Riwaya ya kipelelezi: Wakala wa Siri

WAKALA WA SIRI 16
Mtunzi: Robert Heriel
0693322300

ILIPOISHIA
Akaacha kulikung’uta na kuanza kukitafuta hicho kilichoanguka, aliangaza macho yake huku na huku, upande huu na upande huu lakini hakuweza kukiona kitu hicho ambacho alikisikia kimeanguka wakati akiwa anakung’uta lile koti. Fernanda akahisi huenda alisikia vibaya, akapuuza lakini kabla hajaendelea kukung’uta alihamaki kukiona kitu mfano wa funguo karibu na miguu yake, akajua ndio kile kitu alichokisikia kikianguka,

INAENDELEA
Fernanda akahisi huenda alisikia vibaya, akapuuza lakini kabla hajaendelea kukung’uta alihamaki kukiona kitu mfano wa funguo karibu na miguu yake, akajua ndio kile kitu alichokisikia kikianguka,



Aliiokota ile funguo akaanza kuitazama kwa umakini huku akijiuliza ni funguo ya wapi. Akaigeukia ile kabati ya nguo lakini hakuona droo yoyote ambayo ingetumia funguo ile. Fernanda akatoka kwenye kile chumba kisha akaenda kule kilipokuwepo kitanda. Alipofika akaanza kukagua kona na kingo zote za kitanda akitafuta droo ambayo ingetumia funguo zile lakini hakuona droo wala mahali popote ambapo funguo ile ingetumika. Akawa anajiuliza sasa ile funguo inafungulia wapi, na kama haifungulii mule ndani kwa nini Meja Venance Kagoda awe nazo mfukoni. Fernanda akafikiri aende katika vyumba vingine au sebuleni huenda angekuta mahali ambapo funguo ile ingetumika, lakini kabla hajatoka macho yake yalitua kwenye jokofu lililokuwa pembeni kabisa kwenye kona ya kile chumba, Fernanda akalisogelea lile jokofu alafu akafungua mlango wake, macho yake yakapokelewa chupa za pombe na wine mbalimbali, lakini chini kabisa ilikuwepo kufuli, moyo wa Fernanda ukapiga kite kwa nguvu huku akili yake ikipoteza mhimili wake. Aliitazama ile funguo alafu akaitazama na ile kufuli, akafungua ile kufuli na kuvuta ile droo ya jokofu hapo alishtuka kuona kitambaa cha kijeshi kilichofunika kitu Fulani, kwa shauku ya kutaka kujua kilichofunikwa akanyosha mkono kufungua kile kitambaa, alipokifungua alishtuka kuona simu janja aina ya Samsung A12. Akiwa anaichukua, mara alihisi nyuma yake kuna mtu, na kabla hajathibitisha jambo hilo, akashangaa kitu kigumu cha baridi kikigusa shingo yake kikifuatiwa na sauti kavu iliyombali kabisa na mzaha.

“Weka mikono yako juu, tulia hivyohivyo, udanganyifu wowote utakugharimu” Fernanda bila kuleta ukaidi aliiacha ile simu na kunyosha mikono juu kama mateka, akilini akijiuliza aliyenyuma yake alikuwa nani.

“Unajifanya mjanja sana!! Hahahah! Huwezi shindana na serikali Fernanda” Yule mtu mwenye sauti ya kavu aliongea kwa kejeli huku akijichekesha kwa dharau.

“Nani anashindana na serikali?” Fernanda akauliza akiwa kaweka mikono juu.

“ Humjui? Si wewe na Yule panya buku ajiitaye Sajenti” Yule mtu alimjibu Fernanda bado akiwa kaiweka bastola kwenye kichwa cha Fernanda,

“Adui wa serikali ni huyo bwege aliyekutuma wewe mjinga mwenye akili ya nguruwe; unawezaje kumuita Sajenti adui wa taifa..” Fernanda akasema lakini alikatishwa na ngumi nzito ya kichwa iliyompeleka chini. Akagugumia kwa maumivu makali ya ngumi ya Yule mtu mbaya. Ngumi ile ilimjulisha Fernanda kuwa aliyenyuma yake alikuwa anamikono migumu na mikakamavu.

