Riwaya ya mwanafunzi mchawi

Youngrich 004

Member
Jul 16, 2016
61
77
RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Kwanza
MTUNZI:ENEA FAIDY
Ilikuwa ni majira ya saa moja jioni ambapo mkuu wa while ya Mabango alikuwa ofisini kwake akiwa amechanganyikiwa sana kwani hali ya shule hiyo ilizidi kutisha sana hasa baada ya kutokea kwa vifo vya wanafunzi kumi na tano mfululizo ndani ya wiki moja tu. Tena vifo vya ghafla tu.
Mkuu wa shule mama Dayana Mbeshi alikuwa kwenye wakati mgumu sana kubaini chanzo cha tatizo lakini bado hakupata majibu.Mara ghafla mlango wa ofisi ukagongwa, akaingia mwalimu wa malezi wa shule hiyo akiwa na USO wa huzuni sana hali iliyomshtua sana mkuu wa shule
"vipi kulikoni?"
"hali mbaya mkuu.. wanafunzi wawili wamefariki tena bwenini" mwalimu wa malezi alizungumza kwa huzuni iliyochanganyika na hofu.
"what? mmh! sio bure.. kuna kitu hapa..!" alisikika mwalimu Mbeshi huku akiinamisha kichwa chake chini na kukiegemeza kwenye kiganja chake.
******
Wanafunzi wengi walionekana kuwa na hofu sana baada ya vifo visivotarajiwa kuzidi kutokea katika shule yao. Kila MTU aliwaza sana juu ya vifo vile huku kila mmoja akihisi zamu yake IPO karibu. Nyuso za huzuni ndizo zilizotawala kwa wanafunzi wote si wa kike wala wa kiume. Hakuna aliyetamani kulala wala kukaa mbali na kundi la watu kwani hofu iliwajaa mioyoni mwao, hawakuweza hata kusoma.
Lakini hali ilikuwa tofauti sana kwa binti Doreen ambaye alikuwa na wiki tu toka ahamie shuleni hapo. Alionekana kutoogopa chochote wala kuguswa na misiba ya wanafunzi wenzake. Kila Mara alionekana akiwa na furaha, hali hii iliwatisha wanafunzi wenzake na kuwafanya wawe na maswali mengi juu yake.
Doreen alikuwa msichana mrembo, sura yake nyembamba iliyopambwa na macho makubwa legevu, kope ndefu nyeusi tii, pua nyembamba iliyochongoka vyema na midomo mizuri yenye mvuto wa aina yake vilimfanya awe tishio kila kona kwani alikuwa ni mzuri kupindukia lakini Tabia ilikuwa tofauti na uzuri wake.
Wakati wanafunzi wengine wakiwalilia wenzao Doreen alikuwa amejitenga peke take nyuma ya bweni alilokuwa anakaa na kulikuwa na Giza totoro. Alikuwa uchi wa mnyama huku mikono yake ikiwa imeshikilia vitu fulani huku akitamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe....
Itaendelea.......
 
RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Pili
Mtunzi: Enea Faidy
Ilipoishia sehemu ya kwanza (
kama hukuisoma bofya hapa)
.....Wakati wanafunzi wengine wakiwalilia wenzao Doreen alikuwa amejitenga peke yake nyuma ya bweni alilokuwa anakaa na kulikuwa na Giza totoro. Alikuwa uchi wa mnyama huku mikono yake ikiwa imeshikilia vitu fulani huku akitamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe....
Sehemu ya pili
...DOREEN aliendelea kuongea maneno aliyoyajua mwenyewe akiwa bado yupo uchi wa mnyama nyuma ya bweni alilokuwa anaishi.
Ghafla kipande kidogo cha karatasi nyeupe kikashuka mikononi mwake bila kuonekana kilikotokea. Doreen alicheka kwa sauti Kali ya kutisha sana kisha akalikazia macho karatasi lile, matone ya damu yaliangukia kwenye karatasi lile kutoka kwenye macho yaliyotisha sana ya Doreen kwani yalikuwa na rangi nyeusi halafu yakawa na umbile kama macho ya paka.
