BOMU: Riwaya ya kipelelezi (1)

RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya kumi na sita

"Sijaelewa unazungumzia nini kijana?" Dr Luis alisema hofu dhahiri ikiwa katika sauti yake.

"Nimesema nataka ututengenezee kirusi cha DH+" Imma Ogbo alirudia tena.

"Unafaham nini kuhusu kirusi cha DH+?" Dr Luis aliuliza huku akiwa katika hali ya wasiwasi.

"Hapa kuna mgawanyo wa kazi. Wewe hauna jukumu la kuuliza maswali. Jukumu lako ni moja tu, kutekeleza kila nikwambiacho" Imma Ogbo alisema.

"Hawa watu wamejuaje kuhusu kirusi cha DH+. Dh+ ni kirusi kibaya sana. Endapo nikitengeneza kirusi cha DH+ na kuwakabidhi watu hawa ambao sijui wanataka kukifanyia nini itakuwa ni hatari sana. Katu siwezi kuwatengenezea kirusi cha DH+. Najua madhara yake ambayo hadi sasa yanamtesa Mheshimiwa rais" Dr Luis akawaza.

"Dr Luis umenielewa nikichokwambia?" Imma Ogbo aliuliza.

Dr Luis alikaa kimya.

"Dr Luis, napenda tuumalize mjadala huu kistaarabu. Sitaki tuumizane ili utekeleze nikwambiacho. Utatutengenezea kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.

Dr Luis alikaa kimya.

"Hii ni mara ya mwisho kukwambia kistaarabu. Naona unataka kuujua upande wangu wa pili. Mimi ni tafsiri sahihi ya neno ukatiri!!"

"Nitawatengenezea kirusi cha DH+, lakini kwa masharti mawili" Dr Luis alisema kwa uwoga.

"Haujaja kutupa masharti hapa!!" Imma Ogbo alifoka.

"Basi kama hutaki nikupe masharti, nisrme tu sitowatengenezea hiko kirusi. Nifanyeni mnavyoweza" Dr Luis alisema.

"Narudia kwa mara ya mwisho Dr Luis, sitaki nitumie nguvu ili kutekeleza hiki nikwambiacho!" Imma Ogbo alisema.

Dr Luis alikaa kimya.

"Bila hayo masharti yako, upo tayari ututengenezee kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.

"Siwezi kuwatengenezea" Dr Luis alijibu kwa ufupi. Huku macho yake yalimaanisha alichokuwa amekisema.

Mara, simu ya Imma Ogbo iliita. Alikuwa ni mzee Msangi.

"Eeeh nambie mzee..bado naendelea na mahojiano.." Imma Ogbo alisema simuni.

"Tumesikiliza majadiliano yako na Dr Luis. Naomba mpe nafasi akwambie hayo masharti" Mzee Msangi alisema.

"Ni nje ya utaratibu mzee. Hatuwezi kupewa masharti na mtu tuliyemteka" Imma Ogbo alisema.

"Mimi ni bosi wako hapa. Naomba fanya nilichokuagiza!" Mzee Msangi alifoka.

"Siwezi kufanya maagizo yako. Hujanileta wewe hapa! Mimi napewa oda na aliyenileta tu, ambaye ni..."

"Come on Imma Ogbo. Toka humo ndani!!" Mzee Msangi alifoka.

"Mzee unajua unachokifanya. Kwanza umekosea kufatilia majadiliano haya. Ndio maana kamera zote za huku zimezimwa. Bila shaka umeweka kamera zako za siri. Hilo ni kosa. Haya ni majadiliano ya siri. Kwahiyo ulikuwa unanichunguza? Umeniuzi sana. Na sasa unataka kuingilia kazi isiyokuhusu. Jua haya si majukumu yako. Na sipo tayari kuteleza usemayo" Imma Ogbo alisema.

Kwa hasira Mzee Msangi alikata simu.

"Twendeni huko shimoni!" Mzee Msangi aliwaambia wenzake. Kila mmoja akatoa bastola yake.

"Imma Ogbo hastahili kuifanya kazi hii" Mzee msangi alisema wakiwa katika korido kuelekea katika chumba cha mateso kilichokuwa chini kabisa ya jengo hilo.

Dakika saba ziliwafikisha shimoni. Cha kushangaza waliukuta mlango wazi. Na tangu kimejengwa chumba hiko hakikuwahi kuwa wazi. Kwa umakini mkubwa wakina mzee Msangi waliingia mle ndani.

Walikutana na jambo la kushangaza sana..

Hakuwepo Imma Ogbo wala Dr Luis...

Harakaharaka Dr Luis alitoa simu yake na kumpigia mkuu wa ulinzi wa lile jengo.

"Simon, kuna watu wawili wametoroka humu ndani. Hakikisha hatoki mtu ndani ya jengo hili. Fikisha taarifa kwa watu wako wote!" Mzee Msangi alifoka.

"Sawa mkuu" Simon alijibu.

Dakika hiyohiyo msako wa kuwasaka Imma Ogbo na Dr Luis ulianza mle ndani ya nyumba.

"Huyu kijana hajui kwa namna gani amefanya jambo la hatari sana. Hajui Dr Luis ni mtu wa muhimu kwetu kwa kiasi gani? Atajutia kwa hiki alichokifanya" Mzee Msangi aliwaza.

Mara simu yake iliita. Alikuwa Simon.

"Vipi Simon mmewapata?" Mzee Msangi aliuliza.

"Hatujafanikiwa mzee. Lakini nyuma ya nyumba tumekuta walinzi wetu watatu wameuwawa. Bila shaka hawa watu wameruka ukuta kwa nyuma. Msako inabidi utoke ndani ya jengo" Simon alisema.

"Umeruhusuje hilo Simon?" Mzee Msangi aliuliza.

"Jamaa walikata mawasiliano. Hata kamera zetu hazikuweza kuwanasa wakati wanatoroka. Wakati mafundi wakijaribu kurudisha nawasiliano yetu, kumbe hao watu ndio walikuwa wanatoroka" Simon alisema.

"Daah tumefanya kosa kubwa sana. Tutamwambia nini Roho?" Mzee Msangi aliwaza.

"Nitakuelekeza cha kufanya Simon. Ngoja nifikirie kidogo" Mzee Msangi alisema.

Ilipokatika simu ya Simon, mzee Msangi akapiga simu kwa Mark the Sniper.

"Vipi mzee, sisi bado tunaliwinda windo lendo" Mark alisema simuni.

"Mark kuna tatizo huku" Mzee Msangi alisema sauti yake ikiwa na uwoga.

"Tatizo gani tena mzee?" Mark aliuliza.

"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis!!"

"Unasemaje mzee?"

