BOMU: Riwaya ya kipelelezi (1)

RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Tatu

Walikutana na mabaki machache ya moto. Huku mashuhuda wakisema kwamba mabaki yale lilikuwa ni gari ambalo liliwaka moto ghafla. Hawakuwa na haja ya kuuliza. Hisia zao tu ziliwaambia kuwa lile lilikuwa ni gari la meneja Fadhili. Ndio, gari la meneja Fadhili lilikuwa limeteketea kwa moto.

"Kwa mara nyingine tena wametuwahi hawa watu. Hadi sasa sijaelewa ni kwa namna gani wanazipata taarifa zetu. Pale walipogundua kuhusu Kelvin kufuta mawasiliano yake katika simu na pia kuamua kuchoma nyumba yake moto nilihisi kwamba meneja Fadhili anahusika katika kuvujisha siri zetu. Maana ni yeye ndiye tukiyewasiliana kuhusu Kelvin. Lakini sasa meneja fadhili mwenyewe nae ameuwawa kwa bo..." Daniel alipotaka kusema neno Bomu akasita. "Aaaaah nimegundua kitu Adrian..." Daniel alisema.

"Umegundua kitu gani Daniel?" Adrian aliuliza.

"Matukio haya matatu yote yamehusisha kitu cha mripuko. Ambacho katika hisia zangu kinaniambia kuwa ni mabomu. Kule Mkuranga nilishuhudia kwa macho yangu helkopta ikiachia bomu na kuiteketeza ile nyumba tuliyofungiwa. Leo sijaishuhudia nyumba ya Kelvin ikivyoteketea. Ni wewe ndiye uliyeenda. Lakini nahisi nyumba ya Kelvin nayo itakuwa imeripuliwa kwa bomu. Na sasa hili gari la meneja Fadhili. Hili gari limeripul..." Daniel hakumaliza alichotaka kusema. Alimsukuma kwa nguvu Adrian kwa mikono miwili!!.

Adrian aliyumba vibaya na kudondoka chini akifuatiwa na Daniel juu yake!
Sekunde ileile risasi moja ilipita na kuchimba chini, palikuwa ni mahali ambapo kilikuwa kimesimama kifua cha Adrian sekunde moja iliyopita!

E bwana wee!!.

"Mdunguaji" Daniel alimnong'oneza Adrian wakiwa wamelaliana pale chini. Adrian hakulipata neno. Alikuwa haamini kama amenusurika kifo kwa namna ile.

"Mdunguaji yupo juu kule katika hoteli ya Rombo" Daniel alisema tena. Sasa alikuwa na bastola yake mkononi.

Sekunde hii Adrian naye aliupata ufahamu wake. Naye alichomoa bastola yake kiunoni, tayari kwenda kumsaka Mdunguaji ghorofa ya juu katika hoteli ya Rombo.

Mkuumkuu, Daniel Mwaseba na Adrian Kaanan walielekea ilipo hoteli ya Rombo. Huku wakiwaacha watu waliokuwa wakishuhudia ile ajari ya kuungua kwa moto wakiwa hawaelewi ni kitu gani kimetokea. Kilikuwa ni kitendo kilichodumu si zaidi ya dakika moja.

Kule juu ya ghorofa ya hoteli ya Rombo, The sniper alikuwa katika mtatiziko wa nafsi. Alikuwa haamini kilichotokea. Hii, ilikuwa ni mara yake ya kwanza katika maisha yake kukosa shabaha kwa mtu aliyepanga kumdungua. Hakuelewa kwa namna gani wale jamaa waligundua kuwa wanataka kudunguliwa. Na kusukumana namna ile.

The sniper, kwa macho yake mawili, alishuhudia wale jamaa wakisukumana kiajabu na kulaliana vumbini. Huku wakimkosesha shabaha yake matata aliyoilenga kikamilifu.

Harakaharaka, alibadili mwonekano wake.

Dakika moja baadae hakuwa The sniper tena. Alikuwa katika vazi la baibui, huku bunduki yake ya gharama akiitelekeza katika ndoo ya taka kulekule ghorofani. Alijua hawezi kutoka salama ndani ya Rombo hoteli akiwa na silaha.

The sniper alianza kushuka mkuumkuu. Alipokaribia katika ghorofa ya pili alipunguza mwendo. Alipishana na kina Daniel wakiokimbia kwa kasi wakielekea juu katika korido ya ghorofa ya pili. Daniel alibahatika kuusikia uturi wa mwanamke waliyepishana nae akiwa mbiombio. Na huyo ndiye Daniel Mwaseba. Milango yake ya fahamu inafanya kazi kikamilifu wakati wote.

Hakuna aliyehisi kuwa yule mwanamke ndiye waliyekuwa wanamkimbilia kule juu. Haikuwaingia akilini mdunguaji afike pale kwa sekunde zile chache.

Hawakujua. Hawakujua.

Yule hakuwa mwanamke, alikuwa ni The Sniper, Mdunguaji hatari sana!!

Mbio za kina Daniel Mwaseba ziliwafikisha juu kabisa ya hoteli ya Rombo. Baada ya dakika tano za kutafutatafuta, walichobahatika kukutana nacho ni bunduki iliyotelekezwa katika ndoo ya taka. Kwa kutumia kitambaa Daniel aliishika ile bunduki. Kitu kimoja tu kilipita katika pua yake.

Harufu ya uturi..

Ndio, harufu ya uturi waliyopishana nao kutoka kwa mwanamke aliyevaa baibui katika ghorofa la pili, ndio harufu ileile ya uturi aliyosikia katika ile bunduki ya Mdunguaji.

"Tumepishana na Mdunguaji.." Daniel alisema kwa sauti ndogo.

"Tumepishana nae wapi? Wakati hii hoteli haina lift. Na ina njia moja tu. Pia wakati tunakuja huku juu tumepishana na mtu mmoja tu, tena mwanamke kule ghorofa la pili, ambaye kwa vyovyote vile hawezi kuwa ametokea huku. Hakuna mwanadamu mwenye kasi hiyo, ya kutoka huku hadi kufika ghorofa ya pili kwa muda mfupi vile" Adrian alisema.

"Yule mwanamke mwenye buibui ndiye Mdunguaji..." Daniel alisema.

"Kivipi Daniel? Mbona sikuelewi..."

"Nusa hii bunduki yake" Daniel alisema.

Adrian aliinusa ile bunduki. Alistuka sana.

"Namjua mdunguaji..." Adrian alisema.

"Unasemaje Adrian? Unamjua mdunguaji?" Daniel aliuliza kwa wahka mkubwa.

Ghafla, simu yake iliita.

"Namba ngeni..." Adrian alisema huku akiipokea.

"Haloo naweza kuongea na Daniel?" Sauti ya kike ilisema simuni harakaharaka.

"Simu yako..." Adrian akisema huku akimpa simu Daniel.

"Daniel, kuna jambo la kushangaza limetokea.." Mwanamke alisema simuni. Sauti ambayo Daniel alipoisikia tu aliitambua.

Ilikuwa sauti ya Hannan Halfani.

"Jambo gani Hannan?" Daniel aliuliza.

"Nimeipata katika mtandao simu ya meneja Fadhili" Hannan alisema.

"Hannan unasemaje simu ya meneja umeipata? Wapi Hannan?" Daniel aliuliza akiwa haamini.

"Simu ya meneja Fadhili imewashwa maeneo ya Tegeta mwisho. Nyumba namba kumi na saba. Imewashwa ndani ya dakika mbili halafu ikazimwa" Hannan alisema.

"Inawezekana vipi hiyo Hannan? Meneja Fadhili na gari yake wameteketea kwa moto hapa Sinza Legal. Na wakati tukiwa eneo la tukio nasi tukashambuliwa. Hapa tulipo tunamsaka mtu aliyetushambulia" Daniel alisema.

"Inawezekana walimtoa Meneja Fadhili kabla, kisha wakachoma gari moto kupoteza ushahidi. Nendeni Tegeta haraka nakwambia meneja Fadhili yupo huko.." Hannan alisema kwa msisitizo.

"Tupo njiani Hannan" Daniel alisema.

"Do did" Hannan alisema na kukata simu.

Do did lilikuwa ni fumbo lao la siri kati ya Daniel na Hannan. Ni wao tu wawili ndio waliokuwa wanaelewana hapa Duniani baada ya kusema Do did.

Baada ya kuambiwa 'Do did'. Daniel alipatwa na hasira za ajabu sana. Ghafla!! Alimwangalia Adrian kwa jicho la hasira. Adrian hakuelewa ni kitu gani kimetokea.

"Vipi Daniel. Mbona umebadilika ghafla baada tu ya kutoka kuongea na Hannan? Mmeongea nini?" Adrian aliuliza kwa sauti ya hofu.

"Tuna..zun..guka..na.." Daniel alisema kwa sauti ya kukwaruza. Macho yake yakiwa mekundu hayajawahi kutokea hapa duniani.

"Wamenichokoza hawa mabwege. Wamechezea sharubu za simba. Hawanijui. Hawanijui. Hawanijui hata kidogo.. Nitawafanya kitu kibaya sana nakwambia hawa watu. Hawatanisahau. Hawatanisahau kamwe. Vizazi vyao vyote hawatamsahau mtu mwenye jina la Daniel Mwaseba. Maana watasimulia vizazi na vizazi. Nitawaonesha mimi ni nani? Nitawakomesha.." Daniel alisema kwa hasira.

"Mbona sikuelewi Daniel? Ni kitu gani kimetokea kwani? Hannan amekwambia nini?" Adrian aliuliza.

Daniel hakujibu kitu. Badala yake alibonyazabonyaza ile simu ya Adrian, kisha akaiweka sikioni.

Simu ilianza kuita.

Daniel Mwaseba alikuwa anampigia Martin Hisia.

Je nini kitatokea..Inaitwa Bomu na mwandishi wako ni Halfani Sudy..

Tuwe wote keshokutwa.
 
RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Nne

Wakati simu yake inaita, Martin Hisia alikuwa Mlimani city. Alikuwa anasukuma kitorori kilichojaa bidhaa mbalimbali za nyumbani katika duka la Discount centre.

Pembeni yake kulikuwa na msichana mzuri. Mwenyewe, alizoea kumuita Malaika. Msichana huyo mrembo jina lake halisi alikuwa anaitwa Felisia Nyenyembe.

"Simu yako inaita.." Felisia alisema kumwambia Martin.

"Nimeisikia. Ila nikiwa na Malaika wangu sipendi kupokea simu. Nikiwa na wewe napenda niutenge muda wangu kwa ajili yako tu. Sipendi kuchanganya na mambo mengine" Martin alisema bila kujihangaisha kuitoa simu yake mfukoni.

Simu iliita, hadi ikakata.

Baada ya sekunde moja tu, simu yake iliita tena.

"Pokea simu mpenzi wangu. Inawezekana ni simu muhimu" Felisia alisema kwa kubembeleza.

"Hiki sio kimeo kweli.." Martin aliwaza wakati akiitoa simu yake mfukoni.

"Hallo" Martin alisema huku akiomba atakayoisikia isiwe sauti ya kike.

Dua yake ilikubaliwa.

"Daniel, Daniel Mwaseba hapa naongea" Ilikuwa sauti ya kiume.

"Ahhaaa nambie Comrade. Mbona umetumia namba mpya?" Martin alisema.

"Martin nitakueleza kuhusu kutumia simu ngeni. Lakini kwasasa kuna jambo la muhimu sana limenifanya nikupigie" Daniel alisema.

"Jambo gani hilo Daniel?" Martin aliuliza kwa hofu.

"Mama mgonjwa sana Martin. Inabidi twende kijijini Somanga haraka iwezekanavyo" Daniel alisema.

"Mama anaumwa? Upo wapi kwasasa Daniel?" Martin aliuliza.

"Kwasasa nipo Sinza Legal. Ila niambie wewe upo wapi nikufuate" Daniel alisema.

"Nipo Mlimani city hapa" Martin alisema.

"Ndani ya dakika kumi nitakuwa hapo" Daniel alisema na simu ikakatwa.

"Malaika, kanipigia simu kaka Daniel. Amenipa taarifa kwamba mama mgonjwa sana huko kijijini Somanga, inabidi tukamwone" Martin alisema akimpigapiga begani Felisia.

"Tutaenda wote baby, nami nataka nikamwone mama" Felisia alisema.

"Nitaenda nawe siku nyingine Malaika. Hiyo itakuwa safari maalum kwa ajiri yako" Martin alisema.

"Sawa mpenzi wangu" Felisia alikubali kwa shingo upande.

"Ndio maana nakupenda sana Malaika wangu. Tangu nikutane na wewe maisha yangu yamekuwa tofauti sana" Martin alisema. Felisia alicheka kwa aibu.

"Sasa mpenzi, wewe nenda nyumbani na hivi vitu. Mimi nitaenda na kaka Daniel kijijini Somanga leo. Nitakufahamisha hali ya mama nikifika" Martin alisema.

"Sawa mpenzi wangu. Nitakumiss sana" Felisia alisema akilengwalengwa na machozi.

"Nitakumiss pia Malaika wangu" Martin alisema huku akimkumbatia Felisia.

Walipoacha kukumbatiana na kupigana mabusu ya kutosha. Felisia alishika usukani wa kukisukuma kitorori kuelekea nje ya jengo la Mlimani city.

Alipofika katika mlango wa kutokea. Alisogea pembeni. Akatoa simu yake na kuibonyazabonyaza.
Akaiweka sikioni.

"Ulikuwa sahihi Imma Ogbo" Akasema simuni.

"Vipi, mtego wetu wa miezi kadhaa umenasa?" Imma Ogbo aliuliza.

"Hakika, we ni kichwa. Uliyapanga haya mambo ukiwa jijini Lagos nchini Nigeria. Na sasa yanaenda kutokea kama ulivyoyatarajia hapa jijini Dar es salaam nchini Tanzania. Daniel kampigia Martin sasa hivi. Wameongea kwa mafumbo kuwa mama yao mgonjwa hivyo wanataka kumwona. Mwenyewe alidhani ananificha, kwasababu hajui mimi ni nani? Nilielewa kila kitu" Felisia alisema kwa majigambo.

"Mpango wao upoje sasa?" Imma Ogbo aliuliza.

"Wamekubaliana Daniel aje hapa Mlimani city. Mipango yao itaanzia hapa" Felisia alisema.

"Wasitoke salama hapo!!" Imma Ogbo alisema.

"Imma sio tufanye ule mpango wetu wa awali?" Felisia aliuliza.

"Ule mpango ulikuwa mzuri. Na tulitega kila kitu katika nyumba yetu kule Tegeta. Wauaji wapo tayari wakisubiri ujio wa Daniel. Lakini nahisi kama Daniel hajatilia maanani sana" Imma Ogbo alisema.

"Au amefahamu kama mmemteka yule msichana wake kule hospitali?" Felisia aliuliza.

"Hawezi kujua. Tulimpigia Daniel na kumwelekeza aje Tegeta nyumba namba kumi na sita kwa kutumia yule msichana tuliyemteka. Na kila kitu kilienda sawa. Sisi tulitegemea Daniel atakuwa njiani kuelekea Tegeta. Lakini badala yake yeye amempigia simu Martin.." Imma Ogbo alisema.

"Imma, huoni pengine anataka kwenda na Martin huko Tegeta?" Felisia aliuliza.

"Aaah inawezekana Felisia. Umewaza jambo la maana sana. Natuma watu hapo kwa ajili ya kuwafatilia wakina Daniel. Kama uekekeo wao hautakuwa wa Tegeta, itabidi tuwalipue tu kwa Bomu" Felisia alisema.

"Nimekuelewa Imma" Felisia alisema na kukata simu.

Daniel Mwaseba, Adrian Kaanan na David walikuwa njiani wanaelekea Mlimani city.
Kule Sinza Legal kulikuwa shwari sasa. Jeshi la zimamoto wakishirikiana na jeshi la polisi walikuwa wamefanikiwa kuondoa mabaki ya gari la meneja Fadhili lililoteketa kwa moto. Na shughuli katika njia ya Shekilango ziliendelea kama kawaida.

Baada ya Daniel kuongea na Martin Hisia, kidogo hasira zake za ajabu zilikuwa zimepungua. Alihisi ameutua mzigo mzito kwakuwa alijua Martin Hisia kwa kushirikiana na wao wataumaliza mchezo. Lakini, kila dakika, hisia kwamba kuna msaliti miongoni mwao zilikuwa zinautekenya ubongo wake.

Swali gumu lilikuwa, je msaliti kati yao ni nani?.

"Adrian, naomba unisamehe kwa yaliyotokea muda mfupi uliopita. Nilipatwa na hisia za ajabu sana ambazo nilishindwa kuzimiliki" Daniel alisema wakati wakiwa ndani ya gari.

"Wewe ni kaka yangu Daniel. Mwalimu wangu katika uga huu, hauna haja ya kuniomba msamaha.." Adrian alisema.

"Kuomba msamaha hakuangalii cheo, wala umri. Unapohisi umekosea ni huna budi kuomba msamaha" Daniel alisema.

"Basi nimekusamehe Daniel" Adrian alikubali, wakati David akiwa haelewi watu wale wamekoseana nini?.

"Adrian, ulisema unamfahamu mdunguaji?" Daniel aliuliza ghafla.

"Nahisi hivyo Daniel" Adrian alisema.

"Mdunguaji ni nani?" Daniel aliuliza.

"Wakati tupo katika mafunzo ya kijasusi kule Cuba, kuna mwanafunzi mwenzetu mmoja ambaye habari zake hazijulikani hadi sasa. Hayupo katika jeshi lolote lile duniani. Hata ukisachi katika mtandao ni ngumu kuzipata habari zake. Mwanafunzi huyo alikuwa anapenda kutumia uturi unaonukia harufu uliyoninusisha katika bunduki ile. Uturi kutoka Uturuki.." Adrian alisema kwa kirefu.

"Anaitwa nani huyo Mdunguaji?" daniel aliuliza kwa shauku.

"Alikuwa anaitwa Mark. Mwenyewe alikuwa anapenda kujiita The Sniper. Mark alikuwa namba moja katika mafunzo ya udunguaji kule Cuba. Hakuna mtu akiyemkaribia hata robo katika kulenga shabaha.." Adrian alisema.

"Inawezekana Mark akawa ndiye aliyetushambulia pale. Na ndomana alianza kukulenga wewe ambaye anakufahamu" Daniel alisema.

"Ni kweli Daniel. Hivi ulijuaje kama kanilenga yule jamaa?" Ilikuwa zamu ya Adrian sasa kuuliza.

"Mdunguaji alifanya kosa, kosa le.." Daniel hakumalizia kuongea. Adrian aliropoka.

"Tunafatiliwa Daniel.." Adrian alisema huku akiangalia nyuma. Yeye alikuwa amekaa katika siti za nyuma.

Kipindi hiko walikuwa kataka foleni ya mataa ya Ubungo.

Ghafla! David aliyekuwa dereva akatoa bastola yake kiunoni na kumuelekezea Daniel ambaye alikuwa pembeni yake.

"Tulia hivyohivyo! Ukijitikisa tu naipeleka roho yako kuzimu!" David alionya kwa nguvu.

Ilizuka patashika katikati ya foleni pale Ubungo.

IJe nini kitatokea? Inaitwa Bomu na mwandishi wako ni Halfani Sudy.. Tuwe wote hapahapa keshokutwa.
 
Write your reply...Loh sitaki kuamini kwamba nimekwama kwenye foleni ya kuisubiria hii riwaya. umenikumbusha "Nitakupata tu" Mungu ampunguzie adhabu ya kaburi Ibrahim Masimba
 
RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Tano

"Unataka kufanya nini David?" Daniel aliuliza swali huku akitabasamu.

"Fuata maelekezo yangu Daniel!! Mimi sitanii nitakupasua kweli na risasi!!" David alionya.

"Tatizo nini David?" Adrian naye aliuliza kule nyuma.

"Nawe tulia! Usijione upo salama, angalia nyuma yako huko!" David alisema kwa hasira.

Adrian aligeuka nyuma. Ile sehemu ya ndani wanapowekea mizigo. Pua yake iligusana na mdomo mweusi wa bastola.

"Tumetekwa" Adrian alisema akiwa amekata tamaa.

"David, wamekulipa shilingi ngapi hawa watu kiasi ukaamua kuisaliti nchi yako namna hii?" Daniel aliuliza huku tabasamu lake likiwa vilevile.

"Adrian! Ruka katika usukani hapa. Utafuata maelekezo yangu. We Daniel ruka nyuma kule. Ukakutane na muhuni.." David alisema kwa amri.

Daniel Mwaseba na Adrian Kaanan walifanya kama walivyoagizwa.

"Adrian tunaenda Tegeta. Ukileta ujanja wowote ule sitaki kurudia tena kukwambia nitakufanya nini!" David alionya tena.

"Sifiki Tegeta mimi" Daniel alimjibu kimoyomoyo.

Taa ziliruhusu. Gari la kina Daniel ambalo kwasasa lilikuwa linaendeshwa na Adrian lilikata kulia likiifuta barabara ya Sam Nujoma.
Ndani ya gari kulikuwa na utulivu mkubwa. Kila mmoja akiwaza lake moyoni.

Walipita Mlimani city, Daniel alichungulia kwa nje dirishani lakini hakumuona Martin Hisia.

"Tutaonana soon brother" Daniel alisema kwa sauti ndogo.

Gari lilishika kasi. Adrian alikuwa analiendesha bila wasiwasi wowote ule. Hakutishwa na mdomo wa bastola uliokuwa unamgusagusa shingoni. Zilikuwa ni kazi zao kugusana na bastola.

Walifika Mwenge, gari lilikata kushoto kuelekea Tegeta. Adrian na Daniel mara kwa mara walikuwa wanaangaliana kwa kutumia kioo cha kati. Walikuwa wanawasiliana kwa alama zao.
Na walielewana.

Gari liliendelea kusonga mbele.
Kuelekea Tegeta.

Adrian pia aliangalia nyuma yao kwa kutumia vioo vya pembeni. Lile gari aliloliona tangu wakiwa kule Ubungo ambalo alihisi kuwa linawafatilia bado lilikuwa nyuma yao.