"Nenda mpaka ofisi ya mkuu wa shule ukamalize kazi." alisema Doreen akiwa amelinyanyua karatasi like kwa mkono wake wa kushoto. Karatasi likatoweka mkononi mwake na kupepea kwa nguvu kama vile limerushwa na upepo mkali.
Doreen alipomaliza kazi hiyo akasimama vizuri kama mwanajeshi aliyejipanga kwaajili ya gwaride kisha akainamisha kichwa chake chini akapotea eneo lile.
**********
Wanafunzi wa shule ya sekondari Mabango walikuwa wanahofu kubwa sana kila wakikaa walifikiria kifo tu. Usingizi haukuwajia hata Mara moja hivyo usiku waliketi makundi makundi wakizungumza hili na lile.
Wakati huo Dorice rafiki kipenzi wa Doreen alikuwa amejitenga pembeni akizungumza na mpenzi wake aitwaye Eddy, kijana mtanashati, mzuri, mpole na akili nyingi sana darasani.Wasichana wengi shuleni pale walitamani kuwa nae lakini bahati ilimwangukia Dorice pekee.
"Eddy unajua naogopa sana.." ilikuwa sauti ya Dorice akiwa amemkumbatia Eddy kwani kigiza kile cha usiku kiliwaficha wasionekane hivyo wakajiachia.
"unaogopa nini Dorice mpenzi wangu?"
"Naogopa kufa!" binti Huyo wa kinyaturu, mrembo aliyeumbika aliongea kwa sauti ya madeko sana.
"siku zote nakwambia Dorice kama Mungu alipanga huwezi kupangua , mwanadamu asikutishe kwa lolote. Huyu anayeua wenzake naye IPO Siku yake tu!"
"Najua baby Ila hali inatisha"
"Tuzidi kuomba Mungu mpenzi wangu kila unalofanya muombe Mungu."
"Nakupenda "
"Nakupenda pia"
Wakati Eddy na Dorice wakiendelea kuzungumza maneno hayo, Doreen alikuwa nyuma ya mti waliosimama hivyo alisikia kila kitu.
Roho ilimuuma sana kwani tangu alipohamia shuleni hapo alitokea kumpenda sana Eddy na alitamani awe mpenzi wake kwani ndio chaguo la moyo wake lakini Dorice alikuwa kikwazo. .
Suala hilo lilimuumiza Doreen ndani kwa ndani. Akainuka pale kwenye mti na kupita katikati yao, akamwita Dorice pembeni.
"Dorice.. mimi nawahi kulala Ila kesho unione!"
"nikuone?"
"ndio kwani hujaelewa?" alijibu Doreen kwa ukali jambo lililomwachia maswali mengi Dorice. Lakini Doreen hakujali kitu akaondoka zake Ila moyoni alipanga jambo zito la kumfanyia Dorice siku ya kesho yake.
*********
Ilikuwa asubuhi tulivu sana majira ya saa kumi na mbili na nusu asubuhi ambapo mwalimu Dayana Mbeshi aliwahi ofisini kwake kama ilivyokuwa kawaida yake.
Majengo ya ofisi yalimkaribisha kwa shangwe naye akaitikia ukaribisho huo kwa kufungua ofisi yake kisha akasogeza mapazia ya dirishani ili kuruhusu mwangaza wa jua changa uweze kupenyeza vizuri.
Baada ya kukamilisha yote hayo Madam Mbeshi akasogeza kiti chake karibu na meza kisha akaketi halafu akaanza kusogeza vitu vilivyokuwepo mezani pale lakini ghafla akakutana na karatasi chafuchafu mezani kwake lakini ilikuwa na maandishi.
Akashtuka kidogo halafu akaichukua ili aisome vizuri. Mwalimu Mbeshi hakutaka kuamini kile alichokiona, akataharuki kwa hofu na mshangao...............
Itaendelea....