“ Usilete kiburi chako wewe Malaya, nitakuua sasa hivi, usifikiri upo yule mbwa koko wako” Yule mtu aliongea wakati huu Fernanda akiwa amemuona baada ya kuanguka pale chini. Alikuwa mtu mrefu kama jitu, mweusi mwenye kovu kubwa kwenye paji lake, kichwani alikuwa amenyoa kiduku huku shingoni akiwa kava mkufu wa silva. Macho yake yalikuwa mekundu kama damu yaliyoficha dhuluma na ukatili aliowafanyia watu. Mikono yake ilikuwa na mishipa mingi iliyotuna kama mizizi hiyo ilidhihirisha kuwa jitu lile lilikuwa na nguvu nyingi mno. Alivalia Fulana nyeusi na kaptura ya kijeshi iliyopita magoti yake, chini alivalia mabuti marefu meusi yenye soli ngumu. Yule mtu wa kutisha alimtazama Fernanda kifua chake kikiwa kimetuna kwa mazoezi, Fernanda hakuwahi kuona mtu wa kutisha kama Yule katika maisha yake, alimfananisha na zimwi la kivita lenye kiu ya kumwaga damu.

Yule mtu akamsogelea kwa kasi Fernanda na kumrushia teke ambalo lingempiga Fernanda kwenye kichwa lakini Fernanda aliigundua hila yake, akakwepa kwa upesi kama ngedere; alafu akahamia upande wa pili, lakini lile jitu bado halikumuacha, kwa haraka ya upepo Yule mtu alimgeukia Fernanda kwa kasi iliyomshangaza Fernanda na kumpiga ngumi iliyompata Fernanda sawia kwenye bega lake, Fernanda akagugumia kwa maumivu akiwa kalala sakafuni. Yule mtu alikuwa na ngumi nzito yenye maumivu ya mauti.

Yule mtu ambaye Fernanda aliliona kama jitu likamkamata kwa nguvu alafu likamtupa ukutani, looh! Fernanda hakuwa na ujanja, alipiga ukuta na kuanguka chini kama kiroba cha nazi, hapo akajinyonga nyonga kama nyoka aliyejeruhiwa akamwagiwa mafuta ya taa, yalikuwa maumivu makali ambayo Fernanda alihisi uti wa mgongo umevunjika. Licha ya mapigo hayo ya kifo lile jitu bado lilimuandama; likamfuata na kumshika kwenye shingo na kumning’iniza juu. Fernanda aligugumia kwa maumivu akijaribu kujitetea kwa kutoa ile mikono migumu iliyokaba shingo yake kama nyaya. Alipumua kwa shida lakini Yule mtu hakujali.

“Kabla sijakuua kifo kibaya ambacho tangu kuzaliwa hujawahi kukiona wala kukisikia, nambie Sajenti yupo wapi?” Yule mtu akasema huku huku akimkazia macho Fernanda.

“ Hapa.. nitaongeaje wakati umenikaba sana mpaka siwezi kupumua?” Fernanda akaongea sauti yake ikitoka kwa shida kutokana na kukabwa sana. Sauti yake ilishindwa kutoka vizuri.

Yule mtu akampigisha chini akamuachia, kisha akasema;

“Haya nimekuachia, sema wapi alipo Yule Panya buku, usithubutu kuleta ujanja wowote nisije nikaichomoa roho yako bila ganzi”

“ Panya buku…!! mimi simjui” Fernanda alijibu huku akikohoa. Yule mtu akampiga kofi la shavu lililofanya uso wa Fernanda kuwa mwekundu na kuchora alama za vidole kadhaa vya lile jitu.

“Unaleta mzaha eeh! Nafikiri sina haja ya kukuonea huruma sasa, naenda kukuua kabla ya kupambazuka” Yule mtu akaongea huku akimsogelea Fernanda uso wake ukitisha zaidi. Fernanda akaona akileta mchezo pale ule unaweza kuwa mwisho wake. Hivyo akaona ni bora atumie akili kuchelewesha kifo chake hata kama angepaswa afe siku ile.Hata hivyo maneno ya Yule mtu kusema habari za huruma yalimchefua sana Fernanda, kwani mtu Yule hakuwa na sura ya huruma, sura yake ilifanana kwa kiasi kikubwa na Sokwe jeuri lenye ukatili wa kila namna.

“ Subiri! Nitakuambia kila kitu, wala usinipige” Fernanda akasema hapohapo Yule mtu akasimama, akimtazama kama mtu anayesubiri habari ya maana

“Umesema unataka nini kutoka kwangu wewe zimwi baya?” Fernanda aliuliza tena swali lililomghadhibisha sana Yule mtu.

“Wewe Malaya usinichezee akili, nambie wapi alipo Sajent Warioba” Yule mtu aliongea kwa sauti mbaya ambayo Fernanda hakuijua hapo kabla, mtu Yule alisema hayo akiwa kashika kidevu cha Fernanda kwa nguvu huku akimkazia macho yake.