"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis" Mzee Msangi alirudia kusema.

"Kwanini Imma amefikia hatua hiyo?"

"Kulitokea kutoelewana na kutoelewana kidogo kati yangu na Imma. Na yeye nd'o akachukua hatua ya kumtorosha Dr Luis" Mzee Msangi alisema.

"Hilo limewezekana vipi? Katika nyumba yenye kamera za ulinzi na walinzi kama hiyo?"

"Imma Ogbo ameweza, ameua walinzi wetu watatu, huku akiacha ameuharibu kabisa mfumo wetu wa ulinzi" Mzee Msangi alisema.

"Hiyo ni mbaya sana kwetu. Si unajua Roho anarudi leo usiku. Na kesho asubuhi inabidi akutane na Dr Luis kwa mahojiano. Tutamweleza nini sasa na tulishamueleza kuwa yupo mikononi mwetu?"

"Yaani hata sielewi. Hapa nimechanyikiwa. Naomba rudini hapa tuone tunafanya nini? Lakini, lazima tumsake Imma Ogbo, apatikane kabla hakujakuchwa. Hii ni kwa kulinda kazi yetu" Mzee Msangi alisema.

"Sasa kuhusu hawa majamaa. Si unajua Ninja na yule mwanajeshi wamewateka wakina Daniel. Hapa tunaelekea Tegeta kwenda kuwamaliza hawa jamaa" Mark alisema.

"Haina shida. Ninja atamaliza kila kitu. Ninyi rudini kwanza huku ili tulimalize hili. Kisha tutamalizana na hao majamaa, kwakuwa wapo mikononi mwetu hakitoharibika kitu"

"Sawa mzee"
Mark The Sniper alisema. Alimwamuru dereva wao ageuze gari na kuelekea Kigamboni.

Mambo yalikuwa yameharibika. Na mharibuji alikuwa ni Imma Ogbo.

"Jamaa wanageuza gari.." Adrian alisema baada ya kuangalia katika vioo vya pembeni.

"Wamestukia nini kama tumemuua mwenzao?" Daniel aliuliza.

"Sidhani kama wamestukia. Sasa yatupasa na sisi tugeuze tuwafatilie wanaenda wapi??" Adrian alisema.

"Jamani, watoto wanguu.." David alisema kwa kulalama.

Daniel na Adrian walimwangalia tu yule mwanajeshi msaliti. Hakuna aliyesema kitu. Huku hasira dhahiri zikionekana usoni mwao.

Adrian akageuza gari na kuanza kuwafatilia wale majamaa. Sasa mchezo ukageuka. Sasa wafatiliaji wakageuka kuwa wafatiliwaji...

"Bila shaka wanatupeleka alipo Dr Luis" Daniel akawaza.

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
 
Imenogaaaaa
RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya kumi na sita

"Sijaelewa unazungumzia nini kijana?" Dr Luis alisema hofu dhahiri ikiwa katika sauti yake.

"Nimesema nataka ututengenezee kirusi cha DH+" Imma Ogbo alirudia tena.

"Unafaham nini kuhusu kirusi cha DH+?" Dr Luis aliuliza huku akiwa katika hali ya wasiwasi.

"Hapa kuna mgawanyo wa kazi. Wewe hauna jukumu la kuuliza maswali. Jukumu lako ni moja tu, kutekeleza kila nikwambiacho" Imma Ogbo alisema.

"Hawa watu wamejuaje kuhusu kirusi cha DH+. Dh+ ni kirusi kibaya sana. Endapo nikitengeneza kirusi cha DH+ na kuwakabidhi watu hawa ambao sijui wanataka kukifanyia nini itakuwa ni hatari sana. Katu siwezi kuwatengenezea kirusi cha DH+. Najua madhara yake ambayo hadi sasa yanamtesa Mheshimiwa rais" Dr Luis akawaza.

"Dr Luis umenielewa nikichokwambia?" Imma Ogbo aliuliza.

Dr Luis alikaa kimya.

"Dr Luis, napenda tuumalize mjadala huu kistaarabu. Sitaki tuumizane ili utekeleze nikwambiacho. Utatutengenezea kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.

Dr Luis alikaa kimya.

"Hii ni mara ya mwisho kukwambia kistaarabu. Naona unataka kuujua upande wangu wa pili. Mimi ni tafsiri sahihi ya neno ukatiri!!"

"Nitawatengenezea kirusi cha DH+, lakini kwa masharti mawili" Dr Luis alisema kwa uwoga.

"Haujaja kutupa masharti hapa!!" Imma Ogbo alifoka.

"Basi kama hutaki nikupe masharti, nisrme tu sitowatengenezea hiko kirusi. Nifanyeni mnavyoweza" Dr Luis alisema.

"Narudia kwa mara ya mwisho Dr Luis, sitaki nitumie nguvu ili kutekeleza hiki nikwambiacho!" Imma Ogbo alisema.

Dr Luis alikaa kimya.

"Bila hayo masharti yako, upo tayari ututengenezee kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.

"Siwezi kuwatengenezea" Dr Luis alijibu kwa ufupi. Huku macho yake yalimaanisha alichokuwa amekisema.

Mara, simu ya Imma Ogbo iliita. Alikuwa ni mzee Msangi.

"Eeeh nambie mzee..bado naendelea na mahojiano.." Imma Ogbo alisema simuni.

"Tumesikiliza majadiliano yako na Dr Luis. Naomba mpe nafasi akwambie hayo masharti" Mzee Msangi alisema.

"Ni nje ya utaratibu mzee. Hatuwezi kupewa masharti na mtu tuliyemteka" Imma Ogbo alisema.

"Mimi ni bosi wako hapa. Naomba fanya nilichokuagiza!" Mzee Msangi alifoka.

"Siwezi kufanya maagizo yako. Hujanileta wewe hapa! Mimi napewa oda na aliyenileta tu, ambaye ni..."

"Come on Imma Ogbo. Toka humo ndani!!" Mzee Msangi alifoka.

"Mzee unajua unachokifanya. Kwanza umekosea kufatilia majadiliano haya. Ndio maana kamera zote za huku zimezimwa. Bila shaka umeweka kamera zako za siri. Hilo ni kosa. Haya ni majadiliano ya siri. Kwahiyo ulikuwa unanichunguza? Umeniuzi sana. Na sasa unataka kuingilia kazi isiyokuhusu. Jua haya si majukumu yako. Na sipo tayari kuteleza usemayo" Imma Ogbo alisema.

Kwa hasira Mzee Msangi alikata simu.

"Twendeni huko shimoni!" Mzee Msangi aliwaambia wenzake. Kila mmoja akatoa bastola yake.

