Ronaldo de Lima: Barcelona hawana Upendo na Wachezaji wa Kibrazil

bryan2

JF-Expert Member
Jun 8, 2016
3,323
4,667
Mshambuliaji gwiji huyu amefunguka maneno haya wakati akimshauri kijana Coutinho juu ya uhamisho wake kwenda pale Barcelona.

Ronaldo amefunguka na kusema Barcelona hawana upendo na wachezaji wa Kibrazil akiwemo yeye mwenyewe wakati akicheza ndani ya wababe hao wa pasi nyingi pale jimbo la catalunia,ameenda mbali zaidi na kutaja wachezaji kama Romario,Rivaldo na fundi Ronaldodihno na kusema wote hawa hawajaondoka vizuri pale Barcelona.

Pia ametoa mfano wa siku za Karibuni juu ya kijana Neymar na kusema naye hajaondoka vizuri pale Barcelona na kusema mpaka leo kuna kesi juu ya uhamisho wake kwenda kwa matajiri wa Paris PSG(Paris saint German).

Binafsi napenda soka zuri la Barcelona ila haya maneno ya Ronaldo de lima yameniacha na ukakasi kidogo tukumbuke kijana mwingine wa Kibrazil Paulinho yupo pale Barcelona na amekua akipewa muda wa kutosha tu wakucheza na wakali hao wa Katalunia.

Je maneno ya Ronaldo yanaukweli ndani yake au ni chuki binafsi tu?ni muda wa Coutinho kuamua mbivu na mbichi.
 
Nani angeendelea kukaa na Dinho ambaya alikuwa akikesha anangonoka?kama waliondoka vibaya kwa nn hawakufanya vizuri zaidi huko walikokwenda?
Na kuongeza hapo wachezaji wa kibrazil wanatabia za kujisahau sana starehe kwa wingi Copa cabana,ngoma za Samba sidhani kama kuna kocha atavumilia mchezaji asiyejituma.

Ref...Pato,Robinho,Fabinho,Adrian wa inter milan wamepotea wakati dunia bado inawahitaji.
 
Neymar alimkimbia Messi kwani alijua fika hawezi tamba mbele ya Leo Messi na pia kuondoka kwa Dinho si kipimo tosha kuwa FC Barca haiwapendi wachezaji wa kibrazil.. Itoshe kusema tu Barcelona inachukiwa kutokana na mafanikio yake na wale wafuasi Mamluki waliotoka MUFC na kumfuata CR7 ikiwemo mtoa kioja....
 
sio Wabrazil tuu hata ambao. sio. asili ya Catalumya wanatengwa na mwisho sanaondoka kwa fedheha.. ref Erick Abidal na Samuel Etto
Kiongozi huyu Erik Abidal mbona Barcelona wanamjali sana hata baada ya kupata matatizo ya Ini wachezaji walivaa tshrit kumsaport na pia kama Sikosei kwa sasa anafanya kazi kwenye Ofisi za Barcelona mitaa ya Katalunya.

Kwa Etoo sina uhakika ila rumours nlisikia jamaa alibaki kidogo afikie idadi ya magoli ambayo ukifika unajengewa mnara wa Heshima ila nasikia Uafrika wake ukamponza na kumuuza kabla hajafikia hayo magoli.

Walikua hawataki jamaa ajengewe mnara wa heshima ila naziita rumours manake zina chanzo makini cha habari.
 
nawashangaa sana waafrika wanaowashabikia hawa wabaguzi Baecelona.......Barcelona wanawabagua sana wachezaji wenye asili ya Afrika....hii timu siipendi bora ife tu
 
Ronaldinho alikuwa na Halali ya kupigwa chn maana mazoezi alikuwa Hahudhurii....Anakesha Club....starehe nyingi kwahio hakuna kocha angeeza kumvumilia.

Samuel Etoo alikuwa Mbinafsi na Pep kwa Falsafa yake hakutaka Mchezaji Mbinafsi akamuuza etoo akamreplace na zlatan....kumuuza mchezaji mzuri sio ubaguzi bali unakuta ha fit kwenye mipango ya kocha ni kama zidane alivomuuza James na Morata
 
inajulikana wabrazil wanapenda raha sana,coutihno ni mkubwa anajua anacho fanya ikitokea kaenda na yeye akazingua ni yeye na pia Kama bro wake paulihno akiwa na tabia flani ni wazi na yeye anaweza angukia huko huko
 
Mwekundu, Mandella, TheMasson,,PrinceKunta Asanteni sana mmemaliza kila kitu....God bless u

Huyo Ronaldo kitambi kinamsumbua sana, atuondolee ubrazili wake,, hana chochote anatafuta kick tu...nyambafu kabisa.amekuwa nani yeye, pimbi tu!


Huyo Gaucho kiwango chake kilishuka kabisa likawa limzigo sana pale Barca hata yanga wasingempokea kwa kiwango chake. Na huyo coutinho wao sijui kotini hatumuhitaji pale Barca, tunao wengi tu....hawa wabrazili wanataka kuleta ubrazili wao end of the day wanatuharibia timu yetu,,, mfano mzuri kwa Gaucho since ameripoti Barca hakuna mataji mengi ameipatia timu, na isitoshe walikuwepo wakina etoo na henry walikuwa wanakipiga sana tu....Timu ya Barca inataka wachezaji wenye akili zilizotulia na wenye kujituma kama vile KING.
 
Back
Top Bottom