 
RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya Kumi na Tisa
Mtunzi: Enea Faidy
==>Kama hukuisoma sehemu ya 18 <<Bofya Hapa>>
.....DORICE alipozitazama zile nguo zilikuwa ni nguo nzuri sana za kuvutia. Kulikuwa na gauni moja refu linaloacha wazi mikono lenye rangi ya dhahabu inayong'aa sana. Kulikuwa na viatu virefu vinavyoelekeana na rangi ya gauni kidogo, ushungi wenye rangi ya gauni, mkufu wa dhahabu pamoja na hereni.
Dorice alivishangaa vitu vile kwa mshangao wakati huo Mansoor alikuwa akiachia tabasamu mwanana pembeni yake.
"Vaa Dorice!" Ilisikika sauti ya Mansoor ndipo Dorice alipopata nafasi ya kumtazama tena Mansoor. Akapigwa na bumbuwazi baada ya kuona mansoor amevalia nguo tofauti na alizokuwa amevaa mwanzo, alionekana kama mwanaume wa kihindi pale anapofunga ndoa kwa mavazi yake. Dorice alimshangaa sana Mansoor, woga kiasi ukamvaa moyoni mwake kisha akaanza kuzivaa nguo zile alizopewa na Mansoor.
Pindi anapozivaa nguo zile Mansoor alikuwa tayari ameshatoweka eneo lile.Dorice alipovaa nguo zile, alibadilika sana. Alionekana mrembo mno kwa jinsi alivyopendeza. Ukimtazama kwa haraka utadhani msichana kutoka India kumbe ni mnyaturu wa Singida.
Alijitazama kupitia kioo kilichokuwa mbele yake, akajikiri kwamba kweli Mungu hakumkosea katika uumbaji ila alitumia ufundi wa hali ya juu katika kukamilisha sura na umbile lake.
Bada ya kumaliza kuvaa, Mansoor alitokea tena palepale alipokuwa amesimama mwanzo. Alimshtua sana Dorice lakini tayari alikuwa ameshaanza kumzoea Mansoor hivyo hakuogopa sana.
"Umependeza sana Malkia wangu.. Kwa jinsi ulivyositamani hata uende Duniani.. Nahisi wivu sana.." Alisema mansoor huku akimtazama mrembo yule kama waridi likiwa bustanini wakati wa jua la asubuhi.
"Uliniahidi nini?" Aliuliza Dorice kwa hamaki."Usijali... Nitakupeleka duniani kama nilivokuahidi ila nimekuambia tu hisia zangu... Kama unanipenda kweli ni heri ubaki na mimi huku huku kwetu!" Alisema Mansoor kwa sauti ya upole sana. Dorice hakijibu kitu. Wakaondoka pale na kwenda moja kwa moja kwa malkia.
Malkia alifurahi sana kuona kijana wake ameambatana na mtu ampendae. Radi tatu mfululizo zilipigwa ili kudhihirisha furaha aliyokuwa nayo malkia. Mansoor alitabasam akiwa amemshika mkono mkewe mtarajiwa.
"Harusi ya mwanangu Mansoor... Iwe ya furaha sana kwani amepata kile alichokuwa anahitaji.." Alisena malkia kwa sauti kali. Dorice alimtazama Mansoor kwa woga.
"Usiogope malkia wangu.. Na kuanzia Leo nitakuita Aisha..!"
"Aisha! Kwanini?" Alihamaki Dorice.
"Ukiwa mke wangu huwezi kuitwa Dorice.." Alisema Mansoor.
Wakati Dorice akiendelea kushangaa ghafla upepo mkali ukapigwa, halafu kwa muda huohuo walijikuta wapo eneo lingine lililojaa watu wengi ambao Dorice hakuwaelewa elewa kwa jinsi walivyokuwa.
********
Majira ya SAA moja jioni Mr. Alloyce alikuwa amewasili nyumbani kwake. Kichwa kilijaa mawazo tele ambayo hakujua yataisha vipi kwani matatizo aliyokuwa nayo yalikuwa ni mazito kuzidi kilo mia za Mawe. Njia nzima aliwaza na kuwazua lakini bado alijiona yupo kwenye msitu mkubwa wa matatizo ambao hakujua atapenya vipi ili kuepukana nao.