"Imma Ogbo hastahili kuifanya kazi hii" Mzee msangi alisema wakiwa katika korido kuelekea katika chumba cha mateso kilichokuwa chini kabisa ya jengo hilo.

Dakika saba ziliwafikisha shimoni. Cha kushangaza waliukuta mlango wazi. Na tangu kimejengwa chumba hiko hakikuwahi kuwa wazi. Kwa umakini mkubwa wakina mzee Msangi waliingia mle ndani.

Walikutana na jambo la kushangaza sana..

Hakuwepo Imma Ogbo wala Dr Luis...

Harakaharaka Dr Luis alitoa simu yake na kumpigia mkuu wa ulinzi wa lile jengo.

"Simon, kuna watu wawili wametoroka humu ndani. Hakikisha hatoki mtu ndani ya jengo hili. Fikisha taarifa kwa watu wako wote!" Mzee Msangi alifoka.

"Sawa mkuu" Simon alijibu.

Dakika hiyohiyo msako wa kuwasaka Imma Ogbo na Dr Luis ulianza mle ndani ya nyumba.

"Huyu kijana hajui kwa namna gani amefanya jambo la hatari sana. Hajui Dr Luis ni mtu wa muhimu kwetu kwa kiasi gani? Atajutia kwa hiki alichokifanya" Mzee Msangi aliwaza.

Mara simu yake iliita. Alikuwa Simon.

"Vipi Simon mmewapata?" Mzee Msangi aliuliza.

"Hatujafanikiwa mzee. Lakini nyuma ya nyumba tumekuta walinzi wetu watatu wameuwawa. Bila shaka hawa watu wameruka ukuta kwa nyuma. Msako inabidi utoke ndani ya jengo" Simon alisema.

"Umeruhusuje hilo Simon?" Mzee Msangi aliuliza.

"Jamaa walikata mawasiliano. Hata kamera zetu hazikuweza kuwanasa wakati wanatoroka. Wakati mafundi wakijaribu kurudisha nawasiliano yetu, kumbe hao watu ndio walikuwa wanatoroka" Simon alisema.

"Daah tumefanya kosa kubwa sana. Tutamwambia nini Roho?" Mzee Msangi aliwaza.

"Nitakuelekeza cha kufanya Simon. Ngoja nifikirie kidogo" Mzee Msangi alisema.

Ilipokatika simu ya Simon, mzee Msangi akapiga simu kwa Mark the Sniper.

"Vipi mzee, sisi bado tunaliwinda windo lendo" Mark alisema simuni.

"Mark kuna tatizo huku" Mzee Msangi alisema sauti yake ikiwa na uwoga.

"Tatizo gani tena mzee?" Mark aliuliza.

"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis!!"

"Unasemaje mzee?"

"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis" Mzee Msangi alirudia kusema.

"Kwanini Imma amefikia hatua hiyo?"

"Kulitokea kutoelewana na kutoelewana kidogo kati yangu na Imma. Na yeye nd'o akachukua hatua ya kumtorosha Dr Luis" Mzee Msangi alisema.

"Hilo limewezekana vipi? Katika nyumba yenye kamera za ulinzi na walinzi kama hiyo?"

"Imma Ogbo ameweza, ameua walinzi wetu watatu, huku akiacha ameuharibu kabisa mfumo wetu wa ulinzi" Mzee Msangi alisema.

"Hiyo ni mbaya sana kwetu. Si unajua Roho anarudi leo usiku. Na kesho asubuhi inabidi akutane na Dr Luis kwa mahojiano. Tutamweleza nini sasa na tulishamueleza kuwa yupo mikononi mwetu?"

"Yaani hata sielewi. Hapa nimechanyikiwa. Naomba rudini hapa tuone tunafanya nini? Lakini, lazima tumsake Imma Ogbo, apatikane kabla hakujakuchwa. Hii ni kwa kulinda kazi yetu" Mzee Msangi alisema.

"Sasa kuhusu hawa majamaa. Si unajua Ninja na yule mwanajeshi wamewateka wakina Daniel. Hapa tunaelekea Tegeta kwenda kuwamaliza hawa jamaa" Mark alisema.

"Haina shida. Ninja atamaliza kila kitu. Ninyi rudini kwanza huku ili tulimalize hili. Kisha tutamalizana na hao majamaa, kwakuwa wapo mikononi mwetu hakitoharibika kitu"

"Sawa mzee"
Mark The Sniper alisema. Alimwamuru dereva wao ageuze gari na kuelekea Kigamboni.

Mambo yalikuwa yameharibika. Na mharibuji alikuwa ni Imma Ogbo.

"Jamaa wanageuza gari.." Adrian alisema baada ya kuangalia katika vioo vya pembeni.

"Wamestukia nini kama tumemuua mwenzao?" Daniel aliuliza.

"Sidhani kama wamestukia. Sasa yatupasa na sisi tugeuze tuwafatilie wanaenda wapi??" Adrian alisema.

"Jamani, watoto wanguu.." David alisema kwa kulalama.

Daniel na Adrian walimwangalia tu yule mwanajeshi msaliti. Hakuna aliyesema kitu. Huku hasira dhahiri zikionekana usoni mwao.

Adrian akageuza gari na kuanza kuwafatilia wale majamaa. Sasa mchezo ukageuka. Sasa wafatiliaji wakageuka kuwa wafatiliwaji...

"Bila shaka wanatupeleka alipo Dr Luis" Daniel akawaza.

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
 
RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya kumi na sita

"Sijaelewa unazungumzia nini kijana?" Dr Luis alisema hofu dhahiri ikiwa katika sauti yake.

"Nimesema nataka ututengenezee kirusi cha DH+" Imma Ogbo alirudia tena.

"Unafaham nini kuhusu kirusi cha DH+?" Dr Luis aliuliza huku akiwa katika hali ya wasiwasi.

"Hapa kuna mgawanyo wa kazi. Wewe hauna jukumu la kuuliza maswali. Jukumu lako ni moja tu, kutekeleza kila nikwambiacho" Imma Ogbo alisema.

"Hawa watu wamejuaje kuhusu kirusi cha DH+. Dh+ ni kirusi kibaya sana. Endapo nikitengeneza kirusi cha DH+ na kuwakabidhi watu hawa ambao sijui wanataka kukifanyia nini itakuwa ni hatari sana. Katu siwezi kuwatengenezea kirusi cha DH+. Najua madhara yake ambayo hadi sasa yanamtesa Mheshimiwa rais" Dr Luis akawaza.

"Dr Luis umenielewa nikichokwambia?" Imma Ogbo aliuliza.

Dr Luis alikaa kimya.

"Dr Luis, napenda tuumalize mjadala huu kistaarabu. Sitaki tuumizane ili utekeleze nikwambiacho. Utatutengenezea kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.

