ROSTAM Aziz ashindwa kulipa mishahara wafanyakazi wake, waanza kutimka

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Kuna taarifa za uhakika kuwa yule mwandishi mkongwe wa habari Corp, kampuni inayomilikiwa na fisadi Rostam Aziz, Mayage S. Mayage ameikimbia kampuni hiyo kwa kuwa imeshindwa kumuongezea mshahara.

Mayage ameondoka huku akiwa hajalipwa mishahara yake ya Septemba, Oktoba na Novembana mwaka jana. Aidha, Mayage ameondoka huku akiwa anadai kiinua mgongo cha mamilioni ya shilingi baada ya kuitumikia kampuni hiyo kwa miaka 14, tokea ilipokuwa chini ya karani wa Richmond, Salva Rweyemamu.

Taarifa zilizopo ni kwamba Mayage amepanga kumfikisha mahakamani Rostam akitaka kulipwa haki zake. Mbaya mkuu wa Mayage katika hili ni Hussen Bashe na mwandishi mmoja mkongwe aliyepo ndani ya chumba cha habari ambaye aligoma Mayage kuongezwa mshahara. Kuondoka kwa mwandishi huyu, kutaliuwa kabisa gazeti la Rai. Mwenye taarifa nyingine juu ya suala hili, tafadhari atujuze.
 
Kuondoka kwake sio issue kubwa ha jf issue huyo boss wake atekeleze sheria ya ajira hapa nchini na pia atuwezi kujua terms and condition of the contract aliyosign na huyo boss wake well kama amekiuka sheria za ajira then achukuliwe hatua kali za kisheria ila sio swala la kushabikia hapa jf
 
jamani hapa JF tuache mambo ya kuficha uchafu, kwa nini hamumtaji huyo mwandishi mbaya wake na mayage? ama sivyo mtanaonekana wambeya. huyo bwana ni Danny Mwakiteleko huku yeye akiwa analipwa mshahara mkubwa aliyotetewa na kuwekewa na yule mkurugenzi aliyewatoa waandishi tongotongo Rosemary Mwakitwange, yeye anabania wenzake jambo la ajabu kabisa. kuhusu kufa kwa gazeti la RAI hiyo sio business ya JF maana gazeti hili lilishakufa miaka mingi msiwadanganye wakafikiri wana gazeti
 
Back
Top Bottom