Roman Abramovich: Utajiri wa Damu, Risasi na Umafia

ROMAN ABRAMOVICH: UTAJIRI WA DAMU, RISASI NA UMAFIA




SEHEMU YA 11




Kiunzi pekee ambacho kilikuwa kimebaki mbele ya Abaramovich kuifanya RUSAL kuwa kampuni kubwa zaidi ya uzalishaji wa Aluminium ilikuwa ni deal ya kiwanda cha Krasnoyarsk kinachomilikiwa na Anatoly Bykov.

Baada ya kila mbinu kutofanikiwa Abramovich akapata wazo lingine. Mbinu hii ambayo aliitumia mara ya pili inatoa picha ni kwa namna gani Abramovich alikuwa na nguvu ndani ya Russia kipindi kile.

Kama ambavyo nimeeleza kwa msisitizo kwenye sehemu zote zilizopita… biashara aluminium ilikuwa ni sekta ya hatari mno kipindi kile nchini Russia. Maana yake ni kwamba mtu yeyote yule ambaye ameweza 'ku-survive' na kushamiri ndani ya biashara hiyo maana yake ni kwamba alikuwa ni mtu hatari zaidi. Hii ilikuwa inamaanisha kwamba Anatoly Bykov kama wenzake wengine wote, pia hata yeye alikuwa na madudu mengi sana ameyafanya ili kuweza kushamiri kwenye biashara hiyo. Na hii ndio ilikuwa silaha ya mwisho ya Abramovich.

Sasa,

Katika jimbo la Krasnoyarsk ambako Anatoly Bykov alikuwa anaishi, kutokana na utajiri mkubwa aliofanikiwa kuuchuma huku akiwa ni kijana wa umri mdogo tu, ilimfanya kuwa kama 'celebrity' kwenye mji wao. Vyombo vya habari vilikuwa havikauki ofisini kwake.
Siku hiyo alikuwa anafanya mkutano na wanahabari ofisini kwake… kama kawaida pia kulikuwa na kundi la wananachi wakishangaa shangaa.
Kufumba na kufumbua gari tano zikiwa na wanajeshi karibia thelathini wa 'special forces' ziliingia kwa ghafla kwenye eneo la ofisi. Kundi la wananchi waliokusanyika walitawanywa kwa risasi kupigwa juu hewani huku walinzi wa Bykov wakiwekwa chini ya ulinzi. Bykov akanyakuliwa mzobe mzobe kama kuku na kupakiwa kwenye gari na kuondoka naye.

Jioni ya siku hiyo serikali ikatangaza kupitia vyombo vya habari kwamba wamemkamata Anatoly Bykov kwa shutuma ya makosa ya utekaji na mauaji.
Nchi nzima ilizizima… sintofahamu ilitanda kila mtu akijiuliza kwa nini iwe Bykov pekee wakati ni suala linalofahamika wazi kabisa kwamba maoligarch wote wanaojihusha na sekta ya aluminium mikono yao imejaa damu za roho za watu.

Wiki moja baadae Bykov alipandishwa kizimbani. Hati ya mashtaka ilisema kwamba anakabiliwa na kosa la "Kupanga njama ya kuua na utekaji". Kesi iliunguruma na kuteka vyombo vya habari.
Ndani ya miezi miwili kesi ilikuwa imemalizwa kusikilizwa na mahakama ilimkuta Bykov na hatia na kumuhukumu kwenda jela miaka sita.

Miaka sita… ilikuwa inatosha kabisa kwa Abramovich kufanya kile alichokusidia.

Baada ya miezi mitatu tu kwa kutumia mwanya wa Bykov kuwa jela, Abramovich na Deripaska waliishawishi bodi ya wakurugenzi ya Krasnayorsk Aluminium Smelter kuwauzia kiasi kikubwa cha hisa ambacho kiliwafanya kuwa "majority share holders". Na mwanya huo wa wao kuwa wanahisa wakuu wa kampuni wakautumia kushinikiza uamuzi wa kampuni hiyo ya Krasnoyarsk kuuzwa kwa RUSAL.

