BOMU: Riwaya ya kipelelezi (1)

RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya nane

"Dr Luis hajawahi kuoa?" Daniel alishangaa. "Nakumbuka kabisa alinitambulisha kwa mdomo wake mwenyewe kule uwanja wa ndege kuwa yule mwanamke ni mkewe kabisa" Alisema.

"Ni hivyo Daniel, Dr Luis hajawahi kuoa hata kwa bahati mbaya. Lazima kutakuwa na kitu kilichojificha juu ya huyo mwanamke aliyekuja nae na kudai ni mkewe. Jukumu letu ni kukijua hicho kitu kilichojificha" IGP John Rondo alisema.

"Haya mambo yanashangaza sana kwakweli. Haya endelea kutusimulia Daniel ni kitu gani kilitokea baada ya kumpokea Dr Luis na huyo mwanamke aliyekutambulisha kama mkewe" Chifu alisema.

"Nilifanya kama ulivyoniagiza Chifu. Nilimpokea Dr Luis kule uwanja wa ndege na kwenda naye Kijitonyama katika hoteli ya Dos Santos. Baada ya kufikiria kidogo niliona si sahihi kumuacha Dr Luis alale peke yake pale hotelini, na mimi nililala palepale hotelini kwa ajili ya kumlinda Dr Luis.
Lakini cha kushangaza ilipofika saa tisa usiku nilipigiwa simu na mfanyakazi wa hoteli ile akiniambia kuwa Dr Luis amepotea. Nilianza harakati za kumtafuta, na katika harakati za kumtafuta nilijikuta nimetekwa na kupelekwa huko Mkuranga. Nikiwa njiani kama mateka, nilimtaarifu Hannan kwa ishara zetu kuwa nilikuwa katika hali ya hatari, naye alinifuata kwa gari.
Waliponifikisha huko Mkuranga, nilifungiwa kwenye kichumba kidogo. Kabla ya kujiokoa baada ya kusikia milio ya risasi nje. Nilivyotoka tu nilimuona mtu pembeni kabisa ukutani akigalagala. Wakati nikielekea kumuokoa ndipo ilipotokea helkopta yenye rangi ya jeshi na kuilipua ile nyumba..."

"Unasema helkopta yenye rangi za jeshi ndio iliyolipua ile nyumba?" Jenerali Ngoma alishangaa.

"Ndio Mkuu. Kwa macho yangu mawili niliishuhudia helkopta yenye mabaka ya jeshi ikiachia Bomu zito na kuiangamiza ile nyumba!" Daniel alisema.

"Bila shaka wakitaka kuficha kitu ndio maana waliiripua hiyo nyumba" Chifu alisema kwa sauti ndogo.

"Bila shaka. Hawa watu wana siri kubwa sana ambayo waliamua kutumia njia hiyo kuificha. Swali la msingi ni hawa watu ni kina nani? Na kwanini wamemteka Dr Luis?" IGP John Rondo aliuliza.

"Majibu ya maswali hayo uliyoyauliza sisi ndio wenye dhima ya kuyatafuta. Mheshimiwa rais ameacha kazi hii mikononi mwetu. Hivyo tujadiliane hapa ili kujua tunaanzia wapi kumpata Dr Luis? Pia lazima tujue kutekwa kwa Dr Luis kina nani wanahusika?. Tukiunganisha vyombo vyetu vya ulinzi bila shaka tutajua wahusika wa jambo hili" Chifu alisema.

"Umesema kweli Chifu. Hapa tupo viongozi wakuu wa ulinzi wa nchi hii. Lazima tufanye kitu kuhakikisha Dr Luis anapatikana. Mimi ushauri wangu tutoe mtu mmoja kila mmoja wetu katika sekta yake ili kuhakikisha suala hili linafika mwisho" Jenerali Ngoma alisema.

"Huo ni ushauri mzuri, nakubaliana nao" IGP John Rondo alisema.

"Nami pia naafiki" Chifu nae alisema.

"Kwakuwa hili ni jambo la haraka. Na lazima tulifanye kwa haraka kabla hawajamdhuru Dr Luis, pia hawajaleta madhara mengine, tuchague hapahapa watu ambao watachunguza jambo hili" Jenerali Ngoma alisema.

"Sawa, mimi katika jeshi la Polisi nitamtoa kijana wangu mahiri sana, anaitwa Adrian Kaanan" IGP John alisema.

"Mimi katika jeshi la Wananchi wa Tanzania nitamtoa kijana wangu David John. Ni mahiri sana katika uwanja wa vita, lakini kwasasa aliniambia ana hamu sana kujaribu uwezo wake mtaani. Na ishu hii kwakuwa inahusisha ndege ya jeshi basi itamfaa sana" Jenerali Ngoma alisema.

Kisha wote macho yao yakamwangalia Chifu.

"Mimi ninamteua Daniel Mwaseba.."

"Khaaaa!" Jenerali Ngoma na IGP John Rondo walishangaa kwa pamoja.

"Ndio, namwamini Daniel Mwaseba. Ni yeye ndiye aliyelianzisha jambo hili, na kwa kushirikiana na hao mliowachagua bila shaka wataenda kulimaliza" Chifu alisema kwa uhakika.

"Daniel si anaumwa? Unamaanisha tumsubiri Daniel mpaka apone ndipo tuanze operesheni hii? Mheshimiwa rais amesema tufanya haraka kumsaka Dr Luis" IGP John alisema.

"Ninaweza. Nilipata madhara kidogo ya moto kohoni. Lakini ninaweza kuifanya kazi hii kwa umakini mkubwa sana. Nitakuwemo katika kikosi hiko" Daniel alisema.

"Kwakuwa mwenyewe amekubali sawa, tutamuuanganisha na wakina Adrian ili waanze uchunguzi wao" IGP John Rondo alisema.

Baada ya maongezi hayo, IGP John alimpigia simu Adrian Kaanan huku Jenerali Ngoma akimpigia simu David John. Nusu saa tu zilitosha kuwafikisha askari hao katika hospitali ya taifa ya Muhimbili.

"Karibuni sana wakina Adrian. Kuna kazi ya haraka imetokea hapa nchini. Sisi kama viongozi wenu tumewachagua nyinyi katika kuchunguza jambo hili. Kiongozi wenu katika operesheni hii atakuwa Daniel Mwaseba. Najua nyote mnamfahamu Daniel Mwaseba. Ni yeye ndiye atakayewaambia operesheni hii inahusu nini, na ndiye atakayewapa majukumu yenu katika uchunguzi" Jenerali Ngoma alisema.

Adrian Kaanan na David John waliitikia kwa kichwa.

"Jukumu letu kama viongozi wenu limeisha. Sasa kazi hii ipo mikononi mwenu vijana. Daniel, kama mkuu wa kikosi hiki utaripoti moja kwa moja kwa Chifu. Naye atatuarifu sisi. Una ruhusa ya kuongeza mtu au watu katika kazi yako, awe mtu kutoka idara ya usalama wa taifa, jeshi la polisi au jeshi la wananchi la Tanzania. Mna ruhusa ya kutumia chombo chochote kile cha serikali, ili kukamilisha lengo kuu" IGP John alisema.

Baada ya maongezi yaliyodumu kama dakika kumi, viongozi wakaondoka pale hospitali, wakiwaacha wale vijana watatu.

Daniel, aliwaeleza wakina Adrian kila kitu jinsi Dr Luis alivyopotea. Wote walielewa nini wanatakiwa kufanya.

"Kikosi chetu tutakiita kikosi B. Kwa maana kikosi Bomu. Lengo kuu kama nilivyowaambia ni kumsaka Dr Luis popote pale alipo. Na kujua ni kina nani wapo nyuma juu ya utekaji huu. Naamini ninyi wote ni mahiri katika kazi hizi, sasa hii kazi lazima tuoneshe umahiri zaidi.
Tuna siku tatu tu tumepewa za kuhakikisha tunampata Dr Luis, tumeelewana?" Daniel aliuliza.

"Tumeelewana" Waliitikia.

"Na..omb..a mnijum..uish.e katika kik..osi B" Kwa sauti ya kukatakata Hannan alisema.

"Hannan, relax my dear. Ngoja upone kwanza. Hii kazi tunayoenda kuifanya ni ngumu sana, huwezi kuifanya ukiwa katika hali hiyo" Daniel alisema huku akimwangalia Hannan aliyelala kitandani.

"Da..ni.el Nita..ifanya kazi hii..nihesabu ...na mi..mi" Hannan alisema akigugumia.

"Utaifanye kazi hii ukiwa katika hali hiyo? Subiri kwanza upone Hannan" Daniel alisisisitiza.

"K..abla si..jaingia k..atika kaz..i hii nilis..omea IT, nahitaji ko..mpyuta yan..gu tu ni..kiwa hapa kitan..dani, amini ni..tawasaidia..." Hannan alishindwa kuongea.

"Ok tutafanya hivyo. Nitakuletea kompyuta yako hapa. Tuone tutaimalizaje hii kazi" Daniel alikubali.

Hannan alitabasamu.

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo..
 
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Tisa

Saa moja baada ya kikosi cha B1, chini ya kiongozi wake Daniel Mwaseba kupewa kazi ya kuchunguza mahali alipo Dr Luis. Katika nyumba moja kubwa iliyopo huko Kigamboni kulikuwa na kikao cha siri.

Kilikuwa ni kikao cha watu watatu.

"Nashukuru sana tumefanikisha zoezi la kumteka Dr Luis, huyu mzee ni muhimu sana katika hii mpango wetu wa kutengeneza kirusi cha DH+. Kwa kutumia kirusi hicho na jinsi tulivyoipanga mipango yetu lazima tutamfanya Dr Luis akubaliane na matakwa yetu" Mzee mmoja mnene mweusi alisema mle ndani.

"Ni kweli mzee Msangi. Ni suala la kushukuru sana baada ya kufanikiwa kumpata Dr Luis. Na pia tulifanya maamuzi ya busara sana kumteka yule Daniel, na kumripua kwa Bomu kule Mkuranga. Tuna hakika Daniel kingekuwa kikwazo kikubwa sana katika mpango wetu. Lakini kwasasa tumefanikiwa kuondoa hiko kikwazo. Sasa mpango uliobaki ni mmoja tu, kwenda kumfungua Dr Luis atwambie nini lilikuwa lengo la rais kumleta hapa nchini. Pia ni lazima tumpe mpango wetu wa kutengeneza kirusi DH+" Kijana mwengine wa makamo alisema.

"Upo sahihi Lameck. Tufanye hiyo mipango yetu mapema na kwa haraka kabla hawa washenzi hawajajua nini lengo letu" Mzee Msangi alisema.

"Kwani Dr Luis yupo sehemu gani?" Kijana mwengine aliuliza.

"Kwani hujui Luca. Yupo sehemu salama ndani ya nyumba hiihii. Hii nyumba imejengwa maalum kwa kazi kama hizi. Chini kabisa ya nyumba hii kuna chumba cha siri ambacho ndimo Dr Luis amewekwa. Atahojiwa hukohuko. Baada ya kutwambia lengo la rais kumleta hapa nchini. Tutampa Dr Luis mpango wetu wa kutengeneza kirusi DH+" Mzee Msangi alisema.

"Tutaenda na Carlos kumuhoji Dr Luis?" Lameck aliuliza.

"Kwani hujui Lameck. Watu wa kule Mkuranga wote waliuwawa kwa shambulio la Bomu. Roho alipata wasiwasi baada ya kusikia Daniel alikuwa katika harakati za kutoroka mle ndani. Alitoa maamuzi magumu ya kuilipua ile nyumba na wote waliomo ndani. Kina Carlos, Dingo na wote waliuwawa mle ndani, akiwemo Daniel Mwaseba" Mzee Msangi alisema.

"E bwana wee!! Sasa nani ataenda kumfungua Dr Luis huko chini. Carlos ndiye tuliyekuwa tunamtegemea katika kazi ya kuwafanya watu waseme hata yale wasiyoulizwa. Sasa nani ataifanya kazi hiyo kwa Dr Luis?" Luca aliuliza.

"Tuna Imma Ogbo. Imma Ogbo amekuja leo kutoka nchini Nigeria kwa kazi hiyo" Mzee Msangi alisema.

"OK, twendeni na huyo Imma Ogbo kwa Dr Luis tukamfungue" Lameck alisema.

"Hapana, sisi hatutaenda huko chini. Tutashuhudia kila kitu kutokea hapa. Chumba cha mateso kimeunganishwa na kamera ambazo tutashuhudia kila kitu Imma Ogbo atakachofanya" Mzee Msangi alisema.

Watu wote wakatulia.

Mzee Msangi aliwasha runinga kubwa iliyopo ukutani. Akabonyazabonyaza rimoti kisha picha ilionekana katika ile runinga iliyapachikwa ukutani.

Chumba cha siri kilikuwa kinaonekana.

Mzee mmoja aliyechoka wa kizungu alionekana katika kile chumba. Alikuwa amekaa katika kiti akiwa na mawazo mengi.

"Yule ndio Dr Luis" Mzee Msangi alisema.

"Anaonekana ana mawazo mengi" Lameck alisema.

"Tulifanya makusudi kumwacha kwa muda ili aingiwe na wasiwasi. Sasa ni muda muafaka wa Imma Ogbo kwenda kumfungua kila kitu, na kumpa kazi yetu." Mzee Msangi alisema.

Akachukua simu yake na kuibonyaza. Akaitafuta namba ya Imma.
Akapiga.

"Imma, unaweza kwenda sasa kumuhoji Dr Luis. Hakikisha anasema kila kitu. Unaruhusiwa kumtesa uwezavyo, lakini hakikisha hafi. Tunamuhitaji sana Dr Luis katika mambo yetu" Mzee Msangi alisema.

"Usiwe na hofu mzee. Atasema tu huyu mzungu" Imma Ogbo akasema kwa kifupi.

"Nakuamini Imma Ogbo"

"Sijawahi kukosea katika kazi hizi" Imma Ogbo alisema kwa kujiamini.

Mzee Msangi akakata simu.

Kupitia ile runinga ya ukutani ya mzee Msangi walimwona Imma Ogbo akiingia katika kile chumba cha mateso.
Imma alikuwa amezaa suruali ya jeans nyeusi, huku juu akiwa amevaa fulana nyeusi iliyokuwa imembana vyema. Aliingia katika kile chumba bila wasiwasi wowote ule. Alipoingia mle ndani moja kwa moja alimsogelea Dr Luis aliyekuwa amekaa katika kile kiti.

"Ninaitwa Imma Ogbo. Nipo hapa kwa kazi mbili tu ambazo bila shaka ninategemea utanipa ushirikiano" Imma alisema.

Dr Luis aliinua sura yake kivivu na kumwangalia yule kijana.

"Kwanini mmenileta hapa?" Dr Luis aliongea kwa kiswahili.

"Hapa kuna mgawanyo wa majukumu. Mimi kama Imma Ogbo jukumu langu ni kuuliza maswali, na wewe kama Dr Luis jukumu lako ni kujibu tu. Ukifanya vingine utafahamu upande wangu wa pili wa shilingi" Imma alisema kwa utulivu.

Dr Luis alikaa kimya huku akimwangalia yule kijana aliyejitambulisha kwa jina la Imma Ogbo.

"Tunajua umekuja hapa jijini baada ya kupewa mwaliko na rais Mgaya. Swali ni mwaliko huo ulihusu nini?" Imma Ogbo aliuliza.

Dr Luis alikaa kimya.

"Nimekuja hapa kama rafiki. Ninaomba tuhojiane kirafiki bila ya kupeana mateso na kumwaga damu!!" Imma Ogbo alipiga mkwara.

"Kwani mnataka nini ninyi watu? Kama mnataka hela niambieni. Nitawapa kiasi chochote kile cha pesa mnirejeshee uhuru wangu..." Dr Luis alisema kwa kulalama.

Imma Ogbo hakuuliza tena swali. Alienda konani kabisa ya kile chumba ambako kulikuwa na kabati dogo, alilifungua kabati na kutoa kisu, na chupa ndogo nyeupe iliyokuwa na majimaji meupe ndani yake. Bila kufunga lile kabati alimsogelea tena Dr Luis.

"Nadhani hujaelewa nimemaanisha nini niliposema hapa kuna mgawanyo wa majukumu. Ngoja nikuoneshe sasa" Imma Ogbo alisema huku akishika mkono wa Dr Luis.

"Nakukata kidole!! Na natavimaliza vidole vyako vyote endapo utaenda kinyume na ninachokueleza" Imma Ogbo alisema akiwa kaushika mkono wa Dr Luis.

Je nini kitatokea? Tukutane sehemu ijayo.
 
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Tisa

Saa moja baada ya kikosi cha B1, chini ya kiongozi wake Daniel Mwaseba kupewa kazi ya kuchunguza mahali alipo Dr Luis. Katika nyumba moja kubwa iliyopo huko Kigamboni kulikuwa na kikao cha siri.

Kilikuwa ni kikao cha watu watatu.