"Hawa watu ni kina nani? Kwanini wamemteka Dr Luis? Siamini, na David naye ni miongoni mwao? Kajuana nao lini hawa watu wakati muda mwingi alikuwa msituni? Nina maswali mengi sana ambayo yanipasa niyapate majibu. Na nitayapata kutoka kwa David mwenyewe" Daniel aliwaza.

Daniel alikiangalia tena kioo cha kati, na Adrian naye alikiangalia.
Waliangaliana.
Macho yao yaliongea tena.
Walielewana.

Safari iliendelea huku ukimya wa kifo ukiwa umetawala ndani ya garu. Mateka walikuwa kimya, watekaji nao walikuwa kimya.

"Hannan alinipa taarifa kwamba simu ya meneja Fadhili ilionekana imewashwa na kisha kuzimwa Tegeta. Niliamini taarifa ile, na nilitaka kwenda kweli Tegeta. Lakini mwishoni kabisa aliniambia 'Do did'. Najua aliyekuwa nao huko hawakumuekewa. Hilo neno tunalitumia mimi na yeye tu endapo mmoja wetu atakapokamatwa na kulazimishwa kumleta mwenzie mtegoni. 'Do did' leo imetusaidia.
Ila hawa jamaa wana roho mbaya. Unamtoaje mgonjwa katika hali hospitali na kumteka. Lakini lazima watalipa kwa haya mambo wayafanyayo" Daniel aliwaza.

Akanyanyua tena sura yake katika kioo cha kati. Adrian naye alifanya vivo hivo. Akamkonyeza kwa jicho lake la kushoto.

"Its the time" Daniel alisema kwa sauti ndogo aliyoisikia mwenyewe.

Sekunde hiyohiyo, Adrian aliliyumbisha gari kwa nguvu na kwenda kulikwaruza gari la pembeni. Gari lao liliyumba vibaya huku likielekea kugongana uso kwa uso na roli, likilotokea Tegeta. Adrian alikata kona kwa haraka na ustadi mkubwa na kurudi upande wake. Walihitaji mstuko mdogo tu kutoka kwa wale watu.
Na waliopata.
Daniel Mwaseba alikuwa ameshafanya kitu....

Wakati yule jamaa aliyumbishwa na ule myumbo wa kwanza wa gari, Daniel aliitumia nafasi ile kupiga kwa nguvu kiganja cha yule jamaa, na bastola ilidondoka chini. Jamaa alitoa yowe dogo la hofu lisilo na mwendelezo, kwani alikutana na mkono wa kiume wa Daniel ulioizungusha shingo yangu kwa nguvu kuelekea kushoto. Ulisikika mlio kama kijiti kikavu kimevunja. Jamaa alienda katika sayari nyingine palepale. Wakati gari lilkikaa sawa barabarani, Daniel Mwaseba alikuwa ameimaliza kazi.

David alikuwa anatetemeka huku akiwa bado kamuelekea bastola yake Adrian. Hakuna aliyemsemesha.

"Hawa wajinga wanaotufuata watatutambua leo!!" Daniel alisema kwa jazba.

Adrian alifanya alitulia katika usukani. Safari ya kuelekea Tegeta iliendelea..

David akiwa vilevile, na mtetemo wake wa haja huku bastola yake ikiwa imeelekezwa kichwani kwa Adrian Kaanan.

***

Imma Ogbo aliingia katika chumba ambacho alikuwa amewekwa Dr Luis. Safari hii ndio alipanga kwenda kumwambia Dr Luis lengo lao kuu la kumteka. Alimkuta Dr Luis amekaa katika kiti akiwa mwingi wa mawazo.

"Tumekutana tena rafiki yangu.." Imma Ogbo alisema huku akitabasamu.

Dr Luis alimwangalia tu.

"Dr Luis, ni wewe pekee ndiye unayeweza kupigania maisha yako. Huko nje hakuna harakati zozote za kukutafuta. Rafiki yako mheshimiwa rais hana habari na wewe. Hapa ni wewe na wewe tu ndio wenye nafasi ya kujiokoa" Imma Ogbo alisema.

"Kwani mnataka nini kwangu ninyi watu? Kama mnataka kiasi chochote cha pesa mimi nitawapa. Naomba niachieni nirudi kwetu. Mmeniteka bila sababu, maswali yenu yote nimeyajibu sasa mnataka nini tena kutoka kwangu?" Dr Luis alisema.

"Sikiliza Dr Luis. Huu si wakati wa kulalamika. Hapa si mahali sahihi pa kulalamika. Hakuna atakayekuonea huruma kwa malalamiko yako. Sikiliza tutachokwambia, nawe utekekeze. Huo ndio usalama wako"

Dr Luis alibaki kimya.

"Tunataka ututengenezee kirusi cha DH+...." Imma Ogbo alisema kwa sauti ndogo.

"Unasemaje!!!?" Mshangao mkubwa ulionekana katika macho ya Dr Luis.

Hakuamini maneno yale kutoka kwa yule mtu. Kabla ya dakika hii aliamini ni yeye pekee ndiye anayejua kuhusu kirusi cha siri cha DH+ hapa duniani.

Kumbe katu haikuwa hivyo.

Moyoni akahisi, hata siri yake na rais Mgaya sasa itakuwa hadharani kwa hawa watu.

Hili lilikuwa ni Bomu kwake!!!

Je nini kitatokea? Tukutane hapahapa keshokutwa.
 
RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Tano

"Unataka kufanya nini David?" Daniel aliuliza swali huku akitabasamu.

"Fuata maelekezo yangu Daniel!! Mimi sitanii nitakupasua kweli na risasi!!" David alionya.

"Tatizo nini David?" Adrian naye aliuliza kule nyuma.

"Nawe tulia! Usijione upo salama, angalia nyuma yako huko!" David alisema kwa hasira.

Adrian aligeuka nyuma. Ile sehemu ya ndani wanapowekea mizigo. Pua yake iligusana na mdomo mweusi wa bastola.

"Tumetekwa" Adrian alisema akiwa amekata tamaa.

"David, wamekulipa shilingi ngapi hawa watu kiasi ukaamua kuisaliti nchi yako namna hii?" Daniel aliuliza huku tabasamu lake likiwa vilevile.

"Adrian! Ruka katika usukani hapa. Utafuata maelekezo yangu. We Daniel ruka nyuma kule. Ukakutane na muhuni.." David alisema kwa amri.

Daniel Mwaseba na Adrian Kaanan walifanya kama walivyoagizwa.

"Adrian tunaenda Tegeta. Ukileta ujanja wowote ule sitaki kurudia tena kukwambia nitakufanya nini!" David alionya tena.

"Sifiki Tegeta mimi" Daniel alimjibu kimoyomoyo.

Taa ziliruhusu. Gari la kina Daniel ambalo kwasasa lilikuwa linaendeshwa na Adrian lilikata kulia likiifuta barabara ya Sam Nujoma.
Ndani ya gari kulikuwa na utulivu mkubwa. Kila mmoja akiwaza lake moyoni.

Walipita Mlimani city, Daniel alichungulia kwa nje dirishani lakini hakumuona Martin Hisia.

"Tutaonana soon brother" Daniel alisema kwa sauti ndogo.

Gari lilishika kasi. Adrian alikuwa analiendesha bila wasiwasi wowote ule. Hakutishwa na mdomo wa bastola uliokuwa unamgusagusa shingoni. Zilikuwa ni kazi zao kugusana na bastola.

Walifika Mwenge, gari lilikata kushoto kuelekea Tegeta. Adrian na Daniel mara kwa mara walikuwa wanaangaliana kwa kutumia kioo cha kati. Walikuwa wanawasiliana kwa alama zao.
Na walielewana.

Gari liliendelea kusonga mbele.
Kuelekea Tegeta.

Adrian pia aliangalia nyuma yao kwa kutumia vioo vya pembeni. Lile gari aliloliona tangu wakiwa kule Ubungo ambalo alihisi kuwa linawafatilia bado lilikuwa nyuma yao.

"Hawa watu ni kina nani? Kwanini wamemteka Dr Luis? Siamini, na David naye ni miongoni mwao? Kajuana nao lini hawa watu wakati muda mwingi alikuwa msituni? Nina maswali mengi sana ambayo yanipasa niyapate majibu. Na nitayapata kutoka kwa David mwenyewe" Daniel aliwaza.

Daniel alikiangalia tena kioo cha kati, na Adrian naye alikiangalia.
Waliangaliana.
Macho yao yaliongea tena.
Walielewana.

Safari iliendelea huku ukimya wa kifo ukiwa umetawala ndani ya garu. Mateka walikuwa kimya, watekaji nao walikuwa kimya.

"Hannan alinipa taarifa kwamba simu ya meneja Fadhili ilionekana imewashwa na kisha kuzimwa Tegeta. Niliamini taarifa ile, na nilitaka kwenda kweli Tegeta. Lakini mwishoni kabisa aliniambia 'Do did'. Najua aliyekuwa nao huko hawakumuekewa. Hilo neno tunalitumia mimi na yeye tu endapo mmoja wetu atakapokamatwa na kulazimishwa kumleta mwenzie mtegoni. 'Do did' leo imetusaidia.
Ila hawa jamaa wana roho mbaya. Unamtoaje mgonjwa katika hali hospitali na kumteka. Lakini lazima watalipa kwa haya mambo wayafanyayo" Daniel aliwaza.

Akanyanyua tena sura yake katika kioo cha kati. Adrian naye alifanya vivo hivo. Akamkonyeza kwa jicho lake la kushoto.

"Its the time" Daniel alisema kwa sauti ndogo aliyoisikia mwenyewe.

Sekunde hiyohiyo, Adrian aliliyumbisha gari kwa nguvu na kwenda kulikwaruza gari la pembeni. Gari lao liliyumba vibaya huku likielekea kugongana uso kwa uso na roli, likilotokea Tegeta. Adrian alikata kona kwa haraka na ustadi mkubwa na kurudi upande wake. Walihitaji mstuko mdogo tu kutoka kwa wale watu.
Na waliopata.
Daniel Mwaseba alikuwa ameshafanya kitu....

Wakati yule jamaa aliyumbishwa na ule myumbo wa kwanza wa gari, Daniel aliitumia nafasi ile kupiga kwa nguvu kiganja cha yule jamaa, na bastola ilidondoka chini. Jamaa alitoa yowe dogo la hofu lisilo na mwendelezo, kwani alikutana na mkono wa kiume wa Daniel ulioizungusha shingo yangu kwa nguvu kuelekea kushoto. Ulisikika mlio kama kijiti kikavu kimevunja. Jamaa alienda katika sayari nyingine palepale. Wakati gari lilkikaa sawa barabarani, Daniel Mwaseba alikuwa ameimaliza kazi.

David alikuwa anatetemeka huku akiwa bado kamuelekea bastola yake Adrian. Hakuna aliyemsemesha.

"Hawa wajinga wanaotufuata watatutambua leo!!" Daniel alisema kwa jazba.

Adrian alifanya alitulia katika usukani. Safari ya kuelekea Tegeta iliendelea..

David akiwa vilevile, na mtetemo wake wa haja huku bastola yake ikiwa imeelekezwa kichwani kwa Adrian Kaanan.

***

Imma Ogbo aliingia katika chumba ambacho alikuwa amewekwa Dr Luis. Safari hii ndio alipanga kwenda kumwambia Dr Luis lengo lao kuu la kumteka. Alimkuta Dr Luis amekaa katika kiti akiwa mwingi wa mawazo.

"Tumekutana tena rafiki yangu.." Imma Ogbo alisema huku akitabasamu.

Dr Luis alimwangalia tu.

"Dr Luis, ni wewe pekee ndiye unayeweza kupigania maisha yako. Huko nje hakuna harakati zozote za kukutafuta. Rafiki yako mheshimiwa rais hana habari na wewe. Hapa ni wewe na wewe tu ndio wenye nafasi ya kujiokoa" Imma Ogbo alisema.

"Kwani mnataka nini kwangu ninyi watu? Kama mnataka kiasi chochote cha pesa mimi nitawapa. Naomba niachieni nirudi kwetu. Mmeniteka bila sababu, maswali yenu yote nimeyajibu sasa mnataka nini tena kutoka kwangu?" Dr Luis alisema.

"Sikiliza Dr Luis. Huu si wakati wa kulalamika. Hapa si mahali sahihi pa kulalamika. Hakuna atakayekuonea huruma kwa malalamiko yako. Sikiliza tutachokwambia, nawe utekekeze. Huo ndio usalama wako"

Dr Luis alibaki kimya.

"Tunataka ututengenezee kirusi cha DH+...." Imma Ogbo alisema kwa sauti ndogo.

"Unasemaje!!!?" Mshangao mkubwa ulionekana katika macho ya Dr Luis.

Hakuamini maneno yale kutoka kwa yule mtu. Kabla ya dakika hii aliamini ni yeye pekee ndiye anayejua kuhusu kirusi cha siri cha DH+ hapa duniani.

Kumbe katu haikuwa hivyo.

Moyoni akahisi, hata siri yake na rais Mgaya sasa itakuwa hadharani kwa hawa watu.

Hili lilikuwa ni Bomu kwake!!!

Je nini kitatokea? Tukutane hapahapa keshokutwa.
Shusha
 

Similar Discussions

8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom