Its too late, hata aende mkapa bado hali ni tete CCM. Na taarifa yenyewe imetolewa na Nape, mzee wa propaganda!! Kwa hiyo ni sehemu ya kazi zake kuwahadaa wapinzani wake.
Hongera kwa kuamua kujiunga na kutumia jf kama mahali pa kutoa habari na maoni yake kama haki yako ya kikatiba!
Humu jf, viongozi wengi wa cdm, ccm na cuf ni member. Kwahiyo wakujipanga, wakuchukua tahadhari na wakujilinda, wote wamekusoma. Hope wataifanyia kazi hii thread!
Tatizo lenu hamuunganishi doti. kumbukeni mkapa ndo aliyemweka Rostam kuwa mweka hazina wa chana na Kikwete akaja akamtoa na kumweka amos makala. kwa hiyo kupitia kwa mkapa wanaigunga watajua huyu ni swahiba wa mbunge wao waliyekuwa wakimpenda no matter iwe kwa pesa zake au kwa vyovyote vile iwavyo. kwa hiyo mkapa is the right choice at a right time and right place kwa ccm.
Natamani kama ccm wangelipoteza hilo jimbo. it could sound good. walk up wapinzani.
Nadhani atakuwa ni msaada mkubwa sana kwa CCM. Huyu mzee huwa haogopi mtu yeyote, nakumbuka alivyodiriki kuwaita Chadema KOKOTO pale Jangwani. Chadema walilalamika sana lakini jamaa hata hakuogopa.
Ni mkapa yupi huyo! Ben Mkapa wa ccm!?
Huyu aliyejibinafsishia kiwira kwa 70mil baada ya psrc kudhaminisha kwa 700mil?
Ni huyu ambaye baada ya miaka mi3 tu ikulu Mrema akasema amehongwa 500mil na alipomshtaki akashindwa kesi!?
Ni huyu aliyejiuzia nyumba ya serikali masaki kwa 60mil baada ya kuikarabati kwa 60bil!?
Ni huyu serikali yake ilisema hata tukila nyasi, lazima anunuliwe ndege!?
Ni huyu aliyewavua uraia watanzania waliokuwa wakipingana na utawala wake!?
Ni huyu aliyesema anaingiliwa na waingereza waliposema rada imenunuliwa kifisadi!?
Ni huyu ambaye serikali yake chini ya Chenge waliingia mikataba yote ya kinyonyaji ya madini!?
Ni yupi huyo?
Au ni Ken Mkapa wa Yanga!
Kama ni yeye basi amejisahau sana maana alisema hataongea kitu kwa kuwa huwezi kuzuia mtu kusikia ila kuongea ni maamuzi yake!
Hebu ngoja tumsikie!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.