Kila Mara sura ya mkewe mpenzi ilimjia kichwani mwake hakuamini kama kweli amempoteza katika mazingira ambayo ilikuwa vigumu kuyaelewa. Alimfikiria mwanawe Eddy ambaye mpaka Dakika ile hakujua angeanzia wapi kumtafuta ilhali hajui alikoelekea!. Kichwa kilimgonga sana kwa mawazo.
Alifika getini kwake na kumkuta mlinzi wake ambaye alimfungulia. Bila hata ya salamu Mr.Alloyce alipita getini pale na kuelekea ndani lakini alishtushwa sana kuona taa zinawaka ndani pia alisikia sauti kubwa ya muziki. Mr.Alloyce alisitisha mwendo wake kidogo. Akamgeukia mlinzi.
"We Seba nani yupo ndani?"
"Atakuwa Eddy Huyo.."
"Eddy! Eddy gani?" Mr. Alloyce alishtuka sana.
"Kwani kuna Eddy wangapi hapa Mzee..!" Alijibu Mlinzi Seba kwa masihara kwani alikuwa ni MTU wa masihara sana.
"Sipo kwenye utani ujue Seba.. Nani yupo ndani?.." Aliuliza kwa hasira mr. Alloyce kwani alihisi Seba anamtania.
"Eddy Mzee.." Alijibu mlinzi.
Mr.Alloyce alihisi kama nguvu zikimpungua mwilini mwake kwani alikuwa haamini yanayotokea kwenye maisha yake. Alijkuta anapatwa na woga ghafla.
"We Seba hebu twende wote ndani..!" Seba hakusita aliamua kumsindikiza bosi wake. Lakini moyoni mwake alikuwa na maswali mengi kwa nini bosi iweje arudi peke yake tena kwa mguu bila gari?. Alijiuliza ila hakuthubutu kunyanyua mdomo wake kuuliza chochote kwani alishaona hali ya bosi wake siku ile haikuwa nzuri.
Walifika mlangoni na kukuta mlango ukiwa wazi ilhali waliondoka na funguo. Suala like lilizidi kumchanganya Mr.Alloyce.
"Hebu niitie Huyo Eddy kwanza!" Alisema Mr.Alloyce kwani alikuwa anaogopa kuingia ndani ila hakujionesha kwa Seba kuwa alikuwa na hofu.
"Eddy!" Aliita Seba.
"Naaam!" Sauti kutoka ndani ilisikika.
"Muite aje nje.. Haiwezekani afungue mziki kama disco humu.." Alisema Mr Alloyce kwa kujivungisha tu kwani bado alikuwa haamini kama Kweli Eddy yupo nyumbani.
"Njoo huku we bwana mdogo.." Alisema Seba. Punde tu, Eddy alitoka nje na kumkuta baba yake. Mr.Alloyce alishtuka sana akahisi yupo ndotoni lakini ilokuwa sio ndoto Bali kweli. Machozi ya furaha yalimtoka, kwani hakutaraji kama angemkuta mwanaye akiwa yuko hai.
"Daddy! Karibu ndani!" Alisema Eddy kwa uchangamfu sana.
"Asante! Seba waweza kwenda..!" Alisema Mr.Alloyce huku wakiingia ndani na mwanae. Mr.Alloyce alishindwa kuizuia furaha yake, alijikuta anamkumbatia mwanaye kwa nguvu huku chozi likimdondoka.
"Eddy mwanangu umefika SAA ngapi?"
"Nilikuja toka mchana..!"
"Kwanini ulitutoroka?"
"Niliwatoroka wapi?" Aliuliza Eddy kwa mshangao, swali hilo lilimshangaza sana Mr.Alloyce. Ila hakutaka kuendekeza zaidi mada ile akijua kuwa inaweza sababisha mambo mengine.
"Umekula nini?" Aliamua kubadilisha mada Mr.Alloyce.
"Nilipika ugali na samaki zilizokuwemo kwenye jokofu."
"Ulikula ee..?"
