Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Kuna taarifa za uhakika kuwa yule mwandishi mkongwe wa habari Corp, kampuni inayomilikiwa na fisadi Rostam Aziz, Mayage S. Mayage ameikimbia kampuni hiyo kwa kuwa imeshindwa kumuongezea mshahara.
Mayage ameondoka huku akiwa hajalipwa mishahara yake ya Septemba, Oktoba na Novembana mwaka jana. Aidha, Mayage ameondoka huku akiwa anadai kiinua mgongo cha mamilioni ya shilingi baada ya kuitumikia kampuni hiyo kwa miaka 14, tokea ilipokuwa chini ya karani wa Richmond, Salva Rweyemamu.
Taarifa zilizopo ni kwamba Mayage amepanga kumfikisha mahakamani Rostam akitaka kulipwa haki zake. Mbaya mkuu wa Mayage katika hili ni Hussen Bashe na mwandishi mmoja mkongwe aliyepo ndani ya chumba cha habari ambaye aligoma Mayage kuongezwa mshahara. Kuondoka kwa mwandishi huyu, kutaliuwa kabisa gazeti la Rai. Mwenye taarifa nyingine juu ya suala hili, tafadhari atujuze.
Mayage ameondoka huku akiwa hajalipwa mishahara yake ya Septemba, Oktoba na Novembana mwaka jana. Aidha, Mayage ameondoka huku akiwa anadai kiinua mgongo cha mamilioni ya shilingi baada ya kuitumikia kampuni hiyo kwa miaka 14, tokea ilipokuwa chini ya karani wa Richmond, Salva Rweyemamu.
Taarifa zilizopo ni kwamba Mayage amepanga kumfikisha mahakamani Rostam akitaka kulipwa haki zake. Mbaya mkuu wa Mayage katika hili ni Hussen Bashe na mwandishi mmoja mkongwe aliyepo ndani ya chumba cha habari ambaye aligoma Mayage kuongezwa mshahara. Kuondoka kwa mwandishi huyu, kutaliuwa kabisa gazeti la Rai. Mwenye taarifa nyingine juu ya suala hili, tafadhari atujuze.