Six Man
JF-Expert Member
- Dec 19, 2017
- 250
- 884
RIWAYA: BOMU
MWANDISHI: HALFANI SUDY
SIMU: 0652 212391
Sehemu ya Kwanza
DANIEL Mwaseba aliamka ghafla kutoka katika usingizi aliodumu nao kwa saa zisizozidi tatu. Alifumbua macho kwa haraka huku sura yake ikionesha kukereka na kitu kilichomuamsha katikati ya usingizi. Macho yake yote mawili yakiwa wazi huku yakionesha kuwa bado yalihitaji kufumbwa, ili mmiliki wa macho hayo alale. Ndipo simu ya Daniel iliita tena. Hapo ndipo alipogundua kitu kilichomfanya aamke ghafla usiku wa manane, kumbe ilikuwa ni simu yake ya mkononi kuita ule usiku wa manane.
Daniel alinyoosha mkono wake wa kushoto hadi chini ya mto, mahali alipokuwa ameihifadhi simu yake. Aliichukua simu yake na kuipeleka katika paji lake la uso ili kuangalia, ni nani alikuwa mpigaji. Wakati huo bado simu ilikuwa inaendelea kuita. Huku mkono wake wa kushoto ukitetemeshwa kila simu ilipokuwa inatoa mlio.
"Namba ngeni, ni nani huyu anayenipigia simu muda huu?" Daniel alisema kwa sauti ndogo huku akiwa makini kuiangalia ile simu.
Wakati anaipokea simu macho yake yalitua ukutani ambapo kulikuwa na saa kubwa ya mshale ikining'inia katika chumba cha hoteli. Saa ya ukutani ilikuwa inaonesha kuwa yalikuwa majira ya saa tisa na dakika kumi na tatu usiku.
"Hallo" Daniel alisema kivivu simuni.
"Bila shaka naongea na Daniel?" Sauti kavu ya kiume iliuliza simuni. Daniel alihisi kuifahamu ile sauti.
"Ndio, ni Daniel" Daniel alijibu.
"Kuna tatizo kidogo limetokea kwa hawa wageni wenzio uliokuja nao....." Ile sauti ilisema, lakini Daniel hakuiruhusu imalize ilichokuwa inasema.
"Kuna matatizo gani?" Sauti ya Daniel sasa iliingiwa na fadhaha. Aliuliza kwa pupa huku akiinuka kutoka kitandani.
"Hawapo katika vyumba vyao..." Ile sauti ilisema huku ikiambatana na uwoga.
"Wakina Dr Luis hawapo katika vyumba vyao? Haiwezekanii.." Daniel alisema huku akiwa amesimama wima katikati ya chumba cha hoteli. Shuka alilokuwa amejifunika lilikuwa limeanguka chini. Lakini hakujari. Alichokuwa anataka kwenda kukifanya kilikuwa ni bora kwa sasa kuliko lile shuka la hoteli.
Harakaharaka alivua lile pajama la rangi ya bluu alilokuwa amelalia. Alichukua tshirt yake nyeusi juu ya kabati na kuivaa, maandishi mbele ya ile tshirt yalikuwa meupe huku yakisomeka 'Force'. Chini alivaa suruali ya bluu ya 'jeans'. Aliifunga vyema kwa mkanda wake mweusi. Chini alivaa raba nyeusi huku pembeni zikipitiwa na maneno ya rangi nyeupe nayo yakisomeka 'Force'. Alitumia chini ya dakika moja kuvaa vitu vyote hivyo.
Mkuumkuu Daniel alitoka ndani ya chumba cha ile hoteli. Alisimama katikati ya mlango wa kutokea chumbani. Pande zote mbili za kiuno chake akiwa amechomeka bastola nyeusi. Alikuwa tayari kwa kazi. Kazi ya kwenda kumsaka Dr Luis na mkewe waliopotea ndani ya hoteli ya Dos Santos...
***
Daniel Mwaseba, alikuwa ni mfanyakazi katika idara ya usalama wa Taifa. Idara hii ilikuwa inasimamiwa moja kwa moja na ofisi ya rais. Jukumu kuu la idara hii lilikuwa ni kuhakikisha nchi inakuwa salama dhidi ya maadui wote, wa ndani na wa nje, kwa wakati wote.
Asubuhi ya jana, Daniel Mwaseba aliitwa ofisini kwa bosi wake. Baada ya kuitikia wito alipewa jukumu la kwenda kumpokea mgeni majira ya usiku katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere. Mtu aliyepaswa kumpokea alitambulishwa kwa jina la Dr Luis Hamerton, mzee wa kizungu mwenye umri wa miaka themanini na moja, raia wa Marekani.
