Rostam, Msabaha, Kikwete and Richmond - Yes I said it again!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Mwanakijiji,

1. Kuhusu Richmond na Dowans, Bunge lenu lilichunguza likasema hakuna sehemu walipoona kwamba Mh. Rostam Aziz anahusika... sasa nini kifanyike tena...

Hicho ndicho nilichosema nimenotice katika maelezo ya Rostam. Siyo kwamba hakuhusika, na hajawahi kukanusha hicho. Yeye anasema walichunguza na hawakuona jina lake. Vitu hivi ni viwili tofauti. Rostam hajawahi kukana kuhusika na Richmond na Dowans. Sikiliza tena majibu yake alipoulizwa hata jana.
2. Mamlaka za kuchunguza zinachunguza kukiwa na hoja,,, sio kila anachosema mwanakijiji kichunguzwe... wanapoona unaongea utumbo wanakuacha na utumbo wako.

Sasa, kama anachosema "mwanakijiji" ni utumbo kwanini watake ushahidi tena? Hivi nani mmiliki wa Richmond au Dowans? Kuna mtu anajua. Kamati ya Bunge ilishindwa kuonesha ni nani hasa mmiliki wa Richmond. Hebu nikukumbushishe kilichosemwa kuhusu Rostam kwenye ripoti ya Mwakyembe:

Mashahidi wawili, Ndugu Daniel Yona na Mhe. Rostam Aziz, (Mb) walipelekewa hati za kuitwa mbele ya Kamati Teule lakini hawakufika kwa maelezo kwamba walikuwa nje ya nchi.....

Mhe. Rostam Aziz alitakiwa atoe maelezo kuhusu uhusiano wake na Kampuni za Richmond Development Company LLC na Dowans Holdings S.A baada ya mashahidi zaidi ya watano kumtaja kuwa ana uhusiano nazo. Aidha, alitakiwa na Kamati Teule aeleze kwanini anwani ya posta na anwani ya barua pepe ya kampuni yake ya Caspian Construction Company Ltd inatumiwa na Dowans Holdings S.A. Kamati Teule ilipata majina ya baadhi ya wafanyakazi wa Caspian ambao pia wanaitumikia Dowans Holdings S.A.

Na kamati hiyo hiyo teule inasema hivi:

Pamoja na juhudi hizo za wamiliki wa kampuni ya Richmond Development Company LLC, Kamati Teule ilibaini kutokana na ushauri mbalimbali iliopata wa kisheria, kuwa tatizo la uhalali wa Richmond ya Tanzania lilikuwa palepale kwani kifungu cha 3(1) cha Sheria ya Makampuni kinataka watu wawili au zaidi kuwa na uwezo wa kufungua kampuni. Kwa kuwa mmoja wa wanahisa waliofungua kampuni hiyo ya Richmond ya Tanzania ni Richmond Development Company LLC ya Marekani (yenye asilimia 75 ya hisa zote za kampuni hiyo iliyosajiliwa Tanzania) na kwa kuwa kampuni hiyo ya kimarekani haijasajiliwa Marekani wala hapa Tanzania kwa mujibu wa kifungu cha 434 cha Sheria ya Makampuni na kwa kuwa, kutokana na hiyo sababu, kampuni hiyo ya kimarekani haina nguvu wala mamlaka stahili ya kikampuni, Richmond Development Company (T) Limited ina mwanahisa mmoja tu kwa jina Naeem Gire, hali ambayo haikubaliki kisheria.

Ni wazi kuwa picha iliyojengwa kwenye mkataba tunaouongelea hapa kuhusu hadhi na uhalali wa Richmond Development Company LLC nchini Tanzania ilikuwa ya kisanii, ya uongo na isiyo na msingi wowote kisheria.

Sasa kwa mfanyabiashara mzuri na msafi kama Rostam ambaye anasingiziwa tu mambo ya ufisadi, kufanya kazi na biashara na hata kushirikiana anuani na kampuni ya kifisadi ambayo ilishajulikana ni ya kifisadi hakumfanyi yeye fisadi? Inakuwaje kwa mfanyabiashara "msafi" ambaye familia yake imefanya biashara kuanzia 1852 kushindwa kuangalia uhalali wa kampuni anazofanya nazo biashara?