Lengo likatimia…

Kwa akili ya haraka haraka tu suala kama hili haliwezekani likafanyika kwenye nchi za magharibi au hata hapa Afrika leo hii. Lakini hivyo ndivyo mambo yalivyoendeshwa kihuni nchini Rusia miaka ya tisini na mwanzo mwa 2000. Hiyo ndio maana hasa ya 'Wild Wild East.!"

Hii ilikuwa ni mwezi July mwaka 2002. Ndio siku ambayo RUSAL ilipanda ngazi Rasmi kuwa kampuni inayoongoza duniani kwa uzalishaji wa Aluminium. Utajiri wa Abramovich ukapaa kwa kasi ya ajabu. Na ndio hapa kwa mara ya kwanza jina lake likaanza kutajwa tajwa sana hata nje ya Russia.

Ni wazi sasa kwamba Abramovich alikuwa ni Oligarch namba moja ndani ya Rusia. Mtu pekee ambaye alikuwa na nguvu ndani ya Russia kumzidi Abramovich alikuwa ni Putin pekee. Lakini hakukuwa na mwingine yeyote yule ambaye alikuwa ana hata nusu tu ya ushawishi ambao Abramovich alikuwa nao.

Waswahili tuna msemo tunasema kwamba "mti wa riziki, ficho kivuli cha husda." Kwamba ukipata uwe makini maana kuna watu watahisi kupata kwako kunaziba riziki zao.

Kitendo cha kijana aliyetoka familia masikini wa kutupwa. Kijana ambaye alikuwa anauza wanasesere. Kijana aliyeuza matairi chakavu leo hii kuwa mfanyabiashara mwenye ushawishi zaidi na si hivyo tu bali kuwa 'right hand man' wa Rais wa taifa la urusi kiliwaudhi baadhi ya maoligarch.
Abramovich alikuwa anaogopwa pale Moscow na maoligarch waliudhika sana na kitendo hiki. Yaani kinyago walichokichonga wenyewe leo hii kinawatisha?

Ajabu ni kwamba mpaka Berezovsky alichukia.
Yes, Berezovsky mentor wa Abramovich naye alichukia… sijui kama ilikuwa ni wivu au vipi. Maana Abramovich sasa alikuwa na utajiri mkubwa maradufu zaidi ya Berezovsky. Yawezekana ni wivu, au labda ni woga… Berezovsky alikuwa amechukia haswa kitendo cha Abramovich kuwa Oligarch namba moja ndani ya Urusi na ushawishi wa kupitiliza alionao mtaani na ndani ya serikali.

Vikakaliwa vikao vya siri vya maoligarch… wakafikia azimio. Azimio ambalo naamini maoligarch walioko hai mpaka sasa ambao walikuwepo kwenye kikao kile wanatamani hata kurejesha muda nyuma na kufanya azimio tofauti na lile.
Walifikia uamuzi kwamba, kama ukomunisti uliweza kudondoka ndani ya Urusi, na kama juzi juzi tu hapo waliweza kushawishi kuondoka madarakani kwa Rais Boris Yeltsin… Je, huyu anayemkingia kifua Abramovich, anayemlea na kumpa meno ya kutafuna maoligarch wengine… huyu Putin.. Putin ni nani hata wasiweze kumng'oa ili wawe wamekimaliza kabisa kinyago chao walichokichonga, Abramovich, ambacho sasa chawatisha hata usingizi hawalali kwa raha??

Kipindi hiki vita ya Chechenya ilikuwa ndio imepamba moto na Putin alikuwa anafanya ile tunaita "full scale war".
Jamii ya kimataifa ilikuwa inapiga kelele kwamba Putin anavunja haki za binadamu na kufanya uhalifu wa kivita kutokana na ile vita ambayo alikuwa anaiendesha Chechenya.

Tunakumbuka nilieleza kuwa ile televisheni ya taifa Perviy Kanal ambayo ndio yenye kutazamwa zaidi ndani ya Rusaia ni Berezovsky alibinafsishiwa kipindi kile na utawala wa Rais Yeltsin.

Maoligarch waliompinga Abramovich mpango wao ukaanzia hapa.