"Nashukuru sana tumefanikisha zoezi la kumteka Dr Luis, huyu mzee ni muhimu sana katika hii mpango wetu wa kutengeneza kirusi cha DH+. Kwa kutumia kirusi hicho na jinsi tulivyoipanga mipango yetu lazima tutamfanya Dr Luis akubaliane na matakwa yetu" Mzee mmoja mnene mweusi alisema mle ndani.

"Ni kweli mzee Msangi. Ni suala la kushukuru sana baada ya kufanikiwa kumpata Dr Luis. Na pia tulifanya maamuzi ya busara sana kumteka yule Daniel, na kumripua kwa Bomu kule Mkuranga. Tuna hakika Daniel kingekuwa kikwazo kikubwa sana katika mpango wetu. Lakini kwasasa tumefanikiwa kuondoa hiko kikwazo. Sasa mpango uliobaki ni mmoja tu, kwenda kumfungua Dr Luis atwambie nini lilikuwa lengo la rais kumleta hapa nchini. Pia ni lazima tumpe mpango wetu wa kutengeneza kirusi DH+" Kijana mwengine wa makamo alisema.

"Upo sahihi Lameck. Tufanye hiyo mipango yetu mapema na kwa haraka kabla hawa washenzi hawajajua nini lengo letu" Mzee Msangi alisema.

"Kwani Dr Luis yupo sehemu gani?" Kijana mwengine aliuliza.

"Kwani hujui Luca. Yupo sehemu salama ndani ya nyumba hiihii. Hii nyumba imejengwa maalum kwa kazi kama hizi. Chini kabisa ya nyumba hii kuna chumba cha siri ambacho ndimo Dr Luis amewekwa. Atahojiwa hukohuko. Baada ya kutwambia lengo la rais kumleta hapa nchini. Tutampa Dr Luis mpango wetu wa kutengeneza kirusi DH+" Mzee Msangi alisema.

"Tutaenda na Carlos kumuhoji Dr Luis?" Lameck aliuliza.

"Kwani hujui Lameck. Watu wa kule Mkuranga wote waliuwawa kwa shambulio la Bomu. Roho alipata wasiwasi baada ya kusikia Daniel alikuwa katika harakati za kutoroka mle ndani. Alitoa maamuzi magumu ya kuilipua ile nyumba na wote waliomo ndani. Kina Carlos, Dingo na wote waliuwawa mle ndani, akiwemo Daniel Mwaseba" Mzee Msangi alisema.

"E bwana wee!! Sasa nani ataenda kumfungua Dr Luis huko chini. Carlos ndiye tuliyekuwa tunamtegemea katika kazi ya kuwafanya watu waseme hata yale wasiyoulizwa. Sasa nani ataifanya kazi hiyo kwa Dr Luis?" Luca aliuliza.

"Tuna Imma Ogbo. Imma Ogbo amekuja leo kutoka nchini Nigeria kwa kazi hiyo" Mzee Msangi alisema.

"OK, twendeni na huyo Imma Ogbo kwa Dr Luis tukamfungue" Lameck alisema.

"Hapana, sisi hatutaenda huko chini. Tutashuhudia kila kitu kutokea hapa. Chumba cha mateso kimeunganishwa na kamera ambazo tutashuhudia kila kitu Imma Ogbo atakachofanya" Mzee Msangi alisema.

Watu wote wakatulia.

Mzee Msangi aliwasha runinga kubwa iliyopo ukutani. Akabonyazabonyaza rimoti kisha picha ilionekana katika ile runinga iliyapachikwa ukutani.

Chumba cha siri kilikuwa kinaonekana.

Mzee mmoja aliyechoka wa kizungu alionekana katika kile chumba. Alikuwa amekaa katika kiti akiwa na mawazo mengi.

"Yule ndio Dr Luis" Mzee Msangi alisema.

"Anaonekana ana mawazo mengi" Lameck alisema.

"Tulifanya makusudi kumwacha kwa muda ili aingiwe na wasiwasi. Sasa ni muda muafaka wa Imma Ogbo kwenda kumfungua kila kitu, na kumpa kazi yetu." Mzee Msangi alisema.

Akachukua simu yake na kuibonyaza. Akaitafuta namba ya Imma.
Akapiga.

"Imma, unaweza kwenda sasa kumuhoji Dr Luis. Hakikisha anasema kila kitu. Unaruhusiwa kumtesa uwezavyo, lakini hakikisha hafi. Tunamuhitaji sana Dr Luis katika mambo yetu" Mzee Msangi alisema.

"Usiwe na hofu mzee. Atasema tu huyu mzungu" Imma Ogbo akasema kwa kifupi.

"Nakuamini Imma Ogbo"

"Sijawahi kukosea katika kazi hizi" Imma Ogbo alisema kwa kujiamini.

Mzee Msangi akakata simu.

Kupitia ile runinga ya ukutani ya mzee Msangi walimwona Imma Ogbo akiingia katika kile chumba cha mateso.
Imma alikuwa amezaa suruali ya jeans nyeusi, huku juu akiwa amevaa fulana nyeusi iliyokuwa imembana vyema. Aliingia katika kile chumba bila wasiwasi wowote ule. Alipoingia mle ndani moja kwa moja alimsogelea Dr Luis aliyekuwa amekaa katika kile kiti.

"Ninaitwa Imma Ogbo. Nipo hapa kwa kazi mbili tu ambazo bila shaka ninategemea utanipa ushirikiano" Imma alisema.

Dr Luis aliinua sura yake kivivu na kumwangalia yule kijana.

"Kwanini mmenileta hapa?" Dr Luis aliongea kwa kiswahili.

"Hapa kuna mgawanyo wa majukumu. Mimi kama Imma Ogbo jukumu langu ni kuuliza maswali, na wewe kama Dr Luis jukumu lako ni kujibu tu. Ukifanya vingine utafahamu upande wangu wa pili wa shilingi" Imma alisema kwa utulivu.

Dr Luis alikaa kimya huku akimwangalia yule kijana aliyejitambulisha kwa jina la Imma Ogbo.

"Tunajua umekuja hapa jijini baada ya kupewa mwaliko na rais Mgaya. Swali ni mwaliko huo ulihusu nini?" Imma Ogbo aliuliza.

Dr Luis alikaa kimya.

"Nimekuja hapa kama rafiki. Ninaomba tuhojiane kirafiki bila ya kupeana mateso na kumwaga damu!!" Imma Ogbo alipiga mkwara.

"Kwani mnataka nini ninyi watu? Kama mnataka hela niambieni. Nitawapa kiasi chochote kile cha pesa mnirejeshee uhuru wangu..." Dr Luis alisema kwa kulalama.

Imma Ogbo hakuuliza tena swali. Alienda konani kabisa ya kile chumba ambako kulikuwa na kabati dogo, alilifungua kabati na kutoa kisu, na chupa ndogo nyeupe iliyokuwa na majimaji meupe ndani yake. Bila kufunga lile kabati alimsogelea tena Dr Luis.

"Nadhani hujaelewa nimemaanisha nini niliposema hapa kuna mgawanyo wa majukumu. Ngoja nikuoneshe sasa" Imma Ogbo alisema huku akishika mkono wa Dr Luis.

"Nakukata kidole!! Na natavimaliza vidole vyako vyote endapo utaenda kinyume na ninachokueleza" Imma Ogbo alisema akiwa kaushika mkono wa Dr Luis.

Je nini kitatokea? Tukutane sehemu ijayo.
 
Umeirudia mkuu
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Tisa

Saa moja baada ya kikosi cha B1, chini ya kiongozi wake Daniel Mwaseba kupewa kazi ya kuchunguza mahali alipo Dr Luis. Katika nyumba moja kubwa iliyopo huko Kigamboni kulikuwa na kikao cha siri.

Kilikuwa ni kikao cha watu watatu.

"Nashukuru sana tumefanikisha zoezi la kumteka Dr Luis, huyu mzee ni muhimu sana katika hii mpango wetu wa kutengeneza kirusi cha DH+. Kwa kutumia kirusi hicho na jinsi tulivyoipanga mipango yetu lazima tutamfanya Dr Luis akubaliane na matakwa yetu" Mzee mmoja mnene mweusi alisema mle ndani.

"Ni kweli mzee Msangi. Ni suala la kushukuru sana baada ya kufanikiwa kumpata Dr Luis. Na pia tulifanya maamuzi ya busara sana kumteka yule Daniel, na kumripua kwa Bomu kule Mkuranga. Tuna hakika Daniel kingekuwa kikwazo kikubwa sana katika mpango wetu. Lakini kwasasa tumefanikiwa kuondoa hiko kikwazo. Sasa mpango uliobaki ni mmoja tu, kwenda kumfungua Dr Luis atwambie nini lilikuwa lengo la rais kumleta hapa nchini. Pia ni lazima tumpe mpango wetu wa kutengeneza kirusi DH+" Kijana mwengine wa makamo alisema.