"Ndio"
Mr.Alloyce alishangaa sana kusikia vile kwani hakutegemea kama Eddy angekula chakula kwani siku zote alikuwa akikataa chakula akidai ni kichafu. "Leo amekula?" Alijiuliza Mr.Alloyce ama kweli Mungu ametenda.
Mr. Alloyce pia alimshangaa sana mwanaye kwa uchangamfu aliokuwa nao siku ile, alikuwa na furaha ambayo Hakuwahi kumwona akiwa nayo tangu apate matatizo yake. Mr.Alloyce alifurahi ingawa alijiuliza sana imekuwaje?. Baada ya wote kuketi kwenye viti kwa ukimya mzito, ndipo Eddy alipoamua kuvunja ukimya kwa kumtupia swali baba yake. Swali lililoibua simanzi moyoni mwa Mr.Alloyce.
"Mama yuko wapi?"
Swali hilo liliibua machozi kwa Mr. Alloyce, alishindwa amwambie nini mwanaye.
"Daddy mbona unalia kulikoni?" Aliuliza Eddy kwa mshangao.
"Eddy... Mama yako amefariki... Sielewi ntafanyaje... Sielewi ntawaambia nini ndugu zake mpaka wanielewee.. Sielewi..!"
"Amefariki? Kivipi?" Eddy alishtuka sana.
"Amefariki baada ya wewe kutoroka..!"
"Kwani Mimi nimewatoroka wapi?"
"Eddy umesahau au..? "
*********
Mwalimu Amina na Matron walibaki wakishangaana tu kwani walipoingia bwenini alikokuwa amelala Doreen. Hawakumkuta mtu yeyote ila walikaribishwa na harufu kali ya haja kubwa.
Walipotazama chini kulikuwa na hali mbaya sana kwani kinyesi kilikuwa kimetandazwa chini kwa mafungu kama matano. Walikunja sura zao kwa kinyaa hawakutaka hata kuingia bwenini mle.
"Doreen!" Aliita Madam Amina kwa sauti lakini hakujibiwa. Alienda hadi chooni kumwangalia lakini hakuwepo.Madam Amina aliamua kwenda madarasani kumtafuta lakini ilikuwa kazi Bure kwani huko pia hakuwepo.
"Dunia ina mambo..!" Alisema Madam Amina. Matron alibaki anashangaa tu huku anatikisa kichwa kwa masikitiko.
"Ila tusije tukauliwa na sisi...!" Alisema Matron.
"Hakuna kitu kama hicho..!"
" mbona unajiamini sana? Una nini mwenzetu?"
"Mungu tu ndo nilienae ananifanya nijiamini sana..!"
"Mh Haya.. Nimeamini kweli huyu mtoto ni mchawi haswa.. Kweli amejisaidia bwenini namna ile?.. Sasa sijui ameenda wapi.."Alisema matron.
"Bora tu aondoke ili shule ibaki na Amani tu..!" Alisema Madam Amina.
Kiukweli aliwashangaza sana. Ila bado hawakujua binti yule ameenda wapi.
*********
Mwalimu Jason alikuwa ameshikilia kisu kile chenye makali ili atimize sharti alilopewa kwenye karatasi lile la ajabu. Machozu yalimchuruzika sana, alilia kwa uchungu ulioje.
"Judith... Nakupenda... Ila sina budi kufanya hili...!" Alisema mwalimu Jason huku akitamani kusitisha jambo analotaka kufanya lakini alishindwa kutokana na nguvu za Giza zilizokuwa zikimshinikisha kufanya vile. Alimuonea huruma sana Judith, msichana ambaye alimpenda kwa dhati na kuahidi kufunga naye ndoa. Alimtazama Judith kwa simanzi, judith alikuwa akilia sana huku haja ndogo ikimshuka taratibu miguuni mwake. Alitetemeka kwa hofu sana akijuta kwanini alienda kumtembelea Jason.
"Nataka titi lako.."
"Jason kweli we umekuwa katili namna hiyo.. Kwanin lakini Jason.. Nimekosa nini .." Alilalamika Judith machozi yakimchuruzika mashavuni mwake alikuwa mwekundu kama pilipili iliyoiva.