Dr Luis alikaa kimya.

"Hii ni mara ya mwisho kukwambia kistaarabu. Naona unataka kuujua upande wangu wa pili. Mimi ni tafsiri sahihi ya neno ukatiri!!"

"Nitawatengenezea kirusi cha DH+, lakini kwa masharti mawili" Dr Luis alisema kwa uwoga.

"Haujaja kutupa masharti hapa!!" Imma Ogbo alifoka.

"Basi kama hutaki nikupe masharti, nisrme tu sitowatengenezea hiko kirusi. Nifanyeni mnavyoweza" Dr Luis alisema.

"Narudia kwa mara ya mwisho Dr Luis, sitaki nitumie nguvu ili kutekeleza hiki nikwambiacho!" Imma Ogbo alisema.

Dr Luis alikaa kimya.

"Bila hayo masharti yako, upo tayari ututengenezee kirusi cha DH+?" Imma Ogbo aliuliza.

"Siwezi kuwatengenezea" Dr Luis alijibu kwa ufupi. Huku macho yake yalimaanisha alichokuwa amekisema.

Mara, simu ya Imma Ogbo iliita. Alikuwa ni mzee Msangi.

"Eeeh nambie mzee..bado naendelea na mahojiano.." Imma Ogbo alisema simuni.

"Tumesikiliza majadiliano yako na Dr Luis. Naomba mpe nafasi akwambie hayo masharti" Mzee Msangi alisema.

"Ni nje ya utaratibu mzee. Hatuwezi kupewa masharti na mtu tuliyemteka" Imma Ogbo alisema.

"Mimi ni bosi wako hapa. Naomba fanya nilichokuagiza!" Mzee Msangi alifoka.

"Siwezi kufanya maagizo yako. Hujanileta wewe hapa! Mimi napewa oda na aliyenileta tu, ambaye ni..."

"Come on Imma Ogbo. Toka humo ndani!!" Mzee Msangi alifoka.

"Mzee unajua unachokifanya. Kwanza umekosea kufatilia majadiliano haya. Ndio maana kamera zote za huku zimezimwa. Bila shaka umeweka kamera zako za siri. Hilo ni kosa. Haya ni majadiliano ya siri. Kwahiyo ulikuwa unanichunguza? Umeniuzi sana. Na sasa unataka kuingilia kazi isiyokuhusu. Jua haya si majukumu yako. Na sipo tayari kuteleza usemayo" Imma Ogbo alisema.

Kwa hasira Mzee Msangi alikata simu.

"Twendeni huko shimoni!" Mzee Msangi aliwaambia wenzake. Kila mmoja akatoa bastola yake.

"Imma Ogbo hastahili kuifanya kazi hii" Mzee msangi alisema wakiwa katika korido kuelekea katika chumba cha mateso kilichokuwa chini kabisa ya jengo hilo.

Dakika saba ziliwafikisha shimoni. Cha kushangaza waliukuta mlango wazi. Na tangu kimejengwa chumba hiko hakikuwahi kuwa wazi. Kwa umakini mkubwa wakina mzee Msangi waliingia mle ndani.

Walikutana na jambo la kushangaza sana..

Hakuwepo Imma Ogbo wala Dr Luis...

Harakaharaka Dr Luis alitoa simu yake na kumpigia mkuu wa ulinzi wa lile jengo.

"Simon, kuna watu wawili wametoroka humu ndani. Hakikisha hatoki mtu ndani ya jengo hili. Fikisha taarifa kwa watu wako wote!" Mzee Msangi alifoka.

"Sawa mkuu" Simon alijibu.

Dakika hiyohiyo msako wa kuwasaka Imma Ogbo na Dr Luis ulianza mle ndani ya nyumba.

"Huyu kijana hajui kwa namna gani amefanya jambo la hatari sana. Hajui Dr Luis ni mtu wa muhimu kwetu kwa kiasi gani? Atajutia kwa hiki alichokifanya" Mzee Msangi aliwaza.

Mara simu yake iliita. Alikuwa Simon.

"Vipi Simon mmewapata?" Mzee Msangi aliuliza.

"Hatujafanikiwa mzee. Lakini nyuma ya nyumba tumekuta walinzi wetu watatu wameuwawa. Bila shaka hawa watu wameruka ukuta kwa nyuma. Msako inabidi utoke ndani ya jengo" Simon alisema.

"Umeruhusuje hilo Simon?" Mzee Msangi aliuliza.

"Jamaa walikata mawasiliano. Hata kamera zetu hazikuweza kuwanasa wakati wanatoroka. Wakati mafundi wakijaribu kurudisha nawasiliano yetu, kumbe hao watu ndio walikuwa wanatoroka" Simon alisema.

"Daah tumefanya kosa kubwa sana. Tutamwambia nini Roho?" Mzee Msangi aliwaza.

"Nitakuelekeza cha kufanya Simon. Ngoja nifikirie kidogo" Mzee Msangi alisema.

Ilipokatika simu ya Simon, mzee Msangi akapiga simu kwa Mark the Sniper.

"Vipi mzee, sisi bado tunaliwinda windo lendo" Mark alisema simuni.

"Mark kuna tatizo huku" Mzee Msangi alisema sauti yake ikiwa na uwoga.

"Tatizo gani tena mzee?" Mark aliuliza.

"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis!!"

"Unasemaje mzee?"

"Imma Ogbo ametoroka na Dr Luis" Mzee Msangi alirudia kusema.

"Kwanini Imma amefikia hatua hiyo?"

"Kulitokea kutoelewana na kutoelewana kidogo kati yangu na Imma. Na yeye nd'o akachukua hatua ya kumtorosha Dr Luis" Mzee Msangi alisema.

"Hilo limewezekana vipi? Katika nyumba yenye kamera za ulinzi na walinzi kama hiyo?"

"Imma Ogbo ameweza, ameua walinzi wetu watatu, huku akiacha ameuharibu kabisa mfumo wetu wa ulinzi" Mzee Msangi alisema.

"Hiyo ni mbaya sana kwetu. Si unajua Roho anarudi leo usiku. Na kesho asubuhi inabidi akutane na Dr Luis kwa mahojiano. Tutamweleza nini sasa na tulishamueleza kuwa yupo mikononi mwetu?"

"Yaani hata sielewi. Hapa nimechanyikiwa. Naomba rudini hapa tuone tunafanya nini? Lakini, lazima tumsake Imma Ogbo, apatikane kabla hakujakuchwa. Hii ni kwa kulinda kazi yetu" Mzee Msangi alisema.

"Sasa kuhusu hawa majamaa. Si unajua Ninja na yule mwanajeshi wamewateka wakina Daniel. Hapa tunaelekea Tegeta kwenda kuwamaliza hawa jamaa" Mark alisema.