"Upo sahihi Lameck. Tufanye hiyo mipango yetu mapema na kwa haraka kabla hawa washenzi hawajajua nini lengo letu" Mzee Msangi alisema.

"Kwani Dr Luis yupo sehemu gani?" Kijana mwengine aliuliza.

"Kwani hujui Luca. Yupo sehemu salama ndani ya nyumba hiihii. Hii nyumba imejengwa maalum kwa kazi kama hizi. Chini kabisa ya nyumba hii kuna chumba cha siri ambacho ndimo Dr Luis amewekwa. Atahojiwa hukohuko. Baada ya kutwambia lengo la rais kumleta hapa nchini. Tutampa Dr Luis mpango wetu wa kutengeneza kirusi DH+" Mzee Msangi alisema.

"Tutaenda na Carlos kumuhoji Dr Luis?" Lameck aliuliza.

"Kwani hujui Lameck. Watu wa kule Mkuranga wote waliuwawa kwa shambulio la Bomu. Roho alipata wasiwasi baada ya kusikia Daniel alikuwa katika harakati za kutoroka mle ndani. Alitoa maamuzi magumu ya kuilipua ile nyumba na wote waliomo ndani. Kina Carlos, Dingo na wote waliuwawa mle ndani, akiwemo Daniel Mwaseba" Mzee Msangi alisema.

"E bwana wee!! Sasa nani ataenda kumfungua Dr Luis huko chini. Carlos ndiye tuliyekuwa tunamtegemea katika kazi ya kuwafanya watu waseme hata yale wasiyoulizwa. Sasa nani ataifanya kazi hiyo kwa Dr Luis?" Luca aliuliza.

"Tuna Imma Ogbo. Imma Ogbo amekuja leo kutoka nchini Nigeria kwa kazi hiyo" Mzee Msangi alisema.

"OK, twendeni na huyo Imma Ogbo kwa Dr Luis tukamfungue" Lameck alisema.

"Hapana, sisi hatutaenda huko chini. Tutashuhudia kila kitu kutokea hapa. Chumba cha mateso kimeunganishwa na kamera ambazo tutashuhudia kila kitu Imma Ogbo atakachofanya" Mzee Msangi alisema.

Watu wote wakatulia.

Mzee Msangi aliwasha runinga kubwa iliyopo ukutani. Akabonyazabonyaza rimoti kisha picha ilionekana katika ile runinga iliyapachikwa ukutani.

Chumba cha siri kilikuwa kinaonekana.

Mzee mmoja aliyechoka wa kizungu alionekana katika kile chumba. Alikuwa amekaa katika kiti akiwa na mawazo mengi.

"Yule ndio Dr Luis" Mzee Msangi alisema.

"Anaonekana ana mawazo mengi" Lameck alisema.

"Tulifanya makusudi kumwacha kwa muda ili aingiwe na wasiwasi. Sasa ni muda muafaka wa Imma Ogbo kwenda kumfungua kila kitu, na kumpa kazi yetu." Mzee Msangi alisema.

Akachukua simu yake na kuibonyaza. Akaitafuta namba ya Imma.
Akapiga.

"Imma, unaweza kwenda sasa kumuhoji Dr Luis. Hakikisha anasema kila kitu. Unaruhusiwa kumtesa uwezavyo, lakini hakikisha hafi. Tunamuhitaji sana Dr Luis katika mambo yetu" Mzee Msangi alisema.

"Usiwe na hofu mzee. Atasema tu huyu mzungu" Imma Ogbo akasema kwa kifupi.

"Nakuamini Imma Ogbo"

"Sijawahi kukosea katika kazi hizi" Imma Ogbo alisema kwa kujiamini.

Mzee Msangi akakata simu.

Kupitia ile runinga ya ukutani ya mzee Msangi walimwona Imma Ogbo akiingia katika kile chumba cha mateso.
Imma alikuwa amezaa suruali ya jeans nyeusi, huku juu akiwa amevaa fulana nyeusi iliyokuwa imembana vyema. Aliingia katika kile chumba bila wasiwasi wowote ule. Alipoingia mle ndani moja kwa moja alimsogelea Dr Luis aliyekuwa amekaa katika kile kiti.

"Ninaitwa Imma Ogbo. Nipo hapa kwa kazi mbili tu ambazo bila shaka ninategemea utanipa ushirikiano" Imma alisema.

Dr Luis aliinua sura yake kivivu na kumwangalia yule kijana.

"Kwanini mmenileta hapa?" Dr Luis aliongea kwa kiswahili.

"Hapa kuna mgawanyo wa majukumu. Mimi kama Imma Ogbo jukumu langu ni kuuliza maswali, na wewe kama Dr Luis jukumu lako ni kujibu tu. Ukifanya vingine utafahamu upande wangu wa pili wa shilingi" Imma alisema kwa utulivu.

Dr Luis alikaa kimya huku akimwangalia yule kijana aliyejitambulisha kwa jina la Imma Ogbo.

"Tunajua umekuja hapa jijini baada ya kupewa mwaliko na rais Mgaya. Swali ni mwaliko huo ulihusu nini?" Imma Ogbo aliuliza.

Dr Luis alikaa kimya.

"Nimekuja hapa kama rafiki. Ninaomba tuhojiane kirafiki bila ya kupeana mateso na kumwaga damu!!" Imma Ogbo alipiga mkwara.

"Kwani mnataka nini ninyi watu? Kama mnataka hela niambieni. Nitawapa kiasi chochote kile cha pesa mnirejeshee uhuru wangu..." Dr Luis alisema kwa kulalama.

Imma Ogbo hakuuliza tena swali. Alienda konani kabisa ya kile chumba ambako kulikuwa na kabati dogo, alilifungua kabati na kutoa kisu, na chupa ndogo nyeupe iliyokuwa na majimaji meupe ndani yake. Bila kufunga lile kabati alimsogelea tena Dr Luis.

"Nadhani hujaelewa nimemaanisha nini niliposema hapa kuna mgawanyo wa majukumu. Ngoja nikuoneshe sasa" Imma Ogbo alisema huku akishika mkono wa Dr Luis.

"Nakukata kidole!! Na natavimaliza vidole vyako vyote endapo utaenda kinyume na ninachokueleza" Imma Ogbo alisema akiwa kaushika mkono wa Dr Luis.

Je nini kitatokea? Tukutane sehemu ijayo.
 
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi

Nimekuelewa. Nimekuelewa. Nitafanya kama ulivyonielekeza" Dr Luis alisema huku akitetemeka. Aliiona sura ya Imma Ogbo haikuwa na utani hata chembe.

"Nashukuru sana kwa kuwa muelewa Dr Luis. Hapa uko peke yako. Na ukweli wako pekee ndio utakaokutoa salama mikononi mwa nyumba hii" Imma alisema huku akimwangalia Dr Luis. Dr Luis hakutia neno, alikuwa anamwangalia tu yule mwanaume.

"Eeh nambie, nini lengo la Mheshimiwa rais kukuleta hapa nchini?" Imma Ogbo aliuliza tena.

"Kwa kweli mimi sijui lengo la rais kuniita hapa. Nililetewa ujumbe tu kuwa ninahitajika Tanzania kwa kazi maalum. Sijawahi kukutana na rais maana ameenda nchini Nigeria hivyo sijui ni kazi gani maalum aliyoniita" Dr Luis alijibu.

"Huo ujumbe kwamba unaitwa na rais kwa kazi maalum ulitoka kwa nani? Na wewe ulikufikia kwa njia gani?" Imma Ogbo aliuliza tena.

"Mtu aliyeniletea ujumbe alijitambulisha kwa jina la Irene Dembwe. Na alinitumia ujumbe kwa njia ya email" Dr Luis alisema.

"Unamfaham huyo Irene Dembwe?"

"Hapana simfaham. Nilitegemea ni yeye ndiye atakayekuja kunipokea uwanja wa ndege. Lakini hakuja yeye. Kwahiyo hadi sasa simfahamu huyo Irene Dembwe ni nani?" Dr Luis alisema.

"Kwa hisia zako tu, unahisi ni kitu gani alichokuitia rais hapa nchini?" iImma aliuliza.

"Kwakweli mimi sijui. Pengine ningekutana naye ndipo ningejua rais alikuwa anaiitia nini?"

"Hii ni mara yako ya kwanza kuja Tanzania?"