"Yakupasa kwenda uwanja wa ndege saa nne usiku. Kwa maana tumewasiliana na wenzetu wa Marekani kwamba ndege aliyopanda Dr Luis itatua katika ardhi ya Tanzania saa tano na dakika kumi usiku" Mkurugenzi wa usalama wa Taifa alimpa maagizo Daniel hiyo asubuhi.
"Sawa, nimekuelewa Chifu..nitafika muda huo pale uwanja wa ndege" Daniel alikubali kwa utii.
"Ukishampokea utampeleka hoteli yoyote ambayo itakuwa bora kwa huduma na salama kwake. Daniel, hakikisha Dr Luis haimkaribii hatari yoyote ile akiwa hapa nchini. Keshokutwa asubuhi inabidi umpeleke ikulu ili akaonane na Mheshimiwa rais ataporejea kutoka Nigeria. Kumbuka, Dr Luis ni mtu muhimu sana kwetu na kwa Marekani pia, hivyo hakikisha anakuwa salama salmini akiwa hapa nchini. Dr Luis hapaswi kupatwa na baya lolote lile. Na hii ndio maana nimekuchagua wewe Daniel ukampokee Dr Luis. Ninakuamini sana Daniel na ninaamini utaifanya kazi hii ndogo kwa ufanisi mkubwa" Mkurugenzi wa usalama wa Taifa alisisitiza.
"Nimekuelewa Chifu..na ninakuahidi mgeni wetu hatopatwa na baya lolote lile" Daniel aliahidi mbele ya bosi wake.
Waliagana.
Saa nne kamili usiku Daniel alikuwa katika viunga vya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, alisubiri hadi ndege iliyombeba Dr Luis ilipofika.
Kumbe Dr Luis alikuja na mkewe. Hilo kidogo lilitia shaka katika moyo wa Daniel. Maagizo aliyopewa na Chifu ni kuwa Dr Luis atawasili peke yake, leo hii alikuwa na mwanamke wa kichina pembeni yake. Mwanamke aliyemtambulisha Daniel kuwa ni mkewe.
Je huyu mwanamke ni mke Dr Luis kweli? Dr Luis amepoteaje hotelini? Je Daniel atafanikiwa kumpata? Tuwe wote katika sehemu ijayo ya BOMU..
Tukiwa ukingoni mwa Red butterfly, Halfani Sudy anakuja na hii kitu, inaitwa Bomu.
Karibuni sana wasomaji...
=============
SEHEMU YA PILI
RIWAYA; BOMU
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU 0652 212391
Sehemu ya Pili
Daniel aliwapokea Dr Luis na mkewe katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Julius Nyerere. Aliwaingiza katika gari yake. Ndani ya gari ilikuwa kimya. Hakuna aliyeongea neno lolote lile ndani ya gari wakiwa njiani. Ilikuwa kimya cha kaburi, na moja kwa moja aliwapeleka katika hoteli ya Dos Santos iliyopo maeneo ya Kijitonyama.
Walipofika mapokezi walikutana na kijana mmoja mtanashati. Aliwakaribisha vizuri.
"Tunahitaji chumba kimoja cha kulala" Daniel ndiye alisema pale mapokezi.
"Sawa, chumba mmepata. Na karibuni sana katika hoteli ya Dos Santos" Yule kaka wa mapokezi alisema kwa sauti kavu huku akisogeza vizuri kitabu cha wageni pale mezani.
"Sijui niandike nani?" Yule kijana alisema huku akimwangalia usoni Daniel Mwaseba.
"Mgeni wangu anaitwa John Voosx" Daniel alidanganya jina. Yule kijana aliandika bila wasiwasi wowote.
Baada ya kuandika mambo yote yaliyohitajika katika kile kitabu cha wageni, na kulipa, yule kijana wa mapokezi aliwasindikiza hadi chumbani.
Walifika hadi nje ya mlango. Yule kijana alitoa funguo moja na kufungua ule mlango.
"Karibuni sana hoteli Dos Santos..karibuni sana, hiki ni chumba namba sabini na nane" Yule kijana alisema.
"Ahsante sana. Nimefurahishwa sana na huduma zenu hapa, sijui unaitwa nani kaka?" Daniel aliuliza.
"Ni jukumu letu kaka kutoa huduma bora kwa wateja wetu. Ninaitwa Kelvin Mbinu. Ila wengi hapa wamezoea kuniita Kevi" Yule kijana alisema.