"Haina shida. Ninja atamaliza kila kitu. Ninyi rudini kwanza huku ili tulimalize hili. Kisha tutamalizana na hao majamaa, kwakuwa wapo mikononi mwetu hakitoharibika kitu"

"Sawa mzee"
Mark The Sniper alisema. Alimwamuru dereva wao ageuze gari na kuelekea Kigamboni.

Mambo yalikuwa yameharibika. Na mharibuji alikuwa ni Imma Ogbo.

"Jamaa wanageuza gari.." Adrian alisema baada ya kuangalia katika vioo vya pembeni.

"Wamestukia nini kama tumemuua mwenzao?" Daniel aliuliza.

"Sidhani kama wamestukia. Sasa yatupasa na sisi tugeuze tuwafatilie wanaenda wapi??" Adrian alisema.

"Jamani, watoto wanguu.." David alisema kwa kulalama.

Daniel na Adrian walimwangalia tu yule mwanajeshi msaliti. Hakuna aliyesema kitu. Huku hasira dhahiri zikionekana usoni mwao.

Adrian akageuza gari na kuanza kuwafatilia wale majamaa. Sasa mchezo ukageuka. Sasa wafatiliaji wakageuka kuwa wafatiliwaji...

"Bila shaka wanatupeleka alipo Dr Luis" Daniel akawaza.

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
Shusha mzigo
 
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Saba

Martin Hisia bado alikuwa Mlimani city akimsubiri Daniel Mwaseba kama simu ilivyomwagiza.

Baada ya kusubiri zaidi ya nusu saa hisia zake zilimwambia kwamba kuna tatizo. Daniel Mwaseba alikuwa mtu wa kutimiza ahadi, sasa kwanini hadi muda huo alikuwa hajafika?

Felisia Nyenyembe, mpenzi wake alikuwa amekaa katika kona moja akimwangalia Martin Hisia. Alikuwa anasubiri watu ambao wametemwa na Imma Ogbo ili waje waumalize mchezo. Sehemu alipojibanza alikuwa anamwangalia kwa chati Martin huku akihakikisha hafanyi kosa lolote lile. Alikuwa anamjua Martin katika medani hizi.

"Siku Martin akigundua kwamba mimi nimewekwa kwa ajili ya kumchunguza sijui itakuaje?. Martin anaonekana kuniamini sana kwakuwa hajui mimi ni nani? Ila sijui kama nifanyacho ni sahihi? Martin ananipenda sana. Upendo wa Martin kwangu sio wa kawaida. Je ni sahihi kumfanyia ninachotaka kumfanyia Martin. Namuuza Martin..." Felisia aliacha kuwaza. Simu yake ilikuwa inaita.

"Hallo Imma?" Felisia alisema.

"Felisia bado upo Mlimani city?" Imma Ogbo aliuliza.

"Ndio, na jamaa bado anamsubiri Daniel Mwaseba hapa Mlimani city. Nashangaa kwanini amechukua muda mrefu sana kufika hapa" Felisia alisema.

"Mambo yamebadilika Felisia. Hapa nilipo tushavurugana na majamaa" Imma Ogbo alisema.

"Umevurugana na majamaa gani?" Felisia aliuliza.

"Nimevurugana na wakina mzee Msangi. Nimechoka na tabia zao za kufatilia kazi ambazo sio zao" Imma Ogbo alisema.

"Bado sijakuelewa Imma"

"Haya sio mambo ya kuongea simuni. Maana mambo yamebadilika. Nimekuwa adui kwao sasa. Nataka kuungana na wewe ili tuwashinde. Naomba uwe upande wangu" Imma alisema.

"Wewe unanijua Imma kuliko mtu yeyote yule. Sijawahi kuwa na jibu la hapana kwako. Ni wewe ndio ulioniingiza katika misheni hii tangu ukiwa Nigeria. Naanzaje kusema hapana kwako Imma" Felisia alisema.

"Nakuamini sana Felisia. Sasa mimi nipo Vikindu huku, unapajua?"

"Hapana, sipafaham"

"Chukua taksi yoyote hapo Mlimani, mwambie akulete Vikindu. Atakuleta" Imma alisema.

"Sawa Imma. Ninafanya hivyo sasahivi. Vipi kuhusu huyu Martin Hisia?" Felisia aliuliza.

"Achana nae. We njoo Vikindu. Tutapanga mipango yetu kuanzia hapa. Tunaelekea kuwa mabilionea soon" Imma Ogbo alisema.

"Nipo njiani brother" Felisia alisema.

Simu ikakatwa.

"Imma Ogbo amevurugana nini na hawa jamaa zake. Ni yeye ndiye aliyenitambulisha kwa hawa jamaa na nikawa pamoja katika misheni hii ya kumteka Dr Luis. Sasa limetokea tatizo gani tena. Ngoja niende huko Vikindu nikajue" Felisia akawaza.

Felisia alienda mahali wanakopaki teksi. Aliongea na dereva mmoja, wakakubaliana bei. Felisia alikaa siti za nyuma za gari, gari likawashwa.

Safari ya kuelekea Vikindu ikaanza.

Ndani ya gari mawazo yote yalikuwa juu ya misheni hii ambayo kwa sasa imebadilika. Pia alikuwa anawaza Imma Ogbo ataenda kumueleza kitu gani?.

***

Gari ya kina Adrian ilikuwa nyuma ikilifatilia gari la wale majamaa. Ndani ya gari ilikuwa kimya kabla Daniel Mwaseba kumuuliza swali David.

"David, hebu nambie kitu gani kimetokea hadi ukaamua kutusaliti na kuwa upande wa hawa jamaa?"

David akiwa bado amemuelekezea bastola Adrian alisema..

"Daniel, mimi sielewi walijuaje kuhusu mimi?" David alisema kwa majonzi.

"Walijuaje kuhusu nini?" Daniel aliuliza.

"Sikuwa na nia ya kuwasaliti ndugu zangu. Najua jukumu zito lililopo mbele yetu. Na tumiaminiwa sisi katika taifa lenye zaidi ya watu milioni hamsini. Lakini, mambo hayo yalianza ghafla tu nusu saa baada ya kupigiwa simu na mkuu wa majeshi na kupewa kazi hii" David alisema.

"Mbona unafichaficha David?. Kuwa muwazi ili tujue tunakusaidiaje. Kikanuni, si unayajua malipo ya msaliti katika misheni kama hizi? Ni kifo!
Tena kifo cha kuumiza. Huwa hatuhoji wasaliti kama nifanyavyo. Nimekupa nafasi hii adimu sana, naomba itumie. Na ni mara yangu ya kwanza katika maisha yangu kumuhoji msaliti" Daniel alisema.