"Hapana, nimekuja mara nyingi tu Tanzania. Lakini nilikuwa nakuja mwenyewe kwa ajili ya kufanya utalii. Hii ni mara yangu ya kwanza kuja Tanzania kwa kuitwa na rais"

"Sawa Dr Luis. Nimeyasikia naongezi yako. Nina imani haujanidanganya hata kidogo. Ninaenda kuchunguza juu ya haya uliyonambia. Ukiwa umenidanganya tu jua maisha yako yatakuwa matatani" Imma Ogbo alisema..

Dr Luis alikaa kimya.

Imma Ogbo alitoka katika kile chumba alichofungiwa Dr Luis.

***

Daniel Mwaseba, David na Adrian Kaanan walikuwa wamekaa sebuleni katika nyumba ya siri iliyokuwa inamilikiwa na idara ya usalama wa Taifa. Walikuwa wanapanga mipango yao jinsi ya kuifikikisha mwisho kazi waliyopewa.

Daniel alikuwa tayari amepelekea kompyuta yake Hannan kule wodini.

Sasa wote watatu walikuwa tayari kuchunguza mahali alipopelekwa Dr Luis.

"Adrian na David bila shaka tumeona nguvu ya watu tunaoenda kupambana nao. Utumiaji wa helkopta kule Mkuranga na kuachia Bomu katika kupoteza ushahidi inaonesha kwamba hawa sio watu wa mchezo. Hapa, yatupasa kutumia umahiri wetu ili kuhakikisha tunampata Dr Luis. Tena tunampata akiwa hai" Daniel Mwaseba alisema.

"Ni kweli Daniel. Yatupasa kutumia umahiri wetu katika fani hii ya upelelezi, pia umakini mkubwa sana unahitajika. Hatujui nani yupo nyuma ya utekaji wa Dr Luis. Hivyo yatupasa tuwe makini sana" David alisema, huku Adrian akitingisha kichwa kukubaliana nae.

"Mpo sawa ndugu zangu. Kazi yetu inaeleweka, sasa la msingi ni kujua tunaanza wapi katika kuchunguza jambo hili. Muda tuliopewa ni mdogo sana, hivyo lazima tufanye nambo kwa uharaka mkubwa sana" Adrian alisema. Wote wakamwangalia Daniel.

"Siku aliyetekwa Dr Luis nilipigiwa simu na mfanyakazi wa hoteli ya Dos Santos anayeitwa Kelvin. Baadae nikaja kugundua kwamba Kelvin anashirikiana na wale watekaji. Sasa mimi naona tuanze na huyu Kelvin. Tuisake namba ya Kelvin. Kisha tutamwambia Hannah aichunguze namba hiyo tuone alikuwa anawasiliana na nani mara kwa mara kabla ya tukio lile.

Pia lazima tujue Kelvin alikuwa anaishi wapi? Kama tukikuta hakuna mtu wa kumtilia shaka katika mawasiliano ya simu yake tutawauliza majirani ni nani akiyeenda kumtembelea mara kwa mara. Tutaanzia hapo uchunguzi wetu" Daniel alisema.

Adrian na David walitikisa vichwa kuonesha kuwa wamekubaliana na mpango wa Daniel.

"Sasa tunaipataje namba ya kelivin?" David aliuliza.

"Ni jambo dogo sana hilo. Nina namba ya meneja wa hoteli ya Dos Santos katika kitabu changu ninachohifadhi namba zangu muhimu za simu. Ngoja nikachukue tumpigie ili atupatie namba ya Kelvin" Daniel alisema.

Daniel alienda katika chumba kimoja kilichokuwa mle ndani. Akarudi na kitabu kidogo mkononi.

"Hii hapa namba ya meneja wa hoteli ya Dos Santos" Akasema.

David aliichukua kile kijitabu kidogo mikononi mwa Daniel. Akaziandika zile namba katika simu yake na kupiga. Kisha akampa simu Daniel.

"Hallo bosi Fadhili" Daniel akasema.

"Hallo, habari yako?" Meneja Fadhili alijibu.

"Unaongea na Daniel Mwaseba" Meneja Fadhili alisema.

Meneja Fadhili alihema kidogo baada ya Daniel kujitambulisha kisha akasema.

"Aaah Daniel, nambie"

"Nina shida moja ndogo" Daniel akavuta pumzi. "Nahitaji namba ya mfanyakazi wako Kelvin"

"Kelvin?" Mbona aliuwawa katika mripuko wa bomu huko Mkuranga.

"Nafaham, ila naiihitaji namba yake"

" Ook nakutumia"

Ilichukua kama dakika tano. Meneja Fadhili alimtumia namba Daniel. Naye moja kwa moja aliituma kwa Hannan ili aichunguze watu waliowasiliana na namba ile.

Majibu yaliyotoka kwa Hannan, yalimwacha kila mtu mdomo wazi.

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
 
RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Moja

Hannan alimpigia Daniel simu dakika kumi baadae, ili kumpa majibu ya kazi aliyopewa ya kuichunguza namba ya Kelvin aliyekuwa mfanyakazi wa hotel ya Dos Santos.

"Naomba niongee na Daniel, David" Hannan alisema alipopiga simu ya David.

"Hannan huyu hewani anataka kuongea na wewe" David alisema huku akimkabidhi simu Daniel.

"Eeh nambie Hannan, umepata nini katika simu ya Kelvin?" Daniel aliuliza.

"Daniel, hii namba inaonesha imetumika mfululizo kwa miaka mitatu sasa. Na mtumiaji kwa mujibu wa usajili wake ni huyo Kelvin, lakini cha kushangaza hakuna kumbukumbu yoyote ile katika hii namba" Hannan alisema.

"Unasemaje Hannan?"

"Nd'o hivyo Daniel, nimejaribu kuichunguza hii namba, hakuna kumbukumbu yoyote ile. Hakuna kumbukumbu za watu waliompigia, waliopiga wala meseji. Lakini namba inaonesha kwamba ilikuwa inatumika ndani ya miaka mitatu mfululizo" Hannan alirudia tena.

"Wametuwahi hawa mbwa" Daniel alisema kwa sauti ndogo.

"Yani hawa watu wanafanya mambo yao kwa umakini sana. Wamefuta kumbukumbu zote za hii namba" Hannan alisema.

"Wamejaribu lakini bado hawataweza. Lazima tutawagundua tu hawa watu ni kina nani? Na wana nia gani na Taifa hili?" Daniel alisema.

"Nakuombea sana Daniel muwatie mikononi watu hawa. Nina hasira nao sana kwa jinsi walivyotumbukiza risasi katika mwili wangu. Yani natamani ningekuwa mzima ili niungane na nyinyi ili kuwakamata hawa mafedhuli" Hannan alisema kwa hasira.

"Pole sana Hannan. Msaada wako ni mkubwa sana. Hesabu tu nawewe upo ndani ya kazi hii. Jina lako litaandikwa kwa wino wa dhahabu siku tutakayoifanikisha kazi hii. Na kuliacha salama taifa letu. Lakini vipi unaendeleaje kwa sasa Hannan?"

"Operesheni za kuondoa risasi imekwenda vizuri sana. Kwa sasa ninauguza vidonda tu. Nitakuwa sawa sio muda na bila shaka nitaungana na nyinyi katika kikosi B1" Hannan alisema kwa hisia.

"Kila sekunde ninakuombea Hannan. Bila shaka utakuwa sawa mdogo wangu. Tumekumiss sana kazini" Daniel alisema.

Waliongea kidogo na Hannan, kisha waliagana simuni.

Daniel aliwasimulia wakina Adrian taarifa alizopewa na Hannan. Wote walishangaa sana. Sasa mpango ukabaki mmoja tu, wa kwenda nyumbani kwa Kelvin.

***

Imma Ogbo aliwasiliana na kina mzee Msangi juu ya aliyoyapata kutoka kwa Dr Luis. Bila kujua kwamba walisikia na kuona kila kitu. Aliwaambia pia jioni ndio ataenda rasmi kumueleza mpango wa kutengeza kirusi cha DH+.