Kwa upesi Fernanda alijipachua na kumpiga yule mtu teke la makende, yule mtu akagugumia kwa uchungu akiwa kashika nyeti zake. Lilikuwa pigo baya mno lililomuingia sawia. Fernanda aliamka pale chini kisha akampiga yule mtu teke la mdomo, yule mtu akaanguka chini akiwa ameiachia ile bastola na kupiga yowe la uchungu. Fernanda bila ya kupoteza muda akamfuata pale chini akamuongeza teke jingine la uso yule mtu akabamiza ukutani na kauchia kishindo. Fernanda hakulaza damu, hakutaka kumuachia nafasi kwani alijua hatari ambayo ingeweza kumkabili. Akaiwahi ile bastola ya yule mtu iliyoanguka chini, kisha akamuwekea shingoni. Yule mtu hakuamini kilichokuwa kinatokea muda ule, alikuwa akihema kwa pupa mithili ya mnyama aliyekoswa na mtego.

“Umetumwa na nani? Sema upesi kabla sijatoboa hii shingo yako” Fernanda aliongea kwa sauti isiyojali akiwa anathema hema.

“Toboa..wewe itoboe hiyo shingo, sitasema aliyenituma” Yule mtu akasema maumivu bado yakiwa yanamsugua vilivyo. Fernanda akampiga risasi ya begani. Yule mtu alipiga yowe la uchungu alafu akasema;

“ Umechelewa! Haitasaidia kitu hata nikisema”

“ KELELE!”

“Nataka unambia nani amekutuma?” Fernanda aliongea kwa kufoka na kufanya chumba kizima kiwe na uhai. Yule mtu hakutaka aseme jambo lolote, akataka kumgeukia kwa upesi Fernanda lakini alichelewa, hila yake ilishtukiwa na kabla hajafanikiwa kichwa chake kilipasuliwa vipande vipande na risasi. Chumba kizima kilitapakaa damu za jitu lile. Fernanda hakutaka kupoteza muda alichukua ile simu aliyokuwa ameiacha kwenye Jokofu, kisha akarudi kumpekua yule mtu wa kutisha kama zimwi, hakuona la maana kwenye mifuko yake. Akamuacha na kuondoka. Aliiifuata ile korido akiwa kashika bastola mkononi, huku bastola nyingine akiwa ameisunda mafichoni nyuma ya mgongo.

Alitokea sebuleni ambapo kulikuwa na giza kutokana na taa ya sebuleni ilikuwa imezimwa, akatafuta swichi ya kuwashia taa ya pale sebuleni, alipoiona akawasha taa, macho yake yalipokelewa na sebule kubwa iliyosheheni samani za kisasa kabisa, lilikuwepo zulia la manyoya zuri lakini lenye vumbi, juu ya dari ya sebule ilikuwepo Pangaboi nyeupe pamoja na urembo urembo wa dari za kiarabu. Ukutani aliiona saa kubwa ambayo ilikuwa ikionyesha ni saa kumi na dakika hamsini. Upande wa kulia kulikuwa na dirisha kubwa lililoangaliana na korido aliyokuwa ametokea. Dirisha jingine lilikuwa mbele yake, yote yalikuwa na mapazia mazuri ya kisasa kabisa. Luninga kubwa ya inchi hamsini na tano pamoja na seti ya muziki vilikuwa vipo upande usiokuwa na dirisha. Juu ya Luninga kabisa ukutani kulikuwa na picha kubwa iliyomuonyesha Meja Venance Kagoda akiwa na sare ya kijeshi na Kofi kichwani. Huyu ndio yuleyule ambaye mwili wake ulikuwa umeibiwa katika hospitali ya Boreti, ile Cadaver iliyokuwa inafanyiwa uchunguzi.

Meja Venance Kagoda mwili wake ulikutwa umeuawa nyumbani kwake bafuni, huku mke na mtoto wake wakiwa hawajulikani walipo, licha ya uchunguzi mkubwa uliokuwa ukiendelea lakini mpaka muda ule bado haikujulikana kama mke na mtoto wake wako wapi, haikujulikana kama wapo hai au walikwisha uawa na watu wasiojulikana. Taarifa ya kifo cha Meja Venance Kagoda zilizua gumzo kwenye vyombo vya habari na kwenye mitandao ya kijamii.

Fernanda alitoka kwenye ile nyumba akiwa kaichukua ile simu janja.