"Kwa sababu hiyo.. Bora nife Mimi Judith.. Maana nina mawili tu ya kuchagua. ." Jason aliposema hivyo tu akakiinua kisu na kukishusha kwa kasi mpaka kifuani kwake. Kikazama taratibu huku Judith akimshuhudia jinsi Jason anavyojiua..Akataka kupiga kelele lakini akajiziba mdomo kwa hofu na mshangao...
Itaendelea.......
Usikose kufuatilia sehemu inayofuata
 
RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya Ishirini
MTUNZI: ENEA FAIDY
.....EDDY aliumia sana kwa taarifa zile za kifo cha mama yake. Hakutaka kuamini kama kweli mama yake hatakuwa pamoja nao tena. Machozi yalimbubujika kwa kasi huku akimwita mama take kana kwamba alikuwa karibu yake.
Mr.Alloyce alishindwa kuvumilia, alijikuta akiungana na mwanaye kulia. Walilia sana mpaka machozi yaliwakauka, Mr Alloyce alichukua leso yake na kujifuta machozi yake kisha akachukua simu ili awajulishe ndugu na marafiki kuhusu kifo cha mkewe.
Moyo wake ulisita sita sana kwani aliwaza ni jinsi gani ndugu wangeupokea msiba ule wa ghafla bila hata maiti.
"Eddy watanielewaje shemeji zangu? Umesababisha yote haya mwanangu, lakini siwezi kukulaumu!" Alisema Mr Alloyce huku machozi yakimlengalenga.
"Nisamehe dady kwa kuwa chanzo cha matatizo yote!" Alisema Eddy na kuendelea kulia.
Lakini hawakuwa na jinsi ya kufanya kwani tayari maji yalikwisha mwagika na ilikuwa vigumu sana kuzoleka. Ilibidi wakubaliane na kilichotokea ingawa kishingo upande sana.
Mr Alloyce alitafuta namba kwenye simu yake, MTU wa kwanza kumpata alikuwa shemeji yake aishiye jijini Dar ( Dada wa mama Eddy). Simu iliita kisha ikapokelewa, kwa kutetemeka na woga Mr Alloyce akaanzisha mazungumzo.
"Halloo Shem"
"Niambie Shem wake mie.. Kwema huko?" Alisema shemeji take Alloyce kwa uchangamfu sana kama ilivyokuwa kawaida yake. Hakuijua msiba mzito uliokuwa moyoni mwa Mr.Alloyce.
"Huku sio kwema Shem..!" Aliens Mr Alloyce.
"Sio kwema kuna nini?" Alishtuka.
"Sio kwema naomba kesho mfike nyumbani kwangu tafadhali.."
"Kuna nini shemeji? Naomba niambie tu.. Nini kimetokea?"
"Utajua kila kitu kesho..!"
"Hapana..niambie Leo.. Au MPE mama Eddy simu niongee nae..!" Maneno hayo yalimkata maini Baba Eddy hakuelewa ajibu nini akabaki kimya kwa sekunde chache akitafakari cha kujibu lakini ghafla akasikia sauti Kali ya Eddy ikimwita."Daaaaaaaaady!"
Mr Alloyce alishtuka sana kwani Eddy alikuwa ametoka sebuleni pale dakika chache zilizopita wakati yeye akiongea na simu. Hofu ikamkamata ghafla na kumfanya Mr Alloyce atupe simu sofani na kuelekea sauti ya Eddy inakotokea. Eddy aliita tena "Daaaaaaaady!" Mara hii sauti ile iliambatana na mwangwi mkali uliozidi kumtisha Mr Alloyce.
Alitoka sebuleni na kwenda koridoni lakini hakumuona Eddy. Akasikia sauti ikitokea chooni, alikimbia haraka na kwenda chooni lakini hakumuona, ghafla sauti ya Eddy ikasikika tena ikitokea chumbani kwa Eddy ilibidi amfuate haraka lakini cha kusikitisha Mr Alloyce hakumkuta Eddy ila alikuta damu nyingi zikiwa sakafuni. Alishtuka sana.
