Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kashasema amefunga faili wewe unaleta huku JF iweje unadhihirisha ulivyo popoma!
Keshakuwa choCo so amekuwa na maneno mengi
Sasa wewe una matatizo gani mkuu!!? Roma amesema ufunge file lakini wewe umefungua thread humu JF!!! Naona una akili za kuvukia barabara tu!!Akizungumza hivi punde tu na Kituo cha Redio ambacho kinakuja na Kasi ya Kimbunga cha Efm katika Kipindi maarufu cha ' Joto la Asubuhi ' Msanii Ibrahim Musa ( Roma Mkatoliki ) amewataka Watanzania waache sasa kumpa pole kila mara na kila wamuonapo na badala yake amewataka sasa ' wafunge file ' juu ya lililomtokea ( sakata la Kutekwa )
" Unakuta Mtu uko zako barabarani au Kituo cha Mafuta unajaza Mafuta halafu anakuja tu Mtu anakusalimia haraka kisha maongezi yake mengi ni ya kuuliza tu nini kimenitokea hali ambayo huwa inanikera sana na ndiyo maana leo kupitia Redio yenu nasema kuwa naomba tufunge file juu ya kilichonitokea na badala yake sasa tujikite katika maendeleo, harakati na tugange yajayo " alisema Roma Mkatoliki.
Najua hata humu Jamvini JF wapo wale Watu ambao kila kukicha wamekuwa wakijifanya kumpa pole ambazo haziishi na amezichoka mno sasa hivyo Roma Mkatoliki amesema kuwa sasa anataka ' file lifungwe ' rasmi na mgange yajayo.
Kwa tafsiri iliyo fupi sana ambayo inaweza isieleweke vyema kwa wengi ni kwamba hapa Roma Mkatoliki anasema kwamba wengi wa wale wanaojifanya kumpa salamu za pole na kumtia moyo ni ' Wanafiki ' watupu ( ukimuondoa tu GENTAMYCINE pekee ) hivyo amewachoka na mkome!
Kila siku mnajifanya kumpa pole wakati hata Nyumbani Kwake kwenda tu kumtembelea mlishindwa au basi hata tu kumtumia Pesa katika Simu ili angalau zimfute machozi mmeshindwa lakini humu Mitandaoni mnajishebedua na kujitutumua kujifanya mmeumia na kilichomtokea.
Roma Mkatoliki nikupongeze sana na nimefurahi mno leo ulivyowapa ' makavu ' Watanzania wanafiki wanafiki na naungana nawe kwa 100% hasa ulipowaambia kuwa sasa unawataka ' wafunge file ' na wagange yajayo. Na labda nikuibie tu siri Roma Mkatoliki unaweza kukuta katika hao hao wanaojifanya kukupa pole na kukutia moyo wamo wale Watekaji wako au Ndugu zao au hata Wanafamilia wao.
Safi sana Roma Mkatoliki sasa ' wafunge file '.
Nawasilisha.
Ningekuwa kocho nisingekuwa na maneno mengi kama weweNa kama ilivyo kwa Mchawi kumjua Mchawi mwenzio hivyo inawezekana hata ' Kocho ' nae akamjua ' Kocho ' mwenzie.
Ningekuwa kocho nisingekuwa na maneno mengi kama wewe
Humu tunakuchukulia kama mwezi mchanga so kila unaloongea ni upuuzi jazz band tu kakae na mkeo uongee nae upuuziSindano imeshakuingia najua tu!
Humu tunakuchukulia kama mwezi mchanga so kila unaloongea ni upuuzi jazz band tu kakae na mkeo uongee nae upuuzi