Je kweli Rostam hakuijua kabisa hii kampuni? Kwa ukaribu aliokuwa nao inapita akili kufikiria kuwa alikuwa hajui RDC ni nini au kuhusika na mambo yao.


3. Mpaka sasa ni Mambo ya Umbea tu... hakuna kitu Tangible hata kimoja... umaskini wenu tu... kila mkimuona mtu tajiri mnadhani ameiba...

Hakuna umbeya, Rostam alikuwa anahusika na Richmond, that is an established fact. Suala pekee ambalo halikuweza kuonekana (siyo kwamba halipo) ni kuwa halionekani.


4. Narudia... tunaomba kuona -ushare-holding wa Rostam Aziz, kwenye hizo kampuni mnazozungumzia kama hamna... acheni mambo ya kitoto hapa!

sawa kama ni utoto, lakini kwa kutuita watoto hakufanyi hoja zako kuwa na nguvu kama yule ndugu mwingine ambaye asipokubaliana na wengine anawaita wapumbavu! Rostam alikuwa na hisa kwenye RDC... he knows it na mtu yeyote ambaye angeamua kufuatilia suala hili lilipoanza 2006 angeona hivyo. Wengine tulishafanya uchunguzi mapema sana na kuestablish the following facts. (tafuta maswali yangu 10 kwa Mkurugenzi wa TAKUKURU kuhusu Richmond - 2006).

a. RDC iliingia nchini kwa ushirika wa Mhe. Msabaha (Mbunge - Waziri wa Madini)
b. RDC iliingia nchini kwa ushirika wa Jakaya Kikwete (Mbunge)
c. RDC (USA) wametoa mchango mkubwa katika kampeni ya Kikwete na Msabaha
d. Rostam Aziz ndiye mfanyabiashara aliyetengeneza mazingira ya wao RDC kujikita kwenye biashara hiyo ya energy. Yeye mwenyewe akiwa ni shemeji ya Kikwete.
e. Naeem Gire waliingia na asilimia 75 ya RDC (tanzania) na asilimia 25 zilizobakia zikigawanywa miongoni mwa wahusika wakuu.

yes I said it! RDC inahusiana na Msabaha, Kikwete, Rostam na familia ya kina Gire ambao ni wachangiaji wa kampeni za uchaguzi CCM (2005). Kupewa kwa mradi wa bomba la mafuta 2005 na miezi michache baadaye mradi wa majenereta ilikuwa ni shukrani ya CCM kwa michango ya kina Gire katika kampeni za Msabaha na Kikwete na pia kama nafasi ya kuvuna walipopanda hasa baada ya JK alipoingia madarakani kumchukua Msabaha na kumuweka kuwa Waziri wa Nishati na Madini.

so, now you know.
 
MKJJ: Sasa utaona ni wapi Rostam anapata nguvu.

Mimi hoja yangu imekuwa kwa nini tumekuwa tukiwakwepa wengine, na hasa JK, kwenye hili sakata la Richomond? Au ndio tunasubiri atoke madaraka ndio tumbebee bango kama tunavyofanya sasa kwa Mkapa? Huoni kama huu utamaduni hautasaidii sana kwenye haya mapambano yetu?
 
MKJJ: Sasa utaona ni wapi Rostam anapata nguvu.

Mimi hoja yangu imekuwa kwa nini tumekuwa tukiwakwepa wengine, na hasa JK, kwenye hili sakata la Richomond? Au ndio tunasubiri atoke madaraka ndio tumbebee bango kama tunavyofanya sasa kwa Mkapa? Huoni kama huu utamaduni hautasaidii sana kwenye haya mapambano yetu?

Mimi pia nnaamini kabisa kwamba kujitutumua kwa Rostam ni kwa sababu anajua fika ukiingia deep katika suala hili na JK pia anahusika na anhisi kwamba watanzania hawawezi kuwa na courage ya kumprobe Mkapa sembuse the sitting presidoo.. JK?
 