"Nami nitakuita Kevi.." Daniel alisema huku akitabasamu.
"Karibuni tena" Kelvin alisema huku akiwaonesha kwa mkono ndani baada ya kufungua mlango wa kile chumba.
Daniel naye aliwakaribisha ndani ya chumba wageni wake kwa lugha ya kiingereza. Chumbani, waliongea kwa muda wa dakika sita pekee. Huku wakipeana miadi ya kuonana kesho yake asubuhi, kabla Dr Luis hajaonana na mheshiwa rais kesho kutwa.
"Nina wasiwasi sana na usalama wa Dr Luis. Sipaswi kwenda nyumbani kwa Leo, yanipasa na mimi nipange chumba ndani ya hoteli hiihii ili niwe karibu na Dr Luis. Ingawa Chifu hajanambia Dr Luis ni nani hasa, na kwanini kaja nchini lakini bila shaka ni mtu muhimu sana" Daniel Mwaseba alikuwa anawaza wakati akielekea upande wa mapokezi alipokuwa Kelvin.
"Samahani Kevi, naomba nami unipe chumba hapa" Daniel alisema alipofika mapokezi.
"Vyumba vipo kaka" Kelvin alisema huku akivuta kitabu chenye orodha ya wageni.
Daniel naye aliandikishwa kwenye daftari la wateja wa hoteli ya Dos Santos bila kusahau namba ya simu. Daniel akapewa chumba namba tisini na tatu. Hakikuwa mbali sana na chumba walichopewa wakina Dr Luis. Usiku huohuo Daniel alienda katika mgahawa wa hoteli ile na kupata chakula cha usiku. Hadi Daniel anaingia kulala ilikuwa ni saa sita na dakika kumi na tatu usiku.
Daniel alilala kwa muda wa saa tatu tu ndipo simu yake iliita. Baada ya kuipokea ndipo anapewa taarifa za kushangaza kwamba Dr Luis na mkewe wamepotea ndani ya hoteli ya Dos Santos.
Wamepoteaje sasa?
***
Daniel alikuwa anakimbia katika shuruba ndefu ya hoteli ya Dos Santos akielekea upande kulipokuwa chumba namba sabini na nane. Chumba ambacho walikuwa wamepatiwa wakina Dr Luis na mkewe ambao nao walipotelea humo.
Maneno ya aliyopewa na Chifu asubuhi yalikuwa yanarejea kichwani mwa Daniel Mwaseba.
"Ukishampokea utampeleka hoteli yoyote ambayo itakuwa bora kwa huduma na salama kwake. Daniel, hakikisha Dr Luis haimkaribii hatari yoyote ile akiwa hapa nchini. Keshokutwa asubuhi inabidi umpeleke ikulu ili akaonane na Mheshimiwa rais ataporejea kutoka Nigeria. Kumbuka, Dr Luis ni mtu muhimu sana kwetu na kwa Marekani pia, hivyo hakikisha anakuwa salama salmini akiwa hapa nchini. Dr Luis hapaswi kupatwa na baya lolote lile. Na hii ndio maana nimekuchagua wewe Daniel ukampokee Dr Luis. Ninakuamini sana Daniel na ninaamini utaifanya kazi hii ndogo kwa ufanisi mkubwa"
Na sasa hiyo hatari ndio ilikuwa inamkaribia kwa kasi sana Dr Luis.
Sekunde kumi na nane tu zilimfikisha Daniel mbele ya kile chumba. Nje ya chumba kulikuwa na watu saba. Daniel alimtambua mmoja tu kati ya watu wale saba.
Alikuwa Kelvin Mbinu..
"Vipi Kevi? Kimetokea nini?" Daniel aliuliza kwa pupa huku akimfata Kelvin.
"Kuna mambo ya ajabu sana yametokea katika hoteli yetu" Kelvin alisema kwa sauti iliyosawajika.
"Mambo gani hayo Kevi?" Daniel aliuliza huku hofu dhahiri ikitamalaki usoni mwake.
"Kama nilivyokwambia katika simu, wageni wako wametoweka katika mazingira ya kutatanisha sana hapa hotelini" Kelvin alisema.
"Hebu nieleze Kevi, wametowekaji?" Daniel aliuliza.
Je Dr Luis na mkewe wametowekaje. Majibu anayo Kelvin Mbinu..je Daniel ataridhika na majibu ya Kelvin? Na atachukua hatua gani? Tuwe wote katika Bomu sehemu ya tatu.
MWANDISHI: HALFANI SUDY
SIMU: 0652 212391
Sehemu ya Kwanza
DANIEL Mwaseba aliamka ghafla kutoka katika usingizi aliodumu nao kwa saa zisizozidi tatu. Alifumbua macho kwa haraka huku sura yake ikionesha kukereka na kitu kilichomuamsha katikati ya usingizi. Macho yake yote mawili yakiwa wazi huku yakionesha kuwa bado yalihitaji kufumbwa, ili mmiliki wa macho hayo alale. Ndipo simu ya Daniel iliita tena. Hapo ndipo alipogundua kitu kilichomfanya aamke ghafla usiku wa manane, kumbe ilikuwa ni simu yake ya mkononi kuita ule usiku wa manane.
Daniel alinyoosha mkono wake wa kushoto hadi chini ya mto, mahali alipokuwa ameihifadhi simu yake. Aliichukua simu yake na kuipeleka katika paji lake la uso ili kuangalia, ni nani alikuwa mpigaji. Wakati huo bado simu ilikuwa inaendelea kuita. Huku mkono wake wa kushoto ukitetemeshwa kila simu ilipokuwa inatoa mlio.
"Namba ngeni, ni nani huyu anayenipigia simu muda huu?" Daniel alisema kwa sauti ndogo huku akiwa makini kuiangalia ile simu.
Wakati anaipokea simu macho yake yalitua ukutani ambapo kulikuwa na saa kubwa ya mshale ikining'inia katika chumba cha hoteli. Saa ya ukutani ilikuwa inaonesha kuwa yalikuwa majira ya saa tisa na dakika kumi na tatu usiku.
"Hallo" Daniel alisema kivivu simuni.
"Bila shaka naongea na Daniel?" Sauti kavu ya kiume iliuliza simuni. Daniel alihisi kuifahamu ile sauti.
"Ndio, ni Daniel" Daniel alijibu.
"Kuna tatizo kidogo limetokea kwa hawa wageni wenzio uliokuja nao....." Ile sauti ilisema, lakini Daniel hakuiruhusu imalize ilichokuwa inasema.
"Kuna matatizo gani?" Sauti ya Daniel sasa iliingiwa na fadhaha. Aliuliza kwa pupa huku akiinuka kutoka kitandani.
"Hawapo katika vyumba vyao..." Ile sauti ilisema huku ikiambatana na uwoga.
"Wakina Dr Luis hawapo katika vyumba vyao? Haiwezekanii.." Daniel alisema huku akiwa amesimama wima katikati ya chumba cha hoteli. Shuka alilokuwa amejifunika lilikuwa limeanguka chini. Lakini hakujari. Alichokuwa anataka kwenda kukifanya kilikuwa ni bora kwa sasa kuliko lile shuka la hoteli.
Harakaharaka alivua lile pajama la rangi ya bluu alilokuwa amelalia. Alichukua tshirt yake nyeusi juu ya kabati na kuivaa, maandishi mbele ya ile tshirt yalikuwa meupe huku yakisomeka 'Force'. Chini alivaa suruali ya bluu ya 'jeans'. Aliifunga vyema kwa mkanda wake mweusi. Chini alivaa raba nyeusi huku pembeni zikipitiwa na maneno ya rangi nyeupe nayo yakisomeka 'Force'. Alitumia chini ya dakika moja kuvaa vitu vyote hivyo.
Mkuumkuu Daniel alitoka ndani ya chumba cha ile hoteli. Alisimama katikati ya mlango wa kutokea chumbani. Pande zote mbili za kiuno chake akiwa amechomeka bastola nyeusi. Alikuwa tayari kwa kazi. Kazi ya kwenda kumsaka Dr Luis na mkewe waliopotea ndani ya hoteli ya Dos Santos...
***
Daniel Mwaseba, alikuwa ni mfanyakazi katika idara ya usalama wa Taifa. Idara hii ilikuwa inasimamiwa moja kwa moja na ofisi ya rais. Jukumu kuu la idara hii lilikuwa ni kuhakikisha nchi inakuwa salama dhidi ya maadui wote, wa ndani na wa nje, kwa wakati wote.
Asubuhi ya jana, Daniel Mwaseba aliitwa ofisini kwa bosi wake. Baada ya kuitikia wito alipewa jukumu la kwenda kumpokea mgeni majira ya usiku katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere. Mtu aliyepaswa kumpokea alitambulishwa kwa jina la Dr Luis Hamerton, mzee wa kizungu mwenye umri wa miaka themanini na moja, raia wa Marekani.