"Hawa watu wamejuaje kama nilitakiwa kufika siku ile. Mara zote ninapofika Dar es salaam ujio wangu huwa wa siri sana. Ni rais pekee ndiye anayejua kuwa ninakuja. Safari hii nilishangaa sana baada ya rais kuniambia nitapokelewa na mtu mwengine badala ya Irene Dembwe kama ilivyo kawaida yetu. Bila shaka hapo ndipo siri juu ya ujio wangu ilipoanza kupotea. Najua rais Mgaya atachanganyikiwa sana akisikia nimetekwa. Atafanya juu chini kunitafuta, nipatikane ili siri yake isije ikavuja. Hawa watu walioniteka wamehisi nini kitu kinachonifanya nije Tanzania mwanzo na mwisho wa mwezi? Ila hawawezi kujua. Nilitazama sura ya yule mtu aliyekuja kunihoji inaonesha hajui chochote. Pengine kuna mambo yao mengine kabisa yaliyofanya waniteke. Niliahidi nitatunza siri ya rais Mgaya siku zote za maisha yangu. Na itakuwa hivyo. Sitoisema kwa mtu yoyote yule.

Hawa jamaa wanaonekana makatili sana, niliona macho ya yule jamaa yalivyobadilika alivyotaka kunikata kidole. Lakini niseme tu, sitasema kitu chochote kile juu ya siri ya rais Mgaya" Dr Luis alikuwa anawaza.

Kipindi Dr Luis anawaza juu ya kuificha siri ya rais, Daniel Mwaseba, Adrian Kaanan na David John walikuwa wanaelekea nyumbani kwa Kelvin.

Ilikuwa mitaa ya Mikocheni jijini Dar es salaam. Katika nyumba moja yenye geti kubwa jeusi iliyokaribu na hospitali ya Kairuki. Walipewa hadi namba ya nyumba na meneja wa hoteli ya Dos Santos baada ya Daniel kumpigia tena.

Wakiwa njiani walikutana na foleni kubwa sana. Foleni haikuwa ya kawaida. Wakiwa katikati ya foleni ndipo walipoanza kusikia tetesi kwamba mbele kuna nyumba inaungua moto. Wote waliingiwa na uwoga kusikia taarifa hiyo. Kwakuwa mahali walipokuwepo hapakuwa mbali sana na mahali walipoelekezwa kuwa anaishi Kelvin.

Adrian Kaanan alishuka kwenye gari na kuelekea upande ilipokuwa nyumba ya Kelvin.

Alipokaribia, alipigwa na butwaa!!!. Nyumba ya Kelvin ndio iliyokuwa inawaka moto!

Watu wengi walijaa eneo lile wakishuhudia ile nyumba kubwa ikiteketea. Adrian Kaanan aliiweka mikono yake yote miwili mdomoni. Macho yamemtoka pima.

Akiwa haamini. Haamini hata kidogo...

"Wameichoma moto nyumba ya Kelvin. Bila shaka kuna kitu wamekificha tena hapa. Walifuta mawasiliano ya Kelvin wakificha kitu na sasa wameichoma nyumba yake katika mwendelezo wao wa kuficha vitu vyao. Lakini hawa watu waliomteka Dr Luis ni kina nani hasa? Na wana lengo gani?" Adrian Kaanan aliwaza.

Hakukaa tena eneo lile. Maana hakukuwa ni kitu chochote kile ambacho kingemsaidia katika uchunguzi wake. Alirejea kule alipowaacha wakina Daniel.

"Tuambie, umefanikiwa kufika?" Davis aliuliza Adrian alipowasili tu.

"Nimekuta nyumba ya Kelvin inaungua moto!!" Adrian alisema kwa sauti ya kuchoka.

"Ni meneja Fadhili wa Dos Santos" Daniel aliropoka. "Bila shaka ndiye anayevujisha siri zetu. Mpigie Hannan aifatilie simu ya meneja tujue yupo wake. Tumfuate sasahivi. Huu ni mwisho wake wa kutuchezea michezo ya kijinga" Daniel Mwaseba alisema kwa hasira.

Je nini kitatokea. Tuwe wote sehemu ijayo.
 
RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Moja

Hannan alimpigia Daniel simu dakika kumi baadae, ili kumpa majibu ya kazi aliyopewa ya kuichunguza namba ya Kelvin aliyekuwa mfanyakazi wa hotel ya Dos Santos.

"Naomba niongee na Daniel, David" Hannan alisema alipopiga simu ya David.

"Hannan huyu hewani anataka kuongea na wewe" David alisema huku akimkabidhi simu Daniel.

"Eeh nambie Hannan, umepata nini katika simu ya Kelvin?" Daniel aliuliza.

"Daniel, hii namba inaonesha imetumika mfululizo kwa miaka mitatu sasa. Na mtumiaji kwa mujibu wa usajili wake ni huyo Kelvin, lakini cha kushangaza hakuna kumbukumbu yoyote ile katika hii namba" Hannan alisema.

"Unasemaje Hannan?"

"Nd'o hivyo Daniel, nimejaribu kuichunguza hii namba, hakuna kumbukumbu yoyote ile. Hakuna kumbukumbu za watu waliompigia, waliopiga wala meseji. Lakini namba inaonesha kwamba ilikuwa inatumika ndani ya miaka mitatu mfululizo" Hannan alirudia tena.

"Wametuwahi hawa mbwa" Daniel alisema kwa sauti ndogo.

"Yani hawa watu wanafanya mambo yao kwa umakini sana. Wamefuta kumbukumbu zote za hii namba" Hannan alisema.

"Wamejaribu lakini bado hawataweza. Lazima tutawagundua tu hawa watu ni kina nani? Na wana nia gani na Taifa hili?" Daniel alisema.

"Nakuombea sana Daniel muwatie mikononi watu hawa. Nina hasira nao sana kwa jinsi walivyotumbukiza risasi katika mwili wangu. Yani natamani ningekuwa mzima ili niungane na nyinyi ili kuwakamata hawa mafedhuli" Hannan alisema kwa hasira.

"Pole sana Hannan. Msaada wako ni mkubwa sana. Hesabu tu nawewe upo ndani ya kazi hii. Jina lako litaandikwa kwa wino wa dhahabu siku tutakayoifanikisha kazi hii. Na kuliacha salama taifa letu. Lakini vipi unaendeleaje kwa sasa Hannan?"

"Operesheni za kuondoa risasi imekwenda vizuri sana. Kwa sasa ninauguza vidonda tu. Nitakuwa sawa sio muda na bila shaka nitaungana na nyinyi katika kikosi B1" Hannan alisema kwa hisia.

"Kila sekunde ninakuombea Hannan. Bila shaka utakuwa sawa mdogo wangu. Tumekumiss sana kazini" Daniel alisema.

Waliongea kidogo na Hannan, kisha waliagana simuni.

Daniel aliwasimulia wakina Adrian taarifa alizopewa na Hannan. Wote walishangaa sana. Sasa mpango ukabaki mmoja tu, wa kwenda nyumbani kwa Kelvin.

***

Imma Ogbo aliwasiliana na kina mzee Msangi juu ya aliyoyapata kutoka kwa Dr Luis. Bila kujua kwamba walisikia na kuona kila kitu. Aliwaambia pia jioni ndio ataenda rasmi kumueleza mpango wa kutengeza kirusi cha DH+.

"Hawa watu wamejuaje kama nilitakiwa kufika siku ile. Mara zote ninapofika Dar es salaam ujio wangu huwa wa siri sana. Ni rais pekee ndiye anayejua kuwa ninakuja. Safari hii nilishangaa sana baada ya rais kuniambia nitapokelewa na mtu mwengine badala ya Irene Dembwe kama ilivyo kawaida yetu. Bila shaka hapo ndipo siri juu ya ujio wangu ilipoanza kupotea. Najua rais Mgaya atachanganyikiwa sana akisikia nimetekwa. Atafanya juu chini kunitafuta, nipatikane ili siri yake isije ikavuja. Hawa watu walioniteka wamehisi nini kitu kinachonifanya nije Tanzania mwanzo na mwisho wa mwezi? Ila hawawezi kujua. Nilitazama sura ya yule mtu aliyekuja kunihoji inaonesha hajui chochote. Pengine kuna mambo yao mengine kabisa yaliyofanya waniteke. Niliahidi nitatunza siri ya rais Mgaya siku zote za maisha yangu. Na itakuwa hivyo. Sitoisema kwa mtu yoyote yule.

Hawa jamaa wanaonekana makatili sana, niliona macho ya yule jamaa yalivyobadilika alivyotaka kunikata kidole. Lakini niseme tu, sitasema kitu chochote kile juu ya siri ya rais Mgaya" Dr Luis alikuwa anawaza.

Kipindi Dr Luis anawaza juu ya kuificha siri ya rais, Daniel Mwaseba, Adrian Kaanan na David John walikuwa wanaelekea nyumbani kwa Kelvin.

Ilikuwa mitaa ya Mikocheni jijini Dar es salaam. Katika nyumba moja yenye geti kubwa jeusi iliyokaribu na hospitali ya Kairuki. Walipewa hadi namba ya nyumba na meneja wa hoteli ya Dos Santos baada ya Daniel kumpigia tena.