Nimekusoma Mkuu ndio maana pamoja na kelele zote za wazalendo still Kikwete is providing a deaf ear.
I am sorry to appear like I lost hope but sioni kama Watanzania tutapata haki yetu hivi.Maana ni viongozi wangapi so far wameshutumiwa kwa ufisadi na ni lipi lililotendeka?Hamna, na bado hawa watu wanaponda raha kwa kwenda mbele.
 
Nimekusoma Mkuu ndio maana pamoja na kelele zote za wazalendo still Kikwete is providing a deaf ear.
I am sorry to appear like I lost hope but sioni kama Watanzania tutapata haki yetu hivi.Maana ni viongozi wangapi so far wameshutumiwa kwa ufisadi na ni lipi lililotendeka?Hamna, na bado hawa watu wanaponda raha kwa kwenda mbele.

Aisee...I can't recall any....unasikia tu flani anatuhumiwa na hiki na kile.....anajiuzulu....halafu bado anaendelea kupeta....mweeeeeee
 
Kitila... swali kubwa ambalo watu nadhani hawakuliangalia sana kutoka kwenye Kamati Teule ni mambo fulani ambayo yalifunuliwa na ambayo yalikuwa ni kama maswali ya kujaza kwa mistari:

Ni swali ambalo lingehoji: Ni kwanini Kampuni ya Richmond iliyoanzishwa mwaka 2003 (nazungumzia ile ya Marekani) iweze kushirika mchakato wa kutandaza bomba la mafuta kuanzia 2004 na kupewa tenda hiyo 2005, na kushindwa! Miezi michache baadaye inashiriki katika sekta hiyo hiyo ya nishati na kupewa tenda ya majenera ambayo nayo inashindwa kuitekeleza. Katika kesi zote mbili (ya mafuta na ya majenereta) RDC inaonekana kupewa upendeleo maalum. Kamati Teule ikaona hilo na kusema:

Kesho yake, yaani tarehe 1 Aprili 2006 Waziri wa Nishati na Madini, wakati huo Mhe. Dk. Ibrahim Msabaha, (Mb.) akionesha dhahiri kutotaka njia ya international shopping kutumika, akawaita wajumbe wote wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO na kuwaagiza wahakikishe kuwa Bodi ya Zabuni ya shirika inawaita tena wazabuni wote waliojitokeza awali na makampuni mengine yoyote yenye uwezo wa kuingiza nchini mitambo hiyo. Aidha, Mhe. Dk. Ibrahim Msabaha, (Mb.) alisisitiza kwa barua kwamba:

"Mshindi wa tenda ya ununuzi wa mitambo mipya atajulikana baada ya idhini ya Serikali kutolewa. Composition ya wajumbe wa TANESCO Tender Board ibadilishwe na kuimarishwa kwa kuwa na wajumbe wenye uwezo na ni pro-active".

Ni dhahiri kuwa agizo hili la Waziri lilikuwa batili kwani Sheria ya Ununuzi wa Umma haimpi Waziri mamlaka ya kuteua Wajumbe wa Bodi za zabuni za Mashirika yaliyo chini ya Wizara yake.

Na ikaendelea kusema:

Tarehe 10 Aprili 2006, wakati Menejimenti ya TANESCO iko kwenye zoezi la kutekeleza maagizo hayo ya Waziri, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO akasitisha mchakato huo kusubiri maelekezo ya ziada toka Wizarani. Siku mbili baadaye, yaani tarehe 12 Aprili 2006, Waziri akamwandikia barua Mwenyekiti wa Bodi kuwa suala la zabuni hiyo haliko mikononi mwa TANESCO tena, na kusisitiza kwamba:

"Suala la kushugulikia gas turbines za kukodisha lilishashughulikiwa na Mhe. Waziri Mkuu, ambaye aliunda Kamati ya wataalamu watatu: KM Hazina, KM Nishati na AG. Nia ni kuliondoa suala zima kwenye mikono ya Menejimenti ya TANESCO ambayo imeshindwa kulishughulikia kwa ufanisi. Waachie Kamati iliyoteuliwa kufanya kazi hiyo … Pasiwe tena na picha kama vile Menejimenti ya TANESCO imerejeshewa kazi hiyo, maana huko kutakuwa ni kukiuka maagizo ya Mhe. Waziri Mkuu".

Hapa ndipo Lowassa kama Waziri Mkuu anapoingia kichwa kichwa katika sakata la Richmond.

Na hapa ilipokuwa tayari Msabaha akamuandikia ujumbe waziri Mkuu:

Siku hiyo hiyo ya tarehe 19 Juni 2006, Waziri wa Nishati na Madini alimwandikia dokezo Waziri Mkuu Mhe. Edward Ngoyai Lowassa, (Mb) kuwa majadiliano ya awali na Richmond Development Company LLC yamekamilika hivyo Serikali iiteue Kampuni hiyo kwa lengo la kuingia mkataba na TANESCO wa kuzalisha umeme wa dharura kwa miaka miwili. Sehemu ya barua hiyo inasomeka:

"Kamati ya Serikali ya Majadiliano (GNT) inayojumuisha wataalam kutoka Wizara Fedha, Wizara ya Nishati na Madini, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Benki Kuu na TANESCO ilifanya majadiliano na Richmond Development Company LLC ya Houston, Marekani kutoka tarehe 8 hadi 16 Juni 2006, kwa kuzingatia maelekezo yako." (msisitizo tumeongezea

Ni kutokana na haya ndipo Kamati Teule ikahitimisha ifuatavyo:

Kamati Teule inaelewa hisia walizokuwa nazo viongozi wa ngazi mbalimbali wa TANESCO kutokana na uongozi wa kiimla wa Wizara. Tulichokiona hapo juu kwa maana ya mchakato wa Zabuni kuchukuliwa na Wizara, ulikuwa ni ukiukwaji wa sheria na utaratibu mzima wa uwajibikaji. Pamoja na dharura iliyokuwa inailikabili Taifa, Serikali haiwezi kuwa kinara wa kuvunja sheria za nchi.

Ni maoni ya Kamati Teule kuwa Wizara ilikiuka siyo tu masharti ya sheria na kanuni za ununuzi wa umma, bali vilevile maagizo mbalimbali ya Baraza la Mawaziri. Kamati Teule isingelikerwa sana na matukio haya kama Wizara ambayo ni taasisi ya ununuzi (procurement entity) kama ilivyo TANESCO, ingemalizia mchakato wake kwa kusaini mkataba huo yenyewe.

Kuishinikiza TANESCO kusaini mkataba ambao vyombo vyake halali vilikuwa havijaupitia, ni udhalilishaji wa vyombo vya maamuzi ndani ya TANESCO na upotoshaji wa hali ya juu wa taratibu za kazi na sheria. Inashangaza kuwa baada ya kudhalilishwa na Wizara kwa kiwango hicho, chombo kikuu cha maamuzi cha TANESCO, yaani Bodi ya Wakurugenzi, haikuchukua hatua ya heshima ya kujiuzulu.

Na hata pale ambapo Kamati Teule inasema lifuatalo, jibu ni kuwa nguvu ya suala la kubebwa kwa Richmond halikutoka kwa Waziri Mkuu moja kwa moja bali kwa nguvu iliyo juu yake, na Waziri Mkuu kama msaidizi mkuu wa Rais alipaswa kuweka stop, kupinga au kujiuzulu.

Kamati Teule ilishindwa kujua chanzo halisi cha ubabe, ujeuri na kiburi cha Wizara ya Nishati na Madini kama tulivyoshuhudia, kiasi cha kupindisha hata maamuzi ya Baraza la Mawaziri bila wasiwasi wowote, kukaidi ushauri wa kitaalamu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma mara tatu mfululizo kinyume na maagizo ya Baraza la Mawaziri lililotaka Sheria ya Ununuzi wa Umma izingatiwe, kukiuka sheria kwa makusudi kwa kuingilia mchakato wa zabuni wa taasisi nyingine ya ununuzi, kuvipuuza vyombo vya ndani vya maamuzi vya TANESCO (Bodi ya Wakurugenzi, Bodi ya Zabuni n.k), kuilazimisha Bodi ya Menejimenti ya TANESCO kuridhia maamuzi yaliyofanywa na Wizara ya kuibeba Richmond Development Company LLC kinyume cha sheria na taratibu, n.k.