Televisheni ya Perviy Kanal ikaanza kuandaa makala na chambuzi kumkosoa Rais Vladmir Putin na mbinu na nguvu anazotumia kwenye vita ya Chechenya.
Tukumbuke kwamba vyombo hivi hivi vya habari ndivyo ambavyo vilitumika kufanya propaganda ya kuijenga 'image' ya Putin kwa wananchi kipindi kile alipochaguliwa na Rais Yeltsin kuwa Waziri Mkuu. Kwa hiyo walidhani kwamba kama waliweza 'kumchonga' kwa vyombo vyao vya habari wanavyovimiliki basi wanaweza kumbomoa 'image' yake taratibu kwa umma na hatimaye kumuondoa madarakani.

Was a big mistake…. Ni kweli wao walikuwa na vyombo vya habari, lakini mwenzao Putin alikuwa na kitu muhimu zaidi pembeni yake… Roman Abramovich.


Inaendelea…


Bold
To Infinity and Beyond
 
SEHEMU YA 11


Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij addenbwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA
 
SEHEMU YA 11


Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij addenbwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA
Naam mkuu usikose kunitag tafadhali....
 
Habibu B. Anga,
Kwa akili ya haraka haraka tu suala kama hili haliwezekani likafanyika kwenye nchi za magharibi au hata hapa Afrika leo hii. Lakini hivyo ndivyo mambo yalivyoendeshwa kihuni nchini Rusia miaka ya tisini na mwanzo mwa 2000. Hiyo ndio maana hasa ya 'Wild Wild East.!""

Mwandishi, hapo penye kivuli (bolded paragraph) ''nimepatoa kwenye utunzi wako'' hii inafanyika hata sasa tena kote duniani siyo ulaya, Russia, Asia tena Afrika ndiyo watu wanauana kila sekunde kama kuku.

Nafanya, forensic investigation katika financial institutions na crime scenes wengi wao ni mambo hayo yanaendelea tena dunia nzima labda nikusaidie tu kuwa matukio hayo bado yanatokea lakini yamepungua.

Kama unajinadi kuwa una vyanzo vya intelijensia hapo Tanzania na Afrika ya mashariki usingeweza kushindwa kuelewa kuwa mambo hayo yapo kila sekunde.
Kajielimishe tena kuhusu mauaji ya hapo Tanzania na Afrika Mashariki hata Afrika nzima.

Mfano hapo Tanzania ; unaelewa ni kwa nini wahindi wanaishi maisha wanayoishi ?
Mfano, hapo hapo Tanzania, unadhani kuwa distributor /wholesaler wa bidhaa fulani fulani hivi ambazo baadhi ya watu wanajiona kuwa ni haki yao ; unadhania ni watu wangapi wamekufa? Mfano SODA, Vituo vya Mafuta, kumiliki hotels (humu JF tu kuna uzi wa mmiliki mmoja wa hotel hapo Jiji la Makonda alipigwa risasi kisa umiliki wa eneo na hotel, wanajukwaa ndiyo wameandika humu JF ) n.k.
Je, unajua ni watu wangapi wamekufa kwa sababu ya kutaka kuuza bidhaa hizo hapo tu Tanzania?.

Twende Kenya , kwao ni biashara na siasa wanauana kila wakati; mfano miaka 2 tu iliyopita Kenya walimzingira kigogo (biashara na siasa chanzo cha kifo chake) wakamtoa roho yake mbele ya familia yake (mke na watoto wakishuhudia).

Rwanda ndiyo usiseme kwa jinsi palivyochafuka. (Rwanda mwezi hauishi), sasa Uganda nako hali tete.
Afrika ya Kusini, Nigeria, kote tunaelewa.

Nchi za Magharibi hasa huko USA, wanamuziki wanauana kama kuku kwa risasi, sumu, ajali za barabarani za kutengenezwa.

Hivyo, ukiandika kuwa Ulaya, USA hata Afrika hakuna hayo sijui unazungumzia dunia nyingine yenye majina haya au ni hii tuijuayo wote?

Kama nawe u mtu wa intelijensia huko uliko yaani utakuwa ni mzigo kwa hiyo taasisi.

Boy, you got wrong information from your secret service compatriots.
 
79 Reactions
Reply
Back
Top Bottom