"Daniel, jamaa wameiteka familia yangu..."

"Wameiteka familia yako? Lini? Mbona hukutuambia David?" Adrian akiwa katika usukani alidakia.

"Waliiteka familia yangu nusu saa tu baada ya kupewa kazi hii. Mke wangu, Hellen na watoto wangu mapacha, Candy na Cindy wapo mikononi mwa hawa jamaa. Walitumia kuiweka mateka familia yangu ili kunishinikiza niwaambie kuhusu mipango yetu" David alisema.

"Inamaana ni wewe ndiye ukiyewaambia mambo yetu?" Daniel aliuliza akishangaa.

"Samahanini sana brothers. Nimefanya kosa kubwa sana. Hapa nafsi inanisuta. Ila jamaa walinishika pabaya sana. Familia yangu ni kila kitu kwangu. Nimeshinda vikwazo vingi vigumu katika medani huko msituni, lakini kikwazo hiki nilishindwa kabisa" David alisema.

"Lakini kwanini usituambie kabla David ili tuone namna ya kuiokoa familia yako?" Daniel aliuliza.

"Walinionya nisithubutu kuwaambia lolote. Huku wakinipa kazi ya kuwaeleza direction yetu. Na hilo ndio kosa kubwa sana nililolifanya" David alisema.

"Mimi ninakusamehe David. Hii ni misheni yako ya kwanza mjini, ulizoea misheni za msituni. Na hili ni kosa lako la kwanza pia. Lakini bado nina maswali kwako"

David alitingisha kichwa kukubali.

"Ulikuwa unawasiliana vipi na hao watu?" Daniel aliuliza.

"Kuna mtu mmoja alikuwa ananipigia simu, na wakati mwengine tukiwasiliana kwa meseji" David alisema.

"Na ni wewe ndiye uliyewaambia kuhusu Hannan?"

"Ni mimi" David alisema kwa majonzi.

"Ulikosea sana David. Ona umemweka Hannan katika hatari kubwa sana. Anaweza kuuwawa muda wowote ule" Daniel alisema.

"Naamini atakuwa salama. Walimchukua Hannan kama chambo kukusaka wewe. Ninaapa nitaungana nanyi, tumsake Hannan mpaka tumpate. Na ninaomba sana nanyi mnisaidie kuiokoa familia yangu.." David alisema.

"Nakuahidi nitakusaidia. Na tutawapa mke na watoto wako. Wewe unahisi ni nani aliyewaambia hao watu uhusika wako nusu saa tu baada ya kuchaguliwa?" Daniel aliuliza.

"Mimi sifahamu. Lakini kuna watu sita ninawahisi, kati ya hao kuna mmoja au zaidi wanahusika" David alisema.

"Ni watu gani hao?" Adrian alirukia.

"Ni mkuu wa majeshi, mkuu wa Polisi, Chifu, wewe, Daniel ama Hannan. Watu hao sababu ndio pekee walijua kuchaguliwa kwangu katika misheni hii. Nahisi aliyepanga mpango wa kuiteka familia yangu yupo kati ya watu hao sita" David alisema kwa uhakika.

Daniel na Adrian walitazamana kupitia kioo cha kati. Kipindi hiko walikuwa wanapita juu ya daraja la Kigamboni wakiifatilia ile gari.

"David umeongea jambo zito sana. Lakini tutalifanyia kazi tujue ni nani yupo nyuma ya hawa watu." Daniel alisema.

"Hiyo namba ukiyowasiliana nayo iko wapi?" Adrian aliuliza.

"Hii hapa" David alisema huku akiitoa simu yake mfukoni.

"Ninamuhitaji sana Hannan kipindi hiki. Ni yeye ndiye angeichunguza hii namba ya nani? Tumpoteza Hannan, lakini hii kazi lazima iendelee. Ngoja nimpigie Mwanasheria mlevi, najua kwasasa yupo katika kitengo cha mawasiliano pale usalama wa Taifa. Ni yeye ndiye atakayetupa majibu wa ukweli juu ya namba hii" Daniel aliwaza.

"Naomba simu yako nimpigie mtu" Daniel alisema.

"Usiitumie simu yangu Daniel, wameitrack. Watasikia kila kitu" David alisema.

"Nipe simu yako Adrian tumpigie Mwanasheria mlevi..." Daniel alisema.

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
 
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212392

Sehemu ya Kumi na nane

Songelael Ntenga P.A.K Mwanasheria mlevi alikuwa amekaa makao makuu ya usalama wa Taifa. Alikuwa amekaa ofisini, mbele yake kukiwa na meza kubwa yenye mafaili mbalimbali, yakiyopepewa na upepo wa feni.

"Sijazoea kabisa hizi kazi za kukaa ofisini. Mi furaha yangu ni kuwa katika hekaheka mtaani na kuwasaka wahalifu. Lakini kwasasa Chifu amenipa heshima kubwa sana ya kuwa mkuu wa kitengo cha mawasiliano hapa makao makuu. Lakini, roho yangu haijakongeka hata kidogo. Nimemiss sana mikimiki ya mitaani, na kufumbua mafumbo magumu yanayoumiza kichwa. Naupenda sana upelelezi..Hakuna ka.." Mwanasheria mlevi akakatishwa katika mawazo yake. Simu yake ya mkononi iliyokuwa juu ya faili moja, ilikuwa inaita.

"Nani huyu anayenipigia simu? Namba hii wanaojua ni watu wachache sana, lakini sio namba ngeni?" Mwanasheria mlevi alijiuliza.

Akaipokea.

"Daniel Mwaseba hapa naongea" Sauti ilisema simuni.

"Daniel, kulikoni? Mbona umenipigia kwa namba ngeni?" Mwanasheria mlevi aliuliza.

"Tutaongea kwa kirefu baadae Mwanasheria. Lakini kwa sasa kuna kazi moja naomba uisaidie" Daniel aliongea harakaharaka.

"Kazi gani hiyo Daniel?" Mwanasheria aliuliza.

"Najua kwasasa upo katika kitengo cha mawasiliano hapo makao makuu. Sasa kuna namba moja ya simu nataka uichunguze. Nataka unambie namba hiyo inamilikiwa na nani? Na watu gani inayowasiliana nao mara kwa mara?" Daniel alisema.

"Nitumie hiyo namba Daniel. Hesabu hilo limekwisha. Nitakupa majibu soon. Eeh nambie kingine unachohitaji kutoka kwangu?" Mwansheria aliuliza.

"Kwasasa nahitaji hilo tu la namba. Ni muhimu sana, nikitaka kitu kingine nitawasiliana na wewe" Daniel alisema.

"Halafu unadrive Daniel? Unaenda kwa kimada nini?" Mwanasheria mlevi alibadili namba.

"Hapana, ila nipo kwenye gari. Kuna wachawi ninawafukuzia hapa"

Mwanasheria mlevi akapiga ngumi ya nguvu katika meza.


"Nimemiss sana maisha hayo!" Akasema kwa hisia.

Daniel Mwaseba alikuwa ameshakata simu.

Muda huohuo, Mwanasheria mlevi akatoka mle ofisini. Akaenda kwenye chumba cha pili ambapo kulikuwa na kompyuta mbili katika meza tofauti. Akaenda kukaa katika kiti, mbele ya kompyuta mojawapo. Sekunde hiyohiyo, mlio wa meseji ulisikika katika simu yake. Ilikuwa ni namba ya simu aliyotumiwa na Daniel Mwaseba. Akaingiza ile namba katika kompyuta ambayo ilikuwa na program ya kutambua namba za watu.

Majibu aliyokutana nayo huko...yalimwacha mdomo wazi....

***

Viongozi mbalimbali walikuwa wamejaa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Ilikuwa ni siku maalum ambayo rais Mgaya alikuwa amemaliza ziara ya wiki moja nchini Nigeria, hivyo anarejea nyumbani. Ziara ya wiki moja nchini Nigeria iliisha kwa mafanikio makubwa sana, baada ya rais Mgaya na rais Abayo wa Nigeria kusaini mikataba mikubwa mbalimbali ya ushirikiano, lakini mkataba mkuwa ulikuwa ni ushirikiano katika suala la mafuta.

Itifaki ilizingatiwa katika uwanja wa ndege. Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kama mkuu wa mkoa mwenyeji alikuwa amesimama na viongozi mbalimbali. Makamu wa rais, waziri mkuu, spika wa bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na jaji mkuu walikuwa wakipiga makofi wakati rais Mgaya akishuka ndani ya ndege ya shirika la ndege la Tanzania.

Vikundi mbalimbali vya ngoma vilikuwa vinaburudisha pale uwanjani. Huku wanasarakasi nao wakibiringita ardhini kuonesha umahiri wao.

Rais Mgaya, aliyekuwa amevaa suti nzuri ya kijivu. Alikuwa anashuka katika ngazi ndefu za ndege akifuatiwa na walinzi wake kwa nyuma. Alionekana ni mtu mwenye furaha machoni kwa kumwangalia, hakuna aliyekuwa anajua lililokuwa linapita kichwani mwake. Alikuwa hana furaha hata chembe.

Pale uwanja wa ndege ilifanyika hafla fupi ya pongezi. Viongozi mbalimbali walihutubia, na mwishoni kabisa hotuba ikimaliziwa na mheshimiwa rais Mgaya.

Baada ya hotuba hiyo, msafara ulianza kuelekea ikulu. Ndani ya gari rais Mgaya alitulia kimya. Alionekana ndani ya gari kimwili, lakini mawazo yake yalikuwa yanawaza kitu kimoja tu, Dr Luis.

"Mzee Msangi ameniangusha sana katika kazi hii. Nimemtumia katika kazi zangu za siri nyingi na ngumu sana. Lakini nashangaa ameshindwa kufanya kazi hii ndogo sana. Kazi ilikuwa ni kumteka Dr Luis na kumuua!!.
Zoezi la kwanza lilifanikiwa kwa ufanisi mkubwa sana, sasa iweje washindwe kumuua mtu aliyekuwa mikononi mwao?.
Ni kosa kubwa sana amefanya, haitakiwi hata kidogo Dr Luis awe hai. Siku akifumbua mdomo wake na kusema siri zangu. Basi ndoto ya kugombea awamu ya pili ya urais itakuwa imefutika. Na hilo sitaki litokee kwa namna yoyote ile. Nitatumia nguvu zangu zote kama rais kuhakikisha Dr Luis anakufa!

Nilitegemea kupokea simu ya mzee Msangi kuwa zoezi limekamilika, eti ananambia Dr Luis ametoroshwa na Imma Ogbo.

Who is Immanuel Ogbo. Ni rais Abayo wa Nigeria ndiye aliyenitambulisha kwa mtu anayeitwa Imma Ogbo. Nikifika Ikulu nitampia simu nimweleze kitendo alichokifanya mtu wake. Hakutumwa kuja kufanya kazi ya kuteka watu hapa..." Rais Mgaya alikatishwa mawazo yake na simu.

Alikuwa ni mkuu wa Polisi IGP John Rondo.

"Shikamoo mheshimiwa rais" IGP Rondo aliamkia.

"Marhaba IGP, vipi mnaendeleaje na kazi ya kumtafuta Dr Luis?" Rais Mgaya aliuliza.

"Na hilo ndilo lililonifanya nikupigie mheshimiwa rais. Nimeongea na Daniel Mwaseba sasahivi. Anasema zoezi linaenda kufika mwisho. Hivi sasa wanaenda mahali alipofichwa Dr Luis huko Kigamboni. Hivyo Dr Luis atakuwa mikononi mwetu sio muda mrefu kutokea sasa" IGP Rondo alisema.

"Kazi nzuri sana IGP wangu. Mimi nipo njiani naelekea ikulu. Nitakupigia nitakapofika ikulu" Rais Mgaya alisema na kukata simu.
Alikuwa ameyakatisha maongezi harakaharaka kwa makusudi.

Kisha akampigia simu mzee Msangi....

Je nini kitatokea? tuwe wote katika sehemu ijayo.
 
Shusha baba
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212392

Sehemu ya Kumi na nane

Songelael Ntenga P.A.K Mwanasheria mlevi alikuwa amekaa makao makuu ya usalama wa Taifa. Alikuwa amekaa ofisini, mbele yake kukiwa na meza kubwa yenye mafaili mbalimbali, yakiyopepewa na upepo wa feni.

"Sijazoea kabisa hizi kazi za kukaa ofisini. Mi furaha yangu ni kuwa katika hekaheka mtaani na kuwasaka wahalifu. Lakini kwasasa Chifu amenipa heshima kubwa sana ya kuwa mkuu wa kitengo cha mawasiliano hapa makao makuu. Lakini, roho yangu haijakongeka hata kidogo. Nimemiss sana mikimiki ya mitaani, na kufumbua mafumbo magumu yanayoumiza kichwa. Naupenda sana upelelezi..Hakuna ka.." Mwanasheria mlevi akakatishwa katika mawazo yake. Simu yake ya mkononi iliyokuwa juu ya faili moja, ilikuwa inaita.

"Nani huyu anayenipigia simu? Namba hii wanaojua ni watu wachache sana, lakini sio namba ngeni?" Mwanasheria mlevi alijiuliza.

