95 bilioni na hivyo fedha za maendeleo kufikia jumla ya Sh262.9 bilioni lakini hadi kufikia Mei mwaka huu fedha za maendeleo zilizotolewa ni jumla ya Sh96.7 bilioni sawa na asilimia 57.6 ya fedha ambayo bunge liliomba kutaka iongezwe.
:israel:saaaafiiii saaana mwakyembee:A S 465:
 
tulipiga kelele sana kuwa mradi wa mabasi hauwezekani UMEWEZEKANA.......sasa tunapiga kelele kuwa hilo la treni haliwezekani MWAKYEMBE na timu yake WANAANZA KUONYESHA WANAWEZA
Sisi TUNAONGEA wao WANAFANYA........mwisho wa siku tutasema wameiba kura kwa sababu mikutano yao haijazi watu....KUMBE WENZETU HAWAONGEI KWA MIDOMO BALI VITENDO

Hapo kwenye red. Hivi kumbe huu mradi umeshaanza kazi?????!!!!!!!
 
waswahili sijui tukoje
kwa nini tusisubiri uanze ndo tuzungumze malalamiko?
bora waanze tu
mengineyo yatashughulikiwa yatakapojitokeza
 
....Mimi najiuliza jinsi watakavyoweza kudhibiti wadandiaji wa njiani watakaokuwa wanataka kusafiri bure kwenda/kutoka mjini kwa kutumia treni hizi ambazo zitakuwa haziendi kasi sana..
Ni njia rahisi tu BabaDesi - kuwa na sheria/kanuni nzuri na utekelezaji wake. Kwa wenzetu wanakofuata sheria (na ustaarabu), mabasi yana mlango wa kuingilia na kutokea), wala hakuna konda au mpiga debe; unalipa kwa dereva anakupa tiketi au kutumia kadi maalumu ya malipo.

Ukiingia kama hutaki kulipa dereva hakuulizi, anapiga simu tu kwa wakaguzi na kabla hujafika uendako mkaguzi kafika. Akikunasa huna tiketi ni mahakamani tu, hakutakiwi ushahidi zaidi ya kuwa huna tiketi. Hakuna aah mie maana yake kwa sababu ilikua. HAPANA, huna tiketi kwa sababu hukukata au hukuitunza ni kosa.Unasomewa shitaka fasta fasta, hakuna kuahirisha kesi, unalipa faini ya kununua basi zima au unakwenda jela. Na wala sio uende kuitia serikali hasara, jela unaenda kwa kulala tu, asubuhi huruhusiwi hupewi hatamaji ya kunawa uso sembuse chai. Fikiria adhabu hiyo mwaka mmoja kamili!

Ni kuwa na utaratibu tu na kuufuata.
 
Kuna tatizo kwa huduma bora ya usafiri kuwalenga waso magari?

Kwani ujamzoea uyo kazi Yake kukosoa kwake hamnajema kwa uwongozi huu hawa niwale watu wakiona mazuri ya nchi hii wananuna coz watakosa chakuandika
 
Kuna tatizo kwa huduma bora ya usafiri kuwalenga waso magari?

Kwani ujamzoea uyo kazi Yake kukosoa kwake hamnajema kwa uwongozi huu hawa niwale watu wakiona mazuri ya nchi hii wananuna coz watakosa chakuandika
 
Watu wa kutoka gongola mboto plus mwakanga kama wanataka kwenda town watashuka tazara HQ then mdogo mdogo mpaka buguruni unadaka TRL mpaka town
Izi reli haziwezi ingiliana as zinatofautiana gauge ya Tazara ni ya kimataifa ndo maana kuna treni monthly inatoka south africa mpaka dsm via hii reli ila kwa TRL gauge yao sio international ndo maana kuna mpango wa kuiboresha
 
Hawa wajamaa huwa wanakurupuka tu. Last time Mh Magufuli alisema kuweka ferry kati ya Kunduchi/Mbezi to town ili kpunguza mafoleni ya magari. Sasa Mh Mwakyembe anakuja na train. Hizo train hazipiti katikati mwa mji sasa itakuwaje mtu aanze kupiga mguu toka stesheni kwenda sehemu mbalimbali katikati mwa mji? Si katikati mwa mji kutajaa madaladala? nauli mtu alipe kwa train na daladala? Huu sio ubunifu bali fikra fupi kujitafutia sifa mtindi. Wawe creative bana.
 
Nilizani pale stesheni na kituo cha kamata ni baadhi ya vituo vilivyo town
Labda Tim kuwa specifiic unamaanisha maeneo gani?
Ivi umetolewa ubungo mpaka stesheni kwa 35min bado huoni ahueni khaa wabongo kuweni na namna ya kuapreciate vitu mwishowe mtataka viwekwe vituo maofisini mwenu
 
Back
Top Bottom