Roman Abramovich: Utajiri wa Damu, Risasi na Umafia

ROMAN ABRAMOVICH: MABILIONI YA DAMU, RISASI NA UMAFIA




SEHEMU YA 12


Mara ya mwisho nilieleza kuhusu vyombo vya habari vinavyomilikiwa na maoligarch wakiongozwa na Berezovsky walinyoanza kumkosoa Putin kwa lengo la kumuharibia kwa wananchi na hatimaye iwe rahisi kwao kumuondoa madarakani. Baada ya ukosoaji huu Putin kwenye moja ya hotuba zake aliwaambia wananchi kwamba kuna ‘genge’ la maoligarch wanaomiliki vyombo vya habari wanaendesha kampeni ya kumchafua kwa malengo yao ya kisiasa.

Unakumbuka nilieleza kwamba katika kipindi hiki Berezovsky alikuwa amejiingiza kwenye siasa. Alikuwa ni mwakilishi kwenye Bunge la Duma (GosDuma). Kwa hiyo madai haya ya Putin kwamba Berezovsky na wenzake wanamchafua kwa malengo ya kisiasa yalipata mashiko kwa sababu Berezovsky alikuwa ni mwanasiasa. Kwa hiyo wananchi waliona hii ilikuwa kama ni ‘move’ ya Berezovsky kuutaka urais wa Urusi. Wengi hawakupendezwa na hili maana walihisi huu haukuwa wakati sahihi kubadili Rais wa nchi kwa kuzingatia kwamba nchi ilikuwa kwenye mzozo mkubwa huko Chechenya na pia ulikuwa umepita muda mchache tu tangu kumbadilisha rais wa awali, Boris Yeltsin.

Ajabu ni kwamba baada ya hotuba hii ya Putin, safari hii sio tu kwamba Berezovsky alitumia vyombo vyake vya habari kumpinga Putin bali aliitisha mkutano na wanahabari na kumkosoa Putin na sera zake wazi wazi.

Putin na Abramovich hawakutaka kukurupuka kumshughulikia Berezovsky. Walikuwa na uwezo wa kutumia vyombo vya ulinzi kumkamata na kumtia gerezani Berezovsky lakini hii isingekuwa na ufanisi sana kwa sababu tatizo halikuwa Berezovsky peke yake bali ni yeye na genge lake. Na isingekuwa busara kuwakamata maoligarch wote na kuwatia gerezani kwani kutokana na ushawishi wao ingeweza kuzua taharuki kubwa kwenye nchi. Sasa wanafanyaje? Wamuache Berezovsky aendelee kutamba kwenye vyombo vya habari na kumchafua Rais?

Hapana… nyoka akiingia ndani ya shimo usizame na wewe kumfuata… msubiri juu. Hawezi kukaa shimoni milele… msubiri atokeze kichwa juu… mfyeke na upanga.

Usiwe na pupa,
Subiri…


Nilieleza kuhusu Badri Patarkatsishvili rafiki mkubwa wa Berezovsky ambaye alimletea Russia kusimamia Televisheni yake. Berezovsky na Badri walikuwa marafiki haswa lakini kulikuwa na mtu ambaye alikuwa rafiki mkubwa zaidi wa Berezovsky, rafiki wa kushibana haswa, rafiki wa damu haswa, mboni ya jicho kweli kweli ya Berezovsky. Huyu alikuwa anaitwa Nikolai Glushkov. Licha ya urafiki wao lakini pia walikuwa washirika wakubwa kwenye biashara.

Sasa turudi nyuma kidogo,
Pale Russia kuna shirika la ndege la umma linaitwa Aeroflot. Shirika hili ni moja ya mashirika kongwe zaidi ya ndege duniani. Mwaka 1995 Glushkov aliteuliwa kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Aeroflot. Baada ya mwaka mmoaja tangu kuteuliwa kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu kuna skandali kubwa aliibua japo haikufika kwa umma wakati ule lakini ilikuwa tafrani kubwa ndani ya ‘system’ ya serikali ya Russia.
Kipindi hicho ndani ya shirika kulitokea mkanganyiko mkubwa sana juu ya mapato ya shirika na matumizi yake. Glushkov akajipa jukumu la kuchimba ni nini hasa kilikuwa kinaendelea. Baada ya uchunguzi wake wa miezi kadhaa akang’amua kwamba fedha zote za shirika ambazo zilikuwa zinapatikana kutokana na mauzo ya tiketi ya ndege zilikuwa zinapelekwa kwenye zaidi ya akaunti 352 zilizotawanyika sehemu mbalimbali duniani. Akaja kugundua kuwa akaunti hizi zilikuwa zinatumiwana mashirika ya Usalama ya FSB, SVR na GRU kw ajili ya kugharamia shughuli za ujasusi nje ya Russia. Nilieleza kuhusu FSB, hawa wanahusika hasa na Couter-Intelligence na usalama wa ndani ya Russia na mipakani. SVR hawa wanahusika hasa na ujasusi nje ya Russia. GRU wao kwa kifupi twaweza kusema ni kama chombo cha intelijensia ya jeshi.
Glushkov akagundua kuwa pia waajiriwa 3,000 katiya waajiriwa wote 14,000 wa shirika la Aeroflot walikuwa ni mashushushu wa FSB, SVR na GRU.

Glushkov akakasirika na kuwaandikia barua vyombo hivyo vyote vya ujasusi. Katika barua hiyo kwanza aliwalalamikia vyombo hivyo kutumia rasilimali vya Aeroflot kwa shughuli zao za ujasusi bila ruhusa ya bodi ya Aeroflot wenyewe. Pili, aliwapa ‘bili’, Kiasi chote cha hela ambao mashirika ya ujasusi yalipokea kutoka Aeroflot na kuwataka warejeshe kwenye shirika.

Glushkov hakuishia hapo tu bali pia alihakikisha fedha zote ambazo zililipwa kwenye akaunti zile 352 ambazo zilikuwa bado hazijatolewa, utaratibu unafanyika akauti wakazi-freeze na kuhakikisha zinatolewa kwenye akaunti hizo. Makosa makubwa yalifanyika hapo…

Unaweza kujiuliza Glushkov aliwezaje kufanya haya dhidi ya shirika la ujasusi kama FSB, SVR na GRU? Lakini tukumbuke kwamba hii ilikuwa ni mwaka 1996 kwenye utawala wa Yeltsin ambapo maoligarch ndio walikuwa ‘wenye nchi’. Glushkov alikuwa anaweza kujitutumua na kufanya yote haya kwa mgongo wa oligarch Boris Berezovsky rafiki yake wa damu wa kufa na kuzikana.

Turudi tulipoishia…. Nyoka akiingia shimoni hatumfuati… tunasubiri atokeze kichwa nje tumfyeke.

Baada ya Berezovsky kuendelea kumkosoa kwa kutumia vyombo vyake vya habari… Abramovich akaja na mkakati wa kumdhibiti.

Abramovich akafukua kaburi skandali ile ya Nikolai Glushkov rafiki kipenzi wa Berezovsky. Jambo moja ambalo kipindi kile mwaka 1996 halikufuatiliwa kwa kina ilikuwa ni namna gani fedha zile zilizobakia kwenye akaunti 352 zilitolewa. Kwa sababu kipindi kile Abramovich alikuwa ni kipenzi pia cha Berezovsky kwa hiyo kuna siri nyingi alikuwa anazijua. Mojawapo ya siri hizi zilikuwa ni nini ambacho kilitokea kwenye fedha ambazo zilihamishwa kutoka kwenye akaunti zile 352.

Fedha zili kwa maelekezo ya Glushkanov zilihamishwa kutoka kwenye akaunti zile 352 za idara za ujasusi na zote kuwekwa akaunti ya kampuni iliyosajiliwa nchini uswisi inayoitwa Andava. Kampuni hii ya Andava ilikuwa inamilikiwa na watu wawili, Nikolai Glushkov na Berezovsky. Kwa maana nyingine ni kwamba Nikolai Glushkov na Berezovsky walikuwa wamejichukulia fedha za kampuni ya umma ya Aeroflot ambazo zilikuwa zimelengwa zitumiwe na FSB, SVR na GRU.

Hii ilikuwa silaha ya kwanza ya Abramvich kumshughulikia Berezovsky.