Akaipokea.

"Daniel Mwaseba hapa naongea" Sauti ilisema simuni.

"Daniel, kulikoni? Mbona umenipigia kwa namba ngeni?" Mwanasheria mlevi aliuliza.

"Tutaongea kwa kirefu baadae Mwanasheria. Lakini kwa sasa kuna kazi moja naomba uisaidie" Daniel aliongea harakaharaka.

"Kazi gani hiyo Daniel?" Mwanasheria aliuliza.

"Najua kwasasa upo katika kitengo cha mawasiliano hapo makao makuu. Sasa kuna namba moja ya simu nataka uichunguze. Nataka unambie namba hiyo inamilikiwa na nani? Na watu gani inayowasiliana nao mara kwa mara?" Daniel alisema.

"Nitumie hiyo namba Daniel. Hesabu hilo limekwisha. Nitakupa majibu soon. Eeh nambie kingine unachohitaji kutoka kwangu?" Mwansheria aliuliza.

"Kwasasa nahitaji hilo tu la namba. Ni muhimu sana, nikitaka kitu kingine nitawasiliana na wewe" Daniel alisema.

"Halafu unadrive Daniel? Unaenda kwa kimada nini?" Mwanasheria mlevi alibadili namba.

"Hapana, ila nipo kwenye gari. Kuna wachawi ninawafukuzia hapa"

Mwanasheria mlevi akapiga ngumi ya nguvu katika meza.


"Nimemiss sana maisha hayo!" Akasema kwa hisia.

Daniel Mwaseba alikuwa ameshakata simu.

Muda huohuo, Mwanasheria mlevi akatoka mle ofisini. Akaenda kwenye chumba cha pili ambapo kulikuwa na kompyuta mbili katika meza tofauti. Akaenda kukaa katika kiti, mbele ya kompyuta mojawapo. Sekunde hiyohiyo, mlio wa meseji ulisikika katika simu yake. Ilikuwa ni namba ya simu aliyotumiwa na Daniel Mwaseba. Akaingiza ile namba katika kompyuta ambayo ilikuwa na program ya kutambua namba za watu.

Majibu aliyokutana nayo huko...yalimwacha mdomo wazi....

***

Viongozi mbalimbali walikuwa wamejaa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Ilikuwa ni siku maalum ambayo rais Mgaya alikuwa amemaliza ziara ya wiki moja nchini Nigeria, hivyo anarejea nyumbani. Ziara ya wiki moja nchini Nigeria iliisha kwa mafanikio makubwa sana, baada ya rais Mgaya na rais Abayo wa Nigeria kusaini mikataba mikubwa mbalimbali ya ushirikiano, lakini mkataba mkuwa ulikuwa ni ushirikiano katika suala la mafuta.

Itifaki ilizingatiwa katika uwanja wa ndege. Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kama mkuu wa mkoa mwenyeji alikuwa amesimama na viongozi mbalimbali. Makamu wa rais, waziri mkuu, spika wa bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na jaji mkuu walikuwa wakipiga makofi wakati rais Mgaya akishuka ndani ya ndege ya shirika la ndege la Tanzania.

Vikundi mbalimbali vya ngoma vilikuwa vinaburudisha pale uwanjani. Huku wanasarakasi nao wakibiringita ardhini kuonesha umahiri wao.

Rais Mgaya, aliyekuwa amevaa suti nzuri ya kijivu. Alikuwa anashuka katika ngazi ndefu za ndege akifuatiwa na walinzi wake kwa nyuma. Alionekana ni mtu mwenye furaha machoni kwa kumwangalia, hakuna aliyekuwa anajua lililokuwa linapita kichwani mwake. Alikuwa hana furaha hata chembe.

Pale uwanja wa ndege ilifanyika hafla fupi ya pongezi. Viongozi mbalimbali walihutubia, na mwishoni kabisa hotuba ikimaliziwa na mheshimiwa rais Mgaya.

Baada ya hotuba hiyo, msafara ulianza kuelekea ikulu. Ndani ya gari rais Mgaya alitulia kimya. Alionekana ndani ya gari kimwili, lakini mawazo yake yalikuwa yanawaza kitu kimoja tu, Dr Luis.

"Mzee Msangi ameniangusha sana katika kazi hii. Nimemtumia katika kazi zangu za siri nyingi na ngumu sana. Lakini nashangaa ameshindwa kufanya kazi hii ndogo sana. Kazi ilikuwa ni kumteka Dr Luis na kumuua!!.
Zoezi la kwanza lilifanikiwa kwa ufanisi mkubwa sana, sasa iweje washindwe kumuua mtu aliyekuwa mikononi mwao?.
Ni kosa kubwa sana amefanya, haitakiwi hata kidogo Dr Luis awe hai. Siku akifumbua mdomo wake na kusema siri zangu. Basi ndoto ya kugombea awamu ya pili ya urais itakuwa imefutika. Na hilo sitaki litokee kwa namna yoyote ile. Nitatumia nguvu zangu zote kama rais kuhakikisha Dr Luis anakufa!

Nilitegemea kupokea simu ya mzee Msangi kuwa zoezi limekamilika, eti ananambia Dr Luis ametoroshwa na Imma Ogbo.

Who is Immanuel Ogbo. Ni rais Abayo wa Nigeria ndiye aliyenitambulisha kwa mtu anayeitwa Imma Ogbo. Nikifika Ikulu nitampia simu nimweleze kitendo alichokifanya mtu wake. Hakutumwa kuja kufanya kazi ya kuteka watu hapa..." Rais Mgaya alikatishwa mawazo yake na simu.

Alikuwa ni mkuu wa Polisi IGP John Rondo.

"Shikamoo mheshimiwa rais" IGP Rondo aliamkia.

"Marhaba IGP, vipi mnaendeleaje na kazi ya kumtafuta Dr Luis?" Rais Mgaya aliuliza.

"Na hilo ndilo lililonifanya nikupigie mheshimiwa rais. Nimeongea na Daniel Mwaseba sasahivi. Anasema zoezi linaenda kufika mwisho. Hivi sasa wanaenda mahali alipofichwa Dr Luis huko Kigamboni. Hivyo Dr Luis atakuwa mikononi mwetu sio muda mrefu kutokea sasa" IGP Rondo alisema.

"Kazi nzuri sana IGP wangu. Mimi nipo njiani naelekea ikulu. Nitakupigia nitakapofika ikulu" Rais Mgaya alisema na kukata simu.
Alikuwa ameyakatisha maongezi harakaharaka kwa makusudi.

Kisha akampigia simu mzee Msangi....

Je nini kitatokea? tuwe wote katika sehemu ijayo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom