Rostam Aziz apewa kibali kujenga Kiwanda kikubwa cha Gesi ya Kupikia jijini Mombasa

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,867
141,804
Bilionea aliyewahi kuwa Mhazini wa CCM na Mbunge wa Igunga ambaye pia aliombwa na Shujaa Hayati Magufuli agombee Ubunge wa Morogoro mjini, Rostam Aziz amepewa kibali cha kujenga kiwanda kikubwa cha Gesi ya kupikia jijini Mombasa

Kibali hicho kimetolewa kwa Rostam Aziz kupitia kampuni yake ya Taifa Gas

Chanzo: The Citizen
==
Kenya imeipa leseni kampuni ya Taifa Gas iliyoanzishwa na bilionea Rostam Aziz kutoka Tanzania kuanzisha kiwanda cha gesi ya kupikia na kituo cha kuhifadhi gesi katika bandari ya Mombasa. Taifa Gas ni kampuni kubwa zaidi ya usambazaji wa gesi ya kupikia nchini Tanzania na sasa inataka kupanua shughuli zake nchini Kenya na kupigania sehemu kubwa ya soko la gesi ya kupikia.

Hii itaanzisha ushindani mkali na wauzaji wengine wa mafuta kama Vivo, Rubis na Total katika udhibiti wa kaya 2.87 milioni za Kenya (asilimia 23.9 ya kaya za Kenya) zinazotumia gesi ya kupikia. Ujenzi wa kiwanda hicho utakuwa karibu na kiwanda cha Africa Gas and Oil Ltd kinachomilikiwa na bilionea Mohamed Jaffer, na unatarajiwa kupunguza gharama za gesi ya kupikia na kuwarahisishia wauzaji kuhamishia punguzo la gharama kwa watumiaji.
 
24 February 2023
Likoni, Mombasa
Kenya

Rais William S. Ruto mgeni rasmi, aweka jiwe la msingi katika mradi mkubwa wa Taifa Gas leo Mombasa



Pia mwenyekiti wa Taifa Gas Bw. Rostam Aziz akazia fursa za uchumi wa gesi akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa Taifa Gas Kenya, shughuli hiyo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh. William S. Ruto.

Rostam Aziz anasema ni wakati wa nchi jirani kufungua mipaka ili kuwezesha biashara zinazovuka mpaka baina ya nchi za Kenya na Tanzania ziweze kuongezeka maradufu kwa manufaa ya uchumi na maisha ya wananchi wa nchi hizi mbili zilizo na uhusiano wa karibu.


Pia hafla hiyo ilihudhuriwa na Naibu wa rais wa Kenya Mh. Geoffrey Rigathi Gachagua pamoja na viongozi wengine wa serikali kuu kama waziri wa uwekezaji Mh. Moses Kuria na maafisa wa serikali ya kaunti wakiongozwa na gavana Abdulswamad Nassir wa kauti ya Mombasa.

Balozi wa Tanzania nchini Kenya Dr. John Stephen Simbachawene naye alipata fursa kuongelea maslahi mapana ya uchumi unaounganisha nchi hizi mbili za Afrika ya Mashariki na balozi kwa niaba ya Rais Dr. Samia S Hassan wa Tanzania aliwasilisha salaam kwa Dr. William S. Ruto na kupongeza ukurasa wa kufungua nchi hizi kiuchumi na kibiashara pia.
Source : State House Kenya
 
Sijui kwann bongo tunamuona namna gani siyo
Mengi walimnyima Kilimanjaro Hotel kisa eti mchaga. Yani nikikumbua inaniuma. Mengi alisema kabisa angekuwa mbali zaidi alivyokuwa isingekuwa kubaniwa na vizingiti. Wakaenda kuwauzia waarabu iyo Kilimanjaro Hotel kwa bei ya kutupwa. Na ndio yule lijamaa linaongeaga broken English aliratibu. Lissu alimpelekeshaga kwenye mahojiano ya shaka ssali straight talk Africa
 
Mengi walimnyima Kilimanjaro Hotel kisa eti mchaga. Yani nikikumbua inaniuma. Mengi alisema kabisa angekuwa mbali zaidi alivyokuwa isingekuwa kubaniwa na vizingiti. Wakaenda kuwauzia waarabu iyo Kilimanjaro Hotel kwa bei ya kutupwa. Na ndio yule lijamaa linaongeaga broken English aliratibu. Lissu alimpelekeshaga kwenye mahojiano ya shaka ssali straight talk Africa
Muhongo alisema uwekezaji wanaouweza ni kwenye juice 😃
 
Mengi walimnyima Kilimanjaro Hotel kisa eti mchaga. Yani nikikumbua inaniuma. Mengi alisema kabisa angekuwa mbali zaidi alivyokuwa isingekuwa kubaniwa na vizingiti. Wakaenda kuwauzia waarabu iyo Kilimanjaro Hotel kwa bei ya kutupwa. Na ndio yule lijamaa linaongeaga broken English aliratibu. Lissu alimpelekeshaga kwenye mahojiano ya shaka ssali straight talk Africa
Tunahusudu passport na VISA
 
ROSTAM AZIZ ATOBOA SIRI NA KUTOA SOMO JUU YA UWEKEZAJI WAKE WA THS. TRILIONI 1 KAMPUNI YA KIMATAIFA YA TIGO UTAKAVYONUFAISHA TANZANIA


Watanzania tuone fahari kuwa biashara kubwa sana kimataifa zikimilikiwa na watanzania maana kuna faida kubwa kupitia kodi, mgao wa faida, matumizi ya faida kutumika ndani, kufaidi teknolojia mpya, pia hali hiyo itavutia wawekezaji wengi zaidi kutoka na mazingira ya kuwepo wawekezaji wa ndani wenye ubavu wa kipesa wenye kuelewa mazingira ya Tanzania.

Mitaji wa uwekezaji ni sawa na bidhaa yoyote inayotafuta soko hivyo ili soko letu liweze kuvutia mitaji mikubwa kimataifa ni lazima nchi kujenga mazingira ya kuvutia soko la mitaji ili wawekezaji wawekeze Tanzania na siyo nchi nyingine au kupitia nchi zingine zinazoonekana ni wajanja zaidi.

Ndiyo maana nchi ya Tanzania sasa inafunguliwa katika awamu hii ya sita na wafanyabiarasha wa kitanzania lazima wawe tayari kunyakua fursa hiyo kwani inawekezaka

Rostam Aziz anasisitiza waTanzania tubadilishe mtizamo (mindset) kuhusu Biashara na Uwekezaji mkubwa tujitutumue na pia tufurahie mtanzania mwenzetu anapopata fursa na
wafanyakazi ktk ofisi za serikali wasiwe vikwazo kwa waTanzania kuingia ubia na makampuni makubwa ya uwekezaji kutpka nje na media za habari pia zibadilike zifurahie watanzania kunufaika.
 
Nyie si mmetoka kuaminishwa kuwa kila mwenye hela ni fisadi/mtu wa madili!!!! Acha tuendelee na ujinga wetu.....
 
Back
Top Bottom