ITAENDELEA

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
zodo.jpg

WAKUU MKIWA MNAENDELEA KUBURUDIKA NA RIWAYA HII, NAPENDA KUWATANGAZIA OFA KABAMBE YA RIWAYA YA "MLIO WA RISASI HARUSINI"

WAHI OFA UPATE UHONDO
 
WAKALA WA SIRI 17
Mtunzi; Robert Heriel
0693322300

INAENDELEA

SURA YA 5

Asubuhi na mapema majira ya saa mbili hivi; Sajenti Warioba aliondoka kwenye Ghetto alilokuwa amepanga, Maeneo ya Mtoni Mtongani, kwa Azizi Ally. Akiwa kavalia suruali ya kadeti yenye rangi ya udongo, Tsheti nyeusi yenye kola huku kichwani akiwa kava Kapero. Chini alivaa viatu vigumu vilivyofanana na American buti vilivyokuwa na rangi nyeusi. Akatembea mpaka ilipobarabara kuu iendayo Mbagala, hapo akasimama akisubiri usafiri. Macho yake yalikuwa makini kutazama mienendo ya wapita njia waliokuwa wakienda na kurudi katika eneo lile. Alijua kuwa bado alikuwa akitafutwa hivyo asingejidanganya kuwa yupo salama.

Kitambo kidogo, alisimamisha Uber akachoma ndani.

“Nipeleke Posta” Sajenti aliongea baada ya kufunguliwa mlango na Derava wa Uber.

“Haina shida Boss” Dereva wa Uber akaongea akiwa anatabasamu kama ishara ya ukarimu kwa mteja wake. Baada ya kufunga mkanda, safari ikaanza ya kuelekea Posta.

Sajenti alichungulia nyuma kukagua usalama wa safari yake kuona kama kuna watu waliokuwa wanamfuatilia, lakini hali ilikuwa shwari. Aliona daladala, na bajaji tuu zilizokuwa zinaheka heka za kusafirisha abiria. Aliingiza mkono mfukoni alafu akatoa ile chipu akawa anaitazama kama mtu mwenye kuchunguza jambo Fulani, akiwa anataitazama akili yake ikamtonya kuwa dereva wa Uber atakuwa anamtazama Kupitia kioo cha gari kilichopo juu ya dereva, Sajenti alinyanyua macho yake kiujanja na kutazama kwenye kile kioo, alishtuka kugongana macho na Dereva wa Uber, kumbe Yule Dereva alikuwa akimtazama.

Sajenti Warioba akanyanyua kichwa chake, muda huo dereva akiwa kaacha kutazama kwenye kioo, alikuwa akitazama mbele huku akiendesha gari. Sajenti aliudadisi uso wa Dereva kuona kama angegundua lolote lakini hakuona tashwishwi yoyote kwa dereva. Ukimya ulikuwa mkubwa mule ndani ya gari, hakuna aliyeongea. Dereva akawasha Redio kufukuza ukimya ule, aliweka stesheni yenye uchambuzi wa Magazeti kwani ilikuwa asubuhi. Watangazaji walikuwa wakisoma vichwa vya habari vilivyokuwa vimeandikwa kwenye magazeti. Sajenti alikuwa katulia naye akisikiliza uchambuzi wa magazeti uliokuwa ukiendelea kwenye Redio. Ghafla alishtuka kusikia mtangazaji akisoma moja ya vichwa vya magazeti, kilichoandikwa; Dokta Beatus Kortin; wizi wa chipu watajwa” moyo wa Sajenti ulilipuka kwa mshtuko, mapigo yake ya moyo yalikimbia na kufanya damu iende kasi sana hali iliyosisimua ngozi yake. Wachambuzi wa magazeti hawakuichambua hiyo habari sana tofauti na habari zingine walizokuwa wamezisoma. Jambo hilo Sajenti alilitambua kuwa ni kutokana na usiri uliomo kwenye chipu yenyewe.

Sajenti Warioba alimtazama yule Dereva wa Uber kumdadisi kama alikuwa amegundua jambo lolote. Lakini Dereva hakuwa na hili wala lile, alikuwa kashika usukani akiwa kaangalia mbele akiendesha gari lake. Hali hiyo ilimfanya Sajenti aumbe tabasamu dogo usoni mwake. Sajenti aligeuka nyuma kuangalia kama kuna gari iliyokuwa inawafuatilia lakini hakuona hatari yoyote.

“Boss nikushushie Posta ipi?” Dereva aliuliza na kumfanya Sajenti ashtuke na kugeuka mbele upesi kwani alikuwa amegeukia nyuma ya gari kutazama usalama wa safari yake.

“anhaa! Nipeleke mpaka ulipo Mtaa wa Madaraka” Sajenti akaongea huku akiangalia mbele mahali alipokuwa akimuelekeza Dereva wa Uber.

ITAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom