Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391
Sehemu ya Tisa
Saa moja baada ya kikosi cha B1, chini ya kiongozi wake Daniel Mwaseba kupewa kazi ya kuchunguza mahali alipo Dr Luis. Katika nyumba moja kubwa iliyopo huko Kigamboni kulikuwa na kikao cha siri.
Kilikuwa ni kikao cha watu watatu.
"Nashukuru sana tumefanikisha zoezi la kumteka Dr Luis, huyu mzee ni muhimu sana katika hii mpango wetu wa kutengeneza kirusi cha DH+. Kwa kutumia kirusi hicho na jinsi tulivyoipanga mipango yetu lazima tutamfanya Dr Luis akubaliane na matakwa yetu" Mzee mmoja mnene mweusi alisema mle ndani.
"Ni kweli mzee Msangi. Ni suala la kushukuru sana baada ya kufanikiwa kumpata Dr Luis. Na pia tulifanya maamuzi ya busara sana kumteka yule Daniel, na kumripua kwa Bomu kule Mkuranga. Tuna hakika Daniel kingekuwa kikwazo kikubwa sana katika mpango wetu. Lakini kwasasa tumefanikiwa kuondoa hiko kikwazo. Sasa mpango uliobaki ni mmoja tu, kwenda kumfungua Dr Luis atwambie nini lilikuwa lengo la rais kumleta hapa nchini. Pia ni lazima tumpe mpango wetu wa kutengeneza kirusi DH+" Kijana mwengine wa makamo alisema.
"Upo sahihi Lameck. Tufanye hiyo mipango yetu mapema na kwa haraka kabla hawa washenzi hawajajua nini lengo letu" Mzee Msangi alisema.
"Kwani Dr Luis yupo sehemu gani?" Kijana mwengine aliuliza.
"Kwani hujui Luca. Yupo sehemu salama ndani ya nyumba hiihii. Hii nyumba imejengwa maalum kwa kazi kama hizi. Chini kabisa ya nyumba hii kuna chumba cha siri ambacho ndimo Dr Luis amewekwa. Atahojiwa hukohuko. Baada ya kutwambia lengo la rais kumleta hapa nchini. Tutampa Dr Luis mpango wetu wa kutengeneza kirusi DH+" Mzee Msangi alisema.
"Tutaenda na Carlos kumuhoji Dr Luis?" Lameck aliuliza.
"Kwani hujui Lameck. Watu wa kule Mkuranga wote waliuwawa kwa shambulio la Bomu. Roho alipata wasiwasi baada ya kusikia Daniel alikuwa katika harakati za kutoroka mle ndani. Alitoa maamuzi magumu ya kuilipua ile nyumba na wote waliomo ndani. Kina Carlos, Dingo na wote waliuwawa mle ndani, akiwemo Daniel Mwaseba" Mzee Msangi alisema.
"E bwana wee!! Sasa nani ataenda kumfungua Dr Luis huko chini. Carlos ndiye tuliyekuwa tunamtegemea katika kazi ya kuwafanya watu waseme hata yale wasiyoulizwa. Sasa nani ataifanya kazi hiyo kwa Dr Luis?" Luca aliuliza.
"Tuna Imma Ogbo. Imma Ogbo amekuja leo kutoka nchini Nigeria kwa kazi hiyo" Mzee Msangi alisema.
"OK, twendeni na huyo Imma Ogbo kwa Dr Luis tukamfungue" Lameck alisema.
"Hapana, sisi hatutaenda huko chini. Tutashuhudia kila kitu kutokea hapa. Chumba cha mateso kimeunganishwa na kamera ambazo tutashuhudia kila kitu Imma Ogbo atakachofanya" Mzee Msangi alisema.
Watu wote wakatulia.
Mzee Msangi aliwasha runinga kubwa iliyopo ukutani. Akabonyazabonyaza rimoti kisha picha ilionekana katika ile runinga iliyapachikwa ukutani.
Chumba cha siri kilikuwa kinaonekana.
Mzee mmoja aliyechoka wa kizungu alionekana katika kile chumba. Alikuwa amekaa katika kiti akiwa na mawazo mengi.
"Yule ndio Dr Luis" Mzee Msangi alisema.
"Anaonekana ana mawazo mengi" Lameck alisema.
"Tulifanya makusudi kumwacha kwa muda ili aingiwe na wasiwasi. Sasa ni muda muafaka wa Imma Ogbo kwenda kumfungua kila kitu, na kumpa kazi yetu." Mzee Msangi alisema.
Akachukua simu yake na kuibonyaza. Akaitafuta namba ya Imma.
Akapiga.
"Imma, unaweza kwenda sasa kumuhoji Dr Luis. Hakikisha anasema kila kitu. Unaruhusiwa kumtesa uwezavyo, lakini hakikisha hafi. Tunamuhitaji sana Dr Luis katika mambo yetu" Mzee Msangi alisema.
"Usiwe na hofu mzee. Atasema tu huyu mzungu" Imma Ogbo akasema kwa kifupi.
"Nakuamini Imma Ogbo"
"Sijawahi kukosea katika kazi hizi" Imma Ogbo alisema kwa kujiamini.
Mzee Msangi akakata simu.
Kupitia ile runinga ya ukutani ya mzee Msangi walimwona Imma Ogbo akiingia katika kile chumba cha mateso.
Imma alikuwa amezaa suruali ya jeans nyeusi, huku juu akiwa amevaa fulana nyeusi iliyokuwa imembana vyema. Aliingia katika kile chumba bila wasiwasi wowote ule. Alipoingia mle ndani moja kwa moja alimsogelea Dr Luis aliyekuwa amekaa katika kile kiti.
"Ninaitwa Imma Ogbo. Nipo hapa kwa kazi mbili tu ambazo bila shaka ninategemea utanipa ushirikiano" Imma alisema.
Dr Luis aliinua sura yake kivivu na kumwangalia yule kijana.
"Kwanini mmenileta hapa?" Dr Luis aliongea kwa kiswahili.
"Hapa kuna mgawanyo wa majukumu. Mimi kama Imma Ogbo jukumu langu ni kuuliza maswali, na wewe kama Dr Luis jukumu lako ni kujibu tu. Ukifanya vingine utafahamu upande wangu wa pili wa shilingi" Imma alisema kwa utulivu.
Dr Luis alikaa kimya huku akimwangalia yule kijana aliyejitambulisha kwa jina la Imma Ogbo.
"Tunajua umekuja hapa jijini baada ya kupewa mwaliko na rais Mgaya. Swali ni mwaliko huo ulihusu nini?" Imma Ogbo aliuliza.
Dr Luis alikaa kimya.
"Nimekuja hapa kama rafiki. Ninaomba tuhojiane kirafiki bila ya kupeana mateso na kumwaga damu!!" Imma Ogbo alipiga mkwara.
"Kwani mnataka nini ninyi watu? Kama mnataka hela niambieni. Nitawapa kiasi chochote kile cha pesa mnirejeshee uhuru wangu..." Dr Luis alisema kwa kulalama.
Imma Ogbo hakuuliza tena swali. Alienda konani kabisa ya kile chumba ambako kulikuwa na kabati dogo, alilifungua kabati na kutoa kisu, na chupa ndogo nyeupe iliyokuwa na majimaji meupe ndani yake. Bila kufunga lile kabati alimsogelea tena Dr Luis.
"Nadhani hujaelewa nimemaanisha nini niliposema hapa kuna mgawanyo wa majukumu. Ngoja nikuoneshe sasa" Imma Ogbo alisema huku akishika mkono wa Dr Luis.
"Nakukata kidole!! Na natavimaliza vidole vyako vyote endapo utaenda kinyume na ninachokueleza" Imma Ogbo alisema akiwa kaushika mkono wa Dr Luis.
Je nini kitatokea? Tukutane sehemu ijayo.
Safi mwendelezo lini tena kamanda?RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391
Sehemu ya Kumi na Moja
Hannan alimpigia Daniel simu dakika kumi baadae, ili kumpa majibu ya kazi aliyopewa ya kuichunguza namba ya Kelvin aliyekuwa mfanyakazi wa hotel ya Dos Santos.
"Naomba niongee na Daniel, David" Hannan alisema alipopiga simu ya David.
"Hannan huyu hewani anataka kuongea na wewe" David alisema huku akimkabidhi simu Daniel.
"Eeh nambie Hannan, umepata nini katika simu ya Kelvin?" Daniel aliuliza.
"Daniel, hii namba inaonesha imetumika mfululizo kwa miaka mitatu sasa. Na mtumiaji kwa mujibu wa usajili wake ni huyo Kelvin, lakini cha kushangaza hakuna kumbukumbu yoyote ile katika hii namba" Hannan alisema.
"Unasemaje Hannan?"
"Nd'o hivyo Daniel, nimejaribu kuichunguza hii namba, hakuna kumbukumbu yoyote ile. Hakuna kumbukumbu za watu waliompigia, waliopiga wala meseji. Lakini namba inaonesha kwamba ilikuwa inatumika ndani ya miaka mitatu mfululizo" Hannan alirudia tena.
"Wametuwahi hawa mbwa" Daniel alisema kwa sauti ndogo.
"Yani hawa watu wanafanya mambo yao kwa umakini sana. Wamefuta kumbukumbu zote za hii namba" Hannan alisema.
"Wamejaribu lakini bado hawataweza. Lazima tutawagundua tu hawa watu ni kina nani? Na wana nia gani na Taifa hili?" Daniel alisema.
"Nakuombea sana Daniel muwatie mikononi watu hawa. Nina hasira nao sana kwa jinsi walivyotumbukiza risasi katika mwili wangu. Yani natamani ningekuwa mzima ili niungane na nyinyi ili kuwakamata hawa mafedhuli" Hannan alisema kwa hasira.
"Pole sana Hannan. Msaada wako ni mkubwa sana. Hesabu tu nawewe upo ndani ya kazi hii. Jina lako litaandikwa kwa wino wa dhahabu siku tutakayoifanikisha kazi hii. Na kuliacha salama taifa letu. Lakini vipi unaendeleaje kwa sasa Hannan?"
"Operesheni za kuondoa risasi imekwenda vizuri sana. Kwa sasa ninauguza vidonda tu. Nitakuwa sawa sio muda na bila shaka nitaungana na nyinyi katika kikosi B1" Hannan alisema kwa hisia.
"Kila sekunde ninakuombea Hannan. Bila shaka utakuwa sawa mdogo wangu. Tumekumiss sana kazini" Daniel alisema.
Waliongea kidogo na Hannan, kisha waliagana simuni.
Daniel aliwasimulia wakina Adrian taarifa alizopewa na Hannan. Wote walishangaa sana. Sasa mpango ukabaki mmoja tu, wa kwenda nyumbani kwa Kelvin.
***
Imma Ogbo aliwasiliana na kina mzee Msangi juu ya aliyoyapata kutoka kwa Dr Luis. Bila kujua kwamba walisikia na kuona kila kitu. Aliwaambia pia jioni ndio ataenda rasmi kumueleza mpango wa kutengeza kirusi cha DH+.
"Hawa watu wamejuaje kama nilitakiwa kufika siku ile. Mara zote ninapofika Dar es salaam ujio wangu huwa wa siri sana. Ni rais pekee ndiye anayejua kuwa ninakuja. Safari hii nilishangaa sana baada ya rais kuniambia nitapokelewa na mtu mwengine badala ya Irene Dembwe kama ilivyo kawaida yetu. Bila shaka hapo ndipo siri juu ya ujio wangu ilipoanza kupotea. Najua rais Mgaya atachanganyikiwa sana akisikia nimetekwa. Atafanya juu chini kunitafuta, nipatikane ili siri yake isije ikavuja. Hawa watu walioniteka wamehisi nini kitu kinachonifanya nije Tanzania mwanzo na mwisho wa mwezi? Ila hawawezi kujua. Nilitazama sura ya yule mtu aliyekuja kunihoji inaonesha hajui chochote. Pengine kuna mambo yao mengine kabisa yaliyofanya waniteke. Niliahidi nitatunza siri ya rais Mgaya siku zote za maisha yangu. Na itakuwa hivyo. Sitoisema kwa mtu yoyote yule.
Hawa jamaa wanaonekana makatili sana, niliona macho ya yule jamaa yalivyobadilika alivyotaka kunikata kidole. Lakini niseme tu, sitasema kitu chochote kile juu ya siri ya rais Mgaya" Dr Luis alikuwa anawaza.
Kipindi Dr Luis anawaza juu ya kuificha siri ya rais, Daniel Mwaseba, Adrian Kaanan na David John walikuwa wanaelekea nyumbani kwa Kelvin.
Ilikuwa mitaa ya Mikocheni jijini Dar es salaam. Katika nyumba moja yenye geti kubwa jeusi iliyokaribu na hospitali ya Kairuki. Walipewa hadi namba ya nyumba na meneja wa hoteli ya Dos Santos baada ya Daniel kumpigia tena.
Wakiwa njiani walikutana na foleni kubwa sana. Foleni haikuwa ya kawaida. Wakiwa katikati ya foleni ndipo walipoanza kusikia tetesi kwamba mbele kuna nyumba inaungua moto. Wote waliingiwa na uwoga kusikia taarifa hiyo. Kwakuwa mahali walipokuwepo hapakuwa mbali sana na mahali walipoelekezwa kuwa anaishi Kelvin.
Adrian Kaanan alishuka kwenye gari na kuelekea upande ilipokuwa nyumba ya Kelvin.
Alipokaribia, alipigwa na butwaa!!!. Nyumba ya Kelvin ndio iliyokuwa inawaka moto!
Watu wengi walijaa eneo lile wakishuhudia ile nyumba kubwa ikiteketea. Adrian Kaanan aliiweka mikono yake yote miwili mdomoni. Macho yamemtoka pima.
Akiwa haamini. Haamini hata kidogo...
"Wameichoma moto nyumba ya Kelvin. Bila shaka kuna kitu wamekificha tena hapa. Walifuta mawasiliano ya Kelvin wakificha kitu na sasa wameichoma nyumba yake katika mwendelezo wao wa kuficha vitu vyao. Lakini hawa watu waliomteka Dr Luis ni kina nani hasa? Na wana lengo gani?" Adrian Kaanan aliwaza.
Hakukaa tena eneo lile. Maana hakukuwa ni kitu chochote kile ambacho kingemsaidia katika uchunguzi wake. Alirejea kule alipowaacha wakina Daniel.
"Tuambie, umefanikiwa kufika?" Davis aliuliza Adrian alipowasili tu.
"Nimekuta nyumba ya Kelvin inaungua moto!!" Adrian alisema kwa sauti ya kuchoka.
"Ni meneja Fadhili wa Dos Santos" Daniel aliropoka. "Bila shaka ndiye anayevujisha siri zetu. Mpigie Hannan aifatilie simu ya meneja tujue yupo wake. Tumfuate sasahivi. Huu ni mwisho wake wa kutuchezea michezo ya kijinga" Daniel Mwaseba alisema kwa hasira.
Je nini kitatokea. Tuwe wote sehemu ijayo.
Tupo tunaisubiri mwendelezoRIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391
Sehemu ya Kumi na Moja
Hannan alimpigia Daniel simu dakika kumi baadae, ili kumpa majibu ya kazi aliyopewa ya kuichunguza namba ya Kelvin aliyekuwa mfanyakazi wa hotel ya Dos Santos.
"Naomba niongee na Daniel, David" Hannan alisema alipopiga simu ya David.
"Hannan huyu hewani anataka kuongea na wewe" David alisema huku akimkabidhi simu Daniel.
"Eeh nambie Hannan, umepata nini katika simu ya Kelvin?" Daniel aliuliza.
"Daniel, hii namba inaonesha imetumika mfululizo kwa miaka mitatu sasa. Na mtumiaji kwa mujibu wa usajili wake ni huyo Kelvin, lakini cha kushangaza hakuna kumbukumbu yoyote ile katika hii namba" Hannan alisema.
"Unasemaje Hannan?"
"Nd'o hivyo Daniel, nimejaribu kuichunguza hii namba, hakuna kumbukumbu yoyote ile. Hakuna kumbukumbu za watu waliompigia, waliopiga wala meseji. Lakini namba inaonesha kwamba ilikuwa inatumika ndani ya miaka mitatu mfululizo" Hannan alirudia tena.
"Wametuwahi hawa mbwa" Daniel alisema kwa sauti ndogo.
"Yani hawa watu wanafanya mambo yao kwa umakini sana. Wamefuta kumbukumbu zote za hii namba" Hannan alisema.
"Wamejaribu lakini bado hawataweza. Lazima tutawagundua tu hawa watu ni kina nani? Na wana nia gani na Taifa hili?" Daniel alisema.
"Nakuombea sana Daniel muwatie mikononi watu hawa. Nina hasira nao sana kwa jinsi walivyotumbukiza risasi katika mwili wangu. Yani natamani ningekuwa mzima ili niungane na nyinyi ili kuwakamata hawa mafedhuli" Hannan alisema kwa hasira.
"Pole sana Hannan. Msaada wako ni mkubwa sana. Hesabu tu nawewe upo ndani ya kazi hii. Jina lako litaandikwa kwa wino wa dhahabu siku tutakayoifanikisha kazi hii. Na kuliacha salama taifa letu. Lakini vipi unaendeleaje kwa sasa Hannan?"
"Operesheni za kuondoa risasi imekwenda vizuri sana. Kwa sasa ninauguza vidonda tu. Nitakuwa sawa sio muda na bila shaka nitaungana na nyinyi katika kikosi B1" Hannan alisema kwa hisia.
"Kila sekunde ninakuombea Hannan. Bila shaka utakuwa sawa mdogo wangu. Tumekumiss sana kazini" Daniel alisema.
Waliongea kidogo na Hannan, kisha waliagana simuni.