Wakiwa njiani walikutana na foleni kubwa sana. Foleni haikuwa ya kawaida. Wakiwa katikati ya foleni ndipo walipoanza kusikia tetesi kwamba mbele kuna nyumba inaungua moto. Wote waliingiwa na uwoga kusikia taarifa hiyo. Kwakuwa mahali walipokuwepo hapakuwa mbali sana na mahali walipoelekezwa kuwa anaishi Kelvin.

Adrian Kaanan alishuka kwenye gari na kuelekea upande ilipokuwa nyumba ya Kelvin.

Alipokaribia, alipigwa na butwaa!!!. Nyumba ya Kelvin ndio iliyokuwa inawaka moto!

Watu wengi walijaa eneo lile wakishuhudia ile nyumba kubwa ikiteketea. Adrian Kaanan aliiweka mikono yake yote miwili mdomoni. Macho yamemtoka pima.

Akiwa haamini. Haamini hata kidogo...

"Wameichoma moto nyumba ya Kelvin. Bila shaka kuna kitu wamekificha tena hapa. Walifuta mawasiliano ya Kelvin wakificha kitu na sasa wameichoma nyumba yake katika mwendelezo wao wa kuficha vitu vyao. Lakini hawa watu waliomteka Dr Luis ni kina nani hasa? Na wana lengo gani?" Adrian Kaanan aliwaza.

Hakukaa tena eneo lile. Maana hakukuwa ni kitu chochote kile ambacho kingemsaidia katika uchunguzi wake. Alirejea kule alipowaacha wakina Daniel.

"Tuambie, umefanikiwa kufika?" Davis aliuliza Adrian alipowasili tu.

"Nimekuta nyumba ya Kelvin inaungua moto!!" Adrian alisema kwa sauti ya kuchoka.

"Ni meneja Fadhili wa Dos Santos" Daniel aliropoka. "Bila shaka ndiye anayevujisha siri zetu. Mpigie Hannan aifatilie simu ya meneja tujue yupo wake. Tumfuate sasahivi. Huu ni mwisho wake wa kutuchezea michezo ya kijinga" Daniel Mwaseba alisema kwa hasira.

Je nini kitatokea. Tuwe wote sehemu ijayo.
Safi mwendelezo lini tena kamanda?
 
RIWAYA; BOMU
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Moja

Hannan alimpigia Daniel simu dakika kumi baadae, ili kumpa majibu ya kazi aliyopewa ya kuichunguza namba ya Kelvin aliyekuwa mfanyakazi wa hotel ya Dos Santos.

"Naomba niongee na Daniel, David" Hannan alisema alipopiga simu ya David.

"Hannan huyu hewani anataka kuongea na wewe" David alisema huku akimkabidhi simu Daniel.

"Eeh nambie Hannan, umepata nini katika simu ya Kelvin?" Daniel aliuliza.

"Daniel, hii namba inaonesha imetumika mfululizo kwa miaka mitatu sasa. Na mtumiaji kwa mujibu wa usajili wake ni huyo Kelvin, lakini cha kushangaza hakuna kumbukumbu yoyote ile katika hii namba" Hannan alisema.

"Unasemaje Hannan?"

"Nd'o hivyo Daniel, nimejaribu kuichunguza hii namba, hakuna kumbukumbu yoyote ile. Hakuna kumbukumbu za watu waliompigia, waliopiga wala meseji. Lakini namba inaonesha kwamba ilikuwa inatumika ndani ya miaka mitatu mfululizo" Hannan alirudia tena.

"Wametuwahi hawa mbwa" Daniel alisema kwa sauti ndogo.

"Yani hawa watu wanafanya mambo yao kwa umakini sana. Wamefuta kumbukumbu zote za hii namba" Hannan alisema.

"Wamejaribu lakini bado hawataweza. Lazima tutawagundua tu hawa watu ni kina nani? Na wana nia gani na Taifa hili?" Daniel alisema.

"Nakuombea sana Daniel muwatie mikononi watu hawa. Nina hasira nao sana kwa jinsi walivyotumbukiza risasi katika mwili wangu. Yani natamani ningekuwa mzima ili niungane na nyinyi ili kuwakamata hawa mafedhuli" Hannan alisema kwa hasira.

"Pole sana Hannan. Msaada wako ni mkubwa sana. Hesabu tu nawewe upo ndani ya kazi hii. Jina lako litaandikwa kwa wino wa dhahabu siku tutakayoifanikisha kazi hii. Na kuliacha salama taifa letu. Lakini vipi unaendeleaje kwa sasa Hannan?"

"Operesheni za kuondoa risasi imekwenda vizuri sana. Kwa sasa ninauguza vidonda tu. Nitakuwa sawa sio muda na bila shaka nitaungana na nyinyi katika kikosi B1" Hannan alisema kwa hisia.

"Kila sekunde ninakuombea Hannan. Bila shaka utakuwa sawa mdogo wangu. Tumekumiss sana kazini" Daniel alisema.

Waliongea kidogo na Hannan, kisha waliagana simuni.

Daniel aliwasimulia wakina Adrian taarifa alizopewa na Hannan. Wote walishangaa sana. Sasa mpango ukabaki mmoja tu, wa kwenda nyumbani kwa Kelvin.

***

Imma Ogbo aliwasiliana na kina mzee Msangi juu ya aliyoyapata kutoka kwa Dr Luis. Bila kujua kwamba walisikia na kuona kila kitu. Aliwaambia pia jioni ndio ataenda rasmi kumueleza mpango wa kutengeza kirusi cha DH+.

"Hawa watu wamejuaje kama nilitakiwa kufika siku ile. Mara zote ninapofika Dar es salaam ujio wangu huwa wa siri sana. Ni rais pekee ndiye anayejua kuwa ninakuja. Safari hii nilishangaa sana baada ya rais kuniambia nitapokelewa na mtu mwengine badala ya Irene Dembwe kama ilivyo kawaida yetu. Bila shaka hapo ndipo siri juu ya ujio wangu ilipoanza kupotea. Najua rais Mgaya atachanganyikiwa sana akisikia nimetekwa. Atafanya juu chini kunitafuta, nipatikane ili siri yake isije ikavuja. Hawa watu walioniteka wamehisi nini kitu kinachonifanya nije Tanzania mwanzo na mwisho wa mwezi? Ila hawawezi kujua. Nilitazama sura ya yule mtu aliyekuja kunihoji inaonesha hajui chochote. Pengine kuna mambo yao mengine kabisa yaliyofanya waniteke. Niliahidi nitatunza siri ya rais Mgaya siku zote za maisha yangu. Na itakuwa hivyo. Sitoisema kwa mtu yoyote yule.

Hawa jamaa wanaonekana makatili sana, niliona macho ya yule jamaa yalivyobadilika alivyotaka kunikata kidole. Lakini niseme tu, sitasema kitu chochote kile juu ya siri ya rais Mgaya" Dr Luis alikuwa anawaza.

Kipindi Dr Luis anawaza juu ya kuificha siri ya rais, Daniel Mwaseba, Adrian Kaanan na David John walikuwa wanaelekea nyumbani kwa Kelvin.

Ilikuwa mitaa ya Mikocheni jijini Dar es salaam. Katika nyumba moja yenye geti kubwa jeusi iliyokaribu na hospitali ya Kairuki. Walipewa hadi namba ya nyumba na meneja wa hoteli ya Dos Santos baada ya Daniel kumpigia tena.

Wakiwa njiani walikutana na foleni kubwa sana. Foleni haikuwa ya kawaida. Wakiwa katikati ya foleni ndipo walipoanza kusikia tetesi kwamba mbele kuna nyumba inaungua moto. Wote waliingiwa na uwoga kusikia taarifa hiyo. Kwakuwa mahali walipokuwepo hapakuwa mbali sana na mahali walipoelekezwa kuwa anaishi Kelvin.

Adrian Kaanan alishuka kwenye gari na kuelekea upande ilipokuwa nyumba ya Kelvin.

Alipokaribia, alipigwa na butwaa!!!. Nyumba ya Kelvin ndio iliyokuwa inawaka moto!

Watu wengi walijaa eneo lile wakishuhudia ile nyumba kubwa ikiteketea. Adrian Kaanan aliiweka mikono yake yote miwili mdomoni. Macho yamemtoka pima.

Akiwa haamini. Haamini hata kidogo...

