Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,316
- 10,782
u! Aidha kumbuka Roma haikujengwa kwa siku moja, ujenzi wa miundombinu ndiyo mwanzo wa maendeleo ya wananchi.
Mara kadhaa huu usemi, “Roma haikujengwa kwa siku moja” umesikika kutoka kwenye vinywa vya wanasiasa na hata wananchi. Leo katika uzi mmoja ambao naona umeshafutwa, nimekutana tena na usemi huo kama inavyoonyesha hapo juu.
Hapa naweka tafakuri yangu juu ya usemi huu.
Huu usemi wa “Roma haikujengwa kwa siku moja” ni excuse kubwa ya CCM. Kwanza huu usemi ulianza kutumiwa na Wafaransa kwenye miaka ya 1100, na kuingia kwenye semi za Waingereza kwenye miaka ya 1500. Hii inaonyesha ni kiasi gani ‘context’ ya namna usemi ulivyoanza. Wafaransa walitumia usemi kama kisingizio cha umasikini wao.
Pili, wanaoendelea kutumia usemi huu, wanasahau mazingira ambayo ‘Roma’ ilikuwa nayo wakati inajengwa na mazingira yaliyopo sasa hivi. Roma ilijengwa kwenye mazingira magumu sana: watu walikufa kwa mafua tu, kiwango cha uelewa, elimu na utaalamu kidogo, teknolojia duni sana n.k.
Ona hapa jinsi mafua yalivyosumbua ‘Waroma’Reviewing the History of Pandemic Influenza: Understanding Patterns of Emergence and Transmission
Ebu angalia hapa magonjwa yaliyowaua ‘Waroma’ wakati wanaanza kuendeleahttps://www.historylearningsite.co.uk/britain-1700-to-1900/industrial-revolution/diseases-in-industrial-cities-in-the-industrial-revolution/
Leo hii kuna maendeleo makubwa sana kwenye nyanja za afya, elimu na teknolojia duniani. Hivyo haiwezekani ati taifa liendelee kwa spidi ambayo ‘Roma’ ilitumia.
Angalia hapa baadhi ya maendeleo kwenye sekta ya afya:
10 Biggest Technological Advancements for Healthcare in the Last Decade
The reach of technological innovation continues to grow, changing all industries as it evolves. In healthcare, technology is increasingly playing a role in almost all processes, from patient registration to data monitoring, from lab tests to self-care tools. Devices like smartphones and tablets...
www.beckershospitalreview.com
Cleveland Clinic Unveils Top 10 Medical Innovations for 2019
Alternate therapies for pain. The use of artificial intelligence in healthcare. Expanded window to treat stroke patients. These are some of the innovations that will enhance healing and change healthcare in the coming year, according to a distinguished panel of doctors and researchers...
newsroom.clevelandclinic.org
Maendeleo kwenye elimu:5 Emerging Trends in 21st-Century Education | Getting Smart
Maendeleo kwenye teknolojia:StackPath
Kama ingekuwa kwamba “Roma haikujengwa kwa siku moja” kwa mazingira ya maendeleo hayo, Taiwan, Hong Kong, Korea ya Kusini na Singapore zilizokuwa masikini kama Tanzania nazo hadi sasa zingekuwa masikini. Hizi zinajulikana kama the “Asian tigers”. Zimekuwa kwa kasi kwa ndani ya miaka 30 tu (1960s - 1990s).
Jifunze kidogo kuhusu ‘the Asian miracle’ hapa:Tiger Economy.
Na hapa:
Hizi ziliwekeza haswa kwenye elimu ambayo ikafanya uwekezaji wa viwanda kuwa na maendeleo makubwa na athari chanya kwenye chumi zao. Soma hapa: https://content.taylorfrancis.com/b...-X&isbn=9781134677153&format=googlePreviewPdf
Hizi nchi hazikukubali kuingizwa mkenge na Benki ya Dunia na sera zake za uliberali mamboleo. Hazikukubali kuendeshwa kutokea Washington - kwa the
Soma hapa kuhusu sera ya viwanda ambayo hizi nchi zilienda nayo:https://ora.ox.ac.uk/objects/uuid:3...at=application/pdf&type_of_work=Working+paper
Malizia na hii kuelewa namna ambavyo the Asian tigers walijiweka mbali na sera za Benki ya Dunia: https://www.researchgate.net/profil.../Graduated-Sovereignty-in-South-East-Asia.pdf
Sasa ndugu zangu wa CCM, ebu niambieni hiyo ‘model’ anayoitumia Magufuli na serikali yake ni ya wapi? Ya kuwekeza kwenye miundombinu kwa pesa nyingi hivyo, ili taifa kuendelea.
Hakuna haja ya ku “invent the wheel”, ilhali blueprints mbalimbali zipo. Ni kiasi cha kuiga tu na kuzirekebisha ili ziendane na mazingira yetu. Maendeleo makubwa kabisa katika nyanja nilizozitaja hapo juu yanatuwezesha tuweze kuendelea kwa kasi zaidi ya the Asian tigers. Reinventing the wheel, matokeo yake ni kupiga mark-time tu: kila anayekuja anaanza na vyake. Kwa staili hii hakika inakuwa sahihi kusema ‘Roma haikujengwa siku moja’.
Nawatakieni msimu mzuri wa sikukuu.