*****
Doreen aliamua kuondoka katika shule ya mabango kwani mambo yake yalikwishaanza kuharibika hivyo aliona heri aondoke zake kabla mambo makubwa hayajampata. Na yote hiyo ilitokana na maombi makali aliyokuwa akiyafanya Nadia Joseph ili kuinusuru shule yake kwa majanga yanayoikumba kila kukicha. Aliamua kujitesa kwa kufunga kila siku ili mradi tu shule yao ikomboke na irudi katika mstari ulionyooka.
Hakika Sikio la Mungu si zito ili lisisikie, Mungu alisikia maombi ya Nadia ndio maana alianza kuharibu mambo ya Doreen taratibu.Doreen alimchukia sana Nadia, akaahidi kumfanyia kitu kibaya sana ili alipize kisasi
"Ipo siku yake... Nitamwadhibu huyu mshe** kwa alichonifanyia... Nimeondoka kwasababu yake... Ila hata ipite miaka kumi ntampata tu!" Alijisemea Doreen na kusonya. Wakati huo akiwa njiani kuelekea nyumbani kwa mwalimu Jason kwani alipajua vizuri sana.
Alitembea kwa haraka kwa mwendo wa nusu SAA nzima hatimaye akawasili ndani ya nyumba ya Mwalimu Jason ili akatazame kinachoendelea.
Aliongia mdani na kukutana na ukimya mzito. Kwa ujasiri na kujiamini sana Doreen aliingia chumbani kwa Mwalimu Jason na kukuta harufu Kali ya damu na mwili wa mwalimu Jason.
Kwa wakati huo Judith alikuwa tayari amechapa lapa ili kuiepuka kesi ya mauaji ambayo ingemkabili. Na kama angekuwepo ndani mle basi ingekuwa nyama ya Doreen kwani angetumia vizuri nafasi ile kupata titi la Judith.
Doreen aliutazama mwili wa Jason kisha akaachia sonyo Kali. Akakisogelea kitanda na kutafuta karatasi lake, akalikuta chini ya mto. Akachukua na kulitia kwenye mkoba wake kisha akaondoka zake.
Akashika njia kuelekea kituo cha mabasi cha mkoani Iringa ili atafute gari liendalo mkoani Mbeya aende huko.Alipokuwa njiani alitazama pesa aliyokuwa nayo alishtuka kidogo kwani ilikuwa ni shilingi elfu moja tu ambayo haitoshi kwa lolote. Akawaza kwa sekunde kadhaa jinsi ya kufanya akapata jibu kisha akaendelea na safari yake.Alipofika mbele kidogo aliona duka kubwa limeandikwa Sanga Mini Market akaingia mle.
"Karibu! " sauti ya mwanaume mwenye duka ilimkaribisha.
"Asante! Nataka pop corn moja!"
"OK.. Ya 500 au 1000?."
"Nipe ya 500.." Alisema Doreen na alijua kabisa ana shilingi elfu moja. Lakini kuna kitu alitaka kufanya, alitaka kuiba pesa kwa kutumia ile shilingi elfu moja yake.
Mzee yule alitoa popcorn na kumkabidhi Doreen.Doreen alichukua shilingi elfu moja kwenye mkoba wake na kumpa Muuza duka. Muuza duka alipokea akataka kumrudishia chenji lakini ghafla akasita.
"We mtoto unanichezea? Hebu rudisha hizo popcorn... Shika hela yako.. Mpuuzi mkubwa wewe unataka kuniletea wanga wako hapa?" Alifoka muuza duka yule kwa jazba kwani alipoipokea hela ile akaugundua mchezo mzima wa Doreen aliotaka kuifanya. Doreen alishtuka, akaona aibu.
"Kwani vipi baba?" Alisema Doreen kwa upole kwani uligundua Mzee yule in kiboko zaidi yake.
"Wewe mtoto ntakuumbua hapa? Toka zako...." Mzee yule aliitupa chini hela Doreen na kumnyang'anya kwa nguvu ile popcorn.
"Unafikiri tunauza kizembe? Wachezee huko huko hii namba tasa sio shufwa..!" Alisema Mzee yule Doreen akiwa anaondoka.Doreen aliona aibu sana lakini hakukata tamaa kwani alijua tu atapata mtu ambaye hana zindiko lolote.
Uzuri wake uliwachanganya wengi sana kwani kila alipopita alikuwa akitazamwa kama nyota ya alfajiri huku wengine wakimpigia miruzi na wengine wakijaribu kumwita majina wanayoyajua wenyewe ili tu wabahatishe jina lake. Ni kweli Doreen alikuwa mzuri kupindukia, aling'aa kama m balamwezi ila tabia zake za ndani zilitisha zilokuwa mbaya kama Israel mtoa roho.
Alitembea taratibu na kuingia kwenye mgahawa mmoja wa vyakula. Aliketi kisha akaagiza chipsi kavu za shilingi mia saba.
"Sahani moja elfu moja?"
"Samahani Dada nina mia saba tu nisaidie.. Nimetoka mbali na nina njaa sana..!" Alisema Doreen kwa upole sana ambapo aliweza kumshawishi kirahisi muuzaji, akamkubalia kwa kumuonea huruma.
Watu walikuwa wengi mhahawani mle, Doreen alijiinamia chini tu akisubiri aletewe chipsi zake. Kwa muoneakano wa haraka ilikuwa vigumu sana kubaini tabia za Doreen kwani alionekana mpole na mkarimu sana.
Chipsi sake zikaletwa, ilibidi atoe hela na arudishiwe chenji yake. Chenji ambayo ilikuwa tofauti na kiwango kinachostahili.
*****
Ulimi wa Mwalimu John ulikuwa mzito kutamka neno lolote. Kila akijaribu kusema chochote maneno yalikuwa hayaeleweki ndipo mkewe akabaini kuwa tayari mumewe amekuwa bubu. Roho ilimuuma sana kwani mumewe asingeweza kufanya kazi tena. Wataishi vipi mjini bila kazi? Aliwaza mkewe.
Lakini licha ya kuumia moyo ila alimshukuru Mungu kwa uhai alioachiwa mumewe. Siku zikaendelea kusonga.Ilikuwa saa mbili usiku nyumbani kwa mwalimu John.Ukimya ulitawala sebuleni pale kwani ndugu wote walikuwa wameenda majumbani mwao hivyo walibaki wawili tu, ghafla mlango uligongwa.
"Karibu! " alikaribisha Leyla mke wa mwalimu John. Bila kutegemea aliingia Judith, kwani alikuwa akipafahamu vizuri nyumbani kwa mwalimu John. Na hii ilitokana na ukaribu waliokuwa nao mwalimu John na Jason, hivyo mwalimu Jason alimtambulisha Judith kama mkewe mtarajiwa.
"Karibu.." Alimkaribisha Leyla.
"Asante.. Za hapa!"
"Nzuri kiasi.. Umefika lini?"
"Tangu juzi.." Alisema Judith lakini alionekana mwenye hofu na mawazo mengi.
"Karibu.. Ulikuwa kwa Jason?"
Swali like liliibua kumbukumbu ya tukio aliloshuhudia kwa mpenzi wake. Machozi yalimshuka kwa kasi, lakini alishangaa sana kwanini tangu amefika Mwalimu John hajasema lolote.
"Hamjasikia chochote kuhusu Jason?"
"Ndio.. Kwani kuna nini?" Alishtuka sana Leyla.
"Ni stori ndefu sana ila mwalimu Jason alijiua!"
"Ati nini?"
"Ndio.. Inaniuma sana... Alitaka kuniua Mimi lakini akabadili msimamo na kusema bora ajiue yeye.." Aliendelea Julia Judith
"Kwanini?"
"Alisema ana sharti la.." Kabla Judith hajaendelea....
itaendelea.....
KWANINI DOREEN ANAKUWA KATILI KIASI KILE? ATAFANIKIWA KUPATA TITI? NA NINI HATMA YAKE USIACHE KUFUATILIA.
Usikose kufuatilia
 
Back
Top Bottom