"Wameichoma moto nyumba ya Kelvin. Bila shaka kuna kitu wamekificha tena hapa. Walifuta mawasiliano ya Kelvin wakificha kitu na sasa wameichoma nyumba yake katika mwendelezo wao wa kuficha vitu vyao. Lakini hawa watu waliomteka Dr Luis ni kina nani hasa? Na wana lengo gani?" Adrian Kaanan aliwaza.

Hakukaa tena eneo lile. Maana hakukuwa ni kitu chochote kile ambacho kingemsaidia katika uchunguzi wake. Alirejea kule alipowaacha wakina Daniel.

"Tuambie, umefanikiwa kufika?" Davis aliuliza Adrian alipowasili tu.

"Nimekuta nyumba ya Kelvin inaungua moto!!" Adrian alisema kwa sauti ya kuchoka.

"Ni meneja Fadhili wa Dos Santos" Daniel aliropoka. "Bila shaka ndiye anayevujisha siri zetu. Mpigie Hannan aifatilie simu ya meneja tujue yupo wake. Tumfuate sasahivi. Huu ni mwisho wake wa kutuchezea michezo ya kijinga" Daniel Mwaseba alisema kwa hasira.

Je nini kitatokea. Tuwe wote sehemu ijayo.
Tupo tunaisubiri mwendelezo
 
RIWAYA; BOMU
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652212391

Sehemu ya kumi na mbili

David aliitoa simu yake mfukoni na kumpigia Hannan.

"Inaita simu.." David alisema wakati akimpatia simu Daniel.

"Hallo Daniel ?" Hannan alisema simuni pindi tu alipopokea simu ya David.

"Hannan unaendeleaje?" Daniel aliuliza.

"Naendelea vizuri kwasada. Alikuja daktari kuniona dakika chache zilizopita. Kaniambia afya yangu inaimarika kwa kasi sana." Hannan alijibu.

"Safi sana. Nakuombea sana kwa Mungu upone Hannan. Ni mimi ndiye nilikuingiza katika hayo matatizo. Na ninakuahidi nitawatia mikononi watu wote waliokufanyia kitendo hiko cha kikatili" Daniel alisema.

"Sawa Hannan. Ingawa usisikitike sana. Nilikuwa katika majukumu yangu niliyoapa. Hii ni ajari kazini.

"Ni kweli, ingawa ahadi yangu kwa hawa washenzi ipo palepale. Lazima wajutie kwa hiki walichokufanyia" Daniel alisema. Kisha akaendelea "Sasa Hannan tuna kazi ya kufanya nataka utusaidie.."

"Ninakusikiliza Daniel. Nipo kwa ajili yenu"

"Nataka uichunguze namba ya meneja wa Dos Santos. Kuna mambo yanatia shaka kidogo juu yake" Daniel alisema.

"Ninarudia tena nipo kwa ajili hiyo kazi. Pamoja na kutaka sana hao wahalifu wakamatwe pia nina kisasi binafsi juu yao kwa hiki walichonifanyia. Nitumie hiyo namba sasahivi"

"Ninakutumia" Daniel akasema.

Simu ikakatwa.

Sekunde hiyohiyo, Daniel alimtumia namba ya meneja Fadhili, Hannan.
Baada ya kama dakika kumi Hannan alipiga simu.

"Hallo Daniel? Nimefanikiwa kuichunguza namba ya meneja Fadhili" Hannan alisema baada ya Daniel kupokea simu.

"Eeh yupo eneo gani kwa sasa?" Daniel aliuliza.

"Kwa mujibu wa simu yake Meneja Fadhili yupo eneo la Sinza Kijiweni, yupo katika nyumba inayotazamana na hoteli ya Deluxe. Nimejaribu kudukua taarifa katika mtandao wa hoteli ya Dos Santis, nimegundua mahali hapo ndipo anapoishi meneja wao" Hannan alisema.

"Nashukuru sana Hannan, kazi nzuri sana. Tupo njiani tukielekea Sinza Kijiweni. Tutawasiliana kadri ya tutakavyokaribia eneo hilo" Daniel alisema na kukata simu.

"Twendeni Sinza Kijiweni sasahivi. Lazima tumuwahi meneja Fadhili. David chepuka pembeni ya barabara tuwahi haraka sana" Daniel alisema.

David alilitoa gari katikati ya foleni na kuanza kupita pembeni ya barabara. Hawakutembea hata dakika tano wakasimamishwa na askari wa usalama barabarani. Kabla yule askari hajasema kitu David alionesha kitambulisho chake.

"Tupo kazini afande" Akasema.

Askari hakuwa na neno. Mkukumkuku wakina Daniel walielekea Sinza Kijiweni.

Wakati wakiwa maeneo ya Sayansi simu ya David iliita tena.

"Hannan anapiga" David alisema huku akimkabidhi simu Daniel Mwaseba.

"Target yetu inasogea" Hannan alisema pindi tu simu ilipopokelewa.

"Inaelekea wapi?" Daniel aliuliza.

"Kwa sasa ipo stendi ya Sinza Kijiweni, inaelekea barabara ya Shekilango" Hannan alisema.

"Sawa Hannan. Sisi tupo Sayansi hapa. Endelea kumfuatilia.." Daniel alisema.

"Jitahidini mumuwahi Daniel" Hannan alisema.

Simu ikakatwa.

David aliongeza kasi ya gari. Pale Sayansi alikata kushoto akipita barabara ya mchepuko iliyokuwa inapita nyuma ya chuo cha Ustawi wa Jamii. Njia hiyo iliwafikisha hadi katika baa ya Hongera, ambapo walikata kushoto tena kuishika njia inayoelekea Shekilango. Mwendo ambao gari lilikuwa linaendeshwa haukuwa wa kawaida. Walikuwa wanamuwahi meneja Fadhili ambaye walihisi kuna kitu anahusiana nacho na hii misheni yao.

Walipofika maeneo ya Sinza Mapambano simu ya David iliita. Kwakuwa simu alikuwa nayo Daniel akaipokea.

"Daniel kuna jambo la kushangaza kidogo limetokea sasahivi" Hannan alisema kwa wahka mkubwa.

"Jambo gani hilo Hannan?" Daniel aliuliza.

"Niliifatilia target yetu hadi usawa wa hoteli ya Rombo. Cha kushangaza target yetu imepotelea hapohapo. Siioni kabisa simu ya meneja Fadhili katika laptop yangu" Hannan alisema.

"Ni kitu gani unahisi kimetokea Hannan?" Daniel aliuliza.

"Meneja Fadhili amezima simu. Bila shaka amegundua kama anafatiliwa" Hannan alisema.

"Kwanini unahisi hivyo?" Daniel aliuliza.

"Nilianza kupatwa na wasiwasi kutokea alipotoka kule nyumbani kwake Sinza Kijiweni. Target yetu ilikuwa inaenda kwa kasi sana. Bila shaka alikuwa anakimbiza gari. Hivyo nilihisi anawakimbia ninyi. Lakini kupotea ghafla simu ya meneja Fadhili katika laptop yangu imeniaminisha hisia zangu. Meneja Fadhili hajazima simu yake kwa bahati mbaya. Imepangwa." Hannan alisema.

"Amejuaje sasa kama tunamfatilia?" Daniel aliuliza.

"Hiyo hata mimi sijajua bado. Lakini hisia zangu zinaniambia hivyo. Meneja Fadhili amegundua kama anafatiliwa" Hannan alisema.

"Hannan ngoja kwanza. Naona kuna wingu la moshi mbele. Bila shaka kuna nyumba inaungua moto" Daniel alisema harakaharaka na kukata simu.

"Ni nini ile?" Daniel aliuliza huku akionesha kwa kidole mbele. Kipindi hiko gari lilikuwa linapita pembeni ya barabara maana foleni ilikuwa imeanza tena.

"Sijui kuna nini? Kuna moshi mzito mbele umeanza sekunde chache baada ya wewe kuanza kuongea na Hannan" Adrian alisema.

Gari ikatembea kidogo ikasimama kabisa. Foleni ilikuwa imeshamiri. Hakukuwa na namna tena ya kusogea mbele.

"David baki hapa na gari. Mimi na Adrian tutakodi pikipiki kwenda kuona kitu gani kimetokea?" Daniel alisema.

"Sawa Daniel"

Daniel na Adrian walishuka katika ile gari. Na kukodi pikipiki mbili ziwafikishe maeneo ya hoteli ya Rombo. Ambapo walihisi moshi ule wanaouona ndipo ulipoanzia.

Dakika tano tu kwa kutumia pikipiki ziliwafikisha mahali ambapo ilikuwa ndipo chanzo cha ule moto. Walichokutana nacho, wote walipigwa na butwaa...

Je nini kitatokea? Tuwe wote katika sehemu ijayo.
 

Similar Discussions

8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom