Rostam: "Ni Rahisi Kuagiza bidhaa kutoka China, India au Ulaya kuliko Kuagiza Kenya au Uganda"

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
42,727
49,419
Habari za Leo mdau.

Rostam Aziz mfanyabiashara mashuhuri Tanzania amesema ni ghali zaidi kuagiza bidhaa baina ya Nchi za Afrika ambazo ziko jirani kuliko Kuagiza bidhaa hizo hizo Ulaya,Asia au India.

Rostam alikuwa akizungumza kwenye utiaji saini wa Ujenzi wa mradi wake wa uwekezaji Nchini Kenya.

Rostam amesema Nchi za Kiafrika zinathamini zaidi wazungu kuliko kujithamini wenyewe.

My Take.
Hivi Waafrika tulirogwa au Kuna shida mahali? Kwa nini tunashindwa kuweka mazingira ya Intra-Afrika Trade ambayo itakuza ustawi wa watu Wetu na kufanya tupate uchumi Kwa haraka na kuwa na sauti kwenye majukwaa ya Kimataifa?

Yaani tatizo Huwa ni gani kwenye hizi Nchi zetu? Leo hii ukitaka usafiri wa kwenda West Afrika lazima uende Dubai nk ndio utapata usafiri wa kwenda huko..

Kuna mtu mmja alipata soko la bidhaa za kahawa nk West Afrika ila gharama za usafiri ni kama kutoka Tanzania kwenda Marekani Sasa huu upuuzi Hadi lini?

Maelfu ya watu wa Afrika wanakimbia Bara hili sababu za ujinga wa kama hivi,napenda kufahamu shida hasa ni zipi Hadi inakuwa ngumu Kwa Nchi za Afrika kuwa na mtengamano wa biashara?

Mwisho Afrika itabadili Vyama na Vyama Watawala huyu na yule ila bila kukata mzizi wa fitina wa mambo yanayokwamisha maendelea na Biashara tutaishia kupigana na kuuana hakuna Maendelea yeyote.mfano ni huko Nigeria, Ghana,Kenya,Malawi ,Zambia nk.



Binafsi ndio maana Huwa naunga mkono Rais yeyote kutoka chama chochote ambae ana mtizamo wa biashara na Huwa napinga sana Watu wenye mitizamo ya kijima na Kijamaa..

Namkubali Rais Samia Kwa sababu hii na namponga Mwendazake Kwa sababu ya sera za Kijima.Nadhani Kila mtu anaona tofauti ya Sasa na miaka 5 iliyopita.

 
Afrika hii Ina laana mahali sio bure.

Hongera Ruto na Dk Samia Kwa kutambua kwamba zama za kutoaminiana ni upumbavu usio na msingi ,fungueni biashara ondoeni vikwazo vya mipakani tukuze Uchumi na maisha ya watu Wetu.
20230225_085525.jpg
 
Habari za Leo mdau.

Rostam Aziz mfanyabiashara mashuhuri Tanzania amesema ni ghali zaidi kuagiza bidhaa baina ya Nchi za Afrika ambazo ziko jirani kuliko Kuagiza bidhaa hizo hizo Ulaya,Asia au India.

Rostam alikuwa akizungumza kwenye utiaji saini wa Ujenzi wa mradi wake wa uwekezaji Nchini Kenya.

Rostam amesema Nchi za Kiafrika zinathamini zaidi wazungu kuliko kujithamini wenyewe.

My Take.
Hivi Waafrika tulirogwa au Kuna shida mahali? Kwa nini tunashindwa kuweka mazingira ya Intra-Afrika Trade ambayo itakuza ustawi wa watu Wetu na kufanya tupate uchumi Kwa haraka na kuwa na sauti kwenye majukwaa ya Kimataifa?

Yaani tatizo Huwa ni gani kwenye hizi Nchi zetu? Leo hii ukitaka usafiri wa kwenda West Afrika lazima uende Dubai nk ndio utapata usafiri wa kwenda huko..

Kuna mtu mmja alipata soko la bidhaa za kahawa nk West Afrika ila gharama za usafiri ni kama kutoka Tanzania kwenda Marekani Sasa huu upuuzi Hadi lini?

Maelfu ya watu wa Afrika wanakimbia Bara hili sababu za ujinga wa kama hivi,napenda kufahamu shida hasa ni zipi Hadi inakuwa ngumu Kwa Nchi za Afrika kuwa na mtengamano wa biashara?

Mwisho Afrika itabadili Vyama na Vyama Watawala huyu na yule ila bila kukata mzizi wa fitina wa mambo yanayokwamisha maendelea na Biashara tutaishia kupigana na kuuana hakuna Maendelea yeyote.mfano ni huko Nigeria, Ghana,Kenya,Malawi ,Zambia nkView attachment 2529242
Tatizo hatuaminiane na tuna oneana wivu, Mkenye maisha yake yote hapendi Tanzania ifanikiwe jambo lolote la kiuchumi, tuna ishi na majini wa nafiki, Kenya anataka ibaki kua industrial hub ya Africa mashariki, Uganda walivyo aanza kupeleka maziwa yao ya Lato Milk kule Kenya ya kaonekana yana soko, wakayapiga marufuku bila sababu za msingi ya si ingii nchini mwao, bora wanunue Lactroge wa kutoka south Africa, tatizo la Africa mshariki ni Kenya tu.
 
Tatizo hatuaminiane na tuna oneana wivu, Mkenye maisha yake yote hapendi Tanzania ifanikiwe jambo lolote la kiuchumi, tuna ishi na majini wa nafiki, Kenya anataka ibaki kua industrial hub ya Africa mashariki, Uganda walivyo aanza kupeleka maziwa yao ya Lato Milk kule Kenya ya kaonekana yana soko, wakayapiga marufuku bila sababu za msingi ya si ingii nchini mwao, bora wanunue Lactroge wa kutoka south Africa, tatizo la Africa mshariki ni Kenya tu.
Haya mambo ni masuala ya kijinga, nadhani Kwa kuwa tumepata viongozi wenye maono wafanye Kwa vitendo..

Nakumbuka kabla ya Rais Samia kuingia madarakani zama za Jiwe yaani Kenya na Tanzania ni kama paka na panya lakini walikutana na Kenyatta na Ruto na wakaondoa vikwazo robo tatu.

Hadi tunaongea saizi Tanzania ndio inauzia bidhaa nyingi na Zenye thamani kubwa kuliko Kenya wakati miaka yote tulikuwa nyuma.

Mifano kama hii ndio itumike kwenye Nchi zote,sio lazima uongoze Bali inaangalia manufaa mengi..

Sasa watu watapata vipi Ajira,watajiajifi vipi ikiwa masoko ni limited? Ndio maana tuna jamii za watu maskini kisa hofu zisizo na msingi.
 
Ukiwa Kenya ni rahisi kupiga simu Uingereza au South Africa ukitumia safaricom kuliko kupigia mtu ws Tigo Tanzania. Ukiwa Dubai line ya Tanzania ya Tigo hufanya kazi ila ukiwa Uganda line ya Tigo ya Tanzania haina network na haifanyi kazi..... sisi Africa bado sana mpaka tupate viongozi wenye roho safi
 
Tatizo hatuaminiane na tuna oneana wivu, Mkenye maisha yake yote hapendi Tanzania ifanikiwe jambo lolote la kiuchumi, tuna ishi na majini wa nafiki, Kenya anataka ibaki kua industrial hub ya Africa mashariki, Uganda walivyo aanza kupeleka maziwa yao ya Lato Milk kule Kenya ya kaonekana yana soko, wakayapiga marufuku bila sababu za msingi ya si ingii nchini mwao, bora wanunue Lactroge wa kutoka south Africa, tatizo la Africa mshariki ni Kenya tu.
Wana roho mbaya sana hao viumbe,na huwa hawajifichi wanaonyesha wazi wazi chuki zao
 
Ukiwa Kenya ni rahisi kupiga simu Uingereza au South Africa ukitumia safaricom kuliko kupigia mtu ws Tigo Tanzania. Ukiwa Dubai line ya Tanzania ya Tigo hufanya kazi ila ukiwa Uganda line ya Tigo ya Tanzania haina network na haifanyi kazi..... sisi Africa bado sana mpaka tupate viongozi wenye roho safi
Sasa haya mambo ya kipumbavu ndio yanatakiwa Afrika tuyakomeshe.

Biashara za Intra Africa trade Ina manufaa na itaondoa watu wengi kwenye umaskini kuliko kujikomboa Kwa Wazungu.
 
Kinachosikitisha ni kwamba Tanzania inauza zaidi mazao na malighafi Kenya, kwa hali hii tunaendelea kubaki kuwa taifa la wakulima na wafugaji, na bila viwanda vya kuchakata bidhaa hapa kwetu hatutoboi.
Haya mambo ni masuala ya kijinga, nadhani Kwa kuwa tumepata viongozi wenye maono wafanye Kwa vitendo..

Nakumbuka kabla ya Rais Samia kuingia madarakani zama za Jiwe yaani Kenya na Tanzania ni kama paka na panya lakini walikutana na Kenyatta na Ruto na wakaondoa vikwazo robo tatu.

Hadi tunaongea saizi Tanzania ndio inauzia bidhaa nyingi na Zenye thamani kubwa kuliko Kenya wakati miaka yote tulikuwa nyuma.

Mifano kama hii ndio itumike kwenye Nchi zote,sio lazima uongoze Bali inaangalia manufaa mengi..

Sasa watu watapata vipi Ajira,watajiajifi vipi ikiwa masoko ni limited? Ndio maana tuna jamii za watu maskini kisa hofu zisizo na msingi.
 
Haya mambo ni masuala ya kijinga, nadhani Kwa kuwa tumepata viongozi wenye maono wafanye Kwa vitendo..

Nakumbuka kabla ya Rais Samia kuingia madarakani zama za Jiwe yaani Kenya na Tanzania ni kama paka na panya lakini walikutana na Kenyatta na Ruto na wakaondoa vikwazo robo tatu.

Hadi tunaongea saizi Tanzania ndio inauzia bidhaa nyingi na Zenye thamani kubwa kuliko Kenya wakati miaka yote tulikuwa nyuma.

Mifano kama hii ndio itumike kwenye Nchi zote,sio lazima uongoze Bali inaangalia manufaa mengi..

Sasa watu watapata vipi Ajira,watajiajifi vipi ikiwa masoko ni limited? Ndio maana tuna jamii za watu maskini kisa hofu zisizo na msingi.
Sawa lakini mkuu kufanya biashara na Kenya lazime uwe tayari kunyoonywa, Mkenya hawezi kukupa wewe mtanzania nafasi ya economic benefit ukifanya nae biashara, wewe tizama items tunazo uuza Kenya ni agricultural products, raw materials kwa viwanda vyao wakati wenyewe wanauza finished au processed products, ambao ina faida kubwa kuliko raw material tunaxo uza kwao.
 
Habari za Leo mdau.

Rostam Aziz mfanyabiashara mashuhuri Tanzania amesema ni ghali zaidi kuagiza bidhaa baina ya Nchi za Afrika ambazo ziko jirani kuliko Kuagiza bidhaa hizo hizo Ulaya,Asia au India.

Rostam alikuwa akizungumza kwenye utiaji saini wa Ujenzi wa mradi wake wa uwekezaji Nchini Kenya.

Rostam amesema Nchi za Kiafrika zinathamini zaidi wazungu kuliko kujithamini wenyewe.

My Take.
Hivi Waafrika tulirogwa au Kuna shida mahali? Kwa nini tunashindwa kuweka mazingira ya Intra-Afrika Trade ambayo itakuza ustawi wa watu Wetu na kufanya tupate uchumi Kwa haraka na kuwa na sauti kwenye majukwaa ya Kimataifa?

Yaani tatizo Huwa ni gani kwenye hizi Nchi zetu? Leo hii ukitaka usafiri wa kwenda West Afrika lazima uende Dubai nk ndio utapata usafiri wa kwenda huko..

Kuna mtu mmja alipata soko la bidhaa za kahawa nk West Afrika ila gharama za usafiri ni kama kutoka Tanzania kwenda Marekani Sasa huu upuuzi Hadi lini?

Maelfu ya watu wa Afrika wanakimbia Bara hili sababu za ujinga wa kama hivi,napenda kufahamu shida hasa ni zipi Hadi inakuwa ngumu Kwa Nchi za Afrika kuwa na mtengamano wa biashara?

Mwisho Afrika itabadili Vyama na Vyama Watawala huyu na yule ila bila kukata mzizi wa fitina wa mambo yanayokwamisha maendelea na Biashara tutaishia kupigana na kuuana hakuna Maendelea yeyote.mfano ni huko Nigeria, Ghana,Kenya,Malawi ,Zambia nk.