Jibu la chanzo cha kiburi, ujeuri n.k uliooneshwa na Wizara ya Nishati a.k.a Msabaha ni MTU PEKEE ambaye alikuwa na uwezo wa kukomesha jambo hili naye si mwingine bali ni:

...................
 
MKJJ: Sasa utaona ni wapi Rostam anapata nguvu.

Mimi hoja yangu imekuwa kwa nini tumekuwa tukiwakwepa wengine, na hasa JK, kwenye hili sakata la Richomond? Au ndio tunasubiri atoke madaraka ndio tumbebee bango kama tunavyofanya sasa kwa Mkapa? Huoni kama huu utamaduni hautasaidii sana kwenye haya mapambano yetu?


I couldn't agree more! Ni kweli kuwa Kikwete ni mtu muhimu sana katika hii kashfa ya Richmond, hilo halina ubishi kabisa. Hata ushahidi wa kimazingira unasuggest hivyo, na ndio maana yeye kama rais anajaribu kujiweka mbali sana swala hili bila kutoa comments zozote za msingi zinazoweza kusaidia kutatua utata uliopo mpaka sasa. Tunapaswa kuelekeza nguvu zetu kwake kuanzia sasa if by any chance we need to win this battle.
 
NN.. the first thing is to call a spade a spade. In this case.. the evil triune of corruption made of Kikwete, Rostam, and Msabaha ndio waliingiza RDC. Na katika kufanya hivyo wakapata mtu mmoja mwenye nguvu ya kukamilisha hicho kwa amri yake na ambaye ni mtu wa amri.. naye si mwingine bali ni Edward Lowassa.

Tufanye nini? kimsingi hakuna cha kufanya kwa wakati huu, lakini rekodi iwekwe wazi kuwa Rostam si msafi kama anavyojidai, Kikwete si msafi kama wengi wanavyoamini (I already pointed this out over a year ago) na Bangusilo msabaha si msafi licha ya kulia kwake bungeni.

This is what we have, and this is what we have to deal with.
 
Aisee...I can't recall any....unasikia tu flani anatuhumiwa na hiki na kile.....anajiuzulu....halafu bado anaendelea kupeta....mweeeeeee

Nashukuru kwa wewe kulitambua hilo.Ila hiyo signature yako say it all lakini siyo wakati wote Miafrika ndivyo Tulivyo. kuna nchi nyingine kama Botswana imekaza mikataba yake na tukaona manufaa ya wao kufanya hivyo na sisi tukiadhibu hawa mafisadi accordingly na kutengeneza mikataba mizuri tabidi ubadilishe hiyo signature yako ya kwamba'Miafrika ndivo Tulivyo'.
 
Kumbe mwisho wa siku suala hili la Richmond itaamishiwa jeshini pia.

Ndio maana huyu bwana anaomba mwenye ushaidi aende mahakamani.
 
kamati ya mwakyembe ingewahoji hao watu wawili, nafikiri ingeweza kuthibitisha bila doubt nani mmiliki wa richmond na dowans....
lakini kwa vile serkali haikutaka watu hao wahojiwe, ndio ukakuta "wakaenda nje ya nchi" na hawakulazimishwa kutoa ushahidi wowote baadae.
rostam lazima ajitape kwa mengi kwa sababu anajua hawezi kwenda chini peke yake, na kiongozi wajuu kabisa hawezi kuruhusu kuanguka naye.
 
I couldn't agree more! Ni kweli kuwa Kikwete ni mtu muhimu sana katika hii kashfa ya Richmond, hilo halina ubishi kabisa. Hata ushahidi wa kimazingira unasuggest hivyo, na ndio maana yeye kama rais anajaribu kujiweka mbali sana swala hili bila kutoa comments zozote za msingi zinazoweza kusaidia kutatua utata uliopo mpaka sasa. Tunapaswa kuelekeza nguvu zetu kwake kuanzia sasa if by any chance we need to win this battle.

Haya, kama Richmond ina maandishi ya Kikwete kila sehemu (written all over him) na kuna ushahidi wa kutosha kuonyesha hivyo, CCM au mgombea wao, ingekuwa kwingine duniani, uwezekano wa yeye kushinda uchaguzi mkuu wa 2010 ungekuwa mdogo sana. Pamoja na yote haya ya ufisadi, licha ya wananchi kuyajua bado watampigia kura na sitashangaa baadhi ya watu humu humu foramuni wanaompinga nao wakimpigia kura na kumuunga mkono. Ndio maana nasema hatuna recourse yoyote zaidi ya kupiga makelele.........It's just mind boggling
 
NN.. the first thing is to call a spade a spade. In this case.. the evil triune of corruption made of Kikwete, Rostam, and Msabaha ndio waliingiza RDC. Na katika kufanya hivyo wakapata mtu mmoja mwenye nguvu ya kukamilisha hicho kwa amri yake na ambaye ni mtu wa amri.. naye si mwingine bali ni Edward Lowassa.

Tufanye nini? kimsingi hakuna cha kufanya kwa wakati huu, lakini rekodi iwekwe wazi kuwa Rostam si msafi kama anavyojidai, Kikwete si msafi kama wengi wanavyoamini (I already pointed this out over a year ago) na Bangusilo msabaha si msafi licha ya kulia kwake bungeni.

This is what we have, and this is what we have to deal with.

Sasa ndani ya chama cha mapinduzi kuna mapambano kutaka kufukuza mafisadi. Je wanaotaka kufukuza mafisadi wataweza kweli? Mafisadi ni wakuu wa chama. Je wafanyeje?

Kazi ni ngumu kweli kweli ndio maana kuna mtu alisema ufisadi ni ajari ya kisiasa tu
 
Nilitegemea wizara ya sheria ndio ingekuwa full force na hii issue lakini vilaza wanasubiri payroll tuu na hawajui wafanye nini,naanza kupata wasiwasi kama kweli RO ndio fisadi mkubwa maana hata mwakyembe alishindwa kumtaja na hakuna hata mtu amewahi kusema kutuhakikishia hizo kampuni za umeme ni zake,tunachezewa akili tuu hapa waliocheza deal zote za Richmond wanajulikana ila basi tuu spin master wametuzidi akili.
 
Nashukuru kwa wewe kulitambua hilo.Ila hiyo signature yako say it all lakini siyo wakati wote Miafrika ndivyo Tulivyo. kuna nchi nyingine kama Botswana imekaza mikataba yake na tukaona manufaa ya wao kufanya hivyo na sisi tukiadhibu hawa mafisadi accordingly na kutengeneza mikataba mizuri tabidi ubadilishe hiyo signature yako ya kwamba'Miafrika ndivo Tulivyo'.

I am not going to change my signature until Miafrika know how to act and that is to act like Sivyo Tulivyo. But as long as we continue to act and behave the way we do, my signature still holds true. Sasa kama raisi mwenyewe (allegedly) ni fisadi hivi unategemea nini la maana litakalofanyika kutoka kwake? Ni sisi wananchi ndo inabidi tuyashikishe adabu haya matuhumiwa ya ufisadi. Tukishindwa tutakuwa Ndivyo Tulivyo maana siamini kama tukiamua yatatushinda. Yako machache mno kulinganisha na sisi wananchi wa kawaida. Mimi sikumuunga mkono 2005 na 2010 hapati kura yangu, ng'o!!!
 
Kama Kikwete alihusika katika haya yote inakuwaje huyu mtu anajitenga kama vile hakushiriki kwenye kitu chochote?Hivi Tanzania hii kweli hamna vitu kama Orange Revolution ya Ukraine iliyomuondoa madarakani Victor Yanukovich alipoiba kura na kukaa madarakani.Yaani hamna mtu influential wa kuinfluence such a revolution?
 
Back
Top Bottom