Polisi walimkamata Glushkov na kumfungulia mashtaka ya ubadhirifu wa mali za umma. Siku chache baada ya Glushkov kukamatwa Berezovsky alikimbia Russia na kuomba ukimbizi wa kisiasa nchini Uingereza kwa maana alijua kuwa yeye pia alihusika kwenye kosa hilo ambalo Glushkov alishtakiwa nalo.

Hii haikuwa muarobaini kamili wa kumshughulikia Berezovsky kwani japo alikimbilia Uingereza lakini bado alikuwa anamiliki kituo kile cha televisheni na kampuni nyingine kadhaa ambazo zilikuwa na ushawishi kiuchumi na kisiasa ndani ya Russia.

Abramovich akapiga hatua ya pili ya mkakati wake na kusafiri moja kwa moja hadi Uingereza ambako Berezovsky alikuwa amekimbilia…

Inaendelea usiku huu…




Habibu B. Anga "The Bold" - 0759181457
To Infinity and Beyond
 
SEHEMU YA 12
Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij addenbwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA
 
ROMAN ABRAMOVICH: MABILIONI YA DAMU, RISASI NA UMAFIA




SEHEMU YA 12


Mara ya mwisho nilieleza kuhusu vyombo vya habari vinavyomilikiwa na maoligarch wakiongozwa na Berezovsky walinyoanza kumkosoa Putin kwa lengo la kumuharibia kwa wananchi na hatimaye iwe rahisi kwao kumuondoa madarakani. Baada ya ukosoaji huu Putin kwenye moja ya hotuba zake aliwaambia wananchi kwamba kuna ‘genge’ la maoligarch wanaomiliki vyombo vya habari wanaendesha kampeni ya kumchafua kwa malengo yao ya kisiasa.

Unakumbuka nilieleza kwamba katika kipindi hiki Berezovsky alikuwa amejiingiza kwenye siasa. Alikuwa ni mwakilishi kwenye Bunge la Duma (GosDuma). Kwa hiyo madai haya ya Putin kwamba Berezovsky na wenzake wanamchafua kwa malengo ya kisiasa yalipata mashiko kwa sababu Berezovsky alikuwa ni mwanasiasa. Kwa hiyo wananchi waliona hii ilikuwa kama ni ‘move’ ya Berezovsky kuutaka urais wa Urusi. Wengi hawakupendezwa na hili maana walihisi huu haukuwa wakati sahihi kubadili Rais wa nchi kwa kuzingatia kwamba nchi ilikuwa kwenye mzozo mkubwa huko Chechenya na pia ulikuwa umepita muda mchache tu tangu kumbadilisha rais wa awali, Boris Yeltsin.

Ajabu ni kwamba baada ya hotuba hii ya Putin, safari hii sio tu kwamba Berezovsky alitumia vyombo vyake vya habari kumpinga Putin bali aliitisha mkutano na wanahabari na kumkosoa Putin na sera zake wazi wazi.

Putin na Abramovich hawakutaka kukurupuka kumshughulikia Berezovsky. Walikuwa na uwezo wa kutumia vyombo vya ulinzi kumkamata na kumtia gerezani Berezovsky lakini hii isingekuwa na ufanisi sana kwa sababu tatizo halikuwa Berezovsky peke yake bali ni yeye na genge lake. Na isingekuwa busara kuwakamata maoligarch wote na kuwatia gerezani kwani kutokana na ushawishi wao ingeweza kuzua taharuki kubwa kwenye nchi. Sasa wanafanyaje? Wamuache Berezovsky aendelee kutamba kwenye vyombo vya habari na kumchafua Rais?

Hapana… nyoka akiingia ndani ya shimo usizame na wewe kumfuata… msubiri juu. Hawezi kukaa shimoni milele… msubiri atokeze kichwa juu… mfyeke na upanga.

Usiwe na pupa,
Subiri…


Nilieleza kuhusu Badri Patarkatsishvili rafiki mkubwa wa Berezovsky ambaye alimletea Russia kusimamia Televisheni yake. Berezovsky na Badri walikuwa marafiki haswa lakini kulikuwa na mtu ambaye alikuwa rafiki mkubwa zaidi wa Berezovsky, rafiki wa kushibana haswa, rafiki wa damu haswa, mboni ya jicho kweli kweli ya Berezovsky. Huyu alikuwa anaitwa Nikolai Glushkov. Licha ya urafiki wao lakini pia walikuwa washirika wakubwa kwenye biashara.

Sasa turudi nyuma kidogo,
Pale Russia kuna shirika la ndege la umma linaitwa Aeroflot. Shirika hili ni moja ya mashirika kongwe zaidi ya ndege duniani. Mwaka 1995 Glushkov aliteuliwa kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Aeroflot. Baada ya mwaka mmoaja tangu kuteuliwa kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu kuna skandali kubwa aliibua japo haikufika kwa umma wakati ule lakini ilikuwa tafrani kubwa ndani ya ‘system’ ya serikali ya Russia.
Kipindi hicho ndani ya shirika kulitokea mkanganyiko mkubwa sana juu ya mapato ya shirika na matumizi yake. Glushkov akajipa jukumu la kuchimba ni nini hasa kilikuwa kinaendelea. Baada ya uchunguzi wake wa miezi kadhaa akang’amua kwamba fedha zote za shirika ambazo zilikuwa zinapatikana kutokana na mauzo ya tiketi ya ndege zilikuwa zinapelekwa kwenye zaidi ya akaunti 352 zilizotawanyika sehemu mbalimbali duniani. Akaja kugundua kuwa akaunti hizi zilikuwa zinatumiwana mashirika ya Usalama ya FSB, SVR na GRU kw ajili ya kugharamia shughuli za ujasusi nje ya Russia. Nilieleza kuhusu FSB, hawa wanahusika hasa na Couter-Intelligence na usalama wa ndani ya Russia na mipakani. SVR hawa wanahusika hasa na ujasusi nje ya Russia. GRU wao kwa kifupi twaweza kusema ni kama chombo cha intelijensia ya jeshi.
Glushkov akagundua kuwa pia waajiriwa 3,000 katiya waajiriwa wote 14,000 wa shirika la Aeroflot walikuwa ni mashushushu wa FSB, SVR na GRU.

Glushkov akakasirika na kuwaandikia barua vyombo hivyo vyote vya ujasusi. Katika barua hiyo kwanza aliwalalamikia vyombo hivyo kutumia rasilimali vya Aeroflot kwa shughuli zao za ujasusi bila ruhusa ya bodi ya Aeroflot wenyewe. Pili, aliwapa ‘bili’, Kiasi chote cha hela ambao mashirika ya ujasusi yalipokea kutoka Aeroflot na kuwataka warejeshe kwenye shirika.

Glushkov hakuishia hapo tu bali pia alihakikisha fedha zote ambazo zililipwa kwenye akaunti zile 352 ambazo zilikuwa bado hazijatolewa, utaratibu unafanyika akauti wakazi-freeze na kuhakikisha zinatolewa kwenye akaunti hizo. Makosa makubwa yalifanyika hapo…

Unaweza kujiuliza Glushkov aliwezaje kufanya haya dhidi ya shirika la ujasusi kama FSB, SVR na GRU? Lakini tukumbuke kwamba hii ilikuwa ni mwaka 1996 kwenye utawala wa Yeltsin ambapo maoligarch ndio walikuwa ‘wenye nchi’. Glushkov alikuwa anaweza kujitutumua na kufanya yote haya kwa mgongo wa oligarch Boris Berezovsky rafiki yake wa damu wa kufa na kuzikana.

Turudi tulipoishia…. Nyoka akiingia shimoni hatumfuati… tunasubiri atokeze kichwa nje tumfyeke.

Baada ya Berezovsky kuendelea kumkosoa kwa kutumia vyombo vyake vya habari… Abramovich akaja na mkakati wa kumdhibiti.

Abramovich akafukua kaburi skandali ile ya Nikolai Glushkov rafiki kipenzi wa Berezovsky. Jambo moja ambalo kipindi kile mwaka 1996 halikufuatiliwa kwa kina ilikuwa ni namna gani fedha zile zilizobakia kwenye akaunti 352 zilitolewa. Kwa sababu kipindi kile Abramovich alikuwa ni kipenzi pia cha Berezovsky kwa hiyo kuna siri nyingi alikuwa anazijua. Mojawapo ya siri hizi zilikuwa ni nini ambacho kilitokea kwenye fedha ambazo zilihamishwa kutoka kwenye akaunti zile 352.

Fedha zili kwa maelekezo ya Glushkanov zilihamishwa kutoka kwenye akaunti zile 352 za idara za ujasusi na zote kuwekwa akaunti ya kampuni iliyosajiliwa nchini uswisi inayoitwa Andava. Kampuni hii ya Andava ilikuwa inamilikiwa na watu wawili, Nikolai Glushkov na Berezovsky. Kwa maana nyingine ni kwamba Nikolai Glushkov na Berezovsky walikuwa wamejichukulia fedha za kampuni ya umma ya Aeroflot ambazo zilikuwa zimelengwa zitumiwe na FSB, SVR na GRU.

Hii ilikuwa silaha ya kwanza ya Abramvich kumshughulikia Berezovsky.

Polisi walimkamata Glushkov na kumfungulia mashtaka ya ubadhirifu wa mali za umma. Siku chache baada ya Glushkov kukamatwa Berezovsky alikimbia Russia na kuomba ukimbizi wa kisiasa nchini Uingereza kwa maana alijua kuwa yeye pia alihusika kwenye kosa hilo ambalo Glushkov alishtakiwa nalo.

Hii haikuwa muarobaini kamili wa kumshughulikia Berezovsky kwani japo alikimbilia Uingereza lakini bado alikuwa anamiliki kituo kile cha televisheni na kampuni nyingine kadhaa ambazo zilikuwa na ushawishi kiuchumi na kisiasa ndani ya Russia.

Abramovich akapiga hatua ya pili ya mkakati wake na kusafiri moja kwa moja hadi Uingereza ambako Berezovsky alikuwa amekimbilia…

Inaendelea usiku huu…




Habibu B. Anga "The Bold" - 0759181457
To Infinity and Beyond
Asante
 
Habibu B. Anga,
Kwa akili ya haraka haraka tu suala kama hili haliwezekani likafanyika kwenye nchi za magharibi au hata hapa Afrika leo hii. Lakini hivyo ndivyo mambo yalivyoendeshwa kihuni nchini Rusia miaka ya tisini na mwanzo mwa 2000. Hiyo ndio maana hasa ya 'Wild Wild East.!""

Mwandishi, hapo penye kivuli (bolded paragraph) ''nimepatoa kwenye utunzi wako'' hii inafanyika hata sasa tena kote duniani siyo ulaya, Russia, Asia tena Afrika ndiyo watu wanauana kila sekunde kama kuku.

Nafanya, forensic investigation katika financial institutions na crime scenes wengi wao ni mambo hayo yanaendelea tena dunia nzima labda nikusaidie tu kuwa matukio hayo bado yanatokea lakini yamepungua.

Kama unajinadi kuwa una vyanzo vya intelijensia hapo Tanzania na Afrika ya mashariki usingeweza kushindwa kuelewa kuwa mambo hayo yapo kila sekunde.
Kajielimishe tena kuhusu mauaji ya hapo Tanzania na Afrika Mashariki hata Afrika nzima.

Mfano hapo Tanzania ; unaelewa ni kwa nini wahindi wanaishi maisha wanayoishi ?
Mfano, hapo hapo Tanzania, unadhani kuwa distributor /wholesaler wa bidhaa fulani fulani hivi ambazo baadhi ya watu wanajiona kuwa ni haki yao ; unadhania ni watu wangapi wamekufa? Mfano SODA, Vituo vya Mafuta, kumiliki hotels (humu JF tu kuna uzi wa mmiliki mmoja wa hotel hapo Jiji la Makonda alipigwa risasi kisa umiliki wa eneo na hotel, wanajukwaa ndiyo wameandika humu JF ) n.k.
Je, unajua ni watu wangapi wamekufa kwa sababu ya kutaka kuuza bidhaa hizo hapo tu Tanzania?.

Twende Kenya , kwao ni biashara na siasa wanauana kila wakati; mfano miaka 2 tu iliyopita Kenya walimzingira kigogo (biashara na siasa chanzo cha kifo chake) wakamtoa roho yake mbele ya familia yake (mke na watoto wakishuhudia).

Rwanda ndiyo usiseme kwa jinsi palivyochafuka. (Rwanda mwezi hauishi), sasa Uganda nako hali tete.
Afrika ya Kusini, Nigeria, kote tunaelewa.

Nchi za Magharibi hasa huko USA, wanamuziki wanauana kama kuku kwa risasi, sumu, ajali za barabarani za kutengenezwa.

Hivyo, ukiandika kuwa Ulaya, USA hata Afrika hakuna hayo sijui unazungumzia dunia nyingine yenye majina haya au ni hii tuijuayo wote?

Kama nawe u mtu wa intelijensia huko uliko yaani utakuwa ni mzigo kwa hiyo taasisi.

Boy, you got wrong information from your secret service compatriots.
Uwiii sasa ulikichokiandika ni nini sasa, pumba mwanzo mwisho mzee jitathin kwanza, mwenzio kaja na uzi mzuri wewe hata wakutudanganyia huna unakosoa nn Sasa wakati mwenzio anazungumzia enzi za miaka ya 90 Rushia, utaolewa mapema
 
ashidodi, post: 33091663, member: 385259"]
Uwiii sasa ulikichokiandika ni nini sasa, pumba mwanzo mwisho mzee jitathin kwanza, mwenzio kaja na uzi mzuri wewe hata wakutudanganyia huna unakosoa nn Sasa wakati mwenzio anazungumzia enzi za miaka ya 90 Rushia, utaolewa mapema
[/QUOTE]


Yaani huelewi kabisa. Wewe endelea tu.
 
ashidodi, post: 33091663, member: 385259"]
Uwiii sasa ulikichokiandika ni nini sasa, pumba mwanzo mwisho mzee jitathin kwanza, mwenzio kaja na uzi mzuri wewe hata wakutudanganyia huna unakosoa nn Sasa wakati mwenzio anazungumzia enzi za miaka ya 90 Rushia, utaolewa mapema


Yaani huelewi kabisa. Wewe endelea tu.[/QUOTE]Watu wajinga wajinga kama nyie muwe mnakaa kimya, sasa huu uzi au mleta uzi anakuhusu nini? Ungesoma ukapita kuleeeeeeeee siyo kuja na maneno kanga humu, Kama unaakili lete uzi, manna
 
the bold niekuwa nakusoma tu ila sijawahi kuchangia kiukweli una kipaji sana ya uandishi na usomaji wa mambo mengi tofauti tofauti umesoma fani gani mkuu nakuona kama multigenius. Sio wa kchezo mchezo ukiamua kufuatilia jambo. nimekuwa na wewe kwa mara ya kwanza kwenye kisa cha malaysian airways, septemba eleven, ujasusi sebuleni kwetu na hii hapa ya abramovich unatakiwa kupewa kazi na idara yetu nyeti ya taifa kama bado.

Heko sana kwa umri wako mdogo unafanya mambo kama ya abramovich nimeipenda jinsi unavyojua kufuatilia wakati mwingine mpaka nashtuka sana kwa jinsi ulivyo informed.
 
ashidodi, post: 33091663, member: 385259"]
Uwiii sasa ulikichokiandika ni nini sasa, pumba mwanzo mwisho mzee jitathin kwanza, mwenzio kaja na uzi mzuri wewe hata wakutudanganyia huna unakosoa nn Sasa wakati mwenzio anazungumzia enzi za miaka ya 90 Rushia, utaolewa mapema


Yaani huelewi kabisa. Wewe endelea tu.[/QUOTE]Pole kwakuwa Mpumbavu na Mjinga na ajabu zaidi unatetea ujinga na upumbavu wako..
 
ashidodi, post: 33091923, member: 385259"]
Yaani huelewi kabisa. Wewe endelea tu.[/QUOTE]Watu wajinga wajinga kama nyie muwe mnakaa kimya, sasa huu uzi au mleta uzi anakuhusu nini? Ungesoma ukapita kuleeeeeeeee siyo kuja na maneno kanga humu, Kama unaakili lete uzi, manna
[/QUOTE]


Ulivyo panic sasa kama umeshikwa na majibu kwenye chumba cha mtihani.

Teeeeh teeeeh teeeeh , relax guy then read my comments between the lines you will understand my ability to analyse details.
Just go back and re-read my comment no. 1022 , I believe you will get something tangible to feed your empty skull then enhance your brain.
 
Waliosoma comment yangu namba 1022, wengi wamepanic sana. Tatizo mlioisoma hiyo comment hamna uelewa hebu rudieni kuisoma mtaelewa.

Poise, huwa sitaki kudanganywa au kusoma jambo lililopotoshwa kwa makusudi huku naelewa ukweli eti nikubali tu kwa sababu mleta mada ameandika au ameleta mada nyingi siyo usomi huo.

Pia, hii Tasnia aliyoizungumzia kuwa ana taarifa zote za intelijensia za afrika ya mashariki nimeonyesha asivyokuwa na taarifa sahihi au za kweli.

Sasa kinachowasababisha ku-panic hivyo ni kipi kama siyo kuwa nanyi ni walewale wadanganyika?

Mliopanic someni mtapata maarifa na kuelewa mambo kwa usahihi na siyo kusoma kama kuku waliokatwa vichwa.
 
Waliosoma comment yangu namba 1022, wengi wamepanic sana. Tatizo mlioisoma hiyo comment hamna uelewa hebu rudieni kuisoma mtaelewa.

Poise, huwa sitaki kudanganywa au kusoma jambo lililopotoshwa kwa makusudi huku naelewa ukweli eti nikubali tu kwa sababu mleta mada ameandika au ameleta mada nyingi siyo usomi huo.

Pia, hii Tasnia aliyoizungumzia kuwa ana taarifa zote za intelijensia za afrika ya mashariki nimeonyesha asivyokuwa na taarifa sahihi au za kweli.

Sasa kinachowasababisha ku-panic hivyo ni kipi kama siyo kuwa nanyi ni walewale wadanganyika?

Mliopanic someni mtapata maarifa na kuelewa mambo kwa usahihi na siyo kusoma kama kuku waliokatwa vichwa.
Umewahi kusom makala ya the bold, ya the richest man in africa.? Ndyo utajua kwann watu wameishangaa comment yako kuwa hana taarfa sahihi kuhus east afric...
 
Umewahi kusom makala ya the bold, ya the richest man in africa.? Ndyo utajua kwann watu wameishangaa comment yako kuwa hana taarfa sahihi kuhus east afric...

msafwa,

Elewa kuwa Poise, nikisoma post na kuona kuwa imechanganywa ukweli na uongo kidogo basi huwa naangalia logic ya kuwekwa uongo/misleading information as a salient feature which might distort the whole content.

Such style of writing intends to mislead readers or to attract unnecessary attention which is plagiarism and unacceptable too.
 
Waliosoma comment yangu namba 1022, wengi wamepanic sana. Tatizo mlioisoma hiyo comment hamna uelewa hebu rudieni kuisoma mtaelewa.

Poise, huwa sitaki kudanganywa au kusoma jambo lililopotoshwa kwa makusudi huku naelewa ukweli eti nikubali tu kwa sababu mleta mada ameandika au ameleta mada nyingi siyo usomi huo.

Pia, hii Tasnia aliyoizungumzia kuwa ana taarifa zote za intelijensia za afrika ya mashariki nimeonyesha asivyokuwa na taarifa sahihi au za kweli.

Sasa kinachowasababisha ku-panic hivyo ni kipi kama siyo kuwa nanyi ni walewale wadanganyika?

Mliopanic someni mtapata maarifa na kuelewa mambo kwa usahihi na siyo kusoma kama kuku waliokatwa vichwa.
Poise wewe ni mpiga kelele tu humu na tutakuvumilia kwani haitatuzuia kuendelea kupata uhondo toka kwa The Bold. Nina hamu sana na Episode 13! Naisubiria!
 
sweettablet,
Huo ni utumwa wa kuandikiwa na kuletewa machapisho ndiyo matokeo yake, unaona kila kitu kipo sahihi.
Simply, you have nothing in your brain no way you can see fake news, false information and such like.

Poise, huwa nasoma threads ila iliyo na uongo naipinga apo hapo.
Poise in academic grounds you don't just make noise; you falsify what has been stated by giving what you assume to be correct argument by giving data. What you've written is mere words not supported by facts.

The Bold has presented names, dates and events. He has shown connectivity and the like. What have you given? Lamentation, blah, blah, blah! and other rubbish. If you really know "Wild, Wild Africa" give us names, give us dates, give us events, give us location just like The Bold does. If you cannot, you will be very stupid and I'll not argue with you anymore!
 
Back
Top Bottom