Daniel aliwasimulia wakina Adrian taarifa alizopewa na Hannan. Wote walishangaa sana. Sasa mpango ukabaki mmoja tu, wa kwenda nyumbani kwa Kelvin.
***
Imma Ogbo aliwasiliana na kina mzee Msangi juu ya aliyoyapata kutoka kwa Dr Luis. Bila kujua kwamba walisikia na kuona kila kitu. Aliwaambia pia jioni ndio ataenda rasmi kumueleza mpango wa kutengeza kirusi cha DH+.
"Hawa watu wamejuaje kama nilitakiwa kufika siku ile. Mara zote ninapofika Dar es salaam ujio wangu huwa wa siri sana. Ni rais pekee ndiye anayejua kuwa ninakuja. Safari hii nilishangaa sana baada ya rais kuniambia nitapokelewa na mtu mwengine badala ya Irene Dembwe kama ilivyo kawaida yetu. Bila shaka hapo ndipo siri juu ya ujio wangu ilipoanza kupotea. Najua rais Mgaya atachanganyikiwa sana akisikia nimetekwa. Atafanya juu chini kunitafuta, nipatikane ili siri yake isije ikavuja. Hawa watu walioniteka wamehisi nini kitu kinachonifanya nije Tanzania mwanzo na mwisho wa mwezi? Ila hawawezi kujua. Nilitazama sura ya yule mtu aliyekuja kunihoji inaonesha hajui chochote. Pengine kuna mambo yao mengine kabisa yaliyofanya waniteke. Niliahidi nitatunza siri ya rais Mgaya siku zote za maisha yangu. Na itakuwa hivyo. Sitoisema kwa mtu yoyote yule.
Hawa jamaa wanaonekana makatili sana, niliona macho ya yule jamaa yalivyobadilika alivyotaka kunikata kidole. Lakini niseme tu, sitasema kitu chochote kile juu ya siri ya rais Mgaya" Dr Luis alikuwa anawaza.
Kipindi Dr Luis anawaza juu ya kuificha siri ya rais, Daniel Mwaseba, Adrian Kaanan na David John walikuwa wanaelekea nyumbani kwa Kelvin.
Ilikuwa mitaa ya Mikocheni jijini Dar es salaam. Katika nyumba moja yenye geti kubwa jeusi iliyokaribu na hospitali ya Kairuki. Walipewa hadi namba ya nyumba na meneja wa hoteli ya Dos Santos baada ya Daniel kumpigia tena.
Wakiwa njiani walikutana na foleni kubwa sana. Foleni haikuwa ya kawaida. Wakiwa katikati ya foleni ndipo walipoanza kusikia tetesi kwamba mbele kuna nyumba inaungua moto. Wote waliingiwa na uwoga kusikia taarifa hiyo. Kwakuwa mahali walipokuwepo hapakuwa mbali sana na mahali walipoelekezwa kuwa anaishi Kelvin.
Adrian Kaanan alishuka kwenye gari na kuelekea upande ilipokuwa nyumba ya Kelvin.
Alipokaribia, alipigwa na butwaa!!!. Nyumba ya Kelvin ndio iliyokuwa inawaka moto!
Watu wengi walijaa eneo lile wakishuhudia ile nyumba kubwa ikiteketea. Adrian Kaanan aliiweka mikono yake yote miwili mdomoni. Macho yamemtoka pima.
Akiwa haamini. Haamini hata kidogo...
"Wameichoma moto nyumba ya Kelvin. Bila shaka kuna kitu wamekificha tena hapa. Walifuta mawasiliano ya Kelvin wakificha kitu na sasa wameichoma nyumba yake katika mwendelezo wao wa kuficha vitu vyao. Lakini hawa watu waliomteka Dr Luis ni kina nani hasa? Na wana lengo gani?" Adrian Kaanan aliwaza.
Hakukaa tena eneo lile. Maana hakukuwa ni kitu chochote kile ambacho kingemsaidia katika uchunguzi wake. Alirejea kule alipowaacha wakina Daniel.
"Tuambie, umefanikiwa kufika?" Davis aliuliza Adrian alipowasili tu.
"Nimekuta nyumba ya Kelvin inaungua moto!!" Adrian alisema kwa sauti ya kuchoka.
"Ni meneja Fadhili wa Dos Santos" Daniel aliropoka. "Bila shaka ndiye anayevujisha siri zetu. Mpigie Hannan aifatilie simu ya meneja tujue yupo wake. Tumfuate sasahivi. Huu ni mwisho wake wa kutuchezea michezo ya kijinga" Daniel Mwaseba alisema kwa hasira.
Je nini kitatokea. Tuwe wote sehemu ijayo.