TANZIA Rose Nyerere, Mtoto wa Mwisho wa J.K Nyerere afariki dunia

Kikwete atakwenda kumpa pole mama Maria kwani Mwalimu alimlea sana!!! Hata hivyo Kikwete kwenye mambo ya misiba ya watu aliowafahamu huwa hakosi akipata nafasi; juzi nilimuona kwenye msiba wa Costa Ndunguru [ former classmate wake]!
Rais Mstaafu Kikwete akitangaza Nafasi ya Kazi ya Msemaji wake / Afisa Habari wake nakushauri usiache Kuiomba kwani unajua Kumsemea mno.
 
Rais Mstaafu Kikwete akitangaza Nafasi ya Kazi ya Msemaji wake / Afisa Habari wake nakushauri usiache Kuiomba kwani unajua Kumsemea mno.

Huyo kwangu ni bwana mdogo hawezi kuniajiri ingawa ni Rais mstaafu!!! Hapendezewi watu waliomzidi umri kuwa chini yake; ndio maana aliona busara Sitta asiwe Waziri Mkuu chini yake akampa Kuwa speaker na mdogo kwake Lowassa akawa Waziri Mkuu!!!
 
Bila shaka huyo ndiye Rose, huyo Anna kafanana sana na marehemu babaye....

Rose aliye na miwani, Anna wa kulia

gz2(2).jpg
Poleni wafiwa kwa msiba huu mkubwa wa mpendwa wenu Rose!!!
 
Umuofia Kwenu wana JF,

Kheri ya Mwaka Mpya!

Mtoto wa mwisho wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Rose Nyerere amefariki leo mjini Dar es Salaam.

Taarifa za duru za uhakika zinaarifu kuwa Rose amefariki katika hospitali ya Mzena Jijini Dar es Salaam ambako alilazwa kwa muda mrefu. Bwana alitoa bwana ametwaa jina lake lihidimiwe.

View attachment 1665226

KK,
MINJINGU.

Dar es Salaam. Familia ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere imepata msiba wa mtoto wao Rosemary Nyerere aliyefariki jana jioni jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa wanafamilia aliyejitambulisha kwa jina la Sophia Nyerere ameandika katika mtandao wa Instagram kuwa shangazi yake amefariki.
Mwananchi limewatafuta baadhi ya wanafamilia akiwemo Manyerere Jacton aliyethibisha kuwa ndugu yao amefariki.

"Ni kweli dada amefariki jioni hii, lakini taarifa rasmi itatolewa," amesema Manyerere.

Rosemary alikuwa miongoni mwa watoto saba wa Mwalimu Nyerere
Jf hadi leo hamjaipata hio taarifa rasmi?
 
Mike wake aliitwa David Mwamakula alikuwa ni Mhasibu Tanesco HQ na waliishi Keko NHCila wakati anafariki walisha tengana kitambo.
Mtoto wa Rais anaishi na mmewe kotas za NHC Keko Magurumbasi ??!!! Aiseeee..

Ninachojua marehemu pia aliishi kwenye vi flats vya NHC Upanga mitaa ya Palm Beach, I guess baadae aliondoka huko Keko Machungwa.....

Inakuonyesha Nyerere alivyotaka kuishi sawa na watu anaowaongoza, masikini wachafu.

Kuna Rais mmoja mstaafu watoto wake wanamiliki ma apartment buildings na ma condominiums Mikocheni na Sea View!

Sasa unajiuliza kama Rais anaweza kupata ukwasi huo kihalali (mafao, mshahara, mfuko wa Rais, travel allowances, zawadi za matajiri) huyo Nyerere yeye pesa yake ya Urais miaka 25 alikuwa anaipeleka wapi, kuhonga ????
 
Mtoto wa Rais anaishi na mme wake kotas za NHC Keko Magurumbasi ??!!! Aiseeee..

Ninachojua marehemu pia aliishi kwenye vi flats vya NHC Upanga mitaa ya Palm Beach, I guess baadae aliondoka huko Keko Machungwa.....

Inakuonyesha Nyerere alivyotaka kuishi sawa na watu anaowaongoza, masikini wachafu.

Kuna Rais mmoja mstaafu watoto wake wanamiliki ma apartment buildings na ma condominiums Mikocheni na Sea View!

Sasa unajiuliza kama Rais anaweza kupata ukwasi huo kihalali (mafao, mshahara, mfuko wa Rais, travel allowances, zawadi za matajiri) huyo Nyerere yeye pesa yake ya Urais miaka 25 alikuwa anaipeleka wapi, kuhonga ????
Yeye alikuwa analisha watoto wake,kuzaa taifa zima lenye watu zaidi ya milioni Thelathin si kazi ndogo.Anasema ukitembea barabarani ukakutana na mtu ana njaa ama yuko uchi inakuuma ,unasema huu Ni mzigo wangu.Kwa jinsi alivyokuwa utilitarianist asingeweza kujilimbikizia Mali.Alitaka sisi sote watoto wake tufanane,tusiwe na matabaka.
 
Back
Top Bottom