"Yakupasa kwenda uwanja wa ndege saa nne usiku. Kwa maana tumewasiliana na wenzetu wa Marekani kwamba ndege aliyopanda Dr Luis itatua katika ardhi ya Tanzania saa tano na dakika kumi usiku" Mkurugenzi wa usalama wa Taifa alimpa maagizo Daniel hiyo asubuhi.
"Sawa, nimekuelewa Chifu..nitafika muda huo pale uwanja wa ndege" Daniel alikubali kwa utii.
"Ukishampokea utampeleka hoteli yoyote ambayo itakuwa bora kwa huduma na salama kwake. Daniel, hakikisha Dr Luis haimkaribii hatari yoyote ile akiwa hapa nchini. Keshokutwa asubuhi inabidi umpeleke ikulu ili akaonane na Mheshimiwa rais ataporejea kutoka Nigeria. Kumbuka, Dr Luis ni mtu muhimu sana kwetu na kwa Marekani pia, hivyo hakikisha anakuwa salama salmini akiwa hapa nchini. Dr Luis hapaswi kupatwa na baya lolote lile. Na hii ndio maana nimekuchagua wewe Daniel ukampokee Dr Luis. Ninakuamini sana Daniel na ninaamini utaifanya kazi hii ndogo kwa ufanisi mkubwa" Mkurugenzi wa usalama wa Taifa alisisitiza.
"Nimekuelewa Chifu..na ninakuahidi mgeni wetu hatopatwa na baya lolote lile" Daniel aliahidi mbele ya bosi wake.
Waliagana.
Saa nne kamili usiku Daniel alikuwa katika viunga vya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, alisubiri hadi ndege iliyombeba Dr Luis ilipofika.
Kumbe Dr Luis alikuja na mkewe. Hilo kidogo lilitia shaka katika moyo wa Daniel. Maagizo aliyopewa na Chifu ni kuwa Dr Luis atawasili peke yake, leo hii alikuwa na mwanamke wa kichina pembeni yake. Mwanamke aliyemtambulisha Daniel kuwa ni mkewe.
Je huyu mwanamke ni mke Dr Luis kweli? Dr Luis amepoteaje hotelini? Je Daniel atafanikiwa kumpata? Tuwe wote katika sehemu ijayo ya BOMU..
Tukiwa ukingoni mwa Red butterfly, Halfani Sudy anakuja na hii kitu, inaitwa Bomu.
Karibuni sana wasomaji...
=============
SEHEMU YA PILI
RIWAYA; BOMU
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU 0652 212391
Sehemu ya Pili
Daniel aliwapokea Dr Luis na mkewe katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Julius Nyerere. Aliwaingiza katika gari yake. Ndani ya gari ilikuwa kimya. Hakuna aliyeongea neno lolote lile ndani ya gari wakiwa njiani. Ilikuwa kimya cha kaburi, na moja kwa moja aliwapeleka katika hoteli ya Dos Santos iliyopo maeneo ya Kijitonyama.
Walipofika mapokezi walikutana na kijana mmoja mtanashati. Aliwakaribisha vizuri.
"Tunahitaji chumba kimoja cha kulala" Daniel ndiye alisema pale mapokezi.
"Sawa, chumba mmepata. Na karibuni sana katika hoteli ya Dos Santos" Yule kaka wa mapokezi alisema kwa sauti kavu huku akisogeza vizuri kitabu cha wageni pale mezani.
"Sijui niandike nani?" Yule kijana alisema huku akimwangalia usoni Daniel Mwaseba.
"Mgeni wangu anaitwa John Voosx" Daniel alidanganya jina. Yule kijana aliandika bila wasiwasi wowote.
Baada ya kuandika mambo yote yaliyohitajika katika kile kitabu cha wageni, na kulipa, yule kijana wa mapokezi aliwasindikiza hadi chumbani.
Walifika hadi nje ya mlango. Yule kijana alitoa funguo moja na kufungua ule mlango.
"Karibuni sana hoteli Dos Santos..karibuni sana, hiki ni chumba namba sabini na nane" Yule kijana alisema.
"Ahsante sana. Nimefurahishwa sana na huduma zenu hapa, sijui unaitwa nani kaka?" Daniel aliuliza.
"Ni jukumu letu kaka kutoa huduma bora kwa wateja wetu. Ninaitwa Kelvin Mbinu. Ila wengi hapa wamezoea kuniita Kevi" Yule kijana alisema.
"Nami nitakuita Kevi.." Daniel alisema huku akitabasamu.
"Karibuni tena" Kelvin alisema huku akiwaonesha kwa mkono ndani baada ya kufungua mlango wa kile chumba.
Daniel naye aliwakaribisha ndani ya chumba wageni wake kwa lugha ya kiingereza. Chumbani, waliongea kwa muda wa dakika sita pekee. Huku wakipeana miadi ya kuonana kesho yake asubuhi, kabla Dr Luis hajaonana na mheshiwa rais kesho kutwa.
"Nina wasiwasi sana na usalama wa Dr Luis. Sipaswi kwenda nyumbani kwa Leo, yanipasa na mimi nipange chumba ndani ya hoteli hiihii ili niwe karibu na Dr Luis. Ingawa Chifu hajanambia Dr Luis ni nani hasa, na kwanini kaja nchini lakini bila shaka ni mtu muhimu sana" Daniel Mwaseba alikuwa anawaza wakati akielekea upande wa mapokezi alipokuwa Kelvin.
"Samahani Kevi, naomba nami unipe chumba hapa" Daniel alisema alipofika mapokezi.
"Vyumba vipo kaka" Kelvin alisema huku akivuta kitabu chenye orodha ya wageni.
Daniel naye aliandikishwa kwenye daftari la wateja wa hoteli ya Dos Santos bila kusahau namba ya simu. Daniel akapewa chumba namba tisini na tatu. Hakikuwa mbali sana na chumba walichopewa wakina Dr Luis. Usiku huohuo Daniel alienda katika mgahawa wa hoteli ile na kupata chakula cha usiku. Hadi Daniel anaingia kulala ilikuwa ni saa sita na dakika kumi na tatu usiku.
Daniel alilala kwa muda wa saa tatu tu ndipo simu yake iliita. Baada ya kuipokea ndipo anapewa taarifa za kushangaza kwamba Dr Luis na mkewe wamepotea ndani ya hoteli ya Dos Santos.
Wamepoteaje sasa?
***
Daniel alikuwa anakimbia katika shuruba ndefu ya hoteli ya Dos Santos akielekea upande kulipokuwa chumba namba sabini na nane. Chumba ambacho walikuwa wamepatiwa wakina Dr Luis na mkewe ambao nao walipotelea humo.
Maneno ya aliyopewa na Chifu asubuhi yalikuwa yanarejea kichwani mwa Daniel Mwaseba.
"Ukishampokea utampeleka hoteli yoyote ambayo itakuwa bora kwa huduma na salama kwake. Daniel, hakikisha Dr Luis haimkaribii hatari yoyote ile akiwa hapa nchini. Keshokutwa asubuhi inabidi umpeleke ikulu ili akaonane na Mheshimiwa rais ataporejea kutoka Nigeria. Kumbuka, Dr Luis ni mtu muhimu sana kwetu na kwa Marekani pia, hivyo hakikisha anakuwa salama salmini akiwa hapa nchini. Dr Luis hapaswi kupatwa na baya lolote lile. Na hii ndio maana nimekuchagua wewe Daniel ukampokee Dr Luis. Ninakuamini sana Daniel na ninaamini utaifanya kazi hii ndogo kwa ufanisi mkubwa"
Na sasa hiyo hatari ndio ilikuwa inamkaribia kwa kasi sana Dr Luis.
Sekunde kumi na nane tu zilimfikisha Daniel mbele ya kile chumba. Nje ya chumba kulikuwa na watu saba. Daniel alimtambua mmoja tu kati ya watu wale saba.
Alikuwa Kelvin Mbinu..
"Vipi Kevi? Kimetokea nini?" Daniel aliuliza kwa pupa huku akimfata Kelvin.
"Kuna mambo ya ajabu sana yametokea katika hoteli yetu" Kelvin alisema kwa sauti iliyosawajika.
"Mambo gani hayo Kevi?" Daniel aliuliza huku hofu dhahiri ikitamalaki usoni mwake.
"Kama nilivyokwambia katika simu, wageni wako wametoweka katika mazingira ya kutatanisha sana hapa hotelini" Kelvin alisema.
"Hebu nieleze Kevi, wametowekaji?" Daniel aliuliza.
Je Dr Luis na mkewe wametowekaje. Majibu anayo Kelvin Mbinu..je Daniel ataridhika na majibu ya Kelvin? Na atachukua hatua gani? Tuwe wote katika Bomu sehemu ya tatu.