Zungumzia kila kitu lakini hili la kutaka usafiri kutoka Tanzania mpaka Nigeria moja kwa moja ni ujinga kulifikiria.Katika biashara ya usafiri wa anga itachukua muda ha huenda isiwezekane. labada ndege ya raisi ndio inaweza kuruka moja kwa moja mpaka Nigeria.
Mashirika kama Airtanzania na Kenya airwaysa hata wakiondoshewa vikwazo vyote vya anga basi hawatokuwa tayari kurusha ndege kwenda nchi ambayo abiria wa kutosha hata wa kujjazia mafuta.
Nchi za ghuba na Uturuki iliyo Ulaya kwa sasa yanatawala soko la usafiri huo kutokana na maeneo yao kijiografia.
 
Wana roho mbaya sana hao viumbe,na huwa hawajifichi wanaonyesha wazi wazi chili zao
Kwenye biashara hakuna kitu kinaitwa roho mbaya ni kufanya fursa..
Mie nimewahi fanya kazi na Wakenya Tanzania hicho kinachoitwa roho mbaya ukweli ni kwamba hawapendi mzaha kweye biashara ni sifa nzuri nilijifunza kwao.

Watzn ni watu wa slope na blaa blaa nyingi.
 
Zungumzia kila kitu lakini hili la kutaka usafiri kutoka Tanzania mpaka Nigeria moja kwa moja ni ujinga kulifikiria.Katika biashara ya usafiri wa anga itachukua muda ha huenda isiwezekane. labada ndege ya raisi ndio inaweza kuruka moja kwa moja mpaka Nigeria.
Mashirika kama Airtanzania na Kenya airwaysa hata wakiondoshewa vikwazo vyote vya anga basi hawatokuwa tayari kurusha ndege kwenda nchi ambayo abiria wa kutosha hata wa kujjazia mafuta.
Nchi za ghuba na Uturuki iliyo Ulaya kwa sasa yanatawala soko la usafiri huo kutokana na maeneo yao kijiografia.
Kwani usafiri ni lazima serikali ipeleke ndege? Nazungumzia private sector isiwekewe mizengwe,mbona mna akili ndogo? Ndio hicho Rostam anazungumzia.

Pia Kuna meli,Nchi za Afrika zinatakiwa kufahamu Kwa nini Iko hivyo ,Kwa nini hakuna huo usafiri na Je kwani hatuuhitaji? Kuna meli na Barabara ,anga na reli lazima vipatikane tufanye biashara
 
Kinachosikitisha ni kwamba Tanzania inauza zaidi mazao na malighafi Kenya, kwa hali hii tunaendelea kubaki kuwa taifa la wakulima na wafugaji, na bila viwanda vya kuchakata bidhaa hapa kwetu hatutoboi.
Ni kwambie ukweli siku Tanzania itabadilisha badala ya kuuza miogo kenya itegenze bisikuti na iuuze kenya badala ya kuuza mifugo itegeneze dairy products kama processed packed meat, wakenya walivo kua na roho mbaya watafunga mipaka yao na Tanzania ili tusiingize hiyo bidhaa, tena Mkenya ni Mkeya iwe Mkikuuyu awe Mkalejini au Mja Luo wote wana fitna kwa Tz na uganda
 
Kwenye biashara hakuna kitu kinaitwa roho mbaya ni kufanya fursa..
Mie nimewahi fanya kazi na Wakenya Tanzania hicho kinachoitwa roho mbaya ukweli ni kwamba hawapendi mzaha kweye biashara ni sifa nzuri nilijifunza kwao.

Watzn ni watu wa slope na blaa blaa nyingi.
Mswahili ni mtu wa bla bla sana hilo tuna kubaliana nalo, ila hilo halimaanishi kwamba Mkenya hana roho mbaya, ....neenda ukapate duka pale kisumu wewe Mtanzania af ufanye biashara inoyo fanana na Mjaluo, kama utadumu, kwanza wa takutangaza kwamba wewe ni mtanzania mtaa mzima kwamba wewe ni foreigner. Huwezi kupata wateja, we achana na mkenya unae mkuta Tz we neenda kwao ndo utaona roho mbaya yao.
 
Labda kama tumekubali wametuzidi akili na kujisalimisha kwao, lakini zipo njia nyingi za kupambana na Wakenya kibiashara na tukafanikiwa vizuri, ni sisi tu hatajaamua na kuwa serious au tuna ufinyu/uvivu wa akili.

Tunapaswa kuwa na watu smart wa kuwatengenezea tarrifs na quotas za kuwapa mbinyo wa kutosha mpaka wakubali wote tuwe katika win-win trade. Tanzania iko katika eneo la kimkakati sana kwa kila sekta katika bara hili, ni ujinga wetu tu ndio unatafanya tuzidi kuwa maskini na wanyonge.
Ni kwambie ukweli siku Tanzania itabadilisha badala ya kuuza miogo kenya itegenze bisikuti na iuuze kenya badala ya kuuza mifugo itegeneze dairy products kama processed packed meat, wakenya walivo kua na roho mbaya watafunga mipaka yao na Tanzania ili tusiingize hiyo bidhaa, tena Mkenya ni Mkeya iwe Mkikuuyu awe Mkalejini au Mja Luo wote wana fitna kwa Tz na uganda
 
Unasahau kwamba mazingira ya biashara ni changamoto sana Tanzania, sisi tukiboresha mazingira ya biashara, Tanzania ni nchi yenye fursa za kutosha kwa kila raia. Hakuna hata haja ya kwenda kupambania kufungua maduka nchi nyingine, labda ofisi za matawi ya kampuni kubwa.
Mswahili ni mtu wa bla bla sana hilo tuna kubaliana nalo, ila hilo halimaanishi kwamba Mkenya hana roho mbaya, ....neenda ukapate duka pale kisumu wewe Mtanzania af ufanye biashara inoyo fanana na Mjaluo, kama utadumu, kwanza wa takutangaza kwamba wewe ni mtanzania mtaa mzima kwamba wewe ni foreigner. Huwezi kupata wateja, we achana na mkenya unae mkuta Tz we neenda kwao ndo utaona roho mbaya yao.
 
Labda kama tumekubali wametuzidi akili na kujisalimisha kwao, lakini zipo njia nyingi za kupambana na Wakenya kibiashara na tukafanikiwa vizuri, ni sisi tu hatajaamua na kuwa serious au tuna ufinyu/uvivu wa akili.

Tunapaswa kuwa na watu smart wa kuwatengenezea tarrifs na quotas za kuwapa mbinyo wa kutosha mpaka wakubali wote tuwe katika win-win trade. Tanzania iko katika eneo la kimkakati sana kwa kila sekta katika bara hili, ni ujinga wetu tu ndio unatafanya tuzidi kuwa maskini na wanyonge.
Katika Africa mashariki custom charter kuna free movement of goods and services originated from sister country sasa hizo quotas na tariff utaziweka je? Wenyewe hutumia mbinu za harassment na political pamoja na military, wanaweza kuzuia gari lako baada ya kuvuka mpaka bila sabb lazima uiche hiyo biashara
 
Bidhaa nyingi za Kenya ni Standard sana, kuanzia plastic products, mafuta

Kenya wanajua packaging, angalia UNGA zao hawapimi pimi hovyo, unaenda dukani unachukua packed tayari unaenda tumia.


Na pia wana kampuni nyingi sana, kuanzia za UNGA etc

Tanzania packaging zetu za hovyo sana

Tukifungulia mipaka wakenya watanunua kwetu malighafi, ila sisi tutanunua kwao packaged foods.

Tujiulize kwanini Tanzania kuna plastic products nyingi za Kenya kuliko za Viwanda vya Tz, na kwanini zashindana bei wakati kutoka Nairobi hadi Dsm kuna safari ndefu sana
 
Afrika hii Ina laana mahali sio bure.

Hongera Ruto na Dk Samia Kwa kutambua kwamba zama za kutoaminiana ni upumbavu usio na msingi ,fungueni biashara ondoeni vikwazo vya mipakani tukuze Uchumi na maisha ya watu Wetu.View attachment 2529243
Mkuu acha kulialia. Kikubwa ni ngono na mkono kwenda kinywani baas ukisubiria kufa. Wote tutaondoka na wengine watakuja na hao pia wataondoka na wengine zaidi watakuja.
